TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI | ONGEZA FURAHA YAKO MU KAZI YA KUHUBIRI
Fundisha Wanafunzi wa Biblia Namna ya Kujikulisha Wenyewe Kiroho
Ili kutosheleza uhitaji wao wa kiroho na kufanya maendeleo ya kiroho, wanafunzi wa Biblia wanapaswa kujifunza mambo mingi zaidi ya ile yenye tuko nawafundisha. (Mt 5:3; Ebr 5:12–6:2) Wanapaswa pia kujifunza namna ya kujikulisha wenyewe kiroho.
Wakati tu unaanza kujifunza Biblia na mutu, umuonyeshe namna ya kujitayarisha kwa ajili ya funzo, na umutie moyo akuwe nafanya vile. (mwb18.03 uku. 6) Umuitie moyo akuwe naanza na sala mbele ya kujitayarisha kwa ajili ya funzo. Umusaidia ajue namna ya kupata vyombo vya kielektroniki kwa ajili ya funzo, na umuonyeshe namna ya kuvitumia. Umufasirie namna ya kukuwa napata mambo ya mupya ku jw.org na ku JW Télédiffusion. Ukuwe namutia moyo hatua kwa hatua akuwe nasoma Biblia kila siku, akuwe najitayarisha kwa ajili ya mikutano, na kutafuta majibu ya maulizo yenye iko nayo. Umusaidie akuwe nafikiri sana juu ya mambo yenye iko najifunza.
MUANGALIE VIDEO SAIDIA WANAFUNZI WAKO WAJIKULISHE WENYEWE KIROHO, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani Neeta alisaidia Rose aelewe kama kujifunza haiko tu kupata majibu ya maulizo?
Ni nini ilisaidia Rose akuwe hakika kama Yehova iko na haki ya kukataza kufanya ngono mbele ya ndoa?
Fundisha wanafunzi wako wajue namna ya kujifunza na kutumikisha mambo yenye wako najifunza
Rose alielewa kama kufikiri sana maana yake nini?