HABARI YA KUJIFUNZA YA 13
WIMBO 4 “Yehova Ni Muchungaji Wangu”
Mukono wa Yehova Hauko Mufupi
“Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?”—HES. 11:23.
WAZO KUBWA
Kuwa hakika kama Yehova atatutimizia mahitaji yetu ya kimwili na kumutumainia zaidi.
1. Namna gani Musa alionyesha kama alimutumainia Yehova wakati aliongoza Waisraeli kutoka Misri?
KITABU ya Waebrania inazungumuzia batu mingi benye balionyesha imani. Kwa mufano, Musa alionyesha imani ya ajabu. (Ebr. 3:2-5; 11:23-25) Alionyesha imani wakati aliongoza Waisraeli kutoka Misri. Hakuogopa Farao na maaskari wake. Juu alimutumainia kabisa Yehova, aliongoza batu wakati balivuka Bahari Nyekundu na alibaongoza mu jangwa. (Ebr. 11:27-29) Waisraeli wengi waliacha kutumainia kama Yehova iko na uwezo wa kutimiza mahitaji yao. Lakini Musa aliendelea kumutumainia Mungu. Musa hakukosea kumutumainia Yehova, juu kwa muujiza Yehova alitolea batu yake chakula na maji mu ile jangwa ya kukauka.a—Kut. 15:22-25; Zb. 78:23-25.
2. Juu ya nini Mungu alimuuliza Musa: “Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana”? (Hesabu 11:21-23)
2 Hata kama Musa alikuwa na imani ya nguvu, mwaka moya hivi kisha Yehova kuokoa Waisraeli kwa muujiza kutoka Misri, Musa alijiuliza ikiwa Yehova ataweza kutolea batu yake nyama. Waisraelil walikuwa wengi sana mu jangwa, na Musa alijiuliza namna gani Yehova ataweza kutolea bale batu yote nyama. Kwa hiyo Yehova alimuuliza Musa hivi: “Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?” (Soma Hesabu 11:21-23.) Hapa, maneno “mukono wa Yehova” inamaanisha roho takatifu ya Mungu ao nguvu yake ya kutenda. Ni sawa vile Yehova alikuwa namuuliza Musa, ‘Unawaza ninaweza kushidwa kufanya kitu yenye ninasema?’
3. Juu ya nini ni muzuri tuchunguze habari juu ya Musa na Waisraeli?
3 Ulishakajiuliza ikiwa Yehova atatimiza mahitaji yako ao ya batu ya familia yako? Ikuwe ulishakajiuliza vile ao hapana, kuchunguza mufano wa Musa na wa Waisraeli wenye hawakuamini kama Yehova atawatimizia mahitaji yao, kunaweza kukusaidia. Tutaona kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia tukuwe hakika kama mukono wa Yehova hauko mufupi.
MUFANO WA MUSA NA WAISRAELI UNAKUFUNDISHA NINI?
4. Juu ya nini Waisraeli wengi walianza kushakia kama Yehova atatimiza mahitaji yao ya kimwili?
4 Ona kwanza namna mambo ilikuwa: Waisraeli na “kikundi kikubwa cha watu wenye kuchangamana” wenye hawakukuwa Waisraeli walikuwa wamepitisha wakati fulani mu jangwa wakati walikuwa wanasafiri kutoka Misri kuenda mu Inchi ya Ahadi. (Kut. 12:38; Kum. 8:15) Wale watu wenye hawakukuwa Waisraeli walichoka kula mana na Waisraeli wengi walichoka pia. Kwa hiyo Waisraeli walijiunga na wale watu na wote wakaanza kunungunika. (Hes. 11:4-6) Watu walianza kutamani chakula yenye ilikuwa Misri. Juu wale watu wote walikuwa namunungunikia Musa, aliwaza kama ni yeye njo alipaswa kuwapatia nyama. Lakini hakujua ataitosha wapi.—Hes. 11:13, 14.
5-6. Namna watu wenye hawakukuwa Waisraeli walichochea Waisraeli wengi inatufundisha nini?
5 Wale watu wenye hawakukuwa Waisraeli hawakuwa na shukrani na inawezekana wao njo walichochea Waisraeli pia wakuwe vile. Siye pia tunaweza kuchochewa na roho ya kukosa shukrani ya bengine, na ile inaweza kufanya tusitosheke tena na mambo yenye Yehova anatupatia. Mambo inaweza kuwa vile ikiwa tunaanza kutamani vitu vyenye tulikuwa navyo zamani ao ikiwa tunaanza kusikilia bengine wivu juu ya vitu vyenye wako navyo. Lakini tutakuwa na furaha zaidi kama tunatosheka na vitu vyenye tuko navyo.
6 Waisraeli walipaswa kukumbuka kama Mungu aliwakikishia kama wakati watafika mu Inchi ya Ahadi watakuwa na vitu mingi vya kimwili. Ile ahadi ingetimia wakati wangefika mu ile inchi hapana wakati walikuwa nasafiri mu jangwa. Na siye kuliko kukazia akili vitu vyenye hatuna mu dunia ya leo, ni muzuri tufikirie mambo yenye Yehova anaahidi kutupatia mu dunia mupya. Tunaweza pia kutafakari juu ya maandiko yenye inaweza kutusaidia kumutumainia Yehova zaidi.
7. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama mukono wa Yehova hauko mufupi?
7 Lakini, pengine unajiuliza juu ya nini Mungu alimuuliza Musa hivi: “Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?” Wakati Yehova alimuuliza Musa vile, alipenda kumufundisha mambo mbili. Kwanza, nguvu yake haina mipaka, na pili hakuna kwenye mukono wake hauwezi kufika. Mungu alikuwa na uwezo wa kutolea Waisraeli nyama ya mingi hata kama walikuwa mu jangwa ya mbali sana. Kwa “mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa,” Mungu alionyesha nguvu yake. (Zb. 136:11, 12) Kwa hiyo, wakati tuko mu magumu tunapaswa kuwa hakika kama mukono wa Yehova unaweza kufikia kila mumoya wetu kipekee hata akuwe wapi.—Zb. 138:6, 7.
8. Namna gani tunaweza kuepuka kufanya kosa yenye Waisraeli wengi walifanya mu jangwa? (Ona pia picha.)
8 Bila kukawia Yehova alitolea watu nyama ya mingi, aliwatolea ndege kware. Lakini Waisraeli hawakumushukuru Yehova juu ya ile muujiza. Walikuwa na pupa. Walilokota kware wengi usiku wote na muchana yote. Yehova alikasirikia sana wale “wenye walikuwa na tamaa ya uchoyo,” na aliwapatia malipizi . (Hes. 11:31-34) Mufano wao unaweza kutufundisha somo ya maana. Tunapaswa kuwa baangalifu sana juu tusikuwe na pupa. Ikuwe tuko matajiri ao maskini, kujiwekea “hazina mbinguni” njo tunapaswa kutia fasi ya kwanza mu maisha yetu. Tunafanya vile kwa kutia nguvu urafiki wetu pamoya na Yehova na Yesu. (Mt. 6:19, 20; Lu. 16:9) Kama tunafanya vile tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatutimizia mahitaji yetu.
Mu jangwa, Waisraeli wengi walionyesha roho gani, na mufano wao unaweza kutufundisha nini? (Ona fungu ya 8)
9. Tunaweza kuwa hakika na nini?
9 Leo Yehova ananyoosha mukono wake juu ya kusaidia watu wake. Ile haimaanishe kama hatuwezi kukosa makuta ao chakula.b Lakini tunaweza kuwa hakika kama Yehova hawezi kutuachilia, atatutegemeza mu magumu yetu yote. Tuone ni mu hali gani mbili tunaweza kuonyesha kuwa tuko hakika kama Yehova atanyoosha mukono wake juu ya kututimizia mahitaji yetu ya kimwili: (1) wakati tuko na magumu ya kupata makuta, (2) wakati tuko nafikiria namna tutatimiza mahitaji yetu wakati tutazeeka.
WAKATI TUKO NA MAGUMU YA KUPATA MAKUTA
10. Nini njo inaweza kufanya tukuwe na matatizo ya kupata makuta?
10 Vile mwisho uko nakaribia tunaweza kutazamia kama magumu ya kupata makuta itaendelea kuongezeka. Muvurugo mu mambo ya politike, vita, misiba ya asili, ao magonjwa ya mupya ya kuambukiza inaweza kufanya tukuwe na lazima ya makuta zaidi ao tupoteze kazi, vitu, ao nyumba. Pengine tunalazimika kutafuta kazi ingine fasi kwenye tunaishi, ao tunafikiria kuhamisha familia yetu fasi ingine juu tuweze kuwatimizia mahitaji yao. Ni nini inaweza kutusaidia kukamata maamuzi yenye inaonyesha kama tanaamini kuwa mukono wa Yehova hauko mufupi?
11. Ni nini itakusaidia kupambana na matatizo ya kupata makuta? (Luka 12:29-31)
11 Jambo ya kwanza na ya maana sana ya kufanya ni kumuambia Yehova mahangaiko yako. (Mez. 16:3) Muombe akupatie hekima yenye uko nayo lazima juu ya kukamata maamuzi ya muzuri, na akusaidie utulie juu uepuke “kuhangaika sana” juu ya hali yako. (Soma Luka 12:29-31.) Umulilie akusaidie utosheke na mambo ya lazima. (1 Ti. 6:7, 8) Tafuta habari mu vichapo vyetu juu ujue mambo ya kufanya wakati uko na magumu ya kupata makuta. Habari za ku jw.org zenye kuzungumuzia magumu ya kupata makuta zimesaidia watu wengi.
12. Ni mawazo gani inaweza kusaidia Mukristo akamate uamuzi wa muzuri kwa ajili ya famlilia yake?
12 Batu fulani bamekubali kazi yenye iliobaomba baende mbali na famlia, lakini ku mwisho balielewa kama ile haikukuwa uamuzi wa hekima. Mbele ya kuitika kazi ya mupya, usifikirie tu makuta yenye utapata lakini fikiria pia matokeo yenye ile kazi itakuwa nayo juu ya hali yako ya kiroho. (Lu. 14:28) Ujiulize hivi: ‘Kama ninaenda kutumikia mbali, ile itakuwa na matokeo gani juu ya ndoa yangu? Kwenye nitaenda nitakuwa nakusanyika, kuhubiri, na kupitisha wakati pamoya na ndugu na dada kwa ukawaida?’ Kama uko na batoto ujiulize pia hii ulizo ya maana: ‘Namna gani nitakomalisha batoto yangu “katika nizamu na maonyo ya Yehova” kama siishi nabo fasi moya?’ (Efe. 6:4) Mawazo ya Mungu njo ikuongoze, hapana ya batu ya familia ao barafiki benye habaheshimie kanuni za Biblia.c Tony mwenye anaishi mu Asia ya Mangaribi, alipata nafasi za mingi za kutumikia mu inchi ingine na angekuwa napokea makuta mingi. Lakini kisha kusali juu ya ile jambo na kuzungumuza na bibi yake, aliamua kukatala ile kazi. Kisha balifikiria namna banaweza kuishi na makuta kidogo. Leo Tony anasema hivi: “Nimepata pendeleo ya kusaidia batu mingi bamujue Yehova, na batoto yetu banapenda sana kweli. Mu familia yetu tumejifunza kama ikiwa tunafuata shauri yenye kuwa mu Matayo 6:33, Yehova atatuhangaikia.”
NAMNA TUTATIMIZA MAHITAJI YETU WAKATI TUTAZEEKA
13. Tunaweza kufanya nini leo juu ya kupata mambo yenye tutakuwa nayo lazima wakati tutazeeka?
13 Tunaweza kuonyesha kama tunamutumainia Yehova wakati tuko nafanya mipango juu ya namna tutatimiza mahitaji yetu wakati tutazeeka. Biblia inatutia moyo tutumike kwa bidii juu tuweze kuweka kitu pembeni ya kutusaidia kutimiza mahitaji yetu wakati wenye kuya. (Mez. 6:6-11) Kama hali yetu inaruhusu ni muzuri kutia kitu pembeni. Makuta inaletaka ulinzi kwa kadiri fulani. (Muh. 7:12) Lakini kutafuta makuta haipaswe kuwa jambo ya maana zaidi mu maisha yetu.
14. Juu ya nini tunapaswa kufikiria Waebrania 13:5 wakati tuko natayarisha maisha yetu ya kesho?
14 Yesu alitoa mufano wenye ulionyesha kama ni upumbavu kujiwekea makuta bila kuwa “tajiri kwa Mungu.” (Lu. 12:16-21) Hakuna mwenye anajua bya kesho. (Mez. 23:4, 5; Yak. 4:13-15) Zaidi ya ile juu tuko wafuasi wa Kristo, tuko na tatizo ingine. Yesu alisema kama tunapaswa kuwa tayari ‘kuachana’ na vitu vyetu vyote. (Lu. 14:33, maelezo ya chini.) Wakristo wa Yudea wa mu karne ya kwanza walikubali kwa furaha kupoteza vitu vyao. (Ebr. 10:34) Wakati wetu bandugu mingi bamekubali kupoteza vitu ao kazi juu walikatala kujiingiza mu mambo ya politike. (Ufu. 13:16, 17) Nini njo ilibasaidia kufanya vile? Balikuwa hakika kabisa kama Yehova atatimiza hii ahadi yake: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” (Soma Waebrania 13:5.) Tunafanya yenye tunaweza juu ya kutayarisha maisha yetu ya kesho, na kama mambo yenye haikutazamiwa inatokea tuko hakika kama Yehova atatutegemeza.
15. Bazazi banapaswa kuwa na mawazo gani yenye kusawazika juu ya batoto yabo? (Ona pia picha.)
15 Mu desturi fulani sababu kubwa yenye inafanya batu bazale batoto ni juu batoto babategemeze wakati batazeeka. Ni sawa vile banaona batoto kuwa sawa vile “makuta yenye banaweka ku banke.” Biblia inasema kama bazazi banapaswa kuhangaikia mahitaji ya batoto. (2 Ko. 12:14) Ni kweli kama bazazi banaweza kuwa na lazima ya musaada fulani wakati banazeeka, na batoto bamingi banafurahia kubasaidia. (1 Ti. 5:4) Lakini bazazi Bakristo banaelewa kama kitu yenye inaletaka furaha ni kukomalisha batoto benye batamutumikia Yehova, hapana kubakomalisha juu babatimizie mahitaji yabo ya wakati batazeeka.—3 Yo. 4.
Bibi na bwana wenye kumutumainia Yehova banafuata kanuni ya Biblia wakati biko nakamata maamuzi juu ya maisha yabo ya kesho. Kwa mufano, wakati banaamua ikiwa batakuwa na batoto ngapi (Ona fungu ya 15)d
16. Namna gani bazazi banaweza kutayarisha batoto juu baweze kujitimizia mahitaji yabo? (Efe. 4:28)
16 Wakati uko nasaidia batoto yako bajue namna ya kujitimizia mahitaji yabo ubafundishe, kupitia mufano wako, kumutumainia Yehova. Tangu wakati bangali batoto ubafundishe kama ni jambo ya maana kutumika kwa bidii. (Mez. 29:21; soma Waefeso 4:28.) Wakati biko nakomala ubafundishe kama ni jambo ya maana kutumika muzuri ku masomo. Ni muzuri bazazi Bakristo bafanye utafiti juu ya kupata kanuni za Biblia zenye batatumikisha juu ya kusaidia batoto baamue muzuri ni masomo gani batasoma. Ile itafanya baweze kujitimizia mahitaji yabo na wakati uleule bakuwe na wakati mingi ya kupitisha mu mahubiri.
17. Tunapaswa kuwa hakika na nini?
17 Batumishi baaminifu ba Yehova banaweza kuwa hakika kama Yehova iko na nia na uwezo wa kubatimizia mahitaji yabo yote. Vile mwisho uko nakaribia, tutakutana na hali zenye zitaomba tumutumainie Yehova zaidi. Lakini hata nini itokee, tuko hakika kama Yehova atatumia nguvu yake juu ya kututimizia mahitaji yetu ya kimwili. Tunaweza kuwa hakika kama hata siku moya mukono wake wenye nguvu na wenye kunyooka hautakuwa mufupi juu usiweze kutufikia.
Wimbo 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe
a Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 10, 2023.
b Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 9, 2014.
c Ona habari “Hauwezi Kuwatumikia Mabwana Wawili” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 2014.
d MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana benye kumutumainia Yehova biko na mutoto moya tu na bikoko nazungumuza naye. Mutoto wabo iko natumika pamoya na bwana yake ku kazi ya ujenzi wa Jumba ya Ufalme.