TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI | ONGEZA FURAHA YAKO MU KAZI YA KUHUBIRI
Saidia Wanafunzi Wako wa Biblia Waepuke Marafiki Wabaya
Juu wanafunzi wa Biblia wakuwe marafiki wa Yehova, wanapaswa kuchagua muzuri marafiki wao. (Zb 15:1, 4) Marafiki wazuri watawasaidia kufanya mambo ya muzuri.—Mez 13:20; lff somo ya 48.
Wakati uko nasaidia wanafunzi wako wa Biblia waepuke marafiki wabaya, ujitie pa nafasi yao. Inaweza kuwa nguvu kwao kuachana na marafiki wao wa zamani. Kwa hiyo, uonyeshe kama unawahangaikia kabisa, hata mu siku zenye hamujifunzake. Unaweza kuwaandikia, kuwaita ku telefone, ao kuwatembelea. Wakati wanafunzi wako wa Biblia wanafanya maendeleo, unaweza kuwaalika ili mupitishe wakati pamoya na watu wa Mungu. Ile itawasaidia waone waziwazi kama hawapoteze, lakini wako napata mingi zaidi ya ile waliacha. (Mk 10:29, 30) Na weye pia utafurahi kuona vile familia ya Yehova inaongezeka.
MUANGALIE VIDEO SAIDIA WANAFUNZI WAKO WAEPUKE MARAFIKI WABAYA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Mashirika ya mubaya njo nini?—1Ko 15:33
Rose aliwaza Wakristo wanajifurahishaka namna gani?
Namna gani Neeta alisaidia Rose aachane na marafiki wabaya?