HABARI JUU YA MAISHA YA WATU
Yehova ‘Amenyoosha [Njia] Yangu’
SIKU moja, ndugu fulani kijana aliniuliza hivi: “Ni andiko gani njo unapendaka sana?” Mara moja, nilimujibia, “Mezali 3, mustari wa 5 na 6, yenye inasema: ‘Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito [ao njia] yako.’” Kwa kweli, Yehova amenyoosha kabisa njia yangu. Namna gani?
WAZAZI WANGU WALINISAIDIA NIPATE NJIA YA MUZURI
Wazazi wangu walijifunza kweli mu miaka ya 1920 mbele waoane. Nilizaliwa Uingereza ku mwanzo wa mwaka wa 1939. Wakati nilikuwa mutoto, nilikuwa ninasindikiza wazazi wangu ku mikutano ya Kikristo na kisha nilijiandikisha ku Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Mupaka leo, ningali ninakumbuka kipindi yangu ya kwanza. Nilisimama ku sanduku juu nifike muzuri ku kinara cha musemaji. Ile wakati, nilikuwa na miaka sita, na nilikuwa na wasiwasi wakati nilikuwa ninaangalia watu wakubwa wenye walikuwa wananisikiliza.
Niko ninahubiri na wazazi wangu mu barabara
Baba yangu alikuwa ananiandikia maneno ya mwepesi ku karatasi yenye ningeonyesha watu mu mahubiri. Nilikuwa na miaka munane wakati nilihubiri nyumba kwa nyumba peke yangu kwa mara ya kwanza. Nilifurahi sana wakati mwenye nyumba alisoma maneno ya karatasi yangu na akakubali mara moja kitabu “Que Dieu soit reconnu pour vrai”! Nilikimbia kwenye baba yangu alikuwa na nikamuambia. Mahubiri na mikutano iliniletea furaha na ilinisaidia nikuwe na hamu ya kumutumikia Yehova mu utumishi wa wakati wote.
Nilianza kupenda kweli zaidi na zaidi kisha baba yangu kufanya mipango ili nikuwe ninapata kwa ukawaida gazeti Munara wa Mulinzi. Kisha tu kila gazeti kufika, nilikuwa ninaisoma kwa uangalifu. Nilianza kumutumainia Yehova zaidi na zaidi na ile ilifanya niamue kujitoa kwake.
Mu mwaka wa 1950, mimi na wazazi wangu tulihuzuria mukusanyiko wa kimataifa wenye kichwa “Ongezeko la Kiteokrasi” wenye ulifanywa kule New York. Programu ya Siku ya Ine tarehe 3 Mwezi 8, ilikuwa na kichwa “Siku ya Wamisionere.” Ile siku, Ndugu Carey Barber, mwenye alifikia kutumikia mu Baraza Lenye Kuongoza, alitoa hotuba ya ubatizo. Kisha kuuliza wenye watabatizwa maulizo mbili ku mwisho wa hotuba yake, nilisimama na kusema “Ndiyo!” Nilikuwa na miaka 11 lakini nilitambua kama nilikuwa nimekamata uamuzi wa maana sana. Hata vile, niliogopa kuingia mu maji kwa sababu sikukuwa ninajua kuogolea. Baba yangu mudogo alinisindikiza mupaka fasi ya kubatizia na kuniambia kama mambo yote itakuwa muzuri. Kwa kweli, ubatizo ulifanyika haraka sana na miguu yangu haikugusa hata sehemu ya chini ya maji. Ndugu walikuwa wananinyangula. Ndugu mumoja alinibatiza, na mwingine akaninyangula kutoka mu maji. Tangu ile siku ya maana, Yehova ameendelea kunyoosha njia yangu.
NILIAMUA KUMUTEGEMEA YEHOVA
Wakati nilimaliza masomo, nilipenda kuwa painia. Lakini, walimu wangu walinitia moyo nisome masomo ya juu. Nilisikiliza mawazo yao na nikaanza kusoma masomo ya juu. Lakini, kisha wakati kidogo nilitambua kama kukaza akili juu ya masomo hakungenisaidia niendelee kumutumikia Yehova kwa bidii. Kwa hiyo, niliamua kuacha masomo. Nilisali kwa Yehova juu ya uamuzi wangu na nikaandikia wakubwa wa masomo barua ili kuwafasiria kwa upole kama ningeacha masomo mwisho wa mwaka wa kwanza. Nilimutumainia Yehova kabisa, na bila kukawia nikaanza kazi ya upainia.
Mu Mwezi wa 7, 1957, nilianza kufanya kazi ya upainia mu muji wa Wellingborough. Niliomba ndugu wa ku Beteli ya Londres waniambie ndugu painia mwenye uzoefu mwenye ningejiunga naye. Walipendekeza Ndugu Bert Vaisey. Alinifundisha mambo mingi. Alikuwa muhubiri mwenye bidii na alinisaidia nikuwe na programu ya muzuri ya mahubiri. Mu kutaniko letu mulikuwa tu dada sita wenye kuzeeka, ndugu Vaisey na mimi. Kutayarisha na kushiriki ku mikutano yote kulinisaidia nimutumainie Yehova zaidi na nielezee wengine imani yangu.
Kisha kupitisha wakati mufupi mu gereza kwa sababu ya kukataa kazi ya kijeshi, nilikutana na dada mumoja painia wa pekee mwenye aliitwa Barbara. Tulioana mu mwaka wa 1959, na tulikuwa tayari kuenda fasi yoyote kwenye wangetutuma. Mugao wetu wa kwanza ulikuwa katika Lancashire, kaskazini-mangaribi mwa Uingereza. Kisha, mu Mwezi wa 1, 1961, nilialikwa ku Beteli ya Londres ili kusoma Masomo ya Huduma ya Ufalme yenye ilifanya mwezi moja. Nilishangaa sana wakati, ku mwisho wa masomo, nilipewa mugao wa kuwa mwangalizi wa muzunguko. Kwa majuma mbili, nilizoezwa na mwangalizi wa muzunguko mwenye uzoefu katika muji wa Birmingham, na Barbara aliruhusiwa kujiunga na mimi. Kisha, tulienda katika mugao wetu mu maeneo ya Lancashire na Cheshire.
INAKUWAKA TU MUZURI KUMUTEGEMEA YEHOVA
Wakati tulikuwa tumeenda kupumuzika mu Mwezi wa 8, 1962, tulipata barua kutoka ku biro ya tawi. Ndani mulikuwa fomu za Masomo ya Gileadi! Kisha kusali juu ya jambo hilo, mimi na Barbara tulijaza zile fomu na bila kukawia tukazirudisha ku biro ya tawi, sawa vile tuliombwa kufanya. Kisha miezi tano, tulienda Brooklyn, New York, ili kusoma darasa la 38 la Masomo ya Gileadi. Ile masomo ya Biblia ilikamata miezi kumi.
Ku Masomo ya Gileadi, tulijifunza mambo mingi juu ya Neno la Mungu, juu ya tengenezo lake, na juu ya familia yetu ya ndugu na dada. Tulikuwa tungali vijana; nilikuwa na miaka 24, na bibi yangu alikuwa na miaka 23. Kwa hiyo, tulijifunza mambo mingi kutoka kwa wanafunzi wengine wa mu darasa letu. Nilikuwa na pendeleo la kutumika kila siku pamoja na mwalimu wetu mumoja, Ndugu Fred Rusk. Jambo moja la maana lenye alikazia ni kuhakikisha sikuzote kama tunatoa mashauri yenye inategemea kabisa Neno la Mungu. Ndugu wengi wenye uzoefu walikuwa wanatutolea hotuba. Kati yao kulikuwa Nathan Knorr, Frederick Franz, na Karl Klein. Na tulijifunza mambo mingi kupitia mufano wa unyenyekevu wa Ndugu A. H. Macmillan, mwenye alitusaidia kuelewa namna Yehova alisaidia watu wake mu kipindi cha magumu cha kati ya mwaka wa 1914 na mwanzo wa 1919!
TUNAPEWA MUGAO MWINGINE
Ku mwisho-mwisho wa masomo, Ndugu Knorr alituambia kama tumepewa mugao wa kuenda kutumikia Burundi, katika Afrika. Tulienda haraka mu maktaba ya Beteli ili kuangalia mu Kitabu cha Mwaka hesabu ya wahubiri wenye walikuwa wanatumikia mu Burundi ile wakati. Lakini la kushangaza ni kwamba, hatukupata hesabu yoyote kuhusu ile inchi! Kwa kweli, tulikuwa tunaenda mu eneo lenye lilikuwa halijahubiriwa, katika Afrika, kontinenti yenye hatukujua muzuri kabisa. Tulikuwa na wasiwasi sana. Lakini kusali sana kulitusaidia tutulie.
Mu mugao wetu mupya, hali ya hewa, desturi, na luga, vyote vilikuwa tofauti kabisa. Tulipaswa kujifunza Kifaransa. Haikukuwa pia mwepesi kupata fasi ya kuishi. Siku mbili kisha kufika Burundi, Harry Arnott, mwenye tulisoma naye Masomo ya Gileadi alitutembelea wakati alikuwa anarudia mu mugao wake katika Zambia. Alitusaidia kupata nyumba, na ile njo ilikuwa makao yetu ya kwanza ya umisionere. Lakini, kisha wakati kidogo, wakubwa wa serikali wenye hawakujua kitu juu ya Mashahidi wa Yehova walianza kutupinga. Na wakat tu tulianza kufurahia mugao wetu, wakubwa wa serikali walitujulisha kama hatungeendelea kubakia Burundi bila kuwa na kikaratasi cha serikali chenye kinaturuhusu kufanya kazi mu ile inchi. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, tulilazimika kuondoka na kuenda mu inchi ingine. Tulienda Uganda.
Tulikuwa na wasiwasi kwa sababu tulipaswa kuenda Uganda bila kuwa na viza. Lakini, tulimutumainia Yehova. Ndugu mumoja kutoka Kanada, mwenye alikuwa anatumikia fasi kwenye kuwa lazima ya wahubiri katika Uganda alienda kuonana na mukubwa wa serikali mwenye alikuwa anashugulikia mambo ya watu wenye kuhamia mu inchi na akamufasiria hali yetu. Kwa hiyo, ule mukubwa alituambia kama tunaweza kubakia mu inchi kwa miezi fulani mupaka wakati tutapata vikaratasi vya kuturuhusu kubakia kule. Ile ilionyesha kama Yehova alikuwa anatusaidia.
Mu Uganda, hali ilikuwa tofauti na Burundi. Kazi ya kuhubiri ilikuwa inafanywa tayari, hata kama mu inchi yote mulikuwa tu Mashahidi 28. Mu mahubiri, tulipata watu wengi wenye kuzungumuza Kiingereza. Lakini, bila kukawia, tulitambua kama, ilikuwa muzuri tujifunze hata luga moja ya wenyeji ili tuweze kusaidia watu wenye kupendezwa wafanye maendeleo. Tulianza kuhubiri katika muji wa Kampala, kwenye watu wengi wanasema Luganda. Kwa hiyo, tuliamua kujifunza ile luga. Ilituomba miaka mingi ili tujue kuongea muzuri ile luga, lakini ile ilitusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri! Tulianza kuelewa muzuri zaidi mahitaji ya kiroho ya wanafunzi wetu wa Biblia. Na wao pia walitufungulia mioyo yao na kutuelezea namna walijisikia juu ya mambo yenye walikuwa wanajifunza.
SAFARI MBALIMBALI
Katika safari mbalimbali zenye tulifanya Uganda
Tulifurahia sana kusaidia watu kujifunza kweli. Na tulifurahi hata zaidi wakati tuliombwa kufanya kazi ya muzunguko mu inchi yote. Chini ya uongozi wa tawi ya Kenya, tulifanya safari mbalimbali ili kutafuta maeneo yenye ilikuwa na lazima ya mapainia wa pekee. Mara mingi watu wenye hawakukuwa hata wanajua Mashahidi wa Yehova walitukaribisha muzuri. Walifanya tujisikie muzuri na walitutayarishia hata chakula.
Kisha nilifanya safari kutoka Kampala mupaka ku bandari ya Mombasa katika inchi ya Kenya na kisha nilisafiri ili kuenda katika visiwa vya Seychelles, vyenye kuwa mu Bahari ya India. Kisha wakati fulani, kuanzia mwaka wa 1965 mupaka 1972, Barbara alikuwa ananisindikiza wakati nilikuwa ninatembelea visiwa vya Seychelles. Ile wakati, mu vile visiwa mulikuwa tu wahubiri wawili, kisha kukakuwa kikundi, na kisha kutaniko likaanzishwa. Tulitembelea pia ndugu na dada wa Eritrea, Etiopia, na Sudani.
Hali ya kisiasa katika Uganda ilibadilika haraka wakati kikundi cha maaskari kilikamata mamlaka kinguvu. Mambo ya kuogopesha yenye ilitokea mu miaka yenye ilifuata ilionyesha kama ni jambo la hekima kutii amri ya ‘kumulipa Kaisari vitu vya Kaisari.’ (Mk. 12:17) Wakati fulani, watu wa inchi zingine wenye walikuwa wanaishi mu inchi ya Uganda waliombwa wajiandikishe ku biro ya polisi yenye ilikuwa karibu na kwao. Bila kukawia, tulitii ile amri. Kisha masiku fulani, wakati nilikuwa ninatembeza gari katika Kampala, polisi walitukaribia mimi na misionere mwingine. Tuliogopa sana! Walitushitaki kama tulikuwa wapelelezi na wakatupeleka ku biro kubwa ya polisi. Kule tuliwafasiria kama tuko wamisionere, hatuko watu wa muvurugo. Hata kama tuliwaambia kama tulikuwa tumejiandikisha, walikataa kutuamini. Walitufunga na kutupeleka ku biro ya polisi yenye ilikuwa karibu na nyumba ya wamisionere. Moyo wetu ulitulia wakati, ofisa mwenye alijua kama tulikuwa tumejiandikisha, alitutambua na kuambia wale polisi wengine watuachilie!
Ile wakati, mara mingi tulihangaika sana wakati tulisimamishwa na maaskari, zaidi sana maaskari wenye walikuwa wamelewa sana. Lakini, kila wakati, tulisali na tukapata amani ya akili. Kisha walituruhusu kupita kwa usalama. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, mu mwaka wa 1973, wamisionere wote kutoka inchi zingine wenye walikuwa Uganda waliombwa waondoke.
Niko ninafanya kopi za Huduma Yetu ya Ufalme, mu muji wa Abidjan, ku biro ya tawi ya Côte d’Ivoire
Mugao wetu ulibadilika tena. Mara hii tulitumwa Côte d’Ivoire, Afrika ya Mangaribi. Ile ilibadilisha mambo mingi mu maisha yetu. Tulipaswa kujifunza desturi ya mupya kabisa, kuzungumuza tena Kifaransa kila wakati, na kuzoea kuishi na wamisionere wa desturi mbalimbali! Lakini, tulijionea tena namna Yehova alikuwa anatuongoza wakati, bila kukawia, watu wanyenyekevu na wenye moyo muzuri walikubali habari njema. Tulijionea namna wakati tunamutegemea Yehova, ananyoosha njia yetu.
Kisha, bila kutazamia wanganga walivumbua kama Barbara alikuwa na ugonjwa wa kansere. Tulirudia Ulaya mara mingi ili apate matunzo, lakini mu mwaka wa 1983, ilionekana wazi kama hatungeendelea kutumikia mu mugao wetu katika Afrika. Ile ilituhuzunisha sana!
MABADILIKO MU MAISHA YETU
Kansere ya Barbara iliendelea wakati tulikuwa tunatumikia ku Beteli ya Londres, na kisha akakufa. Familia ya Beteli ilinitegemeza sana. Ndugu mumoja na bibi yake walinisaidia niweze kuvumilia na niendelee kumutegemea Yehova. Kisha, nilikutana na Ann, dada mumoja mwenye alikuwa anatumika ku Beteli lakini mwenye hakukuwa anaishi ku Beteli. Zamani, alikuwaka painia wa pekee. Kwa sababu alimupenda Yehova, niliona kama alikuwa mutu wa kiroho. Tulioana mu 1989, na tangu ile wakati tunatumikia ku Beteli ya Londres.
Mimi na Ann mbele ya majengo ya mupya ya Beteli ya Uingereza
Kuanzia mwaka wa 1995 mupaka 2018, nilikuwa mujumbe wa makao makubwa (mwenye zamani alikuwa anaitwa mwangalizi wa eneo la dunia). Nilitembelea inchi karibu 60. Mu kila inchi, nilijionea waziwazi namna Yehova anabariki watu wake mu hali mbalimbali.
Mu mugao wangu wa kutembelea tawi mbalimbali, nilirudia tena Afrika mu mwaka wa 2017. Nilifurahi sana kumupeleka Ann mu inchi ya Burundi kwa mara ya kwanza na tulishangaa kuona namna watu wengi walikuwa wamekubali kweli! Mu ileile barabara yenye nilihubiri nyumba kwa nyumba mu mwaka wa 1964, kulikuwa sasa Beteli ya muzuri yenye inasimamia kazi ya wahubiri zaidi ya 15500.
Nilifurahi sana wakati nilipewa liste ya inchi zenye ningetembelea mu mwaka wa 2018. Inchi ya Côte d’Ivoire ilikuwa ku ile liste. Wakati tulifika Abidjan, muji mukubwa, ilikuwa sawa vile ninafika ku nyumba. Wakati niliangalia liste ya namba za telefone za ndugu wenye kutumika ku Beteli, nilitambua kama ndugu mwenye chumba chake kilikuwa karibu na chumba cha wageni chenye tulikuwa ndani alikuwa ndugu Sossou. Nilikumbuka kama alikuwa mwangalizi wa muji wakati nilikuwa Abidjan. Lakini nilikosea, alikuwa mwingine Sossou, mutoto wa uleule Sossou.
Yehova ametimiza ahadi yake. Mu magumu yote yenye nimepata, nimeona kama wakati tunamutegemea Yehova, bila shaka ananyoosha njia yetu. Sasa tunangojea kwa hamu kuendelea kufuata ile njia yenye haina mwisho yenye itangaa zaidi na zaidi mu ulimwengu mupya.—Mez. 4:18.