Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w20 Mwezi wa 3 uku. 18-23
  • Ni Wakati Gani Inafaa Kusema?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Wakati Gani Inafaa Kusema?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NI WAKATI GANI TUNAPASWA KUSEMA?
  • NI WAKATI GANI TUNAPASWA KUNYAMAZA?
  • NAMNA GANI YEHOVA ANAONA MAMBO YENYE TUNASEMA?
  • Alitenda kwa Busara
    Tuige Imani Yao
  • Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Busara Yako na Ibarikiwe!”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Tutumainie Ndugu na Dada Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
w20 Mwezi wa 3 uku. 18-23

HABARI YA KUJIFUNZA YA 12

Ni Wakati Gani Inafaa Kusema?

“Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa . . . wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema.”​—MUH. 3:1, 7.

WIMBO 124 Washikamanifu Sikuzote

KIFUPI CHA HABARIa

1. Muhubiri 3:1, 7 inatufundisha nini?

WAMOJA kati yetu wanapenda kusema sana. Wengine wanapenda kunyamaza. Kama vile andiko la musingi la habari hii linaonyesha, kuko wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza. (Soma Muhubiri 3:1, 7.) Tunaweza kupenda wamoja kati ya ndugu na dada zetu wakuwe wanasema sana. Na tunaweza kupenda wengine wasikuwe wanasema sana.

2. Ni nani njo iko na haki ya kutuwekea kanuni kuhusu wakati wenye inafaa kusema na namna tunapaswa kusema?

2 Uwezo wa kusema ni zawadi kutoka kwa Yehova. (Kut. 4:10, 11; Ufu. 4:11) Katika Neno lake, anatusaidia kuelewa namna tunaweza kutumia muzuri ile zawadi. Katika habari hii, tutazungumuzia mifano fulani ya watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia. Mifano hiyo itatusaidia kujua wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza. Tutaona pia namna Yehova anaona mambo yenye tunaambia wengine. Tuzungumuzie kwanza ni wakati gani inafaa kusema.

NI WAKATI GANI TUNAPASWA KUSEMA?

3. Kulingana na Waroma 10:14, ni wakati gani tunapaswa kusema?

3 Tunapaswa kuwa tayari sikuzote kuzungumuza na watu juu ya Yehova na juu ya Ufalme. (Mt. 24:14; soma Waroma 10:14.) Wakati tunafanya vile, tunamuiga Yesu. Moja kati ya sababu zenye zilifanya Yesu akuje ku dunia ni kuambia wengine kweli juu ya Baba yake. (Yoh. 18:37) Lakini, tunapaswa kukumbuka kama namna yetu ya kusema ni ya maana pia. Kwa hiyo, wakati tunazungumuza na wengine juu ya Yehova, tunapaswa kufanya vile kwa “upole na heshima kubwa,” na tunapaswa kuheshimia mawazo ya wengine na mambo yenye wanaamini. (1 Pe. 3:15) Kama tunafanya vile, hatutazungumuza tu na watu lakini pia tutawafundisha na pengine tutagusa mioyo yao.

WAKATI WA KUSEMA

  • Wakati unazungumuza na wengine juu ya Yehova, ufanye vile kwa “upole na heshima kubwa,” ni kusema, uheshimie mambo yenye wanaamini (fungu la 3)

  • Wakati tunaona kama mutu fulani anafanya jambo fulani lenye linaweza kumuongoza kwenye kosa kubwa

  • Wazee wanatoa mashauri kwa uvumilivu na kwa ufundi wakati ni lazima kufanya vile

Dada wawili wanauza nguo mu duka la nguo. Dada mumoja anashauria mwenzake kama jupe ya mufupi yenye anakamata haifae.

(Ona fungu la 8)b

Muzee mumoja, mwenye iko na Biblia, anapatia ndugu mumoja kijana mashauri juu ya usafi. Nyumba ya ule ndugu kijana iko mu hali ya ovyo-ovyo.

(Ona fungu la 4, 9)c

4. Kulingana na Mezali 9:9, namna gani maneno yetu inaweza kusaidia wengine?

4 Wazee hawapaswe kusita kusema wakati wanaona kama ndugu ao dada fulani iko na lazima ya mashauri. Lakini, wanapaswa kuchagua wakati wenye kufaa ili wasimupatishe haya. Inaweza kuwa muzuri wangojee mupaka wakati mutu atakuwa peke yake ili wazungumuze naye. Sikuzote wazee wanapaswa kujikaza kusema kwa njia yenye inaonyesha kama wanaheshimia ndugu ao dada mwenye wako wanazungumuza naye. Lakini, hawapaswe kujizuia kuonyesha wengine kanuni za Biblia zenye zinaweza kuwasaidia watende kwa hekima. (Soma Mezali 9:9.) Juu ya nini ni jambo la maana sana tusikuwe tunaogopa kusema wakati ni lazima kufanya vile? Fikiria mifano mbili yenye iko tofauti: Katika mufano wa kwanza, mwanaume mumoja alipaswa kurekebisha wana wake, na katika mufano wa pili, mwanamuke mumoja alipaswa kuzungumuza na mwanaume mwenye angekuwa mufalme.

5. Ni wakati gani Kuhani Mukubwa Eli hakusema wakati ilifaa kusema?

5 Kuhani Mukubwa Eli alikuwa na wana wawili wenye alikuwa anapenda sana. Lakini, wale wana hawakukuwa wanamuheshimia Yehova. Walikuwa na daraka la maana; walikuwa makuhani wenye walikuwa wanatumikia ku tabenakulo. Lakini, walitumia mubaya mamlaka yao, walizarau matoleo yenye watu walikuwa wanamutolea Yehova, na walikuwa wanafanya uasherati waziwazi. (1 Sa. 2:12-17, 22) Kulingana na Sheria ya Musa, wana wa Eli walistahili kufa, lakini kwa sababu Eli alikuwa mutu wa kuachilia mambo, aliwakaripia tu kwa upole na aliwaacha waendelee kutumikia ku tabenakulo. (Kum. 21:18-21) Yehova alikuwa na mawazo gani juu ya namna Eli alishugulikia ile hali? Alimuambia Eli hivi: “Sababu gani unaendelea kuheshimia wana wako kuliko mimi?” Kisha, Yehova aliamua kuua wale wana wawili waovu.​—1 Sa. 2:29, 34.

6. Habari ya Eli inatufundisha nini?

6 Habari ya Eli inatufundisha jambo fulani la maana. Kama tunaona kuwa rafiki ao mutu fulani wa jamaa amevunja sheria ya Mungu, tunapaswa kusema naye, ili kumukumbusha kanuni za Yehova. Kisha tunapaswa kuhakikisha kama wazee wa kutaniko wamemupatia musaada wenye iko nao lazima. (Yak. 5:14) Hatupaswe hata kidogo kuwa kama Eli, kwa kuheshimia rafiki ao mutu fulani wa jamaa kuliko Yehova. Inaomba uhodari ili kuzungumuza na mutu mwenye iko na lazima ya kushauriwa, lakini kufanya vile kunaweza kuleta matokeo ya muzuri. Ona tofauti kati ya mufano wa Eli na mufano wa mwanamuke Mwisraeli mwenye kuitwa Abigaili.

Abigaili anapiga magoti wakati anazungumuza na Daudi.

Abigaili alituachia mufano muzuri kwa kuchagua wakati wenye kufaa wa kusema (Ona fungu la 7-8)d

7. Juu ya nini Abigaili alisema na Daudi?

7 Abigaili alikuwa bibi ya mwanaume tajiri mwenye alikuwa na mashamba mwenye aliitwa Nabali. Wakati Daudi na wanaume wake walikuwa wanamukimbia Mufalme Sauli, walipitisha wakati fulani pamoja na wachungaji wa Nabali na walilinda mifugo ya Nabali ili isiibwe. Je, Nabali alionyesha shukrani juu ya musaada wao? Hapana. Wakati Daudi alimuomba amupatie yeye na wanaume wake chakula kidogo na maji, Nabali alikasirika na aliwatukana kwa sauti kali. (1 Sa. 25:5-8, 10-12, 14) Kwa hiyo, Daudi aliamua kabisa kuua kila mwanaume wa nyumba ya Nabali. (1 Sa. 25:13, 22) Iliomba kufanya nini juu ya kuepuka musiba huo? Abigaili alitambua kama ulikuwa wakati wa kusema, kwa hiyo, bila kuogopa alienda kukutana na wanaume 400 wenye njaa, wenye kukasirika na wenye silaha na akazungumuza na Daudi.

8. Mufano wa Abigaili unatufundisha nini?

8 Wakati Abigaili alikutana na Daudi, alisema kwa uhodari, kwa heshima, na kwa njia yenye kusadikisha. Hata kama haiko Abigaili njo mwenye alikuwa na kosa, alimuomba Daudi musamaha. Alizungumuzia sifa za muzuri za Daudi na alitumaini kama Yehova atamusaidia. (1 Sa. 25:24, 26, 28, 33, 34) Kama Abigaili, tunapaswa kuwa na uhodari wa kusema ikiwa mutu fulani anafanya jambo fulani lenye linaweza kumuongoza kwenye kosa kubwa. (Zb. 141:5) Tunapaswa kuonyesha heshima, lakini tunapaswa pia kuwa na uhodari. Wakati tunatolea kwa upendo mutu fulani mashauri yenye iko nayo lazima, tunaonyesha kama tuko marafiki wa kweli.​—Mez. 27:17.

9-10. Wazee wanapaswa kukumbuka nini wakati wanashauria wengine?

9 Zaidi sana wazee hawapaswe kuogopa kuzungumuza na ndugu na dada wa kutaniko wenye wanakamata hatua ya mubaya. (Gal. 6:1) Wazee wanatambua kwa unyenyekevu kama wao pia hawakamilike na siku moja wanaweza kuwa na lazima ya mashauri. Lakini wazee hawapaswe kujizuia kukaripia wale wenye wako na lazima ya nizamu. (2 Ti. 4:2; Tit. 1:9) Wakati wanashauria mutu fulani, wanajikaza kutumia zawadi yao ya kusema ili kumufundisha kwa ufundi na kwa uvumilivu. Wanapenda ndugu ao dada yao, na upendo huo unawachochea kutenda. (Mez. 13:24) Lakini jambo lenye wanahangaikia sana ni kumutukuza Yehova kwa kutegemeza kanuni zake na kulinda kutaniko lisipatwe na hatari ya kiroho.​—Mdo. 20:28.

10 Mupaka hapa, tumezungumuzia ni wakati gani inafaa kusema. Lakini, kuko wakati wenye tunapaswa kunyamaza kabisa. Ni magumu gani tunaweza kupambana nayo wakati huo?

NI WAKATI GANI TUNAPASWA KUNYAMAZA?

11. Yakobo alitumia mufano gani, na juu ya nini unafaa?

11 Inaweza kuwa nguvu kuzuia ulimi wetu. Yakobo, muandikaji mumoja wa Biblia, alitumia mufano wenye kufaa ili kuzungumuzia tatizo hilo. Alisema hivi: “Kama mutu yeyote hajikwae katika neno, huyo ni mutu mukamilifu, mwenye anaweza kuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia.” (Yak. 3:2, 3) Lijamu inafungwa ku kichwa na sehemu yake fulani inafungwa mu kinywa cha farasi. Kwa kukokota kamba za lijamu za kuongozea farasi, mupanda-farasi anaweza kuongoza farasi ao kuisimamisha. Kama mupanda-farasi hakamate sana kamba za kuongozea farasi, anaweza kushindwa kuongoza farasi na farasi anaweza kujiumiza ao kuumiza mupanda-farasi. Vilevile, kama tunashindwa kuzuia ulimi wetu, ile inaweza kuleta matatizo mingi. Tuzungumuzie basi ni katika hali fulani gani tunapaswa kujizuia kusema.

WAKATI HAIFAE KUSEMA

  • Wakati tunashawishiwa kufunua habari juu ya namna kazi yetu inafanywa mu inchi mbalimbali kwenye kazi yetu inakatazwa

  • Wakati tunajua habari juu ya mambo ya kipekee sana na ya siri ya kutaniko

Ku Jumba la Ufalme, wahubiri wa eneo hilo wanamuzunguka bwana mumoja na bibi yake wenye waliwatembelea na wanawauliza maulizo.

(Ona fungu la 12)e

Muzee anazungumuza ku telefone na anafunga mulango wakati bibi yake iko anajifunza mu chumba kingine.

(Ona fungu la 13-14)f

12. Ni wakati gani tunapaswa kujizuia kusema?

12 Unatenda namna gani wakati ndugu ao dada anajua habari fulani yenye inapaswa kuonwa kuwa siri? Kwa mufano, kama unakutana na mutu fulani mwenye anaishi mu inchi kwenye kazi yetu inakatazwa, je, unashawishiwa kumuuliza habari fulani kuhusu namna kazi yetu inafanywa mu ile inchi? Kwa kweli, unaweza kuwa na nia ya muzuri ya kufanya vile. Tunapenda ndugu na dada zetu na tunaweza kupenda kujua hali yao. Tunapenda pia kusema mambo waziwazi wakati tunasali juu yao. Lakini, huo ni wakati wa kujizuia kusema. Kama tunakaza mutu fulani atuambie mambo yenye kuwa siri, tunaonyesha kama hatuna upendo, ni kusema, hatupendi ule mutu na hatupendi ndugu na dada wenye wanatumaini kama hatasema habari yenye inahusu kazi yao. Kwa kweli, hakuna mutu kati yetu mwenye atapenda aongezee magumu ndugu na dada zetu wenye wanaishi katika inchi mbalimbali kwenye kazi yetu inakatazwa. Vilevile, ndugu ao dada wenye wanaishi katika inchi kama hizo hawapaswe kufunua habari kuhusu namna Mashahidi wenye kuishi kule wanafanya kazi ya kuhubiri ao kazi zingine za Kikristo.

13. Kulingana na Mezali 11:13, wazee wanapaswa kufanya nini, na juu ya nini?

13 Zaidi sana wazee wa kutaniko wanapaswa kutumia kanuni ya Biblia yenye inapatikana mu Mezali 11:13 kwa kuchunga siri. (Soma.) Inaweza kuwa nguvu kufanya vile, zaidi sana kama muzee iko na bibi. Bibi na bwana wanafanya uhusiano wao ukuwe nguvu kwa kuzungumuza mara kwa mara na kwa kuambiana mawazo yao ya ndani kabisa, namna wanajisikia, na mahangaiko yao. Lakini muzee anajua kama hapaswe kufunua “mazungumuzo ya siri,” ni kusema, mambo ya siri ya ndugu na dada wa kutaniko. Kama anafanya vile, ndugu na dada hawatamutumainia tena na ataharibisha sifa yake. Wale wenye kuwa na madaraka katika kutaniko hawapaswe ‘kuwa na ndimi mbili,’ ao wadanganyifu. (1 Ti. 3:8; maelezo ya chini) Maana yake, hawapaswe kudanganya wengine ao kupiga porojo juu ya wengine. Kama muzee anapenda bibi yake, hatamuambia habari zenye hapaswe kujua.

14. Namna gani bibi ya muzee anaweza kumusaidia bwana yake aendelee kuwa na sifa ya muzuri?

14 Bibi ya muzee anaweza kumusaidia bwana yake aendelee kuwa na sifa ya muzuri kwa kuepuka kumukaza amuambie mambo yenye kuwa siri. Wakati bibi anatumia shauri hilo, anategemeza bwana yake na pia anaonyesha heshima kwa wale wenye wameelezea bwana yake mambo yao ya siri. Na jambo la maana zaidi, anamufurahisha Yehova kwa sababu anasaidia kuendeleza amani na umoja katika kutaniko.​—Ro. 14:19.

NAMNA GANI YEHOVA ANAONA MAMBO YENYE TUNASEMA?

15. Yehova alijisikia namna gani juu ya marafiki tatu wa Yobu, na juu ya nini?

15 Kitabu cha Yobu kinaweza kutufundisha mambo mingi juu ya namna ya kusema na wakati gani inafaa kusema. Kisha Yobu kupata misiba mbalimbali yenye kuhuzunisha sana, wanaume ine walienda kumuona juu ya kumufariji na kumupatia mashauri. Wale wanaume walipitisha wakati murefu bila kusema kitu. Lakini maneno yenye wanaume tatu kati yao walisema kisha, ni kusema, Elifazi, Bildadi, na Sofari, inaonyesha waziwazi kama hawakutumia wakati huo ili kufikiria namna wangemusaidia Yobu. Lakini, walikuwa wanafikiria tu namna wangemuonyesha Yobu kama alikuwa amefanya kosa fulani. Walisema mambo fulani ya kweli, lakini mambo mingi yenye walisema juu ya Yobu na juu ya Yehova haikukuwa ya muzuri na haikukuwa ya kweli. Walisema kama Yobu alikuwa mutu mubaya. (Yob. 32:1-3) Yehova alitenda namna gani? Alikasirikia sana wale wanaume tatu. Alisema kama walikuwa wapumbavu na aliwaambia wamuombe Yobu asali kwa ajili yao.​—Yob. 42:7-9.

16. Mufano mubaya wa Elifazi, Bildadi, na Sofari unaweza kutufundisha nini?

16 Mufano mubaya wa Elifazi, Bildadi, na wa Sofari unatufundisha mambo fulani. Jambo la kwanza, hatupaswe kuhukumu ndugu zetu. (Mt. 7:1-5) Lakini, tunapaswa kuwasikiliza kwa uangalifu mbele ya kusema. Ni kisha kuwasikiliza tu njo tunaweza kuelewa hali yao. (1 Pe. 3:8) Jambo la pili, wakati tunasema, tunapaswa kuwa hakika kama tunatumia maneno ya muzuri na ya kweli. (Efe. 4:25) Na jambo la tatu, Yehova iko muangalifu juu ya mambo yenye tunaambia wengine.

17. Mufano wa Elihu unaweza kutufundisha nini?

17 Mwanaume wa ine mwenye alitembelea Yobu alikuwa Elihu, mutu wa jamaa ya Abrahamu. Alisikiliza wakati Yobu na wale wanaume wengine tatu walikuwa wanasema. Ni wazi kama alisikiliza kwa uangalifu mambo yenye walikuwa wanasema kwa sababu aliweza kupatia Yobu mashauri fulani yenye huruma lakini ya wazi yenye ilimusaidia Yobu arekebishe mawazo yake. (Yob. 33:1, 6, 17) Jambo lenye Elihu alihangaikia zaidi lilikuwa kumutukuza Yehova, hapana kujitukuza yeye mwenyewe ao kutukuza mutu mwingine yeyote. (Yob. 32:21, 22; 37:23, 24) Mufano wa Elihu unatufundisha kama kuko wakati wa kunyamaza na kusikiliza. (Yak. 1:19) Tunajifunza pia kama wakati tunatoa mashauri, jambo lenye tunapaswa kuhangaikia zaidi ni kumutukuza Yehova, hapana kujitukuza sisi wenyewe.

18. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona zawadi ya kusema kuwa ya maana?

18 Tunaweza kuonyesha kama tunaona zawadi ya kusema kuwa ya maana kwa kufuata mashauri ya Biblia juu ya wakati wa kusema na namna ya kusema. Sulemani, mufalme mwenye hekima, aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika hivi: “Kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa ni vile pia neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa.” (Mez. 25:11) Wakati tunasikiliza kwa uangalifu mambo yenye wengine wanasema na kuwaza mbele tuseme, maneno yetu inaweza kuwa kama ile matunda ya mutofaa ya zahabu, ni kusema, inaweza kuwa ya maana na ya kupendeza sana. Kisha, ikuwe tunasemaka kidogo ao sana, maneno yetu itajenga wengine, na tutamufurahisha Yehova. (Mez. 23:15; Efe. 4:29) Ile njo njia ya muzuri kabisa ya kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya zawadi hiyo yenye Mungu ametupatia!

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni wakati gani tunapaswa kusema?

  • Ni wakati gani tunapaswa kunyamaza?

  • Mifano ya watu fulani wenye kuzungumuziwa katika Biblia, wenye tumezungumuzia katika habari hii, imekufundisha nini?

WIMBO 82 “Acheni Nuru Yenu Iangaze”

a Neno la Mungu liko na kanuni zenye zinaweza kutusaidia kujua wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza. Wakati tunajua na kutumia mambo yenye Biblia inasema, maneno yetu itamupendeza Yehova.

b MAFASIRIO YA PICHA: Dada anaona kama inafaa kupatia dada mwingine mashauri yenye hekima.

c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu anatoa mapendekezo juu ya usafi.

d MAFASIRIO YA PICHA: Kwa wakati wenye kufaa, Abigaili alizungumuza na Daudi, na matokeo ilikuwa muzuri.

e MAFASIRIO YA PICHA: Bwana mumoja na bibi yake wanajizuia kufunua habari juu ya kazi yetu katika inchi kwenye inakatazwa.

f MAFASIRIO YA PICHA: Muzee iko muangalifu juu mutu mwingine asisikie wakati anazungumuza juu ya mambo ya siri ya kutaniko.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine