Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 1 uku. 8-9
  • Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Sehemu ya 11
    Umusikilize Mungu
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 1 uku. 8-9

Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?

Baba yetu wa mbinguni, Yehova Mungu, iko tayari kusikiliza sala zetu zenye kutoka katika moyo, na anapenda kufanya vile. Lakini kuko mambo yenye inafanyaka asijibie sala zetu. Ni mambo gani, na tunapaswa kukumbuka nini wakati tuko tunasali? Ona mashauri fulani yenye Biblia inatutolea.

Mu kanisa, watu wako wanasoma sala mu kitabu ili kusali.

“Wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.”​—Matayo 6:7.

Yehova hapendi turudilie sala zenye tulishachunga mu akili, ao kusoma sala mu kitabu. Lakini, anapenda tusali kwake kutoka katika moyo. Wazia vile unaweza kujisikia ikiwa uko na rafiki mwenye anakuambiaka maneno ileile kila siku. Marafiki wa kweli wanazungumuzaka waziwazi na wanasemaka mambo yenye inatoka katika moyo. Wakati tunasali kwa Baba yetu wa mbinguni kwa kutumia maneno yetu wenyewe, ile inaonyesha kama tunamuona kuwa rafiki yetu.

Mwanaume mumoja anaangalia juu wakati iko anapalula ticket ya tombola.

“Wakati munaomba, hamupokee kwa sababu munaomba kwa kusudi la mubaya.”​—Yakobo 4:3.

Tunaelewa kama Mungu hawezi kujibia sala zetu ikiwa tunamuomba mambo yenye hapendi tufanye ao tukuwe nayo. Kwa mufano, Yehova anaweza kujibia sala ya mutu mwenye kucheza muchezo wa kupata feza? Anatuambia waziwazi kama hatupaswe kuwa na pupa na kuamini mambo ya bahati. (Isaya 65:11; Luka 12:15) Kwa kweli hatupaswe kutazamia kama Mungu atajibia sala za vile! Ili Mungu ajibie sala zetu, tunapaswa kuhakikisha kama sala zetu zinapatana na mambo yenye anatuambia mu Biblia.

Kiongozi mumoja wa dini iko anasali kwa ajili ya kikundi cha maaskari.

“Mwenye anakataa kusikiliza sheria​—hata sala yake inachukiza.”​—Mezali 28:9.

Zamani, Mungu hakujibia sala za wale wenye hawakutii sheria zake za haki. (Isaya 1:15, 16) Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Kama tunapenda Mungu ajibie sala zetu, tunapaswa kujikaza kuishi kulingana na sheria zake. Tuseme nini kama tulifanyaka mambo ya mubaya zamani? Ile inamaanisha kama Yehova hawezi hata kidogo kusikiliza sala zetu? Jibu ni hapana! Kwa upendo Mungu atatusamehe kama tunabadilisha maisha yetu na kujikaza sana ili kumufurahisha.​—Matendo 3:19.

“Mutu yeyote mwenye anamukaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye iko na kwamba yeye anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.”​—Waebrania 11:6.

Mwanamuke mumoja iko anasoma Biblia.

Sala haiko tu dawa ya kutusaidia tujisikie muzuri wakati tuko na mahangaiko. Inatupatia nafasi ya kuonyesha imani yetu na ni sehemu ya ibada yetu kwa Mungu. Mwanafunzi Yakobo anasema kama ikiwa ‘hatuendelee kuomba kwa imani, tusitazamie kupokea kitu chochote kutoka kwa Yehova.’ (Yakobo 1:6, 7) Ili kuwa na imani katika Mungu, inaomba wakati na kujikaza ili tufikie kumujua kwa kujifunza Biblia. Kufanya vile kutatusaidia tujue mapenzi yake na kutatusaidia kusali kwa imani.

USIVUNJIKE MOYO!

Hata kama Mungu hajibiake sala zote, anajibiaka sala zenye kutoka katika moyo za mamilioni ya watu. Biblia inaonyesha mambo yenye unaweza kufanya ili sala zako zimupendeze Mungu. Habari yenye kufuata itafasiria ile mambo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine