Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 6 uku. 2-7
  • Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 1

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 1
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • RUBENI
  • SIMEONI NA LAWI
  • YUDA
  • Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 2
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Yakobo na Esau Wanasikilizana
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 6 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 24

WIMBO 98 Kila Andiko Limeongozwa na Roho ya Mungu

Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 1

“Mujikusanye pamoja ili niwaambie mambo yenye yatawapata katika kipindi cha mwisho cha zile siku.”—MWA. 49:1.

WAZO KUBWA

Mambo yenye tunajifunza wakati tunachunguza mambo yenye Yakobo alitabiri juu ya Rubeni, Simeoni, Lawi, na Yuda wakati alikaribia kufa.

1-2. Wakati Yakobo alikaribia kufa alifanya nini, na juu ya nini? (Ona pia picha ku.)

WAKATI Yakobo alikuwa alishazeeka sana, alitoka Kanaani na kuenda Misri pamoya na familia yake yote. Kule aliendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka 17. (Mwa. 47:28) Mu ile kipindi, alifurahi kukutana tena na mutoto yake Yosefu na kuona familia yake yote inakuwa tena fasi moya. Lakini sasa Yakobo anaona kama anakaribia kufa. Kwa hiyo anaita batoto yake bote juu abaambie mambo fulani ya maana.—Mwa. 49:28.

2 Zamani, ilikuwa jambo ya kawaida baba wa familia aite batu yote ba familia yake juu ya kubapatia maagizo ya mwisho wakati aliona kama anakaribia kufa. (Isa. 38:1) Mu ile mazungumuzo, inawezekana baba alikuwa nasema pia ni nani njo ataongoza familia kisha yeye kufa.

Yakobo iko ku kitanda, iko natoa unabii kuhusu batoto yake 12 mbele akufe (Ona fungu ya 1-2)


3. Kulingana na Mwanzo 49:1, 2, juu ya nini maneno ya Yakobo ni ya pekee?

3 Soma Mwanzo 49:1, 2. Lakini mazungumuzo yenye Yakobo anakaribia kufanya na batoto yake ni ya pekee. Iko tofauti na mazungumuzo yenye kwa kawaida baba anafanya na batoto yake mbele akufe. Yakobo alikuwa nabii. Yehova alimuongoza aseme mambo ya maana yenye ingefikia batoto yake na bazao yao. Maneno yenye Yakobo aliambia batoto yake mbele akufe ni unabii.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari? (Ona pia kisanduku “Familia ya Yakobo.”)

4 Mu hii habari, tutaona mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake ine: Rubeni, Simeoni, Lawi, na Yuda. Mu habari ya kufuata tutaona mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake bengine munane. Sawa vile tutaona, mambo yenye Yakobo alisema haikuhusu tu batoto yake, lakini ilihusu pia bazao yao benye bangefikia kufanyiza taifa ya Israeli ya zamani. Kuchunguza mambo yenye ilifikia taifa ya Israeli itatusaidia kuona waziwazi namna maneno ya Yakobo ilitimia. Na wakati tutakuwa nachunguza maneno ya Yakobo, tutajifunza mambo ya maana yenye itatusaidia tumufurahishe Yehova Baba yetu wa mbinguni.

Muchoro yenye inaonyesha familia ya Yakobo. Yakobo iko na babibi bawili, Lea na Raheli, na babibi bengine bawili, Bilha na Zilpa. Batoto ya Lea ni Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni, na Dina. Batoto ya Raheli ni Yosefu na Benyamini. Batoto ya Bilha ni Dani na Naftali. Batoto ya Zilpa ni Gadi na Asheri.

RUBENI

5. Pengine Rubeni aliwaza kama baba yake atamupatia mapendeleo gani?

5 Yakobo anaanza na Rubeni. Anamuambia hivi: “Wewe ni muzaliwa wangu wa kwanza.” (Mwa. 49:3) Juu Rubeni alikuwa muzaliwa wa kwanza, pengine aliwaza kama yeye njo atariti bitu mingi kupita badogo yake. Pengine aliwaza pia kama yeye njo angeongoza familia kisha kifo ya baba yake, na kama ile pendeleo ingeendelea kati ya bazao yake.

6. Juu ya nini Rubeni alipoteza haki yake ya muzaliwa wa kwanza? (Mwanzo 49:3, 4)

6 Lakini, Rubeni alipoteza haki yake ya muzaliwa wa kwanza. (1 Ny. 5:1) Juu ya nini? Miaka fulani mbele ya pale alifanya ngono pamoya na Bilha, bibi mwingine wa Yakobo. Bilha alikuwa mutumishi mwanamuke wa Raheli, bibi mupendwa wa Yakobo mwenye alikuwa amekufa. (Mwa. 35:19, 22) Rubeni alikuwa mutoto wa Lea, bibi mwingine wa Yakobo. Kwa hiyo, inawezekana Rubeni alilala na Bilha juu Yakobo asimupende sana Bilha kupita mama yake Lea. Ao pengine Rubeni alishindwa kuzuia tamaa yake ya ngono. Ikuwe ni sababu gani ilimuchochea atende vile, jambo yenye alifanya ilimuhuzunisha sana Yehova na ilimuhuzunisha sana baba yake.—Soma Mwanzo 49:3, 4.

7. Nini njo ilifikia Rubeni na bazao yake? (Ona pia kisanduku “Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe.”)

7 Yakobo alimuambia Rubeni hivi: “Hautakuwa mukubwa.” Ile maneno ilitimia. Hakuna fasi mu Biblia kwenye banaonyesha kama muzao wa Rubeni alifikia kuwa mufalme, kuhani ao nabii. Hata vile Yakobo hakusema kama Rubeni haiko tena mutoto yake, na bazao ba Rubeni balifikia kuwa moya kati ya makabila ya Israeli. (Yos. 12:6) Mu hali zingine Rubeni alionyesha sifa za muzuri, na hakuna kwenye Biblia inasema kama alifanyaka tena uasherati.—Mwa. 37:20-22; 42:37.

Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe

Rubeni.

Mutoto

Rubeni

Unabii

“Hautakuwa mukubwa.”—Mwa. 49:4.

Namna ilitimia

Hakuna hata mutu moya mu kabila ya Rubeni mwenye alifikia kutawala mu taifa ya Israeli.—1 Ny. 5:1, 2.

8. Habari ya Rubeni inatufundisha nini?

8 Tunajifunza nini? Tunapaswa kujikaza kukomalisha sifa ya kujizuia na kuepuka kabisa mwenendo muchafu. Kama tunajaribiwa kufanya zambi, tufikirie namna matendo yetu itaumiza Yehova, batu ya familia yetu, na bengine. Tunapaswa pia kukumbuka kama “kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.” (Gal. 6:7) Mambo yenye ilimufikia Rubeni inatukumbusha pia kama Yehova iko na rehema. Ni kweli kama Yehova hatatulinda juu tusipate matokeo ya mubaya ya makosa yetu. Lakini kama tunajikaza kufanya mambo ya muzuri, atatusamehe na atatubariki.

SIMEONI NA LAWI

9. Juu ya nini Simeoni na Lawi habakumufurahisha Yakobo? (Mwanzo 49:5-7)

9 Soma Mwanzo 49:5-7. Kisha Yakobo anazungumuza na Simeoni na Lawi, na maneno yenye anabaambia inaonyesha kama habakumufurahisha. Miaka fulani mbele ya pale, mwanaume Mukanaani mwenye kuitwa Shekemu alilala kinguvu Dina dada yabo. Ile jambo ilikasirisha sana batoto bote ba Yakobo. Lakini Simeoni na Lawi balishindwa kuzuia kasirani yabo. Balitenda kwa ujanja. Baliambia Shekemu na batu yake kama ikiwa banaume bote banaitika kutahiriwa, batafanya amani pamoya nabo, na bale banaume baliitika. Wakati bale banaume balikuwa bangali na maumivu ya kutahiriwa, Simeoni na Lawi ‘bakakamata kila mumoja upanga wake na kuingia kwa uficho katika muji na bakamuua kila mwanaume.’—Mwa. 34:25-29.

10. Mambo yenye Yakobo alitabiri juu ya Simeoni na Lawi ilitimia namna gani? (Ona pia kisanduku “Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe.”)

10 Yakobo alihuzunika sana juu ya mambo yenye Simeoni na Lawi balifanya. Alitabiri kama batatawanyika mu Israeli yote. Ile maneno ilitimia kisha zaidi ya miaka 200 wakati taifa ya Israeli iliingia mu Inchi ya Ahadi. Kabila ya Simeoni ilipewa miji fulani mu eneo ya kabila ya Yuda, lakini ile miji haikukuwa fasi moya. (Yos. 19:1) Na kabila ya Lawi ilipewa miji 48 yenye ilikuwa fasi mbalimbali mu Israeli.—Yos. 21:41.

Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe

Simeoni.

Mutoto

Simeoni

Unabii

“Niwatawanye katika Yakobo.”—Mwa. 49:7.

Namna ilitimia

Kabila ya Simeoni iliriti miji fulani mu eneo ya kabila ya Yuda, lakini ile miji haikukuwa fasi moya.—Yos. 19:1-8.

Lawi.

Mutoto

Lawi

Unabii

“Niwasambaze katika Israeli.”—Mwa. 49:7.

Namna ilitimia

Kabila ya Lawi ilipewa miji 48 yenye ilikuwa fasi mbalimbali mu Israeli.—Yos. 21:41.

11. Kabila ya Simeoni na ya Lawi ilifanya mambo gani ya muzuri?

11 Bazao ya Simeoni na ya Lawi habakurudilia makosa yenye baba zao walifanyaka. Kabila ya Lawi ilishikamana kabisa na ibada safi. Wakati Musa alienda ku Mulima Sinai kukamata Sheria ya Yehova, Baisraeli mingi balianza kuabudu kitoto cha ngombe. Lakini Balawi habakufanya vile na balisaidia Musa kuharibu benye baliabudu ile sanamu. (Kut. 32:26-29) Yehova alichagua banaume ba mu kabila ya Lawi juu bakuwe makuhani mu Israeli. (Kut. 40:12-15; Hes. 3:11, 12) Kisha, wakati Baisraeli balikuwa nakamata Inchi ya Ahadi, kabila ya Simeoni ilisaidia kabila ya Yuda kufukuza Bakanaani, sawa vile Yehova aliomba bafanye.—Amu. 1:3, 17.

12. Habari ya Simeoni na Lawi inakufundisha nini?

12 Tunajifunza nini? Kasirani inaweza kufanya mutu akamate maamuzi fulani ao afanye mambo fulani. Lakini siye tunapaswa kujikaza kuzuia kasirani yetu. Kama banatutendea mubaya, ao banatendea mubaya mutu mwenye tunapenda, ni jambo ya kawaida kukasirika. (Zb. 4:4) Lakini tunapaswa kukumbuka kama Yehova hatafurahi kama kasirani inatusukuma tuseme ao tutendee mutu mambo ya mubaya. (Yak. 1:20) Wakati banatufanyia mambo ya mubaya, ikuwe mu kutaniko ao inje ya kutaniko, tunapaswa kutenda mu njia yenye itamufurahisha Yehova. Ile itatusaidia tuepuke kusema ao kufanya mambo yenye itaumiza bengine. (Ro. 12:17, 19; 1 Pe. 3:9) Jambo ingine yenye tunajifunza ni hii: Kama bazazi yako biko nafanya mambo yenye haimufurahishe Yehova, ukumbuke kama haulazimike kufuata mufano yao. Usiwaze kama hautaweza kumufurahisha Yehova. Yehova atakusaidia juu uweze kufanya mambo ya muzuri na atakubariki.

YUDA

13. Juu ya nini pengine Yuda alikuwa na wasiwasi wakati baba yake alianza kuzungumuza naye?

13 Sasa Yakobo anaanza kuzungumuza na Yuda. Kisha kusikia mambo yenye Yakobo aliambia bakubwa yake, pengine Yuda alikuwa na wasiwasi juu naye alifanyaka makosa makubwa. Inawezekana alisaidiaka ndugu zake kunyanganya bitu mu muji wa Shekemu. (Mwa. 34:27) Pia, yeye na ndugu zake baliuzisha Yosefu mu utumwa na bakasikilizana juu ya kudanganya baba yao. (Mwa. 37:31-33) Kisha alifanya ngono na Tamari, bibi ya mutoto yake, juu aliwaza kama alikuwa kahaba.—Mwa. 38:15-18.

14. Yuda alifanya mambo gani ya muzuri? (Mwanzo 49:8, 9)

14 Lakini, kwa muongozo ya roho ya Mungu, Yakobo alisema tu mambo ya muzuri juu ya Yuda na kumubariki. (Soma Mwanzo 49:8, 9.) Yuda alionyesha kama alihangaikia sana baba yake mwenye alikuwa alishazeeka, na alionyesha kama alisikilia huruma ndugu yake Benyamini.—Mwa. 44:18, 30-34.

15. Baraka zenye Yakobo alitabiri juu ya Yuda zilitimia namna gani?

15 Yakobo alitabiri kama Yuda ataongoza bandugu yake. Lakini ilikamata wakati juu ule unabii utimie. Miaka 200 hivi kisha pale, njo Biblia inazungumuzia kwa mara ya kwanza namna ule unabii ulianza kutimia. Kisha Waisraeli kukombolewa kutoka Misri, walisafiri mu jangwa juu ya kuenda mu Inchi ya Ahadi. Kabila ya Yuda njo ilikuwa mbele, na makabila ingine ilikuwa naifuata. (Hes. 10:14) Kisha miaka, Yehova aliomba kabila ya Yuda njo ikuwe mbele juu ya kupigana na kukamata Inchi ya Ahadi. (Amu. 1:1, 2) Na Daudi alikuwa mufalme wa kwanza kutoka mu kabila ya Yuda, na kisha yeye kulikuwa wafalme wengine wengi wenye walitoka mu kabila ya Yuda. Lakini ule unabii juu ya Yuda ulitimia pia mu njia zingine.

16. Unabii wenye kuwa mu Mwanzo 49:10 ulitimia namna gani? (Ona pia kisanduku “Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe.”)

16 Yakobo alitabiri pia kama Mutawala wa wanadamu wote atakuwa muzao wa Yuda na atatawala milele. (Soma Mwanzo 49:10 na maelezo ya chini.) Ule Mutawala ni Yesu Kristo, na Yakobo alimuita Shilo. Malaika alisema hivi juu ya Yesu: “Yehova Mungu atamupatia kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Lu. 1:32, 33) Pia, Yesu anaitwa “Simba wa kabila la Yuda.”—Ufu. 5:5.

Mambo Yenye Yakobo Alitabiri Mbele Akufe

Yuda.

Mutoto

Yuda

Unabii

“Fimbo ya ufalme haitatoka kwa Yuda . . . mupaka wakati Shilo atakuja.”—Mwa. 49:10.

Namna ilitimia

Yesu, muzao wa Yuda, alifikia kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu.—Lu. 1:32, 33.

17. Namna gani tunaweza kumuiga Yehova mu namna yetu ya kuona bengine?

17 Tunajifunza nini? Yehova alibariki Yuda hata kama alifanya makosa fulani makubwa. Lakini pengine bandugu ya Yuda balijiuliza juu ya nini Yehova alimubariki vile. Hatujue baliwaza nini, lakini tunajua kama Yehova aliona mambo fulani ya muzuri mu moyo wa Yuda na alimubariki juu ya ile mambo. Namna gani tunaweza kumuiga Yehova? Wakati Mukristo mwenzetu anapata pendeleo fulani ya pekee, tunaweza kuanza kukazia akili makosa yake. Lakini ni muzuri tukumbuke kama Yehova anafurahia sifa za muzuri za ule Mukristo. Yehova anatafutaka mambo ya muzuri kwa waabudu wake. Na siye tujikaze kufanya vile.

18. Juu ya nini ni lazima tukuwe wavumilivu?

18 Habari ya Yuda inatufundisha pia kama ni lazima tukuwe wavumilivu. Yehova anatimizaka mambo yote yenye anaahidi. Lakini haiko kila mara njo anaitimizaka mu wakati wenye siye tulitazamia ao mu njia yenye siye tuliwazia. Batu ya kwanza-kwanza benye baliongoza taifa ya Israeli habakutokaka mu kabila ya Yuda. Kwa mufano, Musa alikuwa Mulawi, Yoshua alikuwa Muefraimu, na Mufalme Sauli alikuwa Mubenyamini. Lakini bazao ba Yuda balitegemeza kwa ushikamanifu bale banaume benye Yehova aliweka. Ni siye tutegemeze mutu yeyote mwenye Yehova anaweka juu ya kutuongoza leo.—Ebr. 6:12.

19. Mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake mbele akufe inatufundisha nini juu ya Yehova?

19 Maneno ya mwisho yenye Yakobo aliambia batoto yake ine mbele akufe inatufundisha nini? Ni wazi kama “Mungu haone kama vile mwanadamu anaona.” (1 Sa. 16:7) Yehova ni muvumilivu sana na iko tayari kusamehe. Ni kweli Yehova haachiliake matendo ya mubaya, lakini hatazamie batumishi yake bakuwe bakamilifu. Anaweza hata kubariki batu benye balifanyaka makosa makubwa zamani kama tu banatubu na banaanza kufanya mambo ya muzuri. Mu habari yenye kufuata tutaona mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake bengine munane.

TUNAJIFUNZA NINI WAKATI TUNACHUNGUZA MAMBO YENYE YAKOBO ALIAMBIA . . .

  • Rubeni?

  • Simeoni na Lawi?

  • Yuda?

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine