Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 7 uku. 26-30
  • “Vita Ni ya Yehova”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Vita Ni ya Yehova”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • BAZAZI YANGU BALIKUWA NA BIDII
  • NAANZA KUTUMIKA KU MAKAO MAKUBWA
  • KAZI YANGU MU IDARA YA MAMBO YA SHERIA
  • KUTETEA HABARI NJEMA NA KUIFANYA IKUBALIWE KISHERIA
  • AKSANTI YEHOVA!
  • Kupigania Uhuru wa Kuabudu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Waliunga Mukono Kwa Ushikamanifu Serikali ya Mungu Tu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Wahubiri Wa Ufalme Wanapeleka Mashitaka Yao Kwenye Tribinali
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kutetea Uhuru wa Dini wa Wenyeji
    Namna Michango Yako Inatumiwa
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 7 uku. 26-30
Philip Brumley.

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

“Vita Ni ya Yehova”

INAELEZWA NA PHILIP BRUMLEY

TAREHE 28 Mwezi wa 1, 2010, nilijikuta mu muji wa muzuri wa Strasbourg, Ufaransa. Lakini sikukuwa kule juu ya kujitembeza. Nilikuwa mu kikundi ya bandugu benye balipaswa kutetea haki ya Mashahidi wa Yehova mbele ya Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya. Serikali ya Ufaransa ilikuwa nasema kama bandugu ba mu ile inchi balipaswa kulipa takse ya mingi sana. Ile takse ilikuwa ya dola 89000000. Tulijikuta ku ile tribinali juu ya kuonyesha kama serikali ya Ufaransa haikukuwa na haki ya kulomba ile makuta. Lakini jambo ya maana zaidi haikukuwa ile makuta. Ikiwa tungepata ushindi, jina ya Yehova ingetukuzwa, batu bangeendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova, na Mashahidi wangeendelea kumuabudu Yehova kwa uhuru mu Ufaransa. Mambo yenye ilipitikana kule ilituhakikishia kama “vita ni ya Yehova.” (1 Sa. 17:47) Acha nifasirie.

Mambo ilianza mu 1990 wakati serikali ya Ufaransa ililomba tawi ilipe takse juu ya michango yenye tawi ilipata kuanzia mwaka wa 1993 mupaka 1996. Tulipeleka ile mambo ku tribinali za Ufaransa. Lakini hatukupata matokeo ya muzuri. Tulilomba tusambe tena juu ya ile jambo lakini uamuzi ulikuwa uleule kisha kusamba tena. Kisha pale serikali ya Ufaransa ilinyanganya makuta yenye biro ya tawi ilikuwa nayo mu banke. Ilibeba zaidi ya dola 6300000. Tumaini yetu ya mwisho ya kupata ile makuta ilikuwa kuenda ku Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya. Lakini mbele tuanze kusamba, tribinali ililomba kikundi yetu na kikundi ya wanasheria wa serikali ya Ufaransa tukutane mbele ya mutu mwenye ile tribinali ilituma, juu tuone kama inawezekana tusikilizane mbele mambo iende mbali.

Tulijua kama inawezekana ule mwanamuke mwenye ile tribinali ilituma, atuombe tulipe hata kipande ya makuta juu mambo iishie pale. Lakini tulielewa kama kulipa hata dola moya ilikuwa kuvunja kanuni za Biblia. Bandugu na dada balitoa ile makuta juu ya kutegemeza kazi ya Ufalme. Ile makuta haikukuwa ya serikali. (Mt. 22:21) Lakini tulienda ku ile mukutano juu ya kuonyesha kama tunaheshimia mupango ya ile tribinali.

Kikundi yetu ya kutetea sheria mbele ya Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya mu 2010

Tulikutana mu jumba moya ya muzuri ya ile tribinali. Mambo haikuanza muzuri. Ku mwanzo tu ya ile mazungumuzo ule mwanamuke mwenye tribinali ilituma alisema kama Mashahidi wa Yehova wa Ufaransa wanapaswa kulipa hata sehemu fulani ya ile takse yenye serikali inalomba. Mara moya tukamuuliza hivi: ‘Unajua kama, tayari serikali ilishanyanganya zaidi ya dola 6300000 ku makuta yenye tulikuwa nayo mu banke?’

Ule mwanamuke alishangala na inaonekana hakufurahia ile mambo yenye serikali ya Ufaransa ilifanya. Wakati wanasheria wa serikali ya Ufaransa walikubali kama vile njo mambo ilikuwa, mara moya ule mwanamuke alibadilisha mawazo yake. Alibakaripia juu ya ile jambo na mara moya akasimamisha ile mukutano. Nilielewa kama Yehova alikuwa amebadilisha mambo juu tuweze kupata ushindi mu njia yenye hatungeweza kuwazia. Tulitoka mu ile mukutano na furaha sana na tulishangala sana juu ya mambo yenye ilikuwa imetokea.

Tarehe 30 Mwezi wa 6, 2011, Tribinali ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu, ilitupatia sheria. Ile tribinali ilisema kama serikali ya Ufaransa haina haki ya kutulipisha ile takse. Baliilomba irudishe ile makuta na batuongezee makuta ingine. Ule uamuzi wa maana unaendelea kulinda haki yetu ya kuabudu mu inchi ya Ufaransa mupaka leo. Ile ulizo tu moya yenye ilikuya palepale yenye tuliuliza, ilikuwa sawa vile jiwe yenye ilipiga ku kichwa ya Goliati. Ilibadilisha mambo mara moya. Juu ya nini tulipata ushindi? Ni juu sawa vile Daudi aliambia Goliati, “vita ni ya Yehova.”—1 Sa. 17:​45-47.

Haiko ile ushindi moya tu njo tumepata ku tribinali. Hata kama serikali za nguvu na batu ya dini bametupinga, tumeweza kushinda kesi 1225 ku tribibali kubwa zaidi za inchi 70 na ku tribinali za kimataifa. Zile ushindi zimetusaidia kulinda haki zetu za musingi, sawa vile haki ya kujiandikisha kisheria, haki yetu ya kuhubiria batu, ya kukatala kujiingiza mu matukio yenye inatukuza taifa, na haki ya kukatala kutiwa damu.

Namna gani miye mwenye nilikuwa natumika ku Makao Makubwa ya Mashahidi wa Yehova mu New York nilijikuta niko natetea haki yetu mbele ya tribinali ya Ulaya?

BAZAZI YANGU BALIKUWA NA BIDII

Bazazi yangu, George na Lucille, balisoma darasa ya 12 ya Masomo ya Gileadi. Nilizawaliwa mu 1956 wakati balikuwa natumikia mu Etiopia. Balinipatia jina Philip, jina ya ule Filipo mweneza-injili wa mu karne ya kwanza. (Mdo. 21:8) Mwaka yenye ilifuata serikali ilikataza kazi yetu. Hata kama nilikuwa mutoto sana, ninakumbuka vile familia yetu ilikuwa namuabudu Yehova mu siri. Juu nilikuwa mutoto, niliona kama ile hali ilikuwa ya kufurahisha. Jambo ya kuhuzunisha ni kama bakubwa ya ile inchi balitulazimisha kutoka mu inchi mu 1960.

Nathan H. Knorr (kushoto) anatembelea familia yetu Addis Ababa, mu Etiopia, 1959

Nilikuwa na dada mukubwa Judy na muloko mwanaume Leslie. Siye bote tulizaliwa Etiopia. Wakati tulihamia Wichita, Kansas, mu Amerika, bazazi yetu baliendelea kuwa na bidii yenye balikuwa nayo wakati balikuwa bamisionere. Balitufundisha kumupenda Yehova na kumutumikia kwa moyo wote. Nilibatizwa na miaka 13. Kisha miaka tatu, familia yetu ilihamia Arequipa, mu Peru kwenye kulikuwa lazima kubwa ya bahubiri.

Mu 1974 wakati nilikuwa na miaka 18, tawi ya Peru ilituweka miye na bandugu bengine ine kuwa mapainia wa pekee. Balitutuma tuhubiri mu maeneo yenye ilikuwa haiyahubiriwaka. Ile maeneo ilikuwa mu milima ya Andes. Tulipaswa kuhubiria wenyeji wenye walikuwa nasema Kikechua na luga ya Aymara. Tulikuwa nasafiri mu gari yenye ilikuwa ilishatengenezwa juu batu baishi ndani. Tulikuwa naita ile gani Safina juu ya namna ilikuwa inaonekana. Nafurahiaka sana wakati ninakumbukaka vile tulikuwa nasomea wenyeji Biblia na kuwaonyesha vile hivi karibuni Yehova atatosha umaskini, magonjwa, na kifo. (Ufu. 21:​3, 4) Ba mingi kati yabo balikubali kweli na balianza kumuabudu Yehova.

Gari yetu iko natembea mu mayi ya mingi.

“Safina,” 1974

NAANZA KUTUMIKA KU MAKAO MAKUBWA

Ndugu Albert Schroeder mwenye alikuwa mu Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova alitembelea Peru mu 1977. Alinitia moyo nijaze fomu juu nitumikie ku Beteli ya Makao Makubwa. Ni vile nilifanya. Kisha wakati kidogo, mu tarehe 17 Mwezi wa 6, 1977, nilianza kutumikia ku Beteli ya Brooklyn. Mu miaka ine yenye ilifuata nilitumikia mu idara yenye ilihangaikia kusafisha na kutunza bitu.

Siku ya ndoa yetu, 1979

Mu Mwezi wa 6, 1978, nilikutana na Elizabeth Avallone ku mukusanyiko wa kimataifa mu Nouvelle-Orleons, Lousianne. Naye alikomalishwa na bazazi benye banamupenda sana Yehova na banamutumikia kwa moyo wote. Elizabeth alikuwa alishafanya miaka ine mu upainia na alipenda kuendelea na utumishi wa wakati wote maisha yake yote. Tuliendelea kuwasiliana na kisha wakati kidogo tulifikia kupendana sana. Tulioana tarehe 20 Mwezi wa 10, 1979, na tukaanza kutumika pamoya ku Beteli.

Bandugu na dada ba mu kutaniko yetu ya kwanza ya Brooklyn ya mu luga ya Kihispania balitukaribisha kwa moyo wote. Tumetumikia mu kutaniko zingine tatu, na bandugu balituonyesha upendo na balitutia moyo tuendelee na utumishi wetu ku Beteli. Tunashukuru sana juu ya musaada ya bale bandugu na dada. Tuko wenye shukrani pia juu ya namna marafiki na batu ya familia balitusaidia kushugulikia bazazi yetu wakati balizeeka.

Philip na Wanabeteli wenzake ku mikutano.

Wanabeteli wenye walikuwa mu kutaniko ya Brooklyn ya Kihispania, 1986

KAZI YANGU MU IDARA YA MAMBO YA SHERIA

Mu Mwezi wa 1, 1982 nilishangala wakati baliniomba nitumikie mu idara ya mambo ya kisheria ya Beteli. Miaka 3 kisha, baliniomba niende ku Université na nisome masomo ya kisheria. Kule ku Université nilishangala sana kuona vile ushindi mbalimbali wenye Mashahidi walipata ku tribinali, umesaidia batu mingi mu Amerika na mu inchi zingine, bapate uhuru wa kufanya mambo mingi. Ku masomo tulizungumuzia sana kuhusu zile kesi za maana.

Mu 1986 wakati nilikuwa tu na miaka 30, baliniweka kuwa musimamizi wa Idara ya Mambo ya Kisheria. Niliiona kuwa pendeleo juu nilikuwa ningali kijana. Lakini nilikuwa pia na wasiwasi juu kulikuwa mambo mingi yenye sikukuwa najua na ile haikukuwa mugao ya teketeke.

Nilipata diplome yangu mu 1988 lakini sikutambua namna ile masomo ilikuwa na matokeo ya mubaya juu yangu na juu ya uhusiano wangu pamoya na Yehova. Masomo ya juu inaweza kufanya mutu akuwe na kiburi na awaze kama yeye njo wa maana zaidi kupita bengine benye habakusoma ile masomo. Elizabeth njo alinisaidia sana. Alinisaidia nirudilie tena programu yangu ya kiroho yenye nilikuwa nayo mbele niende ku Université. Ilikamata wakati lakini polepole hali yangu ya kiroho ilianza kurudia muzuri. Kupitia mambo yenye ilinifikia, naweza kuhakikisha kama kujua bya mingi haiko njo jambo ya maana sana mu maisha. Jambo yenye inafanya maisha yetu ikuwe ya muzuri ni kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova, kumupenda sana na kupenda sana batu yake.

KUTETEA HABARI NJEMA NA KUIFANYA IKUBALIWE KISHERIA

Kisha kumaliza masomo, nilikazia akili kusaidia kupanga kazi mu idara ya mambo ya kisheria ku beteli na kutetea faida za Ufalme mbele ya tribinali. Kazi yangu ilikuwa ya kufurahisha, lakini pia haikukuwa teketeke juu mambo ilikuwa nabadilika haraka mu tengenezo. Kwa mufano, zamani tulikuwa nalomba batu makuta juu ya kubatolea bichapo. Lakini mu 1991 tengenezo ililomba idara ya mambo ya sheria itoe muongozo juu ya namna ya kuachana na ile zoea. Kisha pale, Mashahidi wa Yehova walianza kupatia batu bichapo bila kulomba makuta. Ile ilirahisisha kazi ku Beteli na mu mahubiri, na mupaka leo inaendelea kutuepusha kulipa takse zingine. Batu fulani baliwaza kama ile badiliko itafanya tupoteze makuta ya mingi na tusikuwe na bichapo mingi, na ile ingefanya batu ba mingi basiweze kujifunza kweli. Lakini mambo ilikuwa tofauti. Kuanzia mwaka wa 1990, hesabu ya benye banamutumikia Yehova imeongezeka sana. Na leo batu banaweza kupata chakula ya kiroho yenye kuokoa uzima bila kulipa. Nimejionea kama mabadiliko makubwa yenye tunafanya mu tengenezo inawezekana tu kwa musaada wa Yehova na muongozo wa mutumwa mwaminifu.—Kut. 15:2; Mt. 24:45.

Haiko tu juu tuko na banasheria bamuzuri njo tunapataka ushindi ku tribinali. Mara mingi ni mwenendo muzuri ya batu ya Yehova njo inachochea batu benye mamlaka batutendee muzuri. Kwa mufano, mu 1998 ndugu tatu wa Baraza Yenye Kuongoza na bibi zao balifika ku mukusanyiko wa pekee wa mu Kiba. Balisema kwa upole na heshima. Na ile njo ilihakikishia bakubwa ba serikali, kupita hata mambo yote yenye tulibafasiria wakati tulikutana nabo, kama hatujiingizake mu mambo ya politike.

Lakini, wakati haiwezekane kumaliza mambo mu njia ya kirafiki, tunalazimika ‘kutetea habari njema na kuifanya ikubaliwe kisheria’ mbele ya tribinali. (Flp. 1:7) Kwa mufano, kwa miaka mingi bakubwa fulani mu Ulaya na mu Korea ya Kusini, habakukubali kama tuko na uhuru wa kukatala kufanya kazi ya jeshi. Ile ilifanya bandugu karibu 18000 mu Ulaya, na zaidi ya 19000 mu Korea ya Kusini bafungwe kwa wakati fulani juu zamiri yabo haikubaruhusu kuingia mu kazi ya jeshi.

Mwishowe, tarehe 7 Mwezi wa 7, 2011, Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya, ilikamata uamuzi wa maana sana. Ilitupatia sheria mu kesi kati ya Bayatyan na Arménie. Ule uamuzi ulilazimisha inchi zote za Ulaya ziruhusu mutu kufanya kazi ingine pa nafasi ya kazi ya jeshi kama zamiri ao imani yake haimuruhusu kufanya kazi ya jeshi. Inchi ya Korea pia ilikamata uamuzi wa vile, mu tarehe ya 28 Mwezi wa 6, 2018. Hatungepata zile ushindi ikiwa hata hesabu kidogo ya bandugu vijana habangebakia baaminifu.

Idara ya mambo ya kisheria ya ku makao makubwa na biro za tawi za dunia yote zinatumika sana juu ya kutetea kisheria faida za Ufalme. Ni pendeleo kwetu kusamba kwa ajili ya bandugu na dada benye biko napambana na upinzani. Ikuwe tunapata ushindi ao hapana, ile kusamba inatolea ushahidi watawala, wafalme, na batu ya mataifa. Tunatia maandiko ya Biblia mu mambo yenye tunasema ao kuandika wakati tunasamba. (Mt. 10:18) Kwa hiyo, baamuzi, batu ya serikali, batu ya kutoa habari, ao batu bengine banasikia ile maandiko. Ile inafanya batu batujue muzuri zaidi na bajue kama tunatosha mafundisho yetu yote mu Biblia. Bamoya kati ya bale batu bamefikia kuwa baaminifu benzetu.

AKSANTI YEHOVA!

Miaka 40 yenye imepita nimepata pendeleo ya kutumika mu mambo ya kisheria pamoya na biro za tawi za mu dunia yote, na nimesamba mbele ya tribinali kubwa za mingi, na mbele ya wakubwa wengi wa serikali. Ninapenda na kufurahia sana bandugu benye tunatumika nabo mu idara ya mambo ya kisheria ku Makao Makubwa na idara mbalimbali za mambo ya kisheria ku biro za tawi mu dunia yote. Nimekuwa na maisha ya muzuri na nimepata baraka mingi.

Philip na Elizabeth Brumley.

Mu miaka 45 yenye imepita, ikuwe mu hali za muzuri ao za mubaya, Elizabeth amenitegemeza sana kwa upendo na kwa uaminifu. Namupendaka sana juu anafanyaka ile mambo yote hata kama iko na ugonjwa wenye uko namumaliza nguvu.

Nimefikia kujionea kama haiko juu ya uwezo wetu njo tuko na nguvu na tunapata ushindi. Sawa tu vile Daudi alisema, “Yehova ni nguvu kwa watu wake.” (Zb. 28:8) Kwa kweli, “vita ni ya Yehova.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine