Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 6 uku. 20-25
  • Saidia Banafunzi ya Biblia Baanze Kumutumikia Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Saidia Banafunzi ya Biblia Baanze Kumutumikia Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SAIDIA MWANAFUNZI AJUE NINI INAMUZUIA KUFANYA MAENDELEO
  • SAIDIA MWANAFUNZI AMUPENDE YEHOVA ZAIDI
  • SAIDIA MWANAFUNZI ATIE YEHOVA FASI YA KWANZA
  • SAIDIA MWANAFUNZI APAMBANE NA UPINZANI
  • ONYESHA KAMA UNATUMAINIA MWANAFUNZI
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • “Kwa Hiyo, Muende, na Mufanye Wanafunzi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 6 uku. 20-25

HABARI YA KUJIFUNZA YA 27

WIMBO 79 Tuwafundishe Wakuwe na Imani Yenye Nguvu

Saidia Banafunzi ya Biblia Baanze Kumutumikia Yehova

“Musimame imara katika imani . . . Muendelee kuwa na ujasiri.”—1 KO. 16:13, maelezo ya chini.

WAZO KUBWA

Namna tunaweza kusaidia banafunzi ya Biblia bakuwe na imani ya nguvu na uhodari juu baweze kufanya mabadiliko na baanze kumutumikia Yehova.

1-2. (a) Juu ya nini banafunzi fulani ba Biblia banaogopa kuwa Mashahidi? (b) Tutaona nini mu hii habari?

NA WEYE ulikuwa naogopa kuwa Shahidi wa Yehova? Pengine uliogopa kama bafanyakazi benzako, batu ya familia yako, ao banafunzi benzako batakugeukia. Ao pengine ulikuwa nawaza hautaweza kutii mambo yote yenye Yehova anakulomba. Kama ni vile, unaweza kuelewa muzuri banafunzi ba Biblia benye banaogopa kuwa Mashahidi wa Yehova.

2 Yesu alijua kama boga ya vile inaweza kuzuia mutu kufanya maendeleo ya kiroho. (Mt. 13:20-22) Lakini aliendelea kusaidia bale benye balikuwa na boga ya kumufuata. Na alionyesha banafunzi yake namna ya kusaidia batu benye biko na boga (1) bajue nini njo inabazuia kufanya maendeleo, (2) bamupende Yehova zaidi, (3) batie kazi ya Yehova fasi ya kwanza mu maisha yabo, na (4) bajue mambo ya kufanya wakati bengine banabapinga. Wakati tuko natumikisha kitabu Furahia Maisha Milele, namna gani tunaweza kutumikisha ile mambo ine juu ya kusaidia mwanafunzi aamue kuanza kumutumikia Yehova?

SAIDIA MWANAFUNZI AJUE NINI INAMUZUIA KUFANYA MAENDELEO

3. Pengine nini ilimuzuia Nikodemu kuwa mwanafunzi wa Yesu?

3 Nikodemu alikuwa na mamlaka kati ya Bayahudi. Miezi sita tu kisha Yesu kuanza utumishi wake, Nikodemu alitambua kama Yesu njo Masiya mwenye Mungu alituma. (Yoh. 3:1, 2) Lakini kuko kitu yenye ilikuwa namuzuia kuwa mwanafunzi wa Yesu, ‘aliogopa Bayahudi.’ Njo maana aliamua kukutana na Yesu mu uficho. (Yoh. 7:13; 12:42) Pengine Nikodemu aliogopa kama atapoteza cheo yake na bitu yake fulani kama anakuwa mwanafunzi wa Yesu.a

4. Namna gani Yesu alisaidia Nikodemu aelewe mambo yenye Mungu alipenda afanye?

4 Nikodemu alijua Sheria ya Musa, lakini alikuwa na lazima ya kuelewa mambo yenye Yehova alipenda afanye. Yesu alimusaidia namna gani? Yesu alitoa wakati yake juu ya kumusaidia. Alikuwa hata tayari kukutana naye busiku. Na alimuambia waziwazi mambo yenye alipaswa kufanya juu akuwe mwanafunzi wake. Alimuambia atubu zambi zake, abatizwe mu mayi, na amuamini Mwana wa Mungu.—Yoh. 3:5, 14-21.

5. Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia mwanafunzi atambue mambo yenye iko namuzuia kufanya maendeleo?

5 Hata kama mwanafunzi wa Biblia anaelewa muzuri Maandiko, anaweza kuwa na lazima ya musaada juu ya kujua ni nini iko namuzuia kufanya maendeleo. Kazi ao upinzani wa batu ya familia, inaweza kumuzuia kufanya maendeleo ya kiroho. Kwa hiyo, ukuwe pale juu ya kumusaidia. Unaweza kumualika ku nyumba, munakula pamoya, na kisha unamusindikiza saa anaanza kurudia. Kuzungumuza naye wakati ya vile, yenye haiko saa ya kujifunza, inaweza kufanya ajisikie huru kueleza mambo yenye iko namuhangaisha. Umutie moyo afanye mabadiliko juu anamupenda Yehova, hapana juu anapenda kukufurahisha.

6. Unaweza kusaidia namna gani mwanafunzi wa Biblia apate nguvu ya kutumikisha mambo yenye iko najifunza? (1 Wakorinto 16:13)

6 Wakati mwanafunzi wa Biblia iko hakika kama Yehova atamusaidia kutii kanuni za Biblia, atapata nguvu ya kutumikisha mambo yenye iko najifunza. (Soma 1 Wakorinto 16:13.) Weye muhubiri uko sawa mwalimu ku masomo. Mwalimu muzuri anafundishaka mwanafunzi namna ya kufanya jambo fulani. Zaidi ya ile, anamusaidiaka akuwe hakika kama iko na uwezo wa kufanya ile jambo. Na weye wakati uko nafundisha mwanafunzi Biblia, usimufundishe tu mambo yenye Mungu anapenda tufanye. Lakini umusaidie pia akuwe hakika kama kwa musaada wa Yehova, ataweza kufanya mabadiliko mu maisha yake. Utafanya vile namna gani?

SAIDIA MWANAFUNZI AMUPENDE YEHOVA ZAIDI

7. Yesu alisaidia namna gani benye balikuwa namusikiliza bamupende Yehova zaidi?

7 Yesu alijua kama ikiwa banafunzi yake banapenda sana Mungu, batapata nguvu ya kutumikisha mambo yenye alibafundisha. Mara mingi Yesu alibafundisha mambo yenye ingebasaidia bamupende sana Baba yabo wa mbinguni. Kwa mufano, Yesu alisema kama Yehova iko sawa baba mwenye anapatiaka batoto yake mambo ya muzuri. (Mt. 7:9-11) Inawezekana bamoya kati ya benye balikuwa namusikiliza Yesu, balikomalia mu familia yenye baba hakukuwa na upendo. Wazia namna balijisikia wakati Yesu alibafasiria mufano wa baba mwenye huruma mwenye alikaribisha mutoto wake mwenye alirudia ku nyumba kisha kuishi maisha ya mubaya. Ile mufano ilibasaidia baone kama Yehova anapenda sana batoto yake ba ku dunia, na anabasikiliaka huruma.—Lu. 15:20-24.

8. Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wa Biblia amupende Yehova zaidi?

8 Juu umusaidie mwanafunzi wa Biblia amupende sana Yehova, zungumuzia sana sifa za Yehova wakati muko najifunza. Kila wakati munajifunza, umusaidie aone namna mambo yenye muko najifunza inaonyesha kama Yehova anatupenda. Kwa mufano, wakati muko nazungumuzia bei ya ukombozi umusaidie kuelewa kama Yehova alitoa Mwana wake kwa ajili yake. (Ro. 5:8; 1 Yo. 4:10) Kama mwanafunzi anaelewa kama Yehova anamupenda yeye kipekee, ile inaweza kufanya upendo wake kwa Yehova uongezeke.—Gal. 2:20.

9. Ni nini ilimuchochea Michael abadilishe maisha yake?

9 Fikiria mufano wa Michael wa mu Indonesia. Alijifunza kweli wakati alikuwa mutoto, lakini hakubatizwa. Wakati alikuwa na miaka 18, alihamia mu inchi ingine na akaanza kufanya kazi ya kutembeza magari ya kabambi-kabambi. Kisha wakati, alioa. Lakini aliacha familia yake mu Indonesia na akaendelea kutumikia mu inchi ingine. Mu ile wakati bibi yake na mutoto wake balianza kujifunza Biblia na kufanya maendeleo. Kisha kifo ya mama yake, Michael aliamua kurudia Indonesia juu ya kuhangaikia baba yake. Kisha akaanza tena kujifunza Biblia. Kuko kitu yenye ilimugusa sana. Wakati balikuwa najifunza sehemu, “Tujifunze Mambo Mingi Zaidi” ya mu somo ya 27 ya kitabu Furahia Maisha Milele!, machozi ilimutoka saa alifikiria namna Yehova alijisikia wakati aliona vile Mwana wake iko nateseka. Ile ilimufanya akuwe mwenye shukrani sana juu ya bei ya ukombozi, na ilimuchochea abadilishe maisha yake na abatizwe.

SAIDIA MWANAFUNZI ATIE YEHOVA FASI YA KWANZA

10. Namna gani Yesu alisaidia banafunzi yake ba kwanza-kwanza batie kazi ya kuhubiri fasi ya kwanza? (Luka 5:5-11) (Ona pia picha.)

10 Banafunzi ya kwanza-kwanza ba Yesu balielewa bila kukawia kama Yesu alikuwa Masiya. Lakini balikuwa na lazima ya musaada juu ya kuelewa kama balipaswa kutia kazi ya kuhubiri fasi ya kwanza mu maisha yabo. Kwa mufano Petro na Andrea balikuwa tayari banafunzi ya Yesu wakati Yesu alibaambia baanze sasa kumufuata kila wakati. (Mt. 4:18, 19) Balikuwa nafanya kazi ya kuloba samaki na kazi yabo ilikuwa naendeka muzuri. Na inawezekana balikuwa natumika pamoya na Yakobo na Yohana. (Mk. 1:16-20) Wakati Petro na Andrea ‘baliacha nyavu zao,’ juu ya kumufuata Yesu, inawezekana balikamata mipango juu familia yabo isikose mambo ya lazima. Nini njo ilibachochea baache kazi yabo na batie kazi ya kuhubiri fasi ya kwanza mu maisha yabo? Habari yenye kuwa mu kitabu ya Luka inaonyesha kama Yesu alifanya muujiza wenye ulibasaidia bakuwe hakika kama Yehova atabatimizia mahitaji yabo.—Soma Luka 5:5-11.

Petro na Andrea banaacha mutubwi yabo ya kuloba samaki wakati Yesu anabaambia ba mufuate. Banaume bengine banabakia mu mutumbwi na biko natayarisha wavu.

Namna Yesu alisaidia banafunzi yake batie kazi ya Yehova fasi ya kwanza inatufundisha nini? (Ona fungu ya 10)b


11. Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia mwanafunzi akuwe na imani ya nguvu?

11 Ni kweli hatuwezi kufanya miujiza sawa Yesu. Lakini tunaweza kumuelezea mwanafunzi mifano yenye inaonyesha namna Yehova anategemeza benye banamutia fasi ya kwanza mu maisha yabo. Kwa mufano, unakumbuka namna Yehova alikusaidia wakati ulianza kuenda ku mikutano? Pengine iliomba uzungumuze na mukubwa wako wa kazi juu ya kumufasiria kama siku ya mikutano hautakuwa natumika kisha saa za kazi. Umufasirie mwanafunzi namna imani yako ilitiwa nguvu wakati uliona vile Yehova alikutegemeza juu uliamua kumutia fasi ya kwanza.

12. (a) Juu ya nini ni muzuri ulombe ndugu na dada mbalimbali bakusindikize wakati unaenda kujifunza na mwanafunzi? (b) Namna gani unaweza kutumikisha video wakati uko najifunza na mwanafunzi? Toa mufano.

12 Kitu ingine yenye itasaidia mwanafunzi, ni kusikia namna Bakristo bengine balifanya mabadiliko juu baweze kumutia Yehova fasi ya kwanza mu maisha yabo. Kwa hiyo, omba bahubiri mbalimbali bakusindikize wakati unaenda kujifunza naye. Ubaombe baambie mwanafunzi namna balipata kweli, na mambo yenye balifanya juu ya kutia kazi ya Yehova fasi ya kwanza. Tena wakati muko najifunza, muangalie pamoya na mwanafunzi mavideo yenye iko mu sehemu “Tujifunze Mambo Mingi Zaidi” ao mu sehemu “Habari Zingine” ya mu kitabu Furahia Maisha Milele! Kwa mufano, kisha kuangalia video Yehova Atatupatia Mambo Yenye Tuko Nayo Lazima yenye kuwa mu somo ya 37, muizungumuzie na usaidie mwanafunzi wako aelewe kama Yehova atamusaidia kama anamutia fasi ya kwanza.

SAIDIA MWANAFUNZI APAMBANE NA UPINZANI

13. Yesu alitayarisha namna gani banafunzi yake juu ya upinzani yenye ingebapata?

13 Yesu aliambia mara mingi banafunzi yake kama batapata upinzani, na ile upinzani ingetoka hata ku batu ya familia. (Mt. 5:11; 10:22, 36) Wakati alikaribia kufa, aliambia banafunzi yake kama banaweza hata kuuawa kwa sababu ya imani yao. (Mt. 24:9; Yoh. 15:20; 16:2) Alibaambia bakuwe baangalifu mu mahubiri. Alibashauria basibishane na benye kubapinga na baendelee kuwa baangalifu mu mambo yenye banasema na kufanya juu baendelee kuhubiri.

14. Namna gani tunaweza kusaidia mwanafunzi akuwe tayari juu ya upinzani? (2 Timoteo 3:12)

14 Ni muzuri kuambia mwanafunzi mbele ya wakati kama atapata upinzani. Ile itamusaidia akuwe tayari wakati upinzani itafika. Tunaweza kumutayarisha kwa kumuambia mambo yenye bafanyakazi benzake, barafiki, ao batu ya familia banaweza kusema ao kufanya. (Soma 2 Timoteo 3:12.) Bafanyakazi benzake banaweza kuanza kumucheka juu iko najikaza kutumikisha mambo yenye iko najifunza mu Biblia. Batu bengine ao hata batu ya familia banaweza kusema mubaya juu ya mambo yenye anaamini.

15. Nini njo inaweza kusaidia mwanafunzi wa Biblia avumilie upinzani ya batu ya mu familia yake?

15 Kama mwanafunzi iko napata upinzani kutoka ku batu ya familia yake, umusaidie afikirie sababu zenye pengine zinafanya batu ya familia yake bamupinge. Pengine batu ya familia yake banawaza kama Mashahidi wa Yehova biko namudanganya, ao ni batu babaya. Hata batu ya mu familia ya Yesu habakufurahia mambo yenye alikuwa anafanya. (Mk. 3:21; Yoh. 7:5) Kwa hiyo, saidia mwanafunzi aendelee kuwa muvumilivu na azungumuze na bengine kwa upole, hata batu ya familia yake.

16. Tunaweza kusaidia namna gani mwanafunzi wa Biblia ahubirie bengine mu njia ya muzuri?

16 Kama mutu wa familia anaitika kusikiliza, saidia mwanafunzi aelewe kama haiko muzuri kumuambia mambo yote kulimoya. Kama anafanya vile, mutu wa familia yake ataona kama binapita, ni bya mingi sana; na siku ingine hatasikiliza. Njo maana umutie moyo akuwe nasema mambo kidogo-kidogo juu siku ingine bakuwe tayari kumusikiliza. (Kol. 4:6) Ao pengine anaweza kuambia mutu wa familia yake afungule jw.org. Ile itasaidia ule mutu ajifunze yeye peke polepole mambo mingi juu ya Mashahidi ya Yehova.

17. Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wako akuwe tayari kujibia maulizo yenye batu banaweza kuwa nayo kuhusu Mashahidi? (Ona pia picha.)

17 Juu ya kusaidia mwanafunzi apate majibu ya mwepesi yenye anaweza kujibia batu ya familia ao bafanyakazi benzake, unaweza kutumikisha sehemu “Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana juu ya Mashahidi wa Yehova” yenye iko ku jw.org. (2 Ti. 2:24, 25) Pia usisaabu kutumikisha sehemu “Watu Fulani Wanasemaka” yenye iko ku mwisho wa kila somo ya kitabu Furahia Maisha Milele! Utie mwanafunzi moyo afasirie mu maneno yake mambo yenye anaamini. Na kama uko na mapendekezo juu ya namna anaweza kufasiria muzuri zaidi, umuambie. Kama munafanya mazoezi pamoya, ile itamusaidia ajue namna ya kutetea bila boga mambo yenye anaamini.

Wakati wa funzo dada iko nasaidia mwanafunzi wa Biblia kujitayarisha juu ya mahubiri. Ule mwanafuzi iko najizoeza kwa kupatia dada trakte “Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?”

Juu ya kusaidia mwanafunzi aanze kuhubiri, mukuwe nafanya naye mazoezi wakati muko najifunza (Ona fungu ya 17)c


18. Namna gani unaweza kutia mwanafunzi moyo akuwe muhubiri? (Matayo 10:27)

18 Yesu aliambia banafunzi yake bahubiri habari njema fasi yote. (Soma Matayo 10:27.) Kama mwanafunzi wa Biblia anaanza kuhubiri na kutaniko bila kukawia, ile itamusaidia amutumainie Yehova zaidi. Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia mwanafunzi wako akuwe muhubiri? Kama kampanye fulani ya kuhubiri inakaribia, umusaidie mwanafunzi ajue mambo ya kufanya juu astahili kuwa muhubiri. Umuambie kama mara mingi inakuwaka mwepesi kuanza kuhubiri mu kampanye. Kitu ingine yenye itamusaidia ni mazoezi ya kuzungumuza na batu yenye tunapataka ku mukutano wa katikati ya juma. Kama naye anajikaza juu astahili kupitisha bipindi, ile itamusaidia ajue namna ya kufasiria bila boga mambo yenye anaamini.

ONYESHA KAMA UNATUMAINIA MWANAFUNZI

19. Namna gani Yesu alionyesha kama anatumainia banafunzi yake, na tunaweza kumuiga namna gani?

19 Mbele Yesu apande mbinguni aliambia banafunzi yake kama batakuwaka tena pamoya naye. Lakini banafunzi yake habakuelewa kama alikuwa anazungumuzia tumaini yabo ya kuenda mbinguni. Hata kama banafunzi yake habakuelewa mambo yote ile wakati, Yesu alijua kama balipenda kumufurahisha Yehova. (Yoh. 14:1-5, 8) Alijua kama iliomba wakati juu baelewe mambo fulani, sawa vile tumaini ya kuenda mbinguni. (Yoh. 16:12) Kama Yesu, na siye tunaweza kuonyesha mwanafunzi kama tunajua anapenda kumufurahisha Yehova.

Kama mwanafunzi wa Biblia anaanza kuhubiri na kutaniko bila kukawia, ile itamusaidia amutumainie Yehova zaidi

20. Namna gani dada fulani wa Malawi alionyesha kama anatumainia mwanafunzi wake?

20 Ukuwe hakika kama mwanafunzi anapenda kufanya mambo ya muzuri. Ni vile Chifundo dada wa Malawi alifanya. Alianza kujifunza Biblia pamoya na Alinafe mu kitabu Furahia Maisha Milele!; Alinafe alikuwa Mukatoliki. Ku mwisho wa somo ya 14, Chifundo aliuliza Alinafe anawaza nini juu ya kutumia sanamu mu ibada. Alinafe alikasirika na akajibia hivi: “Miye njo wa kuamua.” Chifundo aliwaza kama Alinafe ataacha kujifunza. Lakini baliendelea kujifunza na Chifundo alivumilia ile hali. Alitumainia kama siku moya Alinafe ataelewa ile mafundisho. Kisha miezi fulani wakati balikuwa mu somo ya 34, Chifundo aliuliza Alinafe hii ulizo: “Kufikia hapa, kujifunza Biblia na kujifunza juu ya Mungu wa kweli Yehova, kumekusaidia namna gani?” Chifundo anaeleza hivi: “Alitaya mambo mingi ya muzuri, alisema kama Mashahidi wa Yehova habafanyake mambo yenye Biblia inakataza.” Wakati kidogo kisha pale, Alinafe aliacha kutumikisha sanamu na alistahili kubatizwa.

21. Tunapaswa kufanya nini juu ya kusaidia mwanafunzi apende kumutumikia Yehova?

21 Ni kweli Yehova njo ‘anakomalisha,’ ni kusema yeye njo anasaidia banafunzi bafanye maendeleo. (1 Ko. 3:7) Lakini kuko mambo yenye na siye tunapaswa kufanya. Zaidi ya kuonyesha mwanafunzi mambo yenye Yehova anapenda afanye, tumusaidie amupende Yehova zaidi. Tumutie moyo aonyeshe kama anamupenda Yehova kwa kutia mambo ya kiroho fasi ya kwanza. Na tumufundishe namna ya kumutumainia Yehova wakati anakutana na upinzani. Zaidi ya ile, wakati tunaonyesha kama tunatumainia mwanafunzi wa Biblia, tunamusaidia akuwe hakika kama ataweza kutumikisha mambo yenye iko najifunza na kuanza kumutumikia Yehova.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUSAIDIA MWANAFUNZI . . .

  • ajue mambo yenye iko namuzuia kufanya maendeleo?

  • amupende Yehova zaidi?

  • atie mambo ya kiroho fasi ya kwanza?

WIMBO 55 Musiwaogope!

a Miaka mbili kisha Nikodemu kukutana na Yesu, alikuwa angali kati ya batu benye balifanyiza tribinali kubwa ya Bayahudi. (Yoh. 7:45-52) Banahistoria fulani banawaza kama Nikodemu alifikia kuwa mwanafunzi wa Yesu kisha Yesu kufa.—Yoh. 19:38-40.

b MAFASIRIO YA PICHA : Petro na bavuvi bengine banaacha kazi yabo ya kuloba samaki na banamufuata Yesu.

c MAFASIRIO YA PICHA: Dada iko nasaidia mwanafunzi wa Biblia akuwe tayari kutetea imani yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine