Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 3 uku. 14-19
  • Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ALIKAZIA AKILI MAPENZI YA YEHOVA
  • ALIKAZIA AKILI UNABII WA BIBLIA
  • ALITEGEMEA MUSAADA WA YEHOVA
  • ALIENDELEA KUWA NA MAWAZO YA MUZURI
  • Namna ya Kufurahia Zaidi Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Upendo Ukuchochee Kuendelea Kuhubiri!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 3 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

WIMBO 57 Tuhubirie Watu Wote

Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri

“Bwana . . . akawatuma wawili-wawili wamutangulie katika kila muji na kila mahali kwenye yeye mwenyewe alipaswa kuenda.”​—LU. 10:1.

WAZO KUBWA

Njia ine za kuiga bidii ya Yesu mu mahubiri.

1. Ni nini inafanya batu ya Yehova bakuwe tofauti na batu bengine?

BATUMISHI ya Yehova banakuwaka na bidii ya kuhubiri,a ile inabafanya bakuwe tofauti na batu bengine benye banajiita Bakristo. (Tit. 2:14) Lakini, wakati fulani unaweza kukosa tu hamu ya kuhubiri. Pengine unajisikiaka sawa muzee moya mwenye anatumikaka sana mu kutaniko mwenye alisema: “Wakati fulani, sikuwake tu na hamu ya kuhubiri.”

2. Ni nini inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuendelea kuhubiri kwa bidii?

2 Tunaweza kufurahia zaidi kufanya aina zingine za utumishi mutakatifu kuliko kufanya kazi ya kuhubiri. Juu ya nini? Wakati tunasaidia kujenga ao kutunza majengo yetu, wakati tunasaidia kutoa misaada, ao wakati tunatia moyo ndugu zetu, pengine tunaona palepale matokeo ya kazi yetu na tunajisikia kuwa tunatimiza jambo fulani ya maana. Tunafurahia hali ya amani na ya upendo yenye inakuwaka wakati tuko natumika pamoya na bandugu yetu, na tunajua kama banaona kazi yetu kuwa ya maana. Lakini, pengine tuko nahubiri mu eneo ileile kwa miaka mingi na ni batu kidogo tu njo banatusikiliza. Ao tunaweza kukutana na batu benye banakatala ujumbe wetu. Na tunajua kama vile mwisho iko nakaribia, batu mingi habatafurahia ujumbe wetu. (Mt. 10:22) Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na bidii ao tuongeze bidii yetu ya kuhubiri?

3. Namna gani Luka 13:6-9 inaonyesha kama Yesu alikuwa na bidii?

3 Kuchunguza mufano wa Yesu kunaweza kutusaidia kuwa na bidii mu mahubiri. Mu utumishi wake ku dunia, Yesu hakupoteza hata siku moya bidii yake. Vile masiku ilikuwa napita, ni vile alikuwa naongeza bidii yake mu mahubiri. (Soma Luka 13:6-9.) Sawa vile mutu mwenye alitumika kwa miaka tatu mu shamba ya mizabibu yenye haikutoa matunda, Yesu alihubiria Wayahudi kwa karibu miaka tatu lakini wengi hawakukubali ujumbe wake. Hata vile, sawa vile ule mutu mwenye kutumika mu shamba ya mizabibu aliendelea kutumainia kama shamba itatoa matunda, Yesu hakuacha kuhubiria batu na hakupunguza bidii yake. Aliongeza bidii yake juu aweze kugusa mioyo ya batu.

4. Tutazungumuzia mambo gani ine yenye mufano wa Yesu unaweza kutufundisha?

4 Mu hii habari, tutaona namna Yesu alionyesha bidii, zaidi sana mu miezi sita ya mwisho ya utumishi wake. Kujifunza mambo yenye alisema na kuiga mambo yenye alifanya, kutatusaidia tuendelee kuwa na bidii leo. Tutaona mambo ine yenye Yesu alifanya, yenye tunaweza kuiga: (1) Alikazia akili mapenzi ya Yehova, (2) alikazia akili unabii wa Biblia, (3) alitegemea Yehova juu amusaidie, na (4) aliendelea kuwa na tumaini kama kutakuwa batu benye batamusikiliza.

ALIKAZIA AKILI MAPENZI YA YEHOVA

5. Namna gani Yesu alionyesha kama alikazia akili mapenzi ya Mungu?

5 Yesu alihubiri kwa bidii “habari njema ya Ufalme” juu alijua kama ile njo ilikuwa kazi yenye Yehova alipenda afanye. (Lu. 4:43) Yesu alitia mahubiri fasi ya kwanza mu maisha yake. Hata ku mwisho-mwisho wa utumishi wake, alisafiri “kutoka muji mupaka muji na kutoka kijiji mupaka kijiji” juu ya kufundisha. (Lu. 13:22) Alizoeza pia banafunzi bengine juu bakuwe bahubiri.​—Lu. 10:1.

6. Namna gani kazi ya kuhubiri iko na uhusiano na kazi zingine zenye tunafanya mu utumishi wa Yehova? (Ona pia picha.)

6 Leo pia, kazi ya kuhubiri habari njema njo kazi ya maana sana yenye Yehova na Yesu banapenda tufanye. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Kazi zingine zote zenye tunafanya mu utumishi wa Yehova, zinategemeza kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, tunajenga majengo mbalimbali ao tunatumika ku Beteli juu ya kutegemeza kazi ya kuhubiri. Tunatoa misaada hapana tu juu ya kusaidia bandugu na badada kimwili lakini pia juu ya kubasaidia barudilie programu ya muzuri ya kiroho yenye inatia ndani kuhubiri. Wakati tunaelewa kama kazi ya kuhubiri ni ya maana sana, na tunakumbuka kama njo kazi ya kwanza yenye Yehova anapenda tufanye, ile inatuchochea kuhubiri kwa ukawaida. János, muzee mu inchi ya Hongrie, anasema hivi: “Ninajikumbushaka kama hakuna kazi ingine mu utumishi wa Yehova yenye inaweza kukamata fasi ya kazi ya kuhubiri. Kuhubiri njo kazi yetu ya kwanza kabisa.”

Picha: 1. Ndugu iko natumika mu kazi ya ujenzi. 2. Ndugu mwingine ni mujitoleaji, iko natumikia kazi ya Beteli ku nyumba. 3. Kisha bale bandugu bawili biko nahubiri pamoya.

Kuhubiri habari njema njo kazi ya kwanza kabisa yenye Yehova na Yesu banapenda tufanye leo (Ona fungu ya 6)


7. Juu ya nini Yehova anapenda tuendelee kuhubiri? (1 Timoteo 2:3, 4)

7 Tunaweza kuongeza bidii yetu ya kuhubiri kama tunaona batu vile Yehova anabaona. Yehova anapenda batu mingi kadiri inawezekana basikie habari njema na baikubali. (Soma 1 Timoteo 2:3, 4.) Njo maana, anatuzoeza juu tukuwe na ufundi zaidi wa kutangazia batu ujumbe wenye unaokoa uzima. Kwa mufano, broshua Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi iko na mapendekezo yenye inaweza kutusaidia tuanzishe mazungumuzo na kusudi ya kufanya wanafunzi. Hata kama batu habakubali ujumbe wetu leo, banaweza kupata nafasi ya kuukubali mbele ya mwisho wa taabu kubwa. Wakati wenye kuya, banaweza kukumbuka mambo yenye tuko nabaambia leo na ile inaweza kubachochea bapende kumutumikia Yehova. Lakini ile itawezekana tu kama tunaendelea kuhubiri.

ALIKAZIA AKILI UNABII WA BIBLIA

8. Kujua unabii wa Biblia kulisaidia Yesu atumie namna gani wakati wake?

8 Yesu alijua namna unabii wa Biblia ungetimia. Alijua kama utumishi wake ku dunia ungefanya tu miaka tatu na nusu. (Da. 9:26, 27) Alijua pia mambo yenye ilitabiriwa kuhusu wakati atakufa na namna atakufa. (Lu. 18:31-34) Juu alijua ile mambo yote, alitumia muzuri wakati wake. Njo maana, alihubiri kwa bidii juu aweze kumaliza kazi yenye Baba yake alimupatia.

9. Juu ya nini maunabii ya Biblia inatuchochea kuhubiri kwa bidii?

9 Kuelewa unabii wa Biblia kunaweza kutuchochea kuhubiri kwa bidii. Tunajua kama kunabakia wakati kidogo mbele mwisho ufike. Tunatambua pia kama matukio na tabia ya batu leo inatimiza mambo yenye Biblia ilitabiri juu ya siku za mwisho. Tuko najionea namna Utawala wa Ulimwengu wa Uingereza na Amerika uko nasukumana na Urusi na wenye wanaiunga, na tunajua kama ile inatimiza unabii kuhusu mufalme wa kusini na mufalme wa kaskazini “katika wakati wa mwisho.” (Da. 11:40) Tunaelewa pia kama migulu ya sanamu yenye kuzungumuziwa mu Danieli 2:43-45 inafananisha Utawala wa Ulimwengu wa Uingereza na Amerika. Tuko hakika kama sawa vile ule unabii unaonyesha, hivi karibuni, karibuni sana Ufalme wa Mungu utaharibu serikali za wanadamu. Ile maunabii yote inaonyesha kama mwisho unakaribia sana na inatuchochea kuona kuhubiri kuwa kazi ya haraka sana.

10. Ni mu njia gani maunabii ya Biblia inatuchochea kuendelea kuhubiri?

10 Unabii wa Biblia unatupatia pia ujumbe wenye tunapenda sana kuambia bengine. Dada Carrie wa mu inchi ya République Dominicaine anasema hivi: “Wakati ninafikiria ahadi za muzuri sana zenye Yehova ametupatia juu ya wakati wenye kuya, ninapenda sana kuziambia bengine.” Carrie anasema tena hivi: “Wakati ninaona magumu yenye batu biko nayo leo, ninaelewa kama haiko miye peke njo niko na lazima ya zile ahadi, nabo pia biko nazo lazima.” Maunabii ya Biblia inatusaidia tusiache kuhubiri juu tunajua kama Yehova iko natutegemeza. Leila, mwenye kuishi Hongrie, anasema hivi: “Isaya 11:6-9 inanichochea nitangaze habari njema hata kwa bale benye banaonekana kama habataikubali. Ninajua kama kwa musaada wa Yehova mutu yeyote anaweza kubadilika.” Ndugu Christophe wa Zambia, naye anasema hivi: “Sawa vile Marko 13:10 ilitabiri, habari njema iko nahubiriwa mu dunia yote, na ninaona kama ni pendeleo kuchangia mu utimizo wa hii unabii.” Na weye, ni unabii gani wa Biblia njo unakuchochea uendelee kuhubiri?

ALITEGEMEA MUSAADA WA YEHOVA

11. Juu ya nini Yesu alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova juu aendelee kuhubiri kwa bidii? (Luka 12:49, 53)

11 Yesu alimutegemea Yehova juu amusaidie kuendelea kuhubiri kwa bidii. Hata kama Yesu alizungumuza kwa busara, alijua kama habari njema ya Ufalme ingefanya batu fulani bakasirike na ingeleta upinzani mukubwa. (Soma Luka 12:49, 53.) Mara kwa mara mahubiri ya Yesu ilifanya viongozi wa dini watafute kumuua. (Yoh. 8:59; 10:31, 39) Lakini Yesu aliendelea kuhubiri juu alijua kama Yehova alikuwa pamoya naye. Alisema hivi: “Siko peke yangu, lakini Baba mwenye alinituma iko pamoja na mimi. . . . hakuniacha peke yangu, kwa sababu sikuzote ninafanya mambo yenye kumupendeza.”​—Yoh. 8:16, 29.

12. Namna gani Yesu alitayarisha banafunzi yake juu baendelee kuhubiri hata wakati banapata upinzani?

12 Yesu alikumbusha banafunzi yake kama balipaswa kumutegemea Yehova. Mara kwa mara alibahakikishia kama Yehova atabasaidia hata wakati bangepata mateso. (Mt. 10:18-20; Lu. 12:11, 12) Juu Yesu alijua kama batu mingi batabapinga, alibashauria bakuwe baangalifu. (Mt. 10:16; Lu. 10:3) Alibaambia basilazimishe batu benye habapendi kusikiliza. (Lu. 10:10, 11) Na alibaambia kama bakibatesa mu eneo moya, bakimbilie mu eneo ingine. (Mt. 10:23) Hata kama Yesu alikuwa na bidii na alimutumainia Yehova, hakujiingiza mu hatari bila sababu.​—Yoh. 11:53, 54.

13. Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama Yehova atakusaidia?

13 Leo tuko lazima na musaada wa Yehova juu tuendelee kuhubiri kwa bidii wakati tunapata upinzani. (Ufu. 12:17) Juu ya nini unapaswa kuwa hakika kama Yehova atakutegemeza? Fikiria sala yenye Yesu alitoa yenye kuwa mu Yohana sura ya 17. Yesu alimuomba Yehova alinde mitume wake, na Yehova alijibia ile sala. Kitabu ya Matendo iko na habari ya namna Yehova alisaidia mitume wahubiri kwa bidii hata wakati waliteswa. Mu ile sala, Yesu alimuomba pia Yehova alinde bote benye batakubali mahubiri ya mitume. Ni kusema akulinde na weye. Yehova anaendelea kujibia ile sala ya Yesu; atakusaidia sawa vile alisaidia mitume.​—Yoh. 17:11, 15, 20.

14. Tunajua namna gani kama tutaendelea kuhubiri kwa bidii? (Ona pia picha.)

14 Kadiri mwisho unakaribia, inawezekana itakuwa nguvu kwetu kuhubiri habari njema kwa bidii. Lakini tukuwe hakika kama Yehova atatutegemeza. (Lu. 21:12-15) Kama Yesu na banafunzi yake, tunaacha batu bajiamulie kama batasikiliza ao hapana, na tunaepuka kubishana nabo. Hata wakati kazi yetu inatiliwa vizuizi, bandugu yetu banaendelea kuhubiri habari njema juu banamutegemea Yehova, habajitegemee. Yehova alipatia batumishi yake ba mu karne ya kwanza nguvu, leo pia anatupatia nguvu juu “kazi ya kuhubiri itimizwe kwa ukamili” mupaka wakati atasema tuache sasa. (2 Ti. 4:17) Unaweza kuwa hakika kama ikiwa unamutegemea Yehova, utaweza kuendelea kuhubiri kwa bidii.

Hata wakati kazi yetu inatiliwa vizuizi, wahubiri wenye bidii wanatafuta namna ya kuhubiri bila kujionyesha waziwazi (Ona fungu ya 14)b


ALIENDELEA KUWA NA MAWAZO YA MUZURI

15. Nini inaonyesha kama Yesu alikuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri?

15 Yesu aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri. Ile ilimusaidia aendelee kuhubiri kwa bidii. Kwa mufano, ku mwisho-mwisho wa mwaka wa 30, Yesu aliona kama batu mingi balikuwa tayari kusikiliza mafundisho yake, na alibalinganisha na shamba yenye ilikuwa tayari kwa ajili ya mavuno. (Yoh. 4:35) Mwaka moya kisha pale, aliambia banafunzi yake hivi: “Mavuno ni mengi.” (Mt. 9:37, 38) Kisha alifikia kusema tena hivi: “Mavuno ni mengi . . . mumuombe Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Lu. 10:2) Yesu aliendelea kuwa na tumaini kama batu bangekubali habari njema, na alifurahi wakati balifanya vile.​—Lu. 10:21.

16. Mifano ya Yesu inaonyesha namna gani kama tunapaswa kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri? (Luka 13:18-21) (Ona pia picha.)

16 Yesu aliambia banafunzi yake baendelee kuwa na mawazo ya muzuri juu ya habari yenye balikuwa natangazia batu. Ile ingefanya baendelee kuhubiri kwa bidii. Kwa mufano, fikiria mifano mbili yenye Yesu alitoa. (Soma Luka 13:18-21.) Yesu alitumia mufano wa mbegu ya haradali juu ya kufundisha kama ujumbe wa Ufalme ungeenea sana na hakuna kitu yenye ingeizuia. Na alitumia mufano wa chachu juu ya kuonyesha kama ujumbe ye Ufalme ungefika mu maeneo ya mbali na kusaidia batu babadilishe maisha yabo hata kama ile haitaonekana mara moya. Kwa hiyo Yesu alisaidia banafunzi yake baone kama ujumbe wenye balikuwa nahubiri ungekuwa na matokeo ya muzuri.

Badada bawili banasimama pembeni ya prezantware fasi kwenye batu mingi banapitaka. Batu mingi biko napita pale bila kusimama.

Kama Yesu, tunaendelea kutumainia kama kungali batu benye batakubali habari njema (Ona fungu ya 16)


17. Ni sababu gani zinapaswa kutuchochea tuendelee kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri?

17 Wakati tunafikiria mambo yote yenye iko natimizwa mu dunia leo, ile inatuchochea tuhubiri kwa bidii. Kila mwaka, mamilioni ya batu benye kupendezwa banafika ku Ukumbusho na banaanza kujifunza Biblia. Maelfu ya batu banabatizwa na banajiunga na siye mu kazi ya kuhubiri. Hatujue ni batu bengine ngapi batatusikiliza, lakini tunajua kama Yehova iko nakusanya kundi kubwa ya batu benye bataokoka taabu kubwa yenye iko nakuya. (Ufu. 7:9, 14) Bwana wa mavuno angali anaona kama kungali batu benye batakubali habari njema, ile inapaswa kutuchochea tuendelee kuhubiri kwa bidii.

18. Tunapenda batu batambue nini wakati banatuona?

18 Tangu zamani banafunzi ya Yesu banajulikana kuwa bahubiri benye bidii. Wakati watu waliona mitume wa Yesu wanahubiri kwa bidii na bila kuogopa, “wakaanza kutambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.” (Mdo. 4:13) Leo wakati batu banatuona mu mahubiri, banaweza kutambua kama na siye tunafuata mufano wa Yesu wa kuhubiri kwa bidii.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUENDELEA KUWA NA BIDII KWA KUIGA NAMNA YESU . . .

  • aliona kazi ya kuhubiri?

  • alimutegemea Yehova?

  • aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri?

WIMBO 58 Tutafute Marafiki wa Amani

a MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu hii habari, neno “bidii” inapenda kuzungumuzia shauku na hamu kubwa yenye Wakristo wanaonyesha wakati wanamuabudu Yehova.

b MAFASIRIO YA PICHA : Ndugu iko fasi ya kutilia esanse na iko nahubiri bila kujionyesha.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine