MAISHA YA MUKRISTO
Mupango wa Kufariji Wale Wenye Wako ku Beteli
Kila mutu anapataka majaribu na iko na lazima ya kufarijiwa na kutegemezwa. Hata wale wenye wako nguvu kiroho ao wenye wako na mapendeleo fulani mu tengenezo ya Yehova wanaweza tu kuvunjika moyo. (Yob 3:1-3; Zb 34:19) Mupango wa kufariji na kutegemeza ndugu na dada wa familia ya Beteli unaweza kutufundisha nini?
MUANGALIE VIDEO “UMUTEGEMEE MUNGU,” NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:
Ndugu na dada wa familia ya Beteli wanapataka magumu gani?
Ni mambo gani ine inafanyiwaka juu ya kuwatia moyo?
Namna gani kufariji wengine kunasaidiaka wale wenye kufariji?