Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w20 Mwezi wa 3 uku. 24-29
  • Mupendane Sana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mupendane Sana
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UKUWE MWENYE KUFANYA AMANI
  • USIKUWE NA UBAGUZI
  • UKUWE MUKARIBISHAJI-WAGENI
  • Kukaribisha Wageni Kunaleta Furaha na Ni Jambo la Maana Sana!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Umupende Yehova Zaidi na Uendelee Kupenda Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Namna ya Kumaliza Kukosana Katika Roho ya Upendo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Namna Tunaweza Kuendelea Kupendana Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
w20 Mwezi wa 3 uku. 24-29

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

Mupendane Sana

“Mupendane sana kutoka katika moyo.”​—1 PE. 1:22.

WIMBO 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

KIFUPI CHA HABARIa

Yesu anazungumuza na mitume wake waaminifu.

Usiku wa mwisho pamoja na mitume wake, Yesu alikazia upendo (Ona fungu la 1-2)

1. Ni amri gani yenye kuwa wazi yenye Yesu alipatia wanafunzi wake? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

USIKU wenye ulitangulia kifo chake, Yesu alipatia wanafunzi wake amri hii yenye kuwa wazi. Aliwaambia hivi: “Kama vile nimewapenda ninyi, ninyi pia mupendane vilevile.” Kisha aliongeza hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.”​—Yoh. 13:34, 35.

2. Juu ya nini ni jambo la maana tupendane?

2 Yesu alisema kama kila mutu atatambua waziwazi wanafunzi wake wa kweli kama wanaonyesha upendo wenye alionyesha. Upendo ulitambulisha Wakristo wa kweli wakati wa mitume, na leo pia ni vile. Njo maana ni jambo la maana sana tupendane hata wakati ni nguvu kufanya vile!

3. Tutajifunza nini katika habari hii?

3 Hali yetu ya kukosa kukamilika inafanya ikuwe nguvu kupendana sana. Lakini, tunapaswa kujikaza kumuiga Kristo. Katika habari hii, tutajifunza namna upendo unatusaidia kuwa wenye kufanya amani, tusikuwe na ubaguzi, na tukuwe wakaribishaji-wageni. Wakati unajifunza habari hii, ujiulize hivi: ‘Mufano wa ndugu na dada wenye wameendelea kupendana hata wakati ni nguvu kufanya vile, unaweza kunifundisha nini?’

UKUWE MWENYE KUFANYA AMANI

4. Kulingana na Matayo 5:23, 24, juu ya nini tunapaswa kufanya amani na ndugu mwenye iko na jambo fulani juu yetu?

4 Yesu alitufundisha kama ni jambo la maana kufanya amani na ndugu ao dada mwenye iko na jambo fulani juu yetu. (Soma Matayo 5:23, 24.) Alikazia kama, ikiwa tunataka kumupendeza Mungu, tunapaswa kuendelea kuwa na uhusiano muzuri na wengine. Yehova anafurahi wakati tunafanya nguvu yetu yote juu ya kufanya amani na ndugu na dada zetu. Hatakubali ibada yetu kama tunawekea mutu fulani kinyongo na kukataa hata kufanya naye amani.​—1 Yo. 4:20.

5. Ni nini ilifanya ikuwe nguvu kwa ndugu mumoja kufanya amani?

5 Inaweza kuwa nguvu kufanya amani. Juu ya nini? Fikiria jambo lenye lilimufikia Mark.b Alijisikia mubaya sana wakati ndugu mumoja alimuchambua na kuambia ndugu na dada wengine wa kutaniko mambo ya mubaya juu yake. Mark alitenda namna gani? Anasema hivi: “Nilishindwa kujizuia na nilikasirika.” Lakini kisha, Mark alihuzunika juu ya matendo yake na alijaribu kumuomba ule ndugu musamaha na kufanya naye amani. Lakini, ule ndugu alikataa kufanya amani na Mark. Ku mwanzo, Mark alijiuliza hivi: ‘Juu ya nini mimi njo niendelee kujaribu kufanya amani kama yeye hapendi?’ Hata hivyo, mwangalizi wa muzunguko alimutia moyo asichoke. Mark alifanya nini?

6. (a)  Namna gani Mark aliendelea kujikaza ili kufanya amani? (b) Namna gani Mark alitumia Wakolosai 3:13, 14?

6 Wakati Mark alichunguza mawazo yake, alitambua kama alikosa unyenyekevu na kama wakati fulani alikuwa anajiona kuwa mutu muzuri kupita wengine. Alielewa kama alipaswa kubadilisha mawazo yake. (Kol. 3:8, 9, 12) Kwa unyenyekevu, alienda kumuona ule ndugu na akamuomba musamaha tena juu ya matendo yake. Pia, Mark aliandikia ule ndugu barua mbalimbali, ili kumuonyesha kama alihuzunika sana juu ya matendo yake na kama alipenda wakuwe tena marafiki. Na hata Mark alimupatia ule ndugu zawadi za kidogo-kidogo zenye aliwaza kama angefurahia. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, ule ndugu aliendelea kuweka kinyongo. Lakini, Mark aliendelea kutii amri ya Yesu ya kupenda ndugu yake na kumusamehe. (Soma Wakolosai 3:13, 14.) Hata kama tunajikaza kufanya amani na wengine lakini wanakataa, upendo wa kweli wa Kikristo utatusaidia tuendelee kuwasamehe na kusali ili mambo ikuwe muzuri.​—Mt. 18:21, 22; Gal. 6:9.

Picha: Dada mumoja anajaribu tena na tena kuonyesha upendo rafiki fulani mwenye amekwaza. 1. Dada mwenye alikwazika anakataa kujibu ku telefone wakati rafiki yake anamuita. 2. Dada mwenye alikwazika anakataa zawadi yenye rafiki yake anamupatia. 3. Dada mwenye alikwazika anasikiliza wakati rafiki yake anamuhakikishia kama anamupenda.

Inaweza kuomba tujaribu njia mbalimbali ili kufanya amani (Ona fungu la 7-8)c

7. (a) Yesu alituomba tufanye nini? (b) Dada mumoja alipambana na hali gani ya nguvu?

7 Yesu alituomba tuendelee kutendea wengine namna tunapenda watutendee. Alisema tena kama hatupaswe tu kupenda wale wenye wanatupenda. (Lu. 6:31-33) Hata kama haiko kawaida, utafanya nini kama mutu fulani mu kutaniko anakuepuka na anakataa kukusalimia? Jambo hilo lilimufikia Lara. Anasema hivi: “Dada mumoja alikuwa ananiepuka, na sikujua ni juu ya nini. Nilijisikia mubaya sana na sikupenda tena kuenda ku mikutano.” Kwanza, Lara aliwaza hivi: ‘Haiko kosa langu. Na wengine pia mu kutaniko wanajua kama dada huyu anakuwaka na tabia ya mubaya.’

8. Lara alifanya nini ili kufanya amani, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?

8 Lara alifanya mambo fulani ili kufanya amani. Alisali kwa Yehova na akaamua kuzungumuza na ule dada. Walizungumuzia tatizo lao, wakakumbatiana, na kufanya amani. Ilionekana kama tatizo lao lilikuwa limemalizika. Lara anaeleza hivi: “Lakini kisha wakati fulani, ule dada alinitendea sawa vile alinitendeaka mbele. Nilivunjika moyo sana.” Kwanza, Lara aliwaza kama angekuwa na furaha ikiwa tu ule dada angebadilisha tabia yake. Lakini kisha wakati fulani, Lara alielewa kama jambo la muzuri zaidi lenye alipaswa kufanya ni kuendelea kumutendea ule dada kwa upendo na ‘kumusamehe kwa kupenda.’ (Efe. 4:32–5:2) Lara alikumbuka kama upendo wa kweli wa Kikristo “hauweke hesabu ya ubaya. Unafunika mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote.” (1 Ko. 13:5, 7) Lara alipata tena amani ya akili. Kisha wakati fulani, ule dada alianza tena kumuchangamukia. Wakati unaendelea kufanya amani na ndugu na dada zako na kuendelea kuwapenda, unaweza kuwa hakika kama ‘Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja na wewe.’​—2 Ko. 13:11.

USIKUWE NA UBAGUZI

9. Kulingana na Matendo 10:34, 35, juu ya nini hatupaswe kuwa na ubaguzi?

9 Yehova hana ubaguzi. (Soma Matendo 10:34, 35.) Wakati tunaepuka ubaguzi, tunaonyesha kama tuko watoto wake. Tunatii amri ya kupenda jirani yetu kama sisi wenyewe, na tunasaidia familia yetu ya kiroho iendelee kuwa na amani.​—Ro. 12:9, 10; Yak. 2:8, 9.

10-11. Dada mumoja alifanya nini ili asiendelee kuwa na mawazo ya mubaya?

10 Inaweza kuwa nguvu kwa watu fulani kuepuka ubaguzi. Kwa mufano, fikiria jambo lenye lilimupata dada mwenye kuitwa Ruth. Wakati alikuwa kijana, mutu fulani wa inchi ingine alimutendea jambo la mubaya sana. Jambo hilo lilifanya Ruth ajisikie namna gani? Anasema hivi: “Nilichukia kila kitu kuhusu ile inchi. Niliwaza kama watu wote wa ile inchi walikuwa vile, hata ndugu na dada.” Ruth alifanya nini ili asiendelee kuwa na ile mawazo ya mubaya?

11 Ruth alitambua kama alipaswa kupiganisha mawazo yake ya mubaya. Alisoma mambo yenye ndugu na dada walikutana nayo na habari fulani mu Kitabu cha Mwaka chenye kuzungumuzia ile inchi. Anasema hivi: “Nilijikaza kuwa na mawazo ya muzuri juu ya watu wa ile inchi. Nilianza kutambua kama ndugu na dada wa ile inchi walikuwa wanamutumikia Yehova kwa bidii. Nilifikia kuelewa waziwazi kama wako pia katika familia yetu ya ndugu na dada ya mu dunia yote.” Polepole, Ruth alielewa kama alipaswa kuwaonyesha upendo. Anaeleza hivi: “Kila mara wakati nilikutana na ndugu na dada wa ile inchi, nilijikaza sana kuwachangamukia. Nilizungumuza nao na nilifikia kuwajua muzuri zaidi.” Matokeo ilikuwa nini? Ruth anasema hivi: “Kisha wakati fulani, sikukuwa tena na mawazo ya mubaya.”

Ku Jumba la Ufalme, bwana wawili na bibi zao wanacheka wakati wanaangalia ku telefone. Nyuma yao, ndugu vijana watatu wanazungumuza na kufurahi. Ndugu mwenye kuzeeka anaonekana kuwa na huzuni kwa sababu hakuna kikundi chenye kinamuita ili kuzungumuza naye.

Kama ‘tunapenda [sana] ushirika muzima wa ndugu,’ tutaepuka kuwa na ubaguzi (Ona fungu la 12-13)d

12. Dada mumoja mwenye kuitwa Sarah alikuwa na tatizo gani?

12 Watu fulani wanaweza kuwa na ubaguzi bila hata kujua. Kwa mufano, Sarah alikuwa anawaza kama hana ubaguzi kwa sababu hakukuwa anahukumu watu kwa kuangalia rangi yao ya ngozi, utajiri wao, ao madaraka yenye walikuwa nayo mu tengenezo. Lakini anasema hivi: “Nilianza kutambua kama nilikuwa kabisa na ubaguzi.” Katika njia gani? Sarah alizaliwa mu familia ya watu wenye walisoma sana na alipenda kufanya urafiki na watu wenye walisoma sana. Siku moja aliambia hata rafiki yake hivi: “Ninafanyaka urafiki na ndugu na dada wenye walisoma sana. Ninaepuka wale wenye hawakusoma sana.” Ni wazi kwamba, Sarah alipaswa kubadilisha mawazo yake. Namna gani?

13. Namna Sarah alibadilisha mawazo yake inaweza kutufundisha nini?

13 Mwangalizi mumoja wa muzunguko alimusaidia Sarah achunguze mawazo yake. Sarah anaeleza hivi: “Alinipongeza juu ya utumishi wangu wa uaminifu, maelezo yangu ya muzuri, na juu ya ujuzi wangu wa Maandiko. Kisha alieleza kama kadiri ujuzi wetu unakomaa, tunapaswa pia kukomalisha sifa za Kikristo, kama vile unyenyekevu, kiasi, na rehema.” Sarah alitumikisha mashauri ya mwangalizi wa muzunguko. Anasema hivi: “Nilielewa kama jambo la maana zaidi ni kutendea wengine kwa fazili na upendo.” Kwa hiyo, alibadilisha mawazo yenye alikuwa nayo juu ya ndugu na dada zake. Anasema hivi: “Nilijikaza kuelewa ni sifa gani zenye wako nazo zenye zinafanya Yehova awaone kuwa wa maana sana.” Halafu sisi? Hatupendi hata kidogo kujiona kuwa wazuri zaidi kupita wengine juu tulisoma sana! Kama ‘tunapenda [sana] ushirika muzima wa ndugu,’ tutaepuka kuwa na ubaguzi.​—1 Pe. 2:17.

UKUWE MUKARIBISHAJI-WAGENI

14. Kulingana na Waebrania 13:16, Yehova anajisikia namna gani wakati tunaonyesha wengine ukaribishaji-wageni?

14 Yehova anafurahi wakati tunaonyesha ukaribishaji-wageni. (Soma Waebrania 13:16.) Anaona ukaribishaji-wageni kuwa sehemu ya ibada yetu, zaidi sana wakati tunasaidia wenye kuwa na lazima ya musaada. (Yak. 1:27; 2:14-17) Njo maana, Maandiko inatutia moyo ‘tufuate njia ya ukaribishaji-wageni.’ (Ro. 12:13) Wakati tunaonyesha wengine ukaribishaji-wageni, tunaonyesha kama tunawahangaikia kabisa, tunawapenda, na tunataka kuwa marafiki wao. Yehova anafurahi wakati tunapatia wengine ikuwe chakula mingi ao kidogo, kinywaji, ao wakati tunapitisha wakati pamoja nao na kuwahangaikia kwa upendo. (1 Pe. 4:8-10) Lakini, kuko mambo fulani yenye inaweza kutuzuia kuonyesha ukaribishaji-wageni.

Dada mumoja mu nyumba yake, anaonyesha chumba chake cha wageni bwana mumoja na bibi yake wenye wako na vyombo vya ujenzi.

“Zamani, nilikuwa ninasita kuonyesha ukaribishaji-wageni, lakini nilibadilisha mawazo yangu na nimepata furaha mingi” (Ona fungu la 16)e

15-16. (a) Juu ya nini watu fulani wanaweza kusita kuonyesha ukaribishaji-wageni? (b) Edit alifanya nini ili akuwe tayari kuonyesha ukaribishaji-wageni?

15 Tunaweza kusita kuonyesha ukaribishaji-wageni kwa sababu ya hali zetu. Fikiria mufano wa mujane mumoja mwenye kuitwa Edit. Mbele akuwe Shahidi, hakukuwa anapenda sana kuwa pamoja na watu wengine. Edit aliwaza kama wengine njo walikuwa na uwezo wa kuonyesha ukaribishaji-wageni.

16 Kisha kuwa Shahidi wa Yehova, Edit alibadilisha mawazo yake. Alikamata hatua fulani ili kuonyesha ukaribishaji-wageni. Anaeleza hivi: “Wakati Jumba letu la Ufalme lilikuwa linajengwa, muzee mumoja aliniambia kama ndugu mumoja na bibi yake walikuwa wanakuja kusaidia ku kazi ya ujenzi, na aliniuliza kama ninaweza kuwapangisha kwa majuma mbili. Nilikumbuka namna Yehova alibariki mujane wa Sarefati.” (1 Fa. 17:12-16) Edit alikubali kuwapangisha. Alipata baraka? Anaeleza hivi: “Nilifurahi sana, kwa sababu hawakubakia kwangu majuma mbili tu, lakini miezi mbili. Wakati huo, tulifanya urafiki wetu ukuwe nguvu sana.” Edit amebarikiwa pia kwa kupata marafiki wa sana mu kutaniko. Sasa iko painia na anafurahia kualika kwake wale wenye anahubiri nao ili kuwapatia chakula kidogo na kinywaji. Anasema hivi: “Kutoa kunanifanya nijisikie muzuri! Na kwa kweli, wakati ninatoa, ninapata baraka mingi.”​—Ebr. 13:1, 2.

17. Luke na bibi yake walifikia kutambua nini?

17 Pengine tayari tuko tunaonyesha ukaribishaji-wageni, lakini tunaweza kufanya zaidi? Kwa mufano, Luke na bibi yake wako wakaribishaji-wageni. Walikuwa wanazoea kualika ku nyumba yao wazazi wao, watu wa jamaa yao, marafiki wao wa sana, na mwangalizi wa muzunguko na bibi yake. Lakini, Luke anasema hivi: “Tulitambua kama tulikuwa tunaalika tu wale wenye tulikuwa nao uhusiano wa karibu.” Luke na bibi yake walifanya nini ili waonyeshe zaidi ukaribishaji-wageni?

18. Luke na bibi yake walifanya nini ili kuonyesha zaidi ukaribishaji-wageni?

18 Luke na bibi yake walibadilisha mawazo yao kisha kufikiria maneno hii ya Yesu: “Kama munapenda wale wenye wanawapenda ninyi, muko na zawabu gani?” (Mt. 5:45-47) Walitambua kama walipaswa kumuiga Yehova, mwenye kuonyesha watu wote ukarimu. Kwa hiyo, waliamua kualika ndugu na dada wenye walikuwa hawajaalikaka. Luke anasema hivi: “Sasa, sisi wote tunafurahia sana wakati huo wenye tunapitisha pamoja. Kila mutu anajisikia kuwa mwenye kutiwa moyo na mwenye kujengwa.”

19. Namna gani tunaonyesha kama tuko wanafunzi wa Yesu, na unaazimia kufanya nini?

19 Tumechunguza namna kupendana sana kunaweza kutusaidia tukuwe wenye kufanya amani, tusikuwe na ubaguzi, na tukuwe wakaribishaji-wageni. Tunapaswa kuachana na mawazo yoyote ya mubaya na kupenda sana ndugu na dada zetu kutoka katika moyo. Kama tunafanya vile, tutakuwa na furaha na tutaonyesha kama tuko kabisa wanafunzi wa Yesu.​—Yoh. 13:17, 35.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUONYESHA KAMA TUNAPENDANA SANA KWA . . .

  • kuwa wenye kufanya amani?

  • kuepuka ubaguzi?

  • kuwa wakaribishaji-wageni?

WIMBO 88 Nijulishe Njia Zako

a Yesu alisema kama upendo njo ungetambulisha Wakristo wa kweli. Kupenda ndugu na dada zetu kunatuchochea tukuwe wenye kufanya amani, tusikuwe na ubaguzi, na tukuwe wakaribishaji-wageni. Haiwezi kuwa mwepesi sikuzote kufanya vile. Habari hii itatoa mashauri fulani yenye kufaa juu ya namna tunaweza kuendelea kupendana sana kutoka katika moyo.

b Majina fulani imebadilishwa katika habari hii.

c MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja hapate matokeo ya muzuri wakati anajaribu kufanya amani kwa mara ya kwanza, lakini haachie pale. Kwa sababu anaendelea kujikaza kuonyesha upendo, anafikia kupata matokeao ya muzuri.

d MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye kuzeeka anawaza kama wengine mu kutaniko wanamuepuka.

e MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja mwenye ku mwanzo alikuwa anasita kuonyesha ukaribishaji-wageni anabadilisha mawazo yake, na kufanya vile kunamuletea furaha zaidi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine