Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 10 uku. 30
  • Ulijua?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ulijua?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 10 uku. 30
Wanamuziki Waisraeli wako napiga tarumbeta na vinubi na wako naimba kwa sauti ili kumuabudu Yehova.

Ulijua?

Tunajua namna gani kama muziki ulikuwa wa maana mu Israeli ya zamani?

MUZIKI ulikuwa jambo ya maana sana mu desturi ya Waisraeli wa zamani. Biblia inazungumuzia mara kwa mara batu benye kupiga vyombo vya muziki na benye kuimba nyimbo. Kwa kweli, sehemu kubwa ya Maandiko ni nyimbo. Kwa mufano Zaburi, Wimbo wa Sulemani, na Maombolezo viliandikwa ili kuimbwa. Kitabu fulani yenye kufasiria namna maisha ilikuwa mu wakati wa zamani inasema hivi: “Waisraeli walitumia muziki mu sehemu mbalimbali ya maisha yao.” (Music in Biblical Life)

Muziki mu maisha ya kila siku. Waisraeli walipiga vyombo vya muziki na kuimba ili kuonyesha namna walikuwa najisikia. (Isa. 30:29) Wanamuke walipiga ngoma za kidogo na wako wanaimba kwa furaha na kucheza wakati wa matukio ya maana sawa vile wakati mufalme mupya aliwekwa, wakati walipata ushindi mu vita na wakati wa sikukuu za ibada. (Amu. 11:34; 1 Sa. 18:​6, 7; 1 Fa. 1:​39, 40) Pia Waisraeli waliimba ili kuonyesha huzuni yao wakati mutu alikufa. (2 Ny. 35:25) Kulingana na Cyclopedia ya McClintock na Strong, “ni wazi kama Waisraeli walipenda sana muziki.”

Muziki mu makao ya kifalme. Wafalme wa Israeli walipenda muziki. Mufalme Sauli alimuita Daudi juu akuwe mupiga-muziki mu nyumba yake ya kifalme. (1 Sa. 16:​18, 23) Kisha, wakati Daudi alikuwa mufalme alitengeneza vyombo vya mupya vya muziki na alipanga wapiga-muziki na waimbaji wenye walifikia kutumikia mu hekalu ya Yehova. (2 Ny. 7:6; Amo. 6:5) Mufalme Sulemani alikuwa na waimbaji wanaume na wanamuke mu nyumba yake ya kifalme.—Muh. 2:8.

Muziki mu ibada. Jambo ya maana zaidi, Waisraeli walitumia muziki ili kumuabudu Yehova. Mu hekalu ya Yerusalemu mulikuwa wanamuziki 4000. (1 Ny. 23:5) Walipiga vyombo vya muziki sawa vile matoazi, vyombo vya kamba, vinubi, na tarumbeta. (2 Ny. 5:12) Lakini haiko tu wale wanamuziki wenye uzoefu njo walikuwa namuabudu Yehova kupitia muziki. Ni wazi kama Waisraeli wengi walimuimbia Yehova nyimbo za safari za kupanda wakati walikuwa naenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu za kila mwaka. (Zb. 120-134) Na kulingana na maandishi ya Wayahudi, Waisraeli walikuwa wanaimba Zaburi za Halelia wakati wa chakula ya Pasaka.

Muziki ungali ya maana kwa watu wa Mungu. (Yak. 5:13) Kuimba ni sehemu ya ibada yetu. (Efe. 5:19) Muziki unatuunganisha na Wakristo wengine. (Kol. 3:16) Muziki unatutia nguvu wakati tuko na magumu. (Mdo. 16:25) Muziki ni njia ya muzuri ya kuonyesha imani yetu kwa Yehova na kuonyesha kama tunamupenda.

a Wayahudi waliita Zaburi 113 mupaka 118 Zaburi za Haleli, zenye waliimba ili kumusifu Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine