Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w21 Mwezi wa 1 uku. 2-7
  • Endelea Kuwa Mutulivu na Umutumainie Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Endelea Kuwa Mutulivu na Umutumainie Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NINI NJO INAWEZA KUFANYA TUKUWE NA MAHANGAIKO?
  • MAMBO SITA YENYE ITATUSAIDIA TUENDELEE KUTULIA
  • Umutupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • “Usihangaike, kwa Maana Niko Mungu Wako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Mtegemee Yehova Kadiri Mwisho Unavyokaribia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mahangaiko
    Amuka!—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
w21 Mwezi wa 1 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 1

Endelea Kuwa Mutulivu na Umutumainie Yehova

ANDIKO LETU LA MWAKA WA 2021: “Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”​—ISA. 30:15.

WIMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

KIFUPI CHA HABARIa

1. Watumishi fulani wa Yehova wanaweza kuuliza ulizo gani?

SISI wote tunapendaka kuwa na maisha yenye kutulia na yenye amani. Hakuna mwenye anapendaka kuwa na mahangaiko. Lakini, wakati fulani tunakuwaka na mahangaiko. Njo maana watumishi fulani wa Yehova wanaweza kuuliza ulizo sawa lenye Mufalme Daudi aliulizaka Yehova: “Nitahangaika kwa wasiwasi mupaka wakati gani, nikiwa na huzuni katika moyo wangu kila siku?”​—Zb. 13:2.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Hata kama sisi wote tunakuwaka na mahangaiko wakati fulani, kuko mambo yenye tunaweza kufanya ili tusihangaike kupita kiasi. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo fulani yenye inaweza kufanya tukuwe na mahangaiko. Kisha, tutazungumuzia mambo sita yenye tunaweza kufanya ili tuendelee kuwa watulivu wakati tuko na magumu.

NINI NJO INAWEZA KUFANYA TUKUWE NA MAHANGAIKO?

3. Ni mambo gani yenye inaweza kutuletea mahangaiko, na je, tunaweza kuizuia?

3 Kuko mambo mingi yenye inaweza kutuletea mahangaiko, na kati ya ile mambo, kuko mambo fulani yenye hatuwezi kuzuia. Kwa mufano, hatuwezi kuzuia watu kupandisha bei ya chakula, ya manguo, ao ya kulipia nyumba. Pia, hatuwezi kuamua ni mara ngapi wafanyakazi wenzetu ao wanafunzi wenzetu watajaribu kutushawishi ili tutende bila unyoofu ao tufanye uasherati. Na tena, hatuwezi kuzuia watu kutenda mambo ya mubaya mu eneo letu. Tunapambana na ile magumu juu tunaishi mu ulimwengu mwenye watu wengi hawafuate kanuni za Biblia. Shetani, mungu wa ulimwengu huu, anajua kama watu fulani wataacha “mahangaiko ya mupangilio huu wa mambo” iwazuie kumutumikia Yehova. (Mt. 13:22; 1 Yo. 5:19) Njo maana hatushangae kuona mu dunia munajaa mambo yenye inafanya watu wakuwe na mahangaiko mingi!

4. Kuhangaika kupita kiasi kunaweza kuwa na matokeo gani?

4 Kuhangaika kupita kiasi kunaweza kufanya tukose amani ya akili. Kwa mufano, tunaweza kuwa na wasiwasi kwa sababu tunawaza kama hatutakuwa na feza za kutusaidia kutimiza mahitaji yetu, ao kwa sababu tunawaza kama tutagonjwa na ile itafanya tushindwe kufanya kazi ao hata tupoteze kazi yetu. Pia, tunaweza kuhangaika kwa sababu tunawaza kama hatutaendelea kuwa waaminifu wakati tutashawishiwa kufanya jambo fulani lenye halimufurahishe Mungu. Karibuni, Shetani atachochea wale wenye kumuunga mukono washambulie watu wa Mungu. Kwa hiyo, tunaweza kuwa na wasiwasi kuhusu namna tutatenda wakati wale watu watatushambulia. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ni mubaya kuhangaika juu ya ile mambo?’

5. Yesu alimaanisha nini wakati alisema: ‘Muache kuhangaika’?

5 Tunajua kama Yesu aliambia wafuasi wake hivi: ‘Muache kuhangaika.’ (Mt. 6:25) Yesu alimaanisha kama hatupaswe kuhangaika hata kidogo? Hapana! Kumbuka kama, zamani, watu fulani wenye walimutumikia Yehova kwa uaminifu walikuwa na mahangaiko. Hata vile, Yehova aliendelea kuwakubali.b (1 Fa. 19:4; Zb. 6:3) Kwa hiyo, wakati Yesu alisema ile maneno, alipenda njo kututia moyo. Hakupenda tuhangaikie sana vitu vya kimwili mupaka tusahau kama kumutumikia Yehova njo jambo la maana zaidi mu maisha yetu. Sasa, tunaweza kufanya nini ili tuepuke kuhangaika kupita kiasi?​—Ona kisanduku chenye kichwa “Mambo ya Kufanya.”

MAMBO SITA YENYE ITATUSAIDIA TUENDELEE KUTULIA

Picha: Dada anasali mara mingi. 1. Mbele akule chakula. 2. Wakati anakaa ku kiti mu bustani. 3. Mbele ajifunze Biblia.

Ona fungu la 6c

6. Kulingana na Wafilipi 4:6, 7, nini njo inaweza kutusaidia tutulie?

6 (1) Usali kila wakati. Wakati uko na mahangaiko, unaweza kusali kwa Yehova ili kumuomba akusaidie. (1 Pe. 5:7) Yehova anaweza kujibia sala zako kwa kukupatia “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote [wa mwanadamu].” (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Anaweza kukupatia roho yake takatifu ili ikusaidie utulie.​—Gal. 5:22.

7. Unapaswa kukumbuka nini wakati uko unasali?

7 Wakati uko unasali kwa Yehova, umufungulie moyo wako. Ukuwe wazi. Umuambie tatizo ni nini, na umufasirie namna uko unajisikia. Kama kuko mambo yenye unaweza kufanya juu ya kumaliza tatizo lako, umuombe hekima ili ukamate maamuzi ya muzuri na umuombe nguvu ya kutimiza ile maamuzi. Kama hakuna jambo lenye unaweza kufanya, umuombe Yehova akusaidie ili usihangaike kupita kiasi. Wakati unamuambia Yehova mambo waziwazi, itakuwa mwepesi kuona namna anajibia sala zako. Kama hajibie sala yako palepale, usiache kusali. Zaidi ya kumuambia mambo waziwazi, Yehova anapenda pia uendelee kusali.​—Lu. 11:8-10.

8. Wakati tuko tunasali, hatupaswe kusahau nini?

8 Wakati uko unamuelezea Yehova mahangaiko yako katika sala, usisahau pia kumushukuru. Hata wakati wa magumu, ni jambo la maana tusikuwe tunasahau mambo ya muzuri yenye tuko nayo. Ikiwa wakati fulani unashindwa kumuambia Yehova namna uko unajisikia kabisa, ukumbuke kama anajibiaka sala, hata kama maneno kidogo yenye mutu anaweza tu kusema ni ‘Tafazali unisaidie!’​—2 Ny. 18:31; Ro. 8:26.

Uleule dada anatumia tablete ili kujifunza Biblia wakati anapumuzika ili kula chakula cha muchana ku kazi.

Ona fungu la 9d

9. Tunapaswa kufanya nini ili kupata usalama wa kweli?

9 (2) Utegemee hekima ya Yehova, hapana yako mwenyewe. Mu karne ya 8 M.K.Y., watu wa Yuda waliogopa kushambuliwa na Waashuru. Kwa hiyo, waliomba Wamisri wawasaidie. (Isa. 30:1, 2) Yehova aliwaonya kama, kutegemea Wamisri kungeleta matokeo ya mubaya. (Isa. 30:7, 12, 13) Kupitia Isaya, Yehova aliwaambia mambo yenye walipaswa kufanya ili wapate usalama wa kweli. Alisema hivi: “Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini” katika Yehova.​—Isa. 30:15b.

10. Ni mu hali gani fulani tunaweza kuonyesha kama tunamutumainia Yehova?

10 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamutumainia Yehova? Fikiria hali fulani: Unapata kazi yenye itakusaidia upate feza mingi. Lakini ile kazi itakukamata wakati mingi na itavuruga programu yako ya kiroho. Ao pengine mufanyakazi mwenzako mwenye haiko Shahidi wa Yehova anapenda uanzishe naye urafiki wa kimapenzi. Ao mutu wa familia yako anakuambia kama atakukataa ikiwa unaendelea kumutumikia Yehova. Mu kila hali, itaomba uamue utafanya nini, lakini Yehova atakupatia muongozo wenye uko nao lazima. (Mt. 6:33; 10:37; 1 Ko. 7:39) Sasa ulizo ni: Utamutumainia Yehova na kufuata muongozo wake?

Ule Biblia anasoma Biblia na kichapo.

Ona fungu la 11e

11. Ni habari gani za Biblia zenye zinaweza kutusaidia tuendelee kuwa watulivu wakati wengine wanatupinga?

11 (3) Ujifunze kupitia mifano ya muzuri na ya mubaya. Mu Biblia muko habari za mingi zenye zinaonyesha faida ya kuendelea kuwa watulivu na kumutumainia Yehova. Wakati uko unajifunza zile habari, ujikaze kuona mambo yenye ilisaidia watumishi wa Yehova waendelee kuwa watulivu wakati wengine waliwapinga. Kwa mufano, wakati tribinali kubwa ya Wayahudi iliamuru mitume waache kuhubiri, hawakuogopa. Lakini, walisema hivi kwa uhodari: “Tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.” (Mdo. 5:29) Hata kisha kupigwa, mitume hawakutetemeka. Juu ya nini? Juu, walijua kama Yehova alikuwa upande wao na kama alifurahia uaminifu wao. Kwa hiyo, waliendelea kuhubiri habari njema. (Mdo. 5:40-42) Vilevile, wakati mwanafunzi Stefano alikuwa karibu kuuawa, aliendelea kuwa mutulivu hivi kwamba uso wake ulionekana “kama uso wa malaika.” (Mdo. 6:12-15) Juu ya nini? Juu, alikuwa hakika kama Yehova alimukubali.

12. Kulingana na 1 Petro 3:14 na 4:14, juu ya nini tunaweza kuwa na furaha wakati tunateswa?

12 Mitume walijionea waziwazi kama Yehova alikuwa anawategemeza. Alikuwa amewapatia uwezo wa kufanya miujiza. (Mdo. 5:12-16; 6:8) Lakini leo, sisi hatuna uwezo wa kufanya miujiza. Hata vile, Yehova anatuhakikishia kupitia Neno lake kama, ikiwa tunateseka kwa sababu ya kufanya mambo ya muzuri, anafurahia uaminifu wetu na roho yake iko inatutegemeza. (Soma 1 Petro 3:14; 4:14.) Kwa hiyo, kuliko kukaza akili juu ya namna pengine tutatenda ikiwa tunateswa mu siku zenye kuja, tunapaswa kukaza akili juu ya mambo yenye tunaweza kufanya leo ili tuendelee kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kututegemeza na kutukomboa. Kama mitume, sisi pia tunapaswa kutumainia ahadi hii ya Yesu: “Nitawapatia ninyi maneno na hekima yenye wapinzani wenu wote pamoja hawataweza kushindana nayo ao kupinga.” Yesu anatuhakikishia hivi: “Kupitia uvumilivu wenu mutaokoa uzima wenu.” (Lu. 21:12-19) Pia, usisahau kama Yehova anakumbuka kila kitu kuhusu watumishi wake waaminifu wenye wamekufa. Kwa hiyo, anaweza kuwafufua.

13. Kujifunza mifano ya watu wenye hawakuendelea kuwa watulivu na wenye hawakumutumainia Yehova kunaweza kutusaidia namna gani?

13 Tunaweza pia kujifunza mambo fulani wakati tunafikiria mifano ya wale wenye hawakuendelea kuwa watulivu na wenye hawakumutumainia Yehova. Kujifunza ile mifano ya mubaya kutatusaidia tusirudilie makosa yenye walifanya. Kwa mufano, ku mwanzo wa utawala wake, Mufalme Asa wa Yuda alimutegemea Yehova wakati jeshi kubwa lilikuja kumushambulia, na Yehova alimusaidia kupata ushindi. (2 Ny. 14:9-12) Kisha wakati fulani, Mufalme Baasha wa Israeli alikuja na jeshi la kidogo ili kumushambulia. Lakini ile wakati, Asa hakumutegemea tena Yehova. Kuliko kufanya vile, alilipa Wasiria ili wamusaidie. (2 Ny. 16:1-3) Na wakati alikaribia kufa, aligonjwa sana, lakini hakumutegemea Yehova.​—2 Ny. 16:12.

14. Makosa ya Asa inaweza kutufundisha nini?

14 Ku mwanzo, Asa alimuomba Yehova musaada wakati alikuwa na magumu. Lakini kisha wakati fulani, aliacha kumutegemea Yehova. Alijaribu kutatua magumu yake yeye mwenyewe. Uamuzi wa Asa wa kuomba Wasiria wamusaidie ulionekana kuwa wa muzuri ku mwanzo. Lakini matokeo ya muzuri yenye walipata ilikuwa ya wakati kidogo tu. Yehova alituma nabii Hanani aambie Asa hivi: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Siria na haukumutegemea Yehova Mungu wako, jeshi la mufalme wa Siria limeponyoka kutoka katika mukono wako.” (2 Ny. 16:7) Sisi pia tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiwaze kama tunaweza kutatua sisi wenyewe magumu yetu bila kutafuta muongozo wenye Yehova anatutolea mu Neno lake. Hata wakati inaomba tukamate uamuzi wa haraka, tunapaswa kutulia na kumutegemea Yehova. Tukifanya vile, atatusaidia tukamate uamuzi wa muzuri.

Ule dada anabandika ku frigo karatasi yenye iko na maneno ya Isaya 30:15.

Ona fungu la 15f

15. Wakati tuko tunasoma Biblia, ni muzuri tujikaze kufanya nini?

15 (4) Uweke maandiko ya Biblia mu akili. Wakati uko unasoma Biblia, kama unaona maandiko yenye inaonyesha faida ya kuendelea kuwa mutulivu na kumutumainia Yehova, ujikaze kuiweka mu akili. Inaweza kuwa muzuri uisome kwa sauti ao uiandike fasi fulani ili uirudilie mara kwa mara. Yehova aliambia Yoshua akuwe anasoma kitabu cha Sheria kwa ukawaida kwa sauti ya chini. Kufanya vile kungemusaidia atende kwa hekima. Pia, mambo yenye angesoma ingemusaidia asiogope wakati alikuwa anaongoza watu wa Mungu. (Yos. 1:8, 9) Mu Biblia muko maneno mingi yenye inaweza kutusaidia tutulie mu hali zenye kwa kawaida zinaweza kutufanya tukuwe na wasiwasi ao tuogope.​—Zb. 27:1-3; Mez. 3:25, 26.

Ule dada iko anazungumuza na dada mwingine mu mahubiri.

Ona fungu la 16g

16. Namna gani Yehova anatumia ndugu na dada ili kutusaidia tuendelee kuwa watulivu na kumutumainia?

16 (5) Upitishe wakati na watu wa Mungu. Yehova anatumia ndugu na dada zetu ili kutusaidia tuendelee kuwa watulivu na kumutumainia. Wakati tuko ku mikutano, hotuba, maelezo ya ndugu na dada, na mazungumuzo yenye kutia moyo yenye tunafanya nao inatusaidiaka sana. (Ebr. 10:24, 25) Pia, wakati tunaelezea marafiki wetu wa karibu mu kutaniko namna tunajisikia, wanaweza kututia moyo sana. “Neno la muzuri” lenye rafiki yetu anatuambia linaweza kutusaidia tupunguze mahangaiko.​—Mez. 12:25.

Ule dada iko anafikiri juu ya baraka zenye Ufalme wa Mungu utaleta.

Ona fungu la 17h

17. Kulingana na Waebrania 6:19, namna gani tumaini letu linaweza kutusaidia tutulie wakati tunapambana na magumu?

17 (6) Uendelee kutia nguvu tumaini lako. Tumaini letu liko “kama nanga ya nafsi.” Linatusaidia tuendelee kutulia wakati tunapambana na magumu ao mahangaiko. (Soma Waebrania 6:19.) Ufikiri sana juu ya maisha ya muzuri yenye Yehova anatuahidi. Wakati ile ahadi itatimia, hakutakuwa mutu mwenye atakuwa na mahangaiko. (Isa. 65:17) Ujiwazie mu ulimwengu mupya wenye amani, kwenye mambo ya mubaya haitakuwa tena. (Mik. 4:4) Jambo lingine lenye unaweza kufanya ili kutia nguvu tumaini lako ni kuelezea wengine juu ya ulimwengu mupya. Ujitoe sana mu kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Ukifanya vile, unaweza “kuwa na uhakika kamili wa tumaini mupaka mwisho.”​—Ebr. 6:11.

“Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”​—ISA. 30:15

Picha: Mambo sita yenye inasaidia dada mumoja aendelee kutulia. Ile mambo inazungumuziwa mu hii habari.

MAMBO YA KUFANYA

  1. 1. Usali kila wakati

  2. 2. Utegemee hekima ya Yehova

  3. 3. Ujifunze kupitia mifano ya zamani

  4. 4. Uweke maandiko ya Biblia mu akili

  5. 5. Upitishe wakati na watu wa Mungu

  6. 6. Uendelee kutia nguvu tumaini lako

18. Tunaweza kupata magumu ya namna gani mu siku zenye kuja, na tunaweza kufanya nini ili kupambana nayo?

18 Kadiri mwisho wa ulimwengu huu unakaribia, tutapata magumu yenye inaweza kutuletea mahangaiko. Andiko letu la mwaka wa 2021 linaweza kutusaidia kupambana na ile magumu na kuendelea kuwa watulivu, hapana kwa nguvu yetu wenyewe, lakini kwa kumutumainia Yehova. Mu hii mwaka, tuendelee basi kuonyesha kupitia matendo yetu kama tunaamini ahadi hii ya Yehova: “Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”​—Isa. 30:15.

UTAJIBIA NAMNA GANI?

  • Juu ya nini haiko mubaya kuwa na mahangaiko kwa kiasi fulani?

  • Ni mambo gani sita yenye tunaweza kufanya ili tuendelee kuwa watulivu?

  • Juu ya nini andiko letu la mwaka wa 2021 linafaa kabisa?

WIMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Letu

a Andiko letu la mwaka wa 2021 linakazia kama ni jambo la maana tumutumainie Yehova ili tuweze kupambana na hali zenye kuleta mahangaiko, zenye zinaweza kutokea leo na wakati wenye kuja. Mu hii habari, tutazungumuzia namna tunaweza kutumikisha shauri lenye kuwa mu andiko letu la mwaka.

b Ndugu na dada fulani waaminifu wako na tatizo lenye linafanyaka wahangaike sana ao waogope sana. Ile ni tatizo ya afya na haiko njo mahangaiko yenye Yesu alikuwa anazungumuzia.

c MAFASIRIO YA PICHA: (1) Dada anasali mara mingi kuhusu mahangaiko yake.

d MAFASIRIO YA PICHA: (2) Ku kazi, wakati anapumuzika ili kula chakula cha muchana, anasoma Neno la Mungu ili kupata hekima.

e MAFASIRIO YA PICHA: (3) Anafikiri sana juu ya mifano ya muzuri na ya mubaya yenye inapatikana mu Biblia.

f MAFASIRIO YA PICHA: (4) Anabandika ku frigo maneno yenye kutia moyo ya andiko lenye anapenda kuweka mu akili.

g MAFASIRIO YA PICHA: (5) Anafurahia kupitisha wakati na rafiki yake mu mahubiri.

h MAFASIRIO YA PICHA: (6) Anatia nguvu tumaini lake kwa kufikiri juu ya ulimwengu mupya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine