Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 5 uku. 26-31
  • Tunaona Jina ya Yehova Kuwa ya Maana Sana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunaona Jina ya Yehova Kuwa ya Maana Sana
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “WATU KWA AJILI YA JINA LAKE”
  • “MUKO MASHAHIDI WANGU”
  • TUNAONA JINA YA YEHOVA KUWA YA MAANA
  • Yesu Anaona Jina ya Yehova Kuwa ya Maana Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • “Musifu Jina la Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • “Muchague . . . Ni Nani Mutatumikia”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 5 uku. 26-31

HABARI YA KUJIFUNZA YA 23

WIMBO 2 Jina Yako Ni Yehova

Tunaona Jina ya Yehova Kuwa ya Maana Sana

“‘Muko mashahidi wangu,’ ni vile Yehova anasema.”—ISA. 43:10.

WAZO KUBWA

Namna tunaweza kusaidia kutakasa jina ya Yehova.

1-2. Nini njo inaonyesha kama Yesu aliona jina ya Yehova kuwa ya maana sana?

YESU anaona jina ya Yehova kuwa ya maana sana. Yeye njo amefanya mambo mingi sana juu ya kujulisha jina ya Yehova. Mu habari yenye ilitangulia tuliona kama Yesu alikuwa tayari kufa juu ya kutakasa na kutetea jina ya Yehova. (Mk. 14:36; Ebr. 10:7-9) Na ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, atakuwa tayari kurudishia Baba yake mamlaka yote juu ya kutukuza jina ya Yehova. (1 Ko. 15:26-28) Mambo yote yenye Yesu amefanya juu ya jina ya Yehova, inaonyesha kama anamupenda sana Baba yake.

2 Yesu alikuya ku dunia mu jina ya Baba yake. (Yoh. 5:43; 12:13) Alijulisha banafunzi yake jina ya Baba yake. (Yoh. 17:6, 26) Alifundisha na kufanya miujiza mu jina ya Yehova. (Yoh. 10:25) Pia aliomba Yehova alinde banafunzi yake kwa “sababu ya jina [lake].” (Yoh. 17:11) Ni wazi kama Yesu aliona jina ya Yehova kuwa ya maana sana. Kwa hiyo, haiwezekane mutu aseme kama ni Mukristo wa kweli lakini hajue jina ya Yehova na haitumikishake.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Juu tuko Bakristo ba kweli tunajikaza kufuata mufano wa Yesu. Na siye tunapenda na kuheshimia jina ya Baba yake. (1 Pe. 2:21) Mu hii habari tutaona juu ya nini Yehova anapatia jina yake bale benye biko natangaza “habari njema ya Ufalme.” (Mt. 24:14) Na tutaona namna kila mumoya wetu anaweza kuonyesha kama anaona jina ya Yehova kuwa ya maana.

“WATU KWA AJILI YA JINA LAKE”

4. (a) Mbele Yesu apande mbinguni aliambia banafunzi yake bafanye nini? (b) Ile inalamusha ulizo gani?

4 Mbele tu Yesu arudie mbinguni aliambia banafunzi yake hivi: “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Ile maneno inaonyesha kama banafunzi ya Yesu bangehubiri habari njema fasi yote, hapana tu mu Israeli. Na batu ya fasi mingi bangefikia kuwa banafunzi ya Yesu. (Mt. 28:19, 20) Lakini juu Yesu alisema, “mutakuwa mashahidi wangu,” je, ile inamaanisha kama banafunzi yake habangekuwa na lazima ya kujua jina ya Yehova, ao kama bangekuwa tu mashahidi wa Yesu? Habari yenye iko mu Matendo sura ya 15 inatusaidia kupata jibu ya ile ulizo.

5. Namna gani mitume na bazee mu Yerusalemu balionyesha kama batu yote banapaswa kujua jina ya Yehova? (Ona pia picha.)

5 Mu mwaka wa 49 K.K.Y., mitume na bazee balikutana Yerusalemu juu ya kuzungumuzia mambo yenye batu ya mataifa benye habatahiriwe balipaswa kufanya juu bakubaliwe kuwa Bakristo. Ku mwisho ya ile mazungumuzo, Yakobo ndugu ya Yesu alisema hivi: “[Petro] ameeleza kikamili namna Mungu kwa mara ya kwanza alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kati yao watu kwa ajili ya jina lake.” Yakobo alikuwa nazungumuzia jina ya nani? Jibu inapatikana mu maneno ya nabii Amosi yenye Yakobo alirudilia. Alisema hivi: “Ili watu wenye wanabakia wamutafute Yehova kwa bidii, pamoja na watu wa mataifa yote, watu wenye wanaitwa kwa jina langu, ni vile Yehova anasema.” (Mdo. 15:14-18) Kwa hiyo, bale banafunzi ba mupya balipaswa kujifunza juu ya Yehova na balipaswa ‘kuitwa kwa jina lake.’ Ni kusema, balipaswa kujulisha bengine ile jina, na batu balipaswa kubajua mu ile jina.

Yakobo iko nazungumuza na mitume na wazee fulani mu Yerusalemu. Bitabu bya kukunjwa bya bandugu bawili biko wazi wakati biko nasikiliza.

Mu mukutano wenye ulifanywa mu karne ya kwanza bandugu ba mu baraza yenye kuongoza balielewa kama Bakristo banapaswa kuitwa mu jina ya Mungu (Ona fungu ya 5)


6-7. (a) Juu ya nini Yesu alikuya ku dunia? (b) Ni jambo ingine gani ya maana zaidi yenye ilipaswa kuhangaikiwa?

6 Jina ya Yesu inamaanisha “Yehova Ni Wokovu.” Ni yeye njo Yehova alitumia juu ya kuokoa banadamu benye kuwa na imani. Yesu alikuya ku dunia juu ya kutoa uzima wake kwa ajili ya banadamu. (Mt. 20:28) Bei ya ukombozi yenye alitoa ilipatia banadamu tumaini ya kuokolewa na kupata uzima wa milele.—Yoh. 3:16.

7 Lakini juu ya nini banadamu balikuwa na lazima ya kuokolewa? Ni juu ya mambo yenye ilipitikanaka mu bustani ya Edeni. Vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, bazazi yetu ba kwanza Adamu na Eva habakumutii Mungu na balipoteza tumaini ya kuishi milele. (Mwa. 3:6, 24) Ni kweli banadamu balikuwa na lazima ya kuokolewa, lakini kulikuwa jambo ingine ya maana zaidi ya kuhangaikia, ni kusema kutakasa jina ya Mungu yenye ilichafuliwa. (Mwa. 3:4, 5) Kuokolewa kwa banadamu kunaenda pamoya na kutakaswa kwa jina ya Yehova, yenye ni jambo ya maana zaidi. Na Yesu njo alistahili kabisa kutakasa jina ya Yehova juu alisema mu jina ya Yehova, na alifanya mambo yote yenye Yehova alimuomba afanye.

Haiwezekane mutu aseme kama ni Mukristo wa kweli lakini hajue jina ya Yehova na haitumikishake.

8. Banafunzi bote ba Yesu banapaswa kujua nini?

8 Banafunzi bote ba Yesu, ikuwe Bayahudi ao Batu ya Mataifa, balipaswa kujua ule mwenye anabapatia wokovu: Yehova Mungu, Baba yake na Yesu. (Yoh. 17:3) Na sawa Yesu, bangeitwa mu jina ya Yehova. Pia, balipaswa kujua kama kutakasa jina ya Yehova ni jambo ya maana sana. Haiwezekane mutu aokolewe kama hatakase jina ya Yehova. (Mdo. 2:21, 22) Kwa hiyo, banafunzi bote baaminifu ba Yesu banapaswa kujifunza juu ya Yehova na juu ya Yesu. Tunaelewa juu ya nini Yesu alimalizia sala yake yenye kuwa mu Yohana 17 na hii maneno: “Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha, ili upendo wenye ulinipenda ukuwe ndani yao na mimi nikuwe katika umoja nao.”—Yoh. 17:26.

“MUKO MASHAHIDI WANGU”

9. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunaona jina ya Yehova kuwa ya maana?

9 Tumeelewa kama Bakristo ba kweli banapaswa kutakasa jina ya Yehova. (Mt. 6:9, 10) Banapaswa kuona jina ya Yehova kuwa ya maana sana kupita majina ingine yote. Na ni mu matendo yabo njo bataonyesha vile. Sasa, tunaweza kufanya mambo gani juu ya kusaidia kutakasa jina ya Yehova, na kuonyesha kama mambo yenye Shetani alisema juu ya Yehova ni ya bongo?

10. Sura ya 42 mupaka 44 ya Isaya inazungumuzia tribinali gani ya mufano? (Isaya 43:9; 44:7-9) (Ona pia picha.)

10 Sura ya 42 mupaka 44 ya kitabu ya Isaya inazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya juu ya kutakasa jina ya Yehova. Zile sura zinazungumuzia tribinali ya mufano. Ku ile tribinali banapenda kujua nani njo Mungu kabisa. Yehova anaambia bale bote benye banajiita kuwa miungu baonyeshe kama ni bamungu kabisa. Pia anasema kama ikiwa kuko mashahidi bakuye batetee miungu yabo. Lakini hakuna hata shahidi moya mwenye anakuya!—Soma Isaya 43:9; 44:7-9.

Picha: Bamalaika biko mu anga yulu ya dunia wakati ndugu na dada ba mu dunia yote biko nafanya mambo mbalimbali juu ya kutakasa jina ya Yehova. 1. Bibi na bwana biko nahubiri ku prezantware. 2. Dada kijana iko napatia mwanafunzi mwenzake karte ya jw.org. 3. Ndugu iko nahubiraa mwanaume fulani mu transport. 4. Maaskari wenye wanavala maske wanafunga ndugu fulani. 5. Dada mwenye iko ku kitanda ya hopitale anaambia munganga uamuzi wake juu ya damu.

Tunaonyesha mu njia za mingi kama tuko namutetea Yehova ku tribinali ya mufano (Ona fungu ya 10-11)


11. Yehova anaambia nini batu yake mu Isaya 43:10-12?

11 Soma Isaya 43:10-12. Yehova anaambia batu yake hivi: “Muko mashahidi wangu, . . . na mimi ni Mungu.” Na anabaambia bajibie hii ulizo: “Je, kuko Mungu mwingine isipokuwa mimi?” (Isa. 44:8) Tuko na pendeleo kubwa sana ya kujibia ile ulizo. Kupitia maneno na matendo yetu, tunaonyesha kama Yehova yeye peke njo Mungu wa kweli. Jina yake iko yulu sana kupita majina ingine yote. Hata Shetani atuletee majaribu gani, tunaonyesha kupitia namna yetu ya kuishi kama tunamupenda sana Yehova na tuko baaminifu kwake. Na wakati tunafanya vile, tunasaidia kutakasa jina ya Yehova.

12. Unabii wenye kuwa mu Isaya 40:3, 5 ulitimia namna gani?

12 Isaya alitabiri pia kama mutu fulani ‘angefungua [ao, ‘kutayarisha’] njia ya Yehova.’ (Isa. 40:3, na maelezo ya chini) Ile ilitimia namna gani? Ilitimia wakati Yohana Mubatizaji alimutayarishia Yesu njia. Lakini ni Yehova njo Yohana alikuwa natayarishia njia juu Yesu alikuya mu jina ya Yehova na alisema mu jina ya Yehova. (Mt. 3:3; Mk. 1:2-4; Lu. 3:3-6) Isaya alitabiri tena hivi: “Utukufu wa Yehova utafunuliwa.” (Isa. 40:5) Utukufu wa Yehova ulifunuliwa namna gani? Wakati Yesu alikuya ku dunia alifunua ao alionyesha muzuri-muzuri Yehova ni mutu wa namna gani. Kwa hiyo, ilikuwa sawa vile ni Yehova yeye peke njo alikuya ku dunia. Na siye wakati tunatetea jina ya Yehova tunamuiga Yesu Kristo.—Yoh. 12:45.

13. Tunaweza kumuiga Yesu namna gani?

13 Kama Yesu, na siye tuko Mashahidi wa Yehova. Tunaitwa mu jina ya Yehova. Na tunaambia batu yote mambo ya ajabu sana yenye amefanya. Lakini juu tukuwe Mashahidi wazuri, tunapaswa pia kuambia batu namna Yesu naye alitakasa jina ya Yehova. (Mdo. 1:8) Yesu njo Shahidi wa kwanza wa Yehova. Na siye tunafuata mufano wake. (Ufu. 1:5) Sasa, kila mumoya wetu anaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama anaona jina ya Yehova kuwa ya maana?

TUNAONA JINA YA YEHOVA KUWA YA MAANA

14. Sawa vile Zaburi 105:3 inaonyesha, tunaona jina ya Yehova namna gani?

14 Tunajisifu juu ya jina ya Yehova. (Soma Zaburi 105:3.) Yehova anafurahi sana wakati tunajisifu juu ya jina yake. (Yer. 9:23, 24; 1 Ko. 1:31; 2 Ko. 10:17) ‘Tunajisifu katika Yehova,’ maana yake tunafurahi sana juu Yehova ni Mungu wetu na tunaona kama ni pendeleo kutukuza jina yake na kuitetea. Hatupaswe kusikia haya ya kuambia batu kama tuko Mashahidi wa Yehova, ikuwe bafanyakazi benzetu, banafunzi benzetu, ao bajirani yetu. Shetani na batu benye anatumikisha banapenda batu basaabu jina ya Yehova. (Yer. 23:26, 27) Njo maana anapenda tuache kuambia bengine juu ya ile jina. (Yer. 11:21; Ufu. 12:17) Lakini juu tunapenda jina ya Yehova tunamusifu “muchana wote.”—Zb. 5:11; 89:16.

15. Kuitia jina ya Yehova maana yake nini?

15 Tunaendelea kuitia jina ya Yehova. (Yo. 2:32; Ro. 10:13, 14) Kuitia jina ya Yehova haiko tu kujua jina yake na kuitumikisha. Lakini inamaanisha kumujua muzuri kabisa, kumutegemea, na kutafuta musaada wake na muongozo wake. (Zb. 20:7; 99:6; 116:4; 145:18) Kuitia jina ya Yehova inamaanisha pia kuambia bengine jina yake na sifa zake, na kubasaidia babadilishe maisha yabo juu bamufurahishe Yehova na baokolewe.—Isa. 12:4; Mdo. 2:21, 38.

16. Tunaweza kuonyesha namna gani kama Shetani ni musema-bongo?

16 Tuko tayari kuteseka juu ya jina ya Yehova. (Yak. 5:10, 11) Wakati tunaendelea kuwa baaminifu kwa Yehova hata mu mateso, tunaonyesha kama Shetani ni musema-bongo. Mu wakati wa Yobu, Shetani alisema hivi juu ya batu yote benye banamutumikia Yehova: “Mutu atatoa kila kitu chenye iko nacho ili aokoe uzima wake.” (Yob. 2:4) Shetani alipenda kusema kama batu batamutumikia Yehova wakati tu mambo inaendeka muzuri, lakini bakipata magumu batamuacha. Juu Yobu alibakia muaminifu, alionyesha kama ile mashitaka ni ya bongo. Na siye leo tuko na nafasi ya kuonyesha kama hata Shetani atuletee magumu gani, hatutamuacha Yehova. Kwa hiyo, tukuwe hakika kama Yehova ataendelea kutulinda kwa sababu ya jina yake.—Yoh. 17:11.

17. Sawa vile 1 Petro 2:12 inaonyesha, tunaweza kufanya nini juu ya kutukuza jina ya Yehova?

17 Tunaheshimia jina ya Yehova. (Mez. 30:9; Yer. 7:8-11) Juu tunaitwa mu jina ya Yehova, mambo yenye tunafanya inaweza kuwa na matokeo juu ya ile jina; tunaweza kuiheshimisha ao kuizaraulisha. (Soma 1 Petro 2:12.) Njo maana tunafanya yetu yote juu mambo yote yenye tunasema na kufanya iletee sifa jina ya Yehova. Hata kama hatukamilike, tukijikaza kufanya vile tutatukuza jina ya Yehova.

18. Ni mu njia gani ingine tunaweza kuonyesha kama tunaona jina ya Yehova kuwa ya maana? (Ona pia maelezo ya chini.)

18 Kuliko kuhangaikia vile batu banatuona, tunahangaikia zaidi jina ya Yehova. (Zb. 138:2) Juu ya nini? Juu mara mingi wakati tunafanya mambo ya kumufurahisha Yehova, batu banatusemaka mubaya.a Ile ilifikiaka Yesu naye. Mu wakati wake, ilikuwa jambo ya haya sana kuhukumiwa kuwa mutenda-maovu. Lakini Yesu aliitika kufa ile kifo ya haya sana juu tu ya kutukuza jina ya Yehova. ‘Alizarau haya,’ ni kusema hakuhangaikia sana namna bengine batamuona. (Ebr. 12:2-4) Jambo yenye alihangaikia sana ni kufanya mapenzi ya Mungu.—Mt. 26:39.

19. Unaona jina ya Yehova namna gani, na juu ya nini?

19 Tunapenda sana jina ya Yehova na tunaona kama ni pendeleo kuitwa Mashahidi wa Yehova. Juu tunapenda sana jina ya Yehova tunaendelea kumusifu hata wakati bengine banatuzarau. Kuliko kuhangaikia vile batu batatuona, tunahangaikia zaidi jina ya Yehova. Kwa hiyo, tuazimie kuendelea kusifu jina ya Yehova hata Shetani atuletee magumu gani. Kama tunafanya vile, tutaonyesha kama, sawa vile Yesu, na siye tunaona jina ya Yehova kuwa ya maana sana.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Nini inaonyesha kama banafunzi ya Yesu banaona jina ya Yehova kuwa ya maana sana?

  • Tunapaswa kutetea nini ku tribinali ya mufano leo?

  • Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona jina ya Yehova kuwa ya maana?

WIMBO 10 Tumusifu Yehova Mungu Wetu!

a Yobu, mutumishi muaminifu wa Yehova, alianza kuhangaikia sana namna bengine balimuona wakati barafiki yake batatu balisema kama alifanya jambo fulani ya mubaya. Ku mwanzo wakati Yobu alipoteza bitu yake yote, na batoto yake bote bakakufa, “hakutenda zambi kwa midomo yake.” (Yob. 1:22; 2:10) Lakini wakati barafiki yake balisema kama alifanya jambo fulani ya mubaya, alianza “mazungumuzo ya ovyoovyo.” Alijitetea kuliko kutakasa jina ya Mungu.—Yob. 6:3; 13:4, 5; 32:2; 34:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine