Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 11 uku. 14-19
  • Ndugu​—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Watumishi wa Huduma?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ndugu​—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Watumishi wa Huduma?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUTUMISHI WA HUDUMA IKO NA KAZI GANI?
  • JUU YA NINI UNAPENDA KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA?
  • NINI NJO INAWEZA KUKUCHOCHEA UPENDE KABISA KUTUMIKIA NDUGU ZAKO?
  • NAMNA YA KUFIKIA KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA
  • Onyesha Shukrani Juu ya “Zawadi Katika Wanadamu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Watumishi wa Huduma Wanafanya Kazi ya Maana
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Ndugu—Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Wazee?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 11 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 46

WIMBO 49 Tufurahishe Moyo wa Yehova

Ndugu—Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Watumishi wa Huduma?

“Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” —MDO. 20:35.

WAZO KUBWA

Kutia moyo ndugu wenye kubatizwa watimize mambo yenye inaombwa juu wafikie kuwa watumishi wa huduma.

1. Paulo aliona namna gani watumishi wa huduma?

WATUMISHI wa huduma wanafanya kazi ya maana sana mu makutaniko. Mutume Paulo alifurahia sana wale wanaume waaminifu. Kwa mufano wakati aliandikia Wafilipi, alisalimia watumishi wa huduma na wazee.—Flp. 1:1.

2. Ndugu Luis anasema nini juu ya mugao wake wa kuwa mutumishi wa huduma?

2 Bandugu mingi benye kubatizwa, ikuwe vijana ao wazee, banafurahia sana kuwa watumishi wa huduma. Kwa mufano, ndugu Devan aliwekwa kuwa mutumishi wa huduma wakati alikuwa na miaka 18. Lakini ndugu Luis aliwekwa kuwa mutumishi wa huduma wakati alikuwa na miaka zaidi ya 50. Maneno yake inaonyesha namna watumishi wa huduma wengi wanajisikiaka. Alisema hivi: “Ninaona kama ni pendeleo kubwa kuwa mutumishi wa huduma, zaidi sana wakati ninafikiria upendo wenye kutaniko imenionyesha!”

3. Tutazungumuzia maulizo gani?

3 Kama uko ndugu mwenye kubatizwa na hauyakuwa mutumishi wa huduma, unaweza kujikaza kufikia ule muradi? Ni nini inaweza kukuchochea kufanya vile? Ni mambo gani Biblia inaomba utimize juu ustahili kuwa mutumishi wa huduma? Mu hii habari tutapata majibu ya ile maulizo. Lakini tuzungumuzie kwanza kazi ya watumishi wa huduma.

MUTUMISHI WA HUDUMA IKO NA KAZI GANI?

4. Mutumishi wa huduma anafanyaka kazi gani? (Ona pia picha.)

4 Mutumishi wa huduma ni ndugu mwenye kubatizwa mwenye anawekwa na roho takatifu juu ya kusaidia wazee kufanya mambo mbalimbali mu kutaniko. Watumishi wa huduma fulani wanahakikisha kama wahubiri wako na eneo ya kuhubiria na vichapo vya kutumikisha mu mahubiri. Wengine wanasaidia kusafisha na kutunza Jumba ya Ufalme. Pia Watumishi wa huduma wanatumika ku ukaribishaji na wanashugulikia vyombo vya kutoa sauti na kuonyesha video wakati wa mikutano. Kazi mingi zenye watumishi wa huduma wanafanya, ni za kusaidia mambo iendeke muzuri. Hata vile, watumishi huduma ni wanaume wa kiroho. Wanamupenda Yehova na wanatii kanuni zake. Wanapenda sana ndugu na dada zao. (Mt. 22:​37-39) Namna gani ndugu mwenye kubatizwa anaweza kujikaza juu afikie kuwa mutumishi wa huduma?

Picha: Watumishi wa huduma wako najitoa juu ya kutumika. 1. Ndugu moya iko naweka vichapo. 2. Ndugu mwingine iko nasafisha W.C. 3. Ndugu mwingine iko nasalimia watu wenye wako nafika ku mukutano. 4. Ndugu iko natumika ku vyomba vya audio-video ku Jumba ya Ufalme.

Watumishi wa huduma wanaiga Yesu kwa kujitoa juu ya kutumikia bengine (Ona fungu ya 4)


5. Ndugu anaweza kufanya nini juu afikie kuwa mutumishi wa huduma?

5 Biblia inaonyesha mambo yenye ndugu wenye kubatizwa wanapaswa kutimiza juu wawekwe kuwa watumishi wa huduma. (1 Ti. 3:​8-10, 12, 13) Unaweza kujikaza juu ufikie ile pendeleo kwa kujifunza juu ya ile mambo na kujikaza sana kuitimiza. Lakini kwanza ni muzuri ufikirie nia yenye inakuchochea kujikaza kufikia ile pendeleo.

JUU YA NINI UNAPENDA KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA?

6. Nini njo inapaswa kukuchochea kufanya kazi yoyote kwa ajili ndugu na dada zako? (Matayo 20:28; ona pia picha ku .)

6 Yesu ni mufano muzuri sana. Upendo njo ulimuchochea kutumikia bengine. Alipenda Baba yake na alipenda batu. Upendo ulimuchochea kutumika kwa bidii na kufanya kazi za hali ya chini juu ya kusaidia bengine. (Soma Matayo 20:28; Yoh. 13:​5, 14, 15) Ikiwa unapenda kuwa mutumishi wa huduma juu unamupenda Yehova na unapenda batu, Yehova atakubariki na atakusaidia ufikie muradi wako wa kuwa mutumishi wa huduma.—1 Ko. 16:14; 1 Pe. 5:5.

Yesu iko nanawisha mitume wake migulu na mitume wengine wanaangalia na kushangala.

Kupitia mufano wake, Yesu alifundisha mitume wake kutumikia bengine kwa unyenyekevu kuliko kutafuta cheo (Ona fungu ya 6)


7. Juu ya nini ndugu anapaswa kuepuka kujitafutia sifa?

7 Mu hii dunia, batu mingi banapendaka batu ya kujitafutia sifa. Lakini mambo haiko vile mu tengenezo ya Yehova. Ndugu mwenye anachochewa na upendo sawa Yesu, hajitafutie mamlaka, cheo, ao kutafuta kuonekana. Kama ndugu mwenye iko najitafutia sifa anapewa madaraka mu kutaniko, inawezekana hatakubali kufanya kazi za hali ya chini zenye inaomba kufanya juu ya kuhangaikia kondoo wa Yehova, wenye Yehova anapenda sana. Anaweza kuona kama zile kazi zinamushushia heshima. (Yoh. 10:12) Yehova hatabariki mutu yeyote mwenye majivuno ao mwenye iko najitafutia sifa.—1 Ko. 10:​24, 33; 13:​4, 5.

8. Yesu alipatia mitume wake shauri gani?

8 Wakati fulani, hata marafiki wa karibu wa Yesu walikuwa na nia ya mubaya wakati walitafuta mapendeleo. Fikiria mambo yenye Yakobo na Yohana, mitume wawili wa Yesu, walifanya; waliomba Yesu awapatie cheo ya juu mu Ufalme wake. Yesu hakuwapongeza juu walijitafutia cheo, lakini aliambia mitume wote 12 hivi: “Kila mutu mwenye anataka kuwa wa kwanza katikati yenu anapaswa kuwa mutumwa wa wote.” (Mk. 10:​35-37, 43, 44) Ndugu wenye wanajikaza kufikia mapendeleo na wako na nia ya muzuri, ni kusema nia ya kutumikia bengine, ni baraka kwa kutaniko.—1 Te. 2:8.

NINI NJO INAWEZA KUKUCHOCHEA UPENDE KABISA KUTUMIKIA NDUGU ZAKO?

9. Unaweza kufanya nini juu upende kabisa kutumikia bengine?

9 Bila shaka unamupenda Yehova na unapenda kutumikia bengine. Hata vile, unaweza kukosa hamu ya kujikaza zaidi juu utimize mambo yenye Biblia inaomba ili kuwa mutumishi wa huduma. Unaweza kufanya nini juu upende zaidi kutumikia bengine? Fikiria furaha yenye utapata wakati unatumikia ndugu na dada zako. Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Yesu alitumikisha ile maneno mu maisha yake. Kutumikia bengine kulimuletea furaha, na weye kunaweza kukuletea furaha.

10. Yesu alionyesha namna gani kama alifurahia kutumikia bengine? (Marko 6:​31-34)

10 Fikiria mufano fulani wenye kuonyesha namna Yesu alifurahia kutumikia bengine. (Soma Marko 6:​31-34.) Siku moya Yesu na mitume wake walichoka sana. Walikuwa naenda fasi kwenye wangekuwa peke yao na kupumuzika. Lakini batu mingi balifika kule mbele yabo na balipenda Yesu abafundishe. Yesu angeweza kusema hapana juu yeye na mitume wake “hawakupata hata wakati wa kula chakula.” Ao Yesu angewafundisha tu jambo moya ao mbili. Lakini juu alikuwa na upendo, ‘alianza kuwafundisha mambo mengi.’ Na aliendelea kuwafundisha mupaka “saa ilikuwa imepita.” (Mk. 6:35) Alifanya vile haiko juu alilazimika, lakini juu ‘aliwasikilia huruma.’ Alipenda kuwafundisha juu aliwapenda. Kutumikia bengine kulimuletea Yesu furaha.

11. Yesu alionyesha mu njia gani ingine kama alihangaikia wasikilizaji wake? (Ona pia picha.)

11 Zaidi ya kufundisha bale batu, Yesu alihangaikia pia mahitaji yao ya kimwili. Kwa muujiza alibatolea chakula. Na aliipatia banafunzi yake juu babagabulie. (Mk. 6:41) Kwa kufanya vile, Yesu alifundisha banafunzi yake namna ya kutumikia bengine. Alionyesha pia kama kazi zenye tunafanyia bengine, sawa kazi zenye watumishi wa huduma wanafanya, ni za maana. Wazia furaha yenye mitume walikuwa nayo ya kutumika pamoya na Yesu juu ya kugabulia batu ile chakula yenye ilitolewa kwa muujiza mupaka “wote wakakula na kushiba”! (Mk. 6:42) Haiko ile mara moya tu njo Yesu alihangaikia kwanza mahitaji ya bengine kisha yake ikafuata nyuma. Alitumia maisha yake yote juu ya kutumikia bengine. (Mt. 4:23; 8:16) Kufundisha bengine na kuhangaikia mahitaji yao kwa unyenyekevu kulimuletea furaha sana. Kwa kweli, na weye utasikia ile furaha kama uko tayari kutumikia bengine kwa kujikaza kuwa mutumishi wa huduma.

Picha: 1. Yesu anafariji mwanamuke fulani na anazungumuza naye kwa huruma. 2. Mu mahubiri, mutumishi wa huduma kijana iko nasaidia ndugu mwenye kuzee mwenye kuwa mu kinga ya vilema.

Kupenda Yehova na kupenda bengine kutakuchochea ufanye jambo yoyote yenye unaweza juu ya kutumikia kutaniko (Ona fungu ya 11)a


12. Juu ya nini hakuna mwenye anapaswa kuwaza kama yeye hawezi kusaidia kutaniko?

12 Kama unawaza kama hauna uwezo fulani wa pekee, usivunjike moyo. Bila shaka uko na sifa zenye zinaweza kusaidia kutaniko. Kusali na kusoma mambo yenye Paulo alisema mu 1 Wakorinto 12:​12-30, kunaweza kukusaidia. Maneno ya Paulo inaonyesha wazi kama kila mutumishi wa Yehova ni wa lazima mu kutaniko, ni kusema na weye uko wa lazima. Kama kwa sasa hauyatimiza mambo yenye inaombwa juu ya kuwa mutumishi wa huduma, usivunjike moyo. Fanya yote yenye unaweza juu ya kumutumikia Yehova na kutumikia ndugu na dada zako. Ukuwe hakika kama wazee watafikiria hali yako na watakupatia mugao wenye uko na uwezo wa kutimiza.—Ro. 12:​4-8.

13. Unapaswa kukumbuka nini juu ya mambo yenye watumishi wa huduma wanapaswa kutimiza?

13 Kuko sababu ingine yenye inapaswa kukuchochea ujikaze kuwa mutumishi wa huduma. Kumbuka kama sifa zenye Biblia inakuomba utimize ni sifa zenye Wakristo wote wanapaswa kukomalisha. Kwa kweli, Wakristo wote wanapaswa kumukaribia Yehova, kutoa kwa furaha, na kuishi maisha yenye kumufurahisha Mungu. Sasa ni mambo gani yenye ndugu anapaswa kutimiza juu astahili kuwa mutumishi wa huduma?

NAMNA YA KUFIKIA KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA

14. “Kuchukua mambo kwa uzito” maana yake nini? (1 Timoteo 3:​8-10, 12)

14 Tuzungumuzie sasa sifa fulani zenye kuwa mu 1 Timoteo 3:​8-10, 12. (Soma.) Mutumishi wa huduma anapaswa “kuchukua mambo kwa uzito.” Ile maneno inaweza pia kutafsiriwa “mwenye kustahili heshima” ao “mwenye kuheshimika.” Ile haimaanishe kama hautachekaka tena ao kufanya muzaha. (Muh. 3:​1, 4) Lakini unapaswa kukamata migao yako yote kwa uzito. Kama unajulikana kuwa mutu mwenye kutumainika, ndugu na dada mu kutaniko watakuheshimia.

15. ‘Kutokuwa na ndimi mbili’ na ‘kutokuwa na pupa ya faida yenye haiko ya haki,’ maana yake nini?

15 ‘Kutokuwa na na ndimi mbili’ maana yake kusema kweli na kuwa mwenye kutumainika. Unatimiza mambo yenye unasema na unaepuka kudanganya bengine. (Mez. 3:32) ‘Kutokuwa na pupa ya faida yenye haiko ya haki’ maana yake hauko mudanganyifu mu mambo ya biashara ao mu mambo ya makuta. Hautatumia uhusiano muzuri wenye uko nao pamoya na ndugu na dada juu ukusaidie kupata makuta zaidi.

16. (a) “Wasikuwe wenye kunywa divai nyingi” maana yake nini? (b) Kuwa na “zamiri safi” maana yake nini?

16 “Wasikuwe wenye kunywa divai nyingi” maana yake unaepuka kunywa pombe kupita kiasi ao haujulikane kuwa mutu mwenye anakunywaka sana. Kuwa na “zamiri safi” maana yake kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yako. Hata kama haukamilike uko na amani ya akili juu uko na uhusiano muzuri pamoya na Yehova.

17. Namna gani ndugu anaweza kuonyesha kama ni mwenye kutumainika wakati ‘anajaribiwa kwanza ili kujua kama anafaa’? (1 Timoteo 3:10; ona pia picha.)

17 “Kujaribiwa kwanza ili kujua kama wanafaa” maana yake ulishaonyesha kama unaweza kutumainika wakati wanakupatia mugao. Kwa hiyo, wakati wazee wanakupatia mugao, fuata kwa uangalifu maagizo yao na muongozo wa tengenezo ya Yehova. Uhakikishe kama unaelewa muzuri mambo yenye unapaswa kufanya juu ya kutimiza mugao wako, na ni wakati gani unapaswa kuumaliza. Kama unatimiza muzuri kila mugao wenye unapewa, bengine mu kutaniko bataona ile na batafurahia maendeleo yako ya muzuri. Wazee mujikaze kuzoeza ndugu wenye kubatizwa. (Soma 1 Timoteo 3:10.) Mu kutaniko yenu muko ndugu wenye kubatizwa wenye kuwa kati ya miaka 10 na 14 ao wenye kuwa na miaka ya chini ya pale? Wako na programu ya muzuri ya kujifunza kipekee? Wanazoea kutoa majibu ku mikutano na wanazoea kuhubiri? Kama ni vile, muwapatie migao yenye inapatana na miaka yao na hali yao. Kama munafanya vile, wale ndugu vijana wanaweza “kujaribiwa kwanza ili kujua kama wanafaa.” Kisha, wakati watakuwa na miaka 17 ao zaidi inawezekana watastahili kuwa watumishi wa huduma.

Ndugu kijana anakamatia mikro mutu mwenye iko najibia ku mukutano.

Wakati wazee wanapatia ndugu wenye kubatizwa migao, wanaweza kuwajaribu “ili kujua kama wanafaa” (Ona fungu ya 17)


18. “Hawana shitaka” maana yake nini?

18 “Hawana shitaka” maana yake hakupaswe kuwa ushuhuda wowote wenye kuonyesha kama uko na mwenendo mubaya. Ni kweli kwamba, Wakristo wanaweza kushitakiwa mambo ya uongo. Hata Yesu alishitakiwa mambo ya uongo na alitabiri kama ile itafikia pia banafunzi yake. (Yoh. 15:20) Lakini kama unaendelea kuwa na mwenendo safi, sawa Yesu, utajulikana mu kutaniko kuwa mutu muzuri.—Mt. 11:19.

19. Kuwa “Bwana wa bibi mumoja” maana yake nini?

19 “Bwana wa bibi mumoja.” Wakati Yehova alianzisha ndoa, alipenda bwana akuwe na bibi mumoya na bibi akuwe na bwana mumoya. Unapaswa kufuata ile kanuni ya ndoa. (Mt. 19:​3-9) Mwanaume Mukristo hapaswe kufanya uasherati. (Ebr. 13:4) Lakini ile inatia ndani mambo ingine. Unapaswa kuwa mushikamanifu kwa bibi yako, haupaswe hata kidogo kupendezwa na banamuke bengine mu njia ya kimapenzi.—Yob. 31:1.

20. Namna gani mwanaume anasimamia nyumba yake “muzuri”?

20 “Mwenye kusimamia muzuri watoto wake na nyumba yake mwenyewe.” Kama uko kichwa ya familia, unapaswa kukamata madaraka yako kwa uzito. Unapaswa kuongoza ibada ya familia kwa ukawaida. Unapaswa kuhubiri pamoya na kila mutu wa mu familia yako kwa ukawaida kadiri inawezekana. Saidia batoto yako bakuwe na urafiki wa karibu pamoya na Yehova. (Efe. 6:4) Mwanaume mwenye anahangaikia familia yake anaonyesha kama anaweza kuhangaikia kutaniko.—Linganisha na 1 Timoteo 3:5.

21. Kama kwa sasa hauko mutumishi wa huduma unaweza kufanya nini?

21 Ndugu, kama hauyakuwa mutumishi wa huduma, tafazali, sali na ufikirie mambo yenye tumezungumuzia mu hii habari. Jifunze sifa zenye watumishi wa huduma wanapaswa kutimiza na ujikaze sana juu ya kuzikomalisha. Fikiria upendo wenye uko nao kwa Yehova na kwa ndugu na dada zako. Upende sana kutumikia bengine. (1 Pe. 4:​8, 10) Utakuwa na furaha sana kama unajikaza kutumikia familia yako ya kiroho. Basi, Yehova abariki sana mambo yote yenye uko najikaza kufanya juu ya kuwa mutumishi wa huduma!—Flp. 2:13.

TUMEJIFUNZA NINI MU MAANDIKO YENYE KUFUATA . . .

  • Matayo 20:28?

  • Marko 6:​31-34?

  • 1 Timoteo 3:​8-10, 12?

WIMBO 17 “Ninataka”

a MAFASIRIO YA PICHA : Kushoto, Yesu iko natumikia banafunzi yake kwa unyenyekevu; kuume mutumishi wa huduma iko nasaidia ndugu mwenye kuzeeka.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine