Unaweza Kuamua Namna Maisha Yako Itakuwa Wakati Wenye Kuja
Kumepita miaka 3 500 hivi, tangu wakati Yehova Mungu aliambia hivi wale wenye walikuwa wanamuabudu kuhusu nini wangefanya juu wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Aliwaambia hivi: “Nimeweka uzima na kifo mbele yako, baraka na laana; na unapaswa kuchagua uzima ili uendelee kuishi, wewe na wazao wako.”—Kumbukumbu la Torati 30:19.
Ili wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja, wale watu walipaswa kukamata uamuzi wa muzuri. Na siye leo ni vile. Biblia inatufasiria namna tunaweza kuchagua kuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja: “Kwa kumupenda Yehova Mungu wako, kwa kusikiliza sauti yake.”—Kumbukumbu la Torati 30:20.
NAMNA GANI TUNAWEZA KUMUPENDA YEHOVA NA KUSIKILIZA SAUTI YAKE?
UJIFUNZE KUPITIA BIBLIA: Juu umupende Yehova, unapaswa kwanza kujifunza ili kumujua kupitia Biblia. Wakati unafanya vile, utavumbua kama Yehova ni Mungu mwenye upendo na mwenye anakutakia tu mambo ya muzuri. Anakuomba usali kwake ‘kwa sababu yeye anakuhangaikia weye.’ (1 Petro 5:7) Biblia inaahidi kama, ikiwa unafanya yako yote ili kumukaribia, ‘naye atakukaribia.’—Yakobo 4:8.
TUMIKISHA MAMBO YENYE UNAJIFUNZA: Kumusikiliza Mungu kunamaanisha kufuata muongozo wake wa hekima wenye kuwa mu Biblia. Wakati unafanya vile, “njia yako itakuwa na matokeo ya muzuri na utatenda kwa hekima.”—Yoshua 1:8.