HABARI YA KUJIFUNZA YA 26
Kujua Kama Yehova Anatupenda Kunatusaidia Tupiganishe Woga
“Yehova iko upande wangu; sitaogopa.”—ZB. 118:6.
WIMBO 105 “Mungu Ni Upendo”
KIFUPI YA HABARIa
1. Watumishi fulani wa Yehova waliogopa nini?
FIKIRIA hali zenye kufuata. Nestor na María bibi yake, walipenda kutumikia fasi kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri.b Juu waweze kufanya vile, walipaswa kujifunza kuishi na makuta kidogo. Lakini, waliogopa kuwa hawatakuwa na furaha kama itaomba waishi na makuta kidogo. Wakati Biniam alifikia kuwa Shahidi wa Yehova mu inchi fulani kwenye kazi yetu inakatazwa, alitambua kama naye pia atateswa. Lakini zaidi sana, aliogopa namna familia yake itatenda wakati ingefikia kujua kama ameingia mu dini ingine. Valérie naye walimupata na kansere ya nguvu sana, na alikuwa na magumu ya kupata munganga mwenye angeheshimia mambo yenye Biblia inasema kuhusu damu. Kwa hiyo, aliogopa kama anaweza kufa.
2. Juu ya nini tunapaswa kupiganisha woga?
2 Na weye ulishakaogopa vile? Wengi kati yetu walishakaogopa. Kama hatujikaze kupiganisha woga, tunaweza kukamata maamuzi yenye itaharibisha urafiki wetu na Yehova. Ile njo yenye Shetani anatafuta. Tena, anajaribu kutumia mambo yenye inatuogopeshaka juu ya kutuchochea tuvunje amri za Yehova, kwa mufano, amri ya kuhubiri habari njema. (Ufu. 12:17) Shetani iko muovu, harudiake nyuma, na iko na nguvu. Lakini unaweza kuepuka mitego yake. Namna gani?
3. Tunapaswa kufanya nini juu Shetani asituogopeshe?
3 Juu Shetani asituogopeshe, tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anatupenda. (Zb. 118:6) Kwa mufano, muandikaji wa Zaburi ya 118 alipambana na hali fulani za nguvu sana. Alikuwa na maadui wengi. Kati ya wale maadui, kulikuwa watu wenye vyeo (mustari wa 9 na wa 10). Wakati fulani, alikuwa na mahangaiko sana (mustari wa 13). Na tena, Yehova alimupatia nizamu kali (mustari wa 18). Ijapokuwa ile yote, ule muandikaji wa Zaburi aliimba hivi: “Sitaogopa.” Juu ya nini alisema vile? Alijua kama, Yehova, Baba yake wa mbinguni, alikuwa namupenda sana hata kama alimupatia nizamu kali. Alikuwa hakika kama hata akuwe mu hali ya namna gani, Mungu wake mwenye kumupenda sana atakuwa tayari kumusaidia.—Zb. 118:29.
4. Ni mambo gani tatu yenye tutaweza kupiganisha kama tuko hakika kuwa Yehova anatupenda?
4 Kila mumoja wetu anapaswa kuwa hakika kama Yehova anamupenda kabisa. Kama tuko hakika na ile jambo, tutaweza kupiganisha hii mambo tatu: (1) kuogopa kama hatutaweza kutimiza mahitaji ya familia, (2) kuogopa mwanadamu, na (3) kuogopa kifo. Ndugu na dada wenye tulizungumuzia mu fungu ya kwanza waliweza kupiganisha woga wao juu walikuwa hakika kama Yehova anawapenda.
KUOGOPA KAMA HATUTAWEZA KUTIMIZA MAHITAJI YA FAMILIA
Ndugu iko karibu na mutoto wake mwanaume, na iko navua samaki juu familia yake ipate mahitaji ya kimwili (Ona fungu ya 5)
5. Kichwa ya familia anaweza kuogopa nini? (Ona picha ku jalada.)
5 Mukristo, mwenye ni kichwa ya familia, anakamataka kwa uzito daraka ya kuhangaikia mahitaji ya kimwili ya familia yake. (1 Ti. 5:8) Kama uko kichwa ya familia, pengine uliogopa kuwa unaweza kupoteza kazi mu hii kipindi ya Coronavirus. Pengine uliogopa kama hautapata chakula kwa ajili ya familia ao hautaweza kulipia nyumba. Pengine pia uliogopa kama ukipoteza kazi, hautapata ingine. Ao sawa vile Nestor na María, wenye tulishazungumuzia, pengine uliwaza kama itakuwa nguvu kuishi na makuta kidogo. Shetani amefanya watu wengi waache kumutumikia Yehova juu walikuwa na woga wa vile.
6. Shetani anajaribu kutufanya tuamini nini?
6 Shetani anajaribu kutufanya tuamini kama Yehova hatuhangaikiake na kama hatatusaidia kutimiza mahitaji ya familia yetu. Kama tunaamini ile mawazo, ile inaweza kutuchochea kufanya yetu yote juu tusipoteze kazi, hata kama itatuomba kuvunja kanuni za Biblia.
7. Yesu anatuhakikishia nini?
7 Yesu, mwenye anamujua Yehova muzuri zaidi kupita siye wote, anatuhakikishia kama Yehova “anajua kile chenye [tuko] nacho lazima hata mbele [tumuombe].” (Mt. 6:8) Tena, Yesu anajua kama Yehova iko tayari kututimizia mahitaji yetu. Siye Wakristo, tuko mu familia ya Yehova. Vile Yehova njo Kichwa ya familia, tuko hakika kama ataheshimia kanuni yenye inapatikana mu 1 Timoteo 5:8.
Yehova atahakikisha kama tuko na mambo yenye tuko nayo lazima. Anaweza kuchochea ndugu na dada watusaidie (Ona fungu ya 8)d
8. (a) Nini njo itatusaidia tukuwe hakika kama tutakuwa na mambo yenye tuko nayo lazima? (Matayo 6:31-33) (b) Vile picha inaonyesha, namna gani tunaweza kuiga bibi na bwana wenye wanaletea dada yetu chakula?
8 Kujua kama Yehova anatupenda na anapenda familia yetu, kutatusaidia tukuwe hakika kama tutakuwa na mambo yenye tuko nayo lazima. (Soma Matayo 6:31-33.) Yehova anapenda kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima. Kusema kweli, hakuna Baba mwenye upendo na mukarimu kama yeye! Wakati aliumba dunia, hakutia ndani tu mambo ya musingi yenye tuko nayo lazima juu tuishi. Lakini zaidi ya ile, aliumba pia mambo ingine ya mingi ya kutusaidia tufurahie maisha. (Mwa. 2:9) Wakati fulani, tunaweza kujikuta tuko na mambo kidogo tu, lakini ni muzuri tufurahi vile tuko hata na ile kidogo. Juu ya nini? Juu ile kidogo inaonyesha kama Yehova hayashindwa kututimizia mahitaji yetu. (Mt. 6:11) Sikuzote tunapaswa kukumbuka kama, mambo yenye tunajiima haiko kitu tukiilinganisha na mambo yenye Mungu wetu mwenye upendo iko natupatia sasa, na yenye atatupatia mu siku zenye ziko nakuya. Njo jambo yenye Nestor na María walifikia kuelewa.—Isa. 65:21, 22.
9. Mufano wa Nestor na María unakufundisha nini?
9 Nestor na María walikuwa na maisha ya muzuri mu inchi ya Kolombia. Wanasema hivi: “Tulipenda kufanya maisha yetu ikuwe mwepesi juu tuweze kufanya mengi zaidi mu kazi ya Yehova, lakini tuliogopa kama itakuwa nguvu kuishi na makuta kidogo.” Nini njo iliwasaidia waache kuogopa? Walifikiria mambo mingi yenye Yehova alikuwa amewatendea, yenye ilionyesha kama anawapenda. Ile iliwahakikishia kama Yehova hatakosa kuwahangaikia. Njo maana, waliacha kazi zao za mushahara muzuri. Waliuzisha nyumba yao na wakahamia mu inchi ingine kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Wanaona namna gani uamuzi wao? Nestor anasema hivi: “Tumejionea kama maneno ya Matayo 6:33 ni ya kweli. Hatuyakosaka kitu na tuko na maisha yenye furaha sasa.”
KUOGOPA MWANADAMU
10. Juu ya nini wanadamu wanaogopaka wanadamu wenzao?
10 Wanadamu wako na tabia ya kutendea mubaya wanadamu wenzao. (Muh. 8:9) Kwa mufano, watu fulani wanatumia mamlaka yao juu ya kutendea wengine mubaya, wengine wanatendea wenzao kwa jeuri, wanafunzi fulani wanatukana na kuogopesha wanafunzi wenzao ku masomo, na watu fulani wanatendea watu wa familia yao kwa ukali. Njo maana wanadamu wanaogopaka wanadamu wenzao! Namna gani Shetani anatumia woga wa mwanadamu?
11-12. Namna gani Shetani anatumia woga wa mwanadamu?
11 Shetani anatumia woga wa mwanadamu juu ya kutufanya tuache kuhubiri na tuvunje sheria za Yehova. Shetani anachochea serikali za wanadamu zikataze kazi yetu na zitutese. (Lu. 21:12; Ufu. 2:10) Mu hii dunia ya Shetani, watu wengi wanaeneza habari za uongo juu ya Mashahidi wa Yehova. Watu wenye wanaamini zile habari za uongo wanaweza kutuchekelea, ao hata kututendea mubaya kimwili. (Mt. 10:36) Zile njia za Shetani zinapaswa kutushangaza? Hapana. Alishakazitumia mu karne ya kwanza.—Mdo. 5:27, 28, 40.
Hata kama watu wa familia yetu wanatupinga, tukuwe hakika kama Yehova anatupenda (Ona fungu ya 12-14)e
12 Zaidi ya kuogopa kupingwa na serikali, Shetani anatumiaka njia zingine. Watu fulani wanaogopa namna watu wa familia yao wanaweza kutenda ikiwa wanakuwa Mashahidi wa Yehova. Wakati fulani, wanaweza kuogopa ile kuliko vile hata wanaweza kuogopa kutendewa mubaya kimwili. Wanapenda sana watu wa familia yao na wangependa wao pia wafikie kumujua Yehova na kumupenda. Na wanasikiaka mubaya wakati watu wa familia yao wanasema mambo ya mubaya juu ya Mungu wa kweli na juu ya watumishi wake. Mu hali fulani, watu wa familia wenye ku mwanzo walikuwa wanapinga kweli, walifikia kuikubali. Lakini, utafanya nini kama watu wa familia yako wanakukatala juu unakuwa Shahidi wa Yehova?
13. Kukuwa hakika kama Yehova anatupenda kunatusaidia namna gani wakati watu wa familia yetu wanatukatala? (Zaburi 27:10)
13 Maneno ya muzuri ya Zaburi 27:10 inaweza kututia moyo. (Soma.) Kama tunakumbuka kuwa Yehova anatupenda sana, hatutaogopa hata kama watu wa familia yetu wanatukatala. Na tutakuwa hakika kama Yehova atatubariki juu ya uvumilivu wetu. Hakuna mutu mwingine mwenye anaweza kututimizia muzuri mahitaji yetu ya kimwili, kihisia, na kiroho sawa vile Yehova! Ile njo Biniam, mwenye tulishazungumuzia, alifikia kuelewa.
14. Mufano wa Biniam unakufundisha nini?
14 Biniam alifikia kuwa Shahidi wa Yehova hata kama alijua kuwa serikali ilikuwa inatesa sana Mashahidi mu inchi yao. Lakini, kujua kama Yehova anamupenda kulimusaidia Biniam apiganishe woga wa mwanadamu. Anasema hivi: “Mashahidi waliteswa sana kuliko vile niliwazia. Lakini, jambo yenye niliogopa hata zaidi kuliko upinzani wa serikali ilikuwa kupingwa na watu wa familia yangu. Niliogopa kama baba yangu mwenye haiko Shahidi atahuzunika sana, na watu wa familia yangu wangeniona kuwa mutu bure juu ninaamua kuwa Shahidi wa Yehova.” Lakini, Biniam alikuwa hakika kama Yehova hakosake kuhangaikia wale wenye anapenda. Biniam anasema hivi: “Nilifikiria namna Yehova amesaidia wengine kuvumilia magumu ya kukosa makuta, ubaguzi, na kutendewa mubaya na vikundi vyenye jeuri. Nilijua kama ikiwa ninashikamana na Yehova, atanibariki. Wakati nilikamatwa mara mingi na hata kutendewa mubaya, nilijionea namna Yehova anatusaidiaka wakati ya magumu ikiwa tunaendelea kuwa waaminifu kwake.” Biniam alijionea namna Yehova ni Baba wa kweli kabisa, na watumishi wa Yehova walikuwa kabisa familia kwake.
KUOGOPA KIFO
15. Juu ya nini tunaogopaka kifo?
15 Biblia inasema kama kifo ni adui. (1 Ko. 15:25, 26) Tunaweza kuogopa kifo, zaidi sana wakati siye ao watu wenye tunapenda ni wagonjwa sana. Juu ya nini tunaogopaka kifo? Juu Yehova alituumba na tamaa ya kufurahia maisha milele. (Muh. 3:11) Kuogopa kifo kwa kiasi fulani kunaweza kutusaidia tusitie uzima wetu mu hatari. Kwa mufano, kunaweza kutuchochea kula chakula yenye kujenga mwili, kufanya mazoezi ya mwili, kuenda kuona munganga na kutafuta dawa wakati inaomba kufanya vile, na kuepuka kutia uzima wetu mu hatari wakati haiko lazima kufanya vile.
16. Shetani anatumiaka namna gani woga wa kifo?
16 Shetani anajua kama tunapenda sana kuishi. Lakini, anasema kama tunaweza kutoa ao kuachana na kila kitu yenye tuko nayo, na hata urafiki wetu na Yehova, juu tu tuendelee kuishi. (Yob. 2:4, 5) Ile ni uongo kabisa! Lakini vile Shetani njo “mwenye kuwa na uwezo wa kutokeza kifo,” anajaribu kutumia woga wa kifo juu ya kutufanya tumuache Yehova. (Ebr. 2:14, 15) Wakati fulani, watu wenye kuchochewa na Shetani wanaweza kutuogopesha kama watatuua ikiwa tunakatala kukana imani yetu. Na wakati ingine, ikiwa Shetani anaona kama tuko wagonjwa sana na tunaweza kufa, anaweza kutumia ile hali juu atufanye tukane imani yetu. Wanganga na watu wa familia wenye hawako Mashahidi wanaweza kutukaza tukubali kutiwa damu, jambo yenye inavunja sheria ya Mungu. Ao mutu fulani anaweza kutuchochea tukubali matunzo yenye inapingana na kanuni za Biblia.
17. Kulingana na Waroma 8:37-39, juu ya nini haiombe kuogopa kifo?
17 Hata kama hatupendake kufa, tunajua kama Yehova hataacha kutupenda ikiwa maisha yetu inafikia mwisho. (Soma Waroma 8:37-39.) Wakati marafiki wa Yehova wanakufa, anaendelea kuwakumbuka. Kwake, ni sawa vile tu wangali wazima. (Lu. 20:37, 38) Anangoya kwa hamu sana kuwafufua. (Yob. 14:15) Yehova alilipa bei kubwa sana juu ‘tupate uzima wa milele.’ (Yoh. 3:16) Tunajua kama Yehova anatupenda sana na kama anatuhangaikia. Kwa hiyo, kuliko kumuacha Yehova wakati tuko wagonjwa ao wakati wanatuogopesha kama watatuua, tunapaswa kumuomba Yehova atufariji, atupatie hekima, na nguvu. Vile njo Valérie na bwana yake walifanya.—Zb. 41:3.
18. Mufano wa Valérie unakufundisha nini?
18 Wakati Valérie alikuwa na miaka 35, walimuvumbula na kansere ya nguvu sana. Lakini, kujua kama Yeova anamupenda kulimusaidia asiogope kifo. Anasema hivi: “Miye na bwana yangu tulihuzunika sana wakati walinivumbula na kansere. Nilipaswa kufanyiwa upasuaji. Nilionana na wanganga wengi, na wote walikatala kunifanya upasuaji bila kutumia damu. Niliogopa sana. Lakini, juu ya kuheshimia sheria ya Mungu, nilikatala kutiwa damu! Yehova amenionyesha upendo mwingi sana. Sasa iliomba na miye nimuonyeshe kama ninamupenda. Kila mara wakati nilipata habari ya mubaya, niliazimia hata zaidi kumufurahisha Yehova, hapana Shetani. Nilifikia kufanyiwa upasuaji bila kutumia damu, na mambo ilipitikana muzuri. Hata kama matatizo yangu ya afya haiyaisha, sikuzote Yehova anatupatia mambo yenye tuko nayo lazima. Kwa mufano, ku mukutano wa mwisho wa juma, mbele wanivumbule na kansere, tulijifunza habari yenye kichwa: ‘Kupambana na Matatizo ya Leo kwa Ujasiri.’c Ile habari ilitufariji sana. Tuliisoma tena na tena. Kujifunza habari sawa ile na kuwa na programu ya muzuri ya kiroho kumenisaidia miye na bwana yangu kuwa na amani ya akili, usawaziko, na kukamata maamuzi ya muzuri.”
TUNAWEZA KUPIGANISHA WOGA
19. Nini njo itatokea karibuni?
19 Kwa musaada wa Yehova, Wakristo mu dunia yote wameweza kupambana na hali za nguvu na kumupinga Ibilisi. (1 Pe. 5:8, 9) Na weye unaweza. Karibuni, Yehova atamuomba Yesu na watawala wenzake ‘wavunje kazi za Ibilisi.’ (1 Yo. 3:8) Kisha pale, watu wa Mungu ku dunia ‘hawataogopa kitu chochote na hawatakuwa na hofu.’ (Isa. 54:14; Mik. 4:4) Lakini kwa sasa, tunapaswa kuendelea kupiganisha woga.
20. Tunapaswa kufanya nini juu tuweze kupiganisha woga?
20 Tunapaswa kuendelea kujihakikishia kabisa kama Yehova anatupenda na kama analindaka watumishi wake. Jambo yenye itatusaidia kufanya vile ni kutafakari na kuzungumuzia namna Yehova alilinda watumishi wake wa zamani. Na tusikuwe nasahau namna alitusaidia kipekee wakati tulikuwa mu hali za nguvu. Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kupiganisha woga!—Zb. 34:4.
WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia
a Haiko mubaya kuogopa juu woga unaweza kutusaidia tuepuke hatari. Lakini woga wenye haufae unaweza kutuletea matokeo ya mubaya. Namna gani? Shetani anaweza kutumia woga juu ya kutufanya tukamate maamuzi ya mubaya. Njo maana, tunapaswa kupiganisha woga wenye haufae. Nini njo itatusaidia? Vile tutajifunza mu hii habari, kama tuko hakika kuwa Yehova iko upande wetu na kama anatupenda, ile itatusaidia tupiganishe woga.
b Majina fulani imebadilishwa.
d MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana wanaletea dada wa mu kutaniko yao chakula. Ni dada mwenye kutumika sana.
e MAFASIRIO YA PICHA: Wazazi wa ndugu moya kijana hawapendi amutumikie Yehova, lakini iko hakika kama Yehova atamutegemeza.