Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 7 uku. 14-19
  • Mafundisho ya Musingi ya Biblia Iendelee Kukusaidia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mafundisho ya Musingi ya Biblia Iendelee Kukusaidia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • YEHOVA ALIUMBA KILA KITU
  • JUU YA NINI MUNGU ANAACHA BATU BATESEKE
  • TUNAISHI MU “SIKU ZA MWISHO”
  • ENDELEA KUONYESHA SHUKRANI JUU YA VIKUMBUSHO VYA YEHOVA
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Unatambua ile Kweli?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Upendo Ukuchochee Kuendelea Kuhubiri!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 7 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 30

WIMBO 97 Uzima Wetu Unategemea Neno ya Mungu

Mafundisho ya Musingi ya Biblia Iendelee Kukusaidia

“Sikuzote ninakusudia kuwakumbusha ninyi mambo haya, hata kama munayajua na muko imara katika kweli.”—2 PE. 1:12.

WAZO KUBWA

Namna mafundisho ya musingi ya Biblia yenye ulijifunzaka zamani inaweza kuendelea kukusaidia leo.

1. Wakati ulijifunza kweli kwa mara ya kwanza, namna gani mafundisho ya Biblia ilikusaidia?

MAFUNDISHO ya musingi ya Biblia, ni kusema mambo ya kwanza-kwanza yenye tulijifunza mu funzo yetu ya Biblia ilibadilisha maisha yetu yote. Kwa mufano wakati tulijifunza kama jina ya Mungu ni Yehova, tulianza kuwa barafiki yake. (Isa. 42:8) Wakati tulijifunza kweli juu ya hali ya wafu, hatukukuwa tena tunajiuliza ikiwa bandugu yetu benye balishakufa biko nateseka. (Muh. 9:10) Na wakati tulijifunza juu ya ahadi ya Mungu ya kuleta Paradiso ku dunia, hatukuogopa tena juu ya maisha yetu ya kesho. Tulikuwa hakika kama tunaweza kuishi milele, hapana tu miaka 70 ao 80.—Zb. 37:29; 90:10.

2. Andiko ya 2 Petro 1:​12, 13 inaonyesha namna gani kama mafundisho ya musingi ya Biblia inaweza kusaidia hata Bakristo benye kukomala kiroho?

2 Mutume Petro aliandikia barua yake ya pili Bakristo benye balikuwa “imara katika kweli.” (Soma 2 Petro 1:​12, 13.) Lakini mu ile wakati, mu kutaniko mulikuwa batu benye balikuwa naeneza mafundisho ya bongo juu ya kuchochea bandugu baache kweli. (2 Pe. 2:​1-3) Petro alipenda kusaidia bandugu babakie baamuminifu na basiangukie mu ile mutego. Njo maana Petro alibakumbusha mafundisho fulani ya musingi yenye balikuwa najua. Ile mafundisho ingebasaidia baendelee kuwa baaminifu mupaka mwisho. Njo sababu na siye hatupaswe kuzarau mafundisho ya musingi ya Biblia.

3. Toa mufano yenye inaonyesha juu ya nini ni jambo ya maana Bakristo bote baendelee kufikiri sana juu ya mafundisho ya musingi ya Biblia.

3 Hata kama tumekomala kiroho, mafundisho ya musingi ya Biblia inaweza kuendelea kutufundisha mambo ingine ya mupya. Tuchukue mufano ya mama na mutoto. Kila mumoya wabo anapiga chakula. Bote banatumikisha biungo bilebile juu ya kupiga ile chakula. Lakini chakula ya mama inatoka butamu sana kupita ya mutoto. Juu ya nini? Ni juu mama amepiga chakula kwa miaka mingi na anajua namna ya kutumikisha bile biungo muzuri zaidi. Ni vile pia kuhusu mutu mwenye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi na mwanafunzi wa Biblia. Mutu mwenye amemutumikia Yehova miaka mingi anaweza kuelewa mambo mingi kuhusu fundisho fulani ya musingi kupita mwanafunzi wa Biblia. Juu ya nini? Juu hali na mapendeleo ya mutu mwenye alibatizwa zamani inaweza kubadilika. Wakati tunafikiria mafundisho ya mingi ya musingi ya Biblia, yenye tulijifunza zamani, tunaweza kupata namna ingine ya mupya ya kuitumikisha mu hali yetu ya leo. Tuone namna mafundisho tatu ya musingi ya Biblia inaweza kusaidia Bakristo benye kukomala kiroho.

YEHOVA ALIUMBA KILA KITU

4. Kujua kama Yehova ni Muumbaji kumetusaidia namna gani?

4 Tunajua kama kuko Muumbaji mwenye hekima sana na mwenye nguvu mingi mwenye aliumba dunia na byote byenye kuwa ndani. Biblia inasema kama: “Ule mwenye alijenga vitu vyote ni Mungu.” (Ebr. 3:4) Lakini hii kweli ya Biblia inaweza kutufundisha mambo ingine ya mingi. Kwa mufano, juu Yehova njo alituumba, anajua kila kitu juu yetu, anatuhangaikia na anajua mambo yenye tuko nayo lazima kabisa. Njo maana kujua kama Yehova njo Muumbaji, kumebadilisha maisha yetu mu njia mbalimbali na kumetusaidia kuwa na kusudi mu maisha.

5. Ni kweli gani yenye inaweza kutusaidia kuwa banyenyekevu? (Isaya 45:​9-12)

5 Kujua kama Yehova njo Muumbaji kunaweza pia kutusaidia kuwa na unyenyekevu. Namna gani? Fikiria mufano wa Yobu. Alijifikiria sana, kuliko kukazia akili mambo ya lazima zaidi. Lakini Yehova Mungu alimukumbusha kama yeye njo Muumbaji Mweza-Yote. (Yob. 38:​1-4) Ile ilisaidia Yobu aone kama namna ya Yehova ya kufanya mambo iko yulu kupita namna ya banadamu ya kufanya mambo. Hata nabii Isaya naye aliandika kama banadamu habapaswe kuwaza hata siku moya kama biko na hekima kupita Muumbaji wabo. Aliandika hivi: “Je, udongo utamuambia mufinyanzi: ‘Unatengeneza nini?’”—Soma Isaya 45:​9-12.

6. Ni wakati gani inaomba kufikiri sana juu ya nguvu na hekima ya Muumbaji wetu? (Ona pia picha.)

6 Wakati Mukristo amemutumikia Yehova kwa miaka mingi, anaweza kuanza kutegemea mawazo yake kuliko kutafuta muongozo wa Yehova na Neno yake. (Yob. 37:​23, 24) Lakini kama anafikiri sana juu ya nguvu na hekima ya ajabu ya Muumbaji wake, ile inaweza kumusaidia. (Isa. 40:22; 55:​8, 9) Ile fundisho ya musingi itamusaidia kuwa munyenyekevu na kuona kama mawazo ya Yehova ni ya maana kupita mawazo yake.

Picha: 1. Muzee moya iko natoa maelezo ku mukutano ya bazee lakini bazee bengine habakubaliane naye. 2. Kisha, ule muzee mwenye alitoa maelezo iko naangalia nyota usiku na anatafakari.

Nini njo inaweza kutusaidia kuelewa kama mawazo ya Yehova iko ya muzuri kupita yetu? (Ona fungu ya 6)d


7. Rahela alifanya nini juu aweze kukubali mabadiliko?

7 Dada Rahela, wa mu Slovenia, aliona kama kufikiri juu ya Muumbaji wake kulimusaidia kukubali mabadiliko yenye ilifanywa mu tengenezo. Anasema hivi: “Wakati fulani haikukuwa mwepesi kwangu kukubali maamuzi yenye bandugu benye kuongoza balikamata. Kwa mufano hata kisha kufuata Ripoti ya 8 ya Baraza Yenye Kuongoza ya 2023, nilikwazika wakati niliona kwa mara ya kwanza ndugu mwenye iko na ndevu anafanya hotuba. Kwa hiyo niliomba Yehova anisaidie nikubali ile mabadiliko.” Rahela alielewa kama juu Yehova ni Muumbaji wa mbingu na Dunia, iko na uwezo wa kuongoza tengenezo yake muzuri. Kama na weye ni nguvu kwako kukubali mwangaza mupya ao namna ya mupya ya kufanya mambo mu tengenezo, kamata wakati ya kufikiria namna Muumbaji wetu iko na hekima na nguvu mingi. —Ro. 11:​33-36.

JUU YA NINI MUNGU ANAACHA BATU BATESEKE

8. Kujifunza juu ya nini Mungu anaruhusu mateso kumekusaidia namna gani?

8 Juu ya nini Mungu anaacha batu bateseke? Batu fulani benye habajue jibu ya ile ulizo, banakasirikia Mungu na bengine banaamini kama Mungu hakuwake! (Mez. 19:3) Lakini weye ulijifunza kama ni zambi na kutokamilika yenye tuliriti njo inaleta mateso, haiko Yehova. Na ulijifunza kama Yehova iko na uvumilivu njo maana anaacha wakati ipite juu ya kusaidia banadamu bamingi bamujue na bajue kama atamaliza mateso lote. (2 Pe. 3:​9, 15) Kujua juu ya nini Yehova anaruhusu mateso kulikufariji na kulikusaidia umukaribie.

9. Ni mu hali gani inaomba tujikumbushe juu ya nini Yehova anaruhusu mateso?

9 Tunaelewa kama ni lazima tukuwe wavumilivu wakati tuko nangoya Yehova amalize mateso. Lakini wakati mutu mwenye tunapenda anakufa ao wakati banatutendea mubaya siye na batu ya familia yetu, tunaweza kuanza kuona kama Yehova anakawia kumaliza mateso. (Hab. 1:​2, 3) Mu ile wakati ni muzuri tukumbuke juu ya nini Yehova anaruhusu batu bazuri bateseke.a (Zb. 34:19) Tunaweza pia kufikiria kusudi yake ya kumaliza magumu ku dunia milele.

10. Ni nini ilimusaidia Anne kutulia kisha mama yake kufa?

10 Kujua juu ya nini Mungu anaacha mateso ifike, kunaweza kutusaidia kuvumilia. Dada Anne, mwenye anaishi ku kisiwa ya Mayotte, yenye kuwa mu bahari ya India anasema hivi: “Mama yangu alikufa kumepita miaka fulani. Ile iliniletea huzuni sana. Lakini mara kwa mara, ninaendelea kujikumbusha kama haiko Yehova njo anatuletea mateso. Yehova iko na hamu kabisa ya kumaliza mateso yote na kufufula bapendwa betu. Kufikiria ile jambo kunaniatiaka moyo na kunanitulizaka mu namna yenye hata miye peke sielewake.”

11. Namna gani kujua juu ya nini Yehova anaruhusu mateso kunatusaidia tuendelee kuhubiri?

11 Kujua juu ya nini Mungu anaacha mateso kunatuchochea tuendelee kuhubiri. Kisha kufasiria kama Yehova ni muvumilivu juu anapenda batu batubu na baokolewe, Petro aliandika hivi: “Mufikirie munapaswa kuwa watu wa namna gani katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ushikamanifu kwa Mungu.” (2 Pe. 3:11) Kazi yetu ya kuhubiri nayo iko kati ya “vitendo vya ushikamanifu kwa Mungu.” Baba yetu Yehova anapenda batu, na siye tunabapenda. Tunapenda batu baishi mu dunia mupya ya Mungu kwenye kutakuwa haki. Juu Yehova ni muvumilivu anapatia batu ya mu eneo yetu nafasi ya kumuabudu. Uko na pendeleo kubwa ya kutumika pamoya na Yehova na kusaidia batu ba mingi bamujue mbele mwisho ifike!—1 Ko. 3:9.

TUNAISHI MU “SIKU ZA MWISHO”

12. Namna gani kujifunza kama tunaishi mu “siku za mwisho” kumetusaidia?

12 Biblia ilifasiria waziwazi namna batu bengekuwa mu “siku za mwisho.” (2 Ti. 3:​1-5) Hatuna lazima ya kutafuta mbali juu tuone namna hii unabii iko natimia. Wakati tunaona vile tabia ya batu inaendelea kuharibika, tunakuwa hakika zaidi kama Neno ya Mungu inasemaka kweli.—2 Ti. 3:​13-15.

13. Mufano yenye kuwa mu Luka 12:​15-21 inatufundisha nini?

13 Kujua kama tunaishi mu siku za mwisho kunatusaidia tujue ni nini tutie fasi ya kwanza mu maisha yetu. Ona mambo yenye tunaweza kujifunza mu mufano yenye kuwa mu Luka 12:​15-21. (Soma.) Juu ya nini ule mwanaume tajiri aliitwa “pumbavu”? Haiko juu alikuwa tajiri, ni juu hakujua mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza. Alijiwekea ‘hazina lakini hakukuwa tajiri kwa Mungu.’ Kufanya vile haikukuwa jambo ya hekima juu alibakia tu na wakati kidogo ya kuishi. Mungu alimuambia hivi ule mwanaume: “Usiku huu wanataka uzima wako.” Hii habari inatusaidia namna gani leo? Kunabakia wakati kidogo tu mbele mwisho ifike. Njo maana ni muzuri tujiulize hivi: ‘Miradi yangu inaonyesha kama niko natumikisha wakati yangu kwa hekima? Tuseme nini juu ya miradi yenye niko nachochea watoto wangu wafuatie? Niko natumikisha wakati wangu na makuta yangu juu ya kujilundikia mali ao niko naitumikisha juu ya kujiwekea hazina mbinguni?’

14. Vile mufano wa Miki unaonyesha, juu ya nini ni jambo ya maana tuendelee kukumbuka kama tunaishi mu siku za mwisho?

14 Wakati tunaelewa kama tunaishi mu siku za mwisho namna yetu ya kuona maisha inaweza kubadilika kabisa. Ile njo ilifikia dada Miki. Anasema hivi: “Wakati nilimaliza masomo ya segondere nilipenda kupata kazi yenye ingenisaidia kujifunza wanyama. Lakini ile kazi ingeniomba kusoma masomo ya mingi. Nilikuwa pia na muradi ya kuwa painia wa kawaida, na kuenda kutumikia fasi kwenye kuko lazima kubwa ya bahubiri. Ndugu na dada fulani mu kutaniko baliniambia niwaze muzuri juu nione ikiwa itawezekana kufanya kazi yenye ninapenda na wakati ileile kuwa painia na kuenda kutumikia fasi kwenye kuwa lazima kubwa ya bahubiri. Balinikumbusha kama mwisho wa hii dunia iko karibu. Lakini mu dunia mupya, juu tutaishi milele, nitakuwa na wakati mingi ya kujifunza banyama bote benye ninapenda. Kwa hiyo, niliamua kufuata programu ya mufupi yenye ingenisaidia kujifunza jambo fulani yenye itanisaidia kupata kazi. Nilipata kazi yenye iliniwezesha kuwa painia wa kawaida, na kisha wakati nilienda mu inchi ya Equateur, kwenye kulikuwa lazima kubwa ya bahubiri.” Leo, Miki na bwana yake banatumika mu muzunguko mu inchi ya Equateur.

15. Namna gani mufano wa Yakobo unaonyesha kama hatupaswe kuacha kuhubiria benye habayakubali habari njema? (Ona pia picha.)

15 Hatupaswe kuvunjika moyo wakati batu banakatala kusikiliza habari njema. Batu banaweza kubadilika. Fikiria mufano wa Yakobo ndugu ya Yesu. Aliona vile Yesu anakomala, anakuwa Masiya, na anaanza kufundisha batu mu njia ya ajabu sana. Lakini kwa miaka mingi, Yakobo hakukuwa mwanafunzi wa Yesu. Ni kisha tu Yesu kufufuliwa njo Yakobo alifikia kuwa mwanafunzi na alikuwa mwanafunzi mwenye bidii sana!b (Yoh. 7:5; Gal. 2:9) Njo maana hatupaswe kuvunjika moyo. Ni jambo ya maana tuendelee kuhubiria batu ya mu familia yetu benye mupaka sasa habayapendezwa na tuendelee kuhubiria batu benye zamani balikatala habari njema. Kumbuka kama tunaishi mu siku za mwisho. Kwa hiyo kazi yetu ya kuhubiri ni ya haraka sana. Pengine batu batakumbukaka mambo yenye tuko nabaambia leo. Banaweza kuikumbuka, hata kisha taabu kubwa kuanza.c

Dada mwenye iko nafanya funzo yake ya kipekee anaita dada yake mwenye haiko Shahidi, ule dada yake iko nanunua vitu mu duka fulani pamoya na mutoto wake mwanamuke.

Nini inaweza kutusaidia tusiache kuhubiria batu ya familia yetu benye habayaamini? (Ona fungu ya 15)e


ENDELEA KUONYESHA SHUKRANI JUU YA VIKUMBUSHO VYA YEHOVA

16. Vikumbusho vya Yehova vimekusaidia namna gani? (Ona pia kisanduku “Tumikisha Kweli za Biblia Juu ya Kusaidia Bengine.”)

16 Chakula fulani ya kiroho inatayarishwa juu ya kusaidia bale benye habajue mafundisho ya musingi ya Biblia. Kwa mufano, hotuba ya watu wote ya ku mukutano wa mwisho wa juma, habari na video fulani ku jw.org, na magazeti ya watu wote, inatayarishwa kwanza kwa ajili ya batu benye habiko Mashahidi. Lakini vikumbusho vyenye kuwa mu zile habari vinatusaidia siye bote. Vinatusaidia tumupende Yehova zaidi, tutumainie zaidi Neno yake, na tufundishe muzuri mafundisho ya musingi ya Biblia.—Zb. 19:7.

Tumikisha Kweli za Biblia Juu ya Kusaidia Bengine

Wakati unasoma habari fulani, unaona video, ao unasikia hotuba yenye ilitayarishwa juu ya wapya wenye wanapendezwa na kweli, fikiria namna unaweza kutumikisha ile mambo juu ya kusaidia bengine. Unaweza kujiuliza hivi:

  • ‘Banasema mambo gani juu ya kusaidia batu baamini hii fundisho ya Biblia?’

  • ‘Ni mufano gani ya muzuri yenye ninaweza kutumikisha wakati niko nafundisha mutu hii kweli ya Biblia?’

  • ‘Nani anaweza kufurahia hii habari na ni wakati gani ninaweza kuzungumuza naye juu ya hii kweli?’

17. Ni mu hali gani unaweza kufikiria mafundisho ya musingi ya Biblia?

17 Siye batu ya Yehova, tunafurahiaka sana wakati tunapata mafasirio ya mupya ya kweli za Biblia. Lakini tunafurahiaka pia sana mafundisho ya musingi ya Biblia yenye ilitusaidia kukubali kweli. Kama wakati moya inatufikia kutafuta kukazia mawazo yetu kuliko kutegemea muongozo wa tengenezo ya Yehova, ni muzuri tukumbuke kama mwenye iko naongoza tengenezo ni Muumbaji mwenye hekima sana na Mweza Yote. Wakati batu benye tunapenda ao siye benyewe tunapata mateso, tunavumilia na tunakumbuka juu ya nini Yehova anaruhusu mateso. Na wakati tuko naamua namna ya kutumikisha wakati na mali yetu, tunakumbuka kama tunaishi siku za mwisho na kunabakia wakati kidogo mbele mwisho ifike. Tuache basi vikumbusho vya Yehova vitusaidie kuwa na hekima na kuendelea kumutumikia kwa uaminifu.

HII MAFUNDISHO YA MUSINGI YA BIBLIA, INAKUFUNDISHA NINI?

  • Yehova ni Muumbaji

  • Juu ya nini Yehova anaacha batu bateseke

  • Tunaishi mu “siku za mwisho”

WIMBO 95 Mwangaza Unaendelea Kuongezeka

a Ona habari “Sababu Kwa Nini Mateso Yote Yatakwisha Karibuni” Mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 2007, uku. 21-25.

b Ona somo ya 8 ya broshua Penda Watu Juu Ufanye Wanafunzi.

c Ona habari “Tunajua Nini Juu ya Namna Yehova Atahukumu Watu?” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 5, 2024 uku. 8-13.

d MAFASIRIO YA PICHA: Muzee moya anatoa wazo yenye bazee bengine habakubali. Kisha, busiku wakati iko naangalia nyota anafikiri sana kuhusu uumbaji na anaelewa kama mapenzi ya Yehova njo ya maana kupita mambo yenye yeye anapenda.

e MAFASIRIO YA PICHA : Mu funzo yake ya kipekee dada iko najifunza mambo yenye inaonyesha kama tunaishi mu siku za mwisho. Ile inamuchochea aite na ahubirie dada yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine