HABARI YA KUJIFUNZA YA 31
WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha
‘Umejifunza Siri’ ya Kutosheka?
“Nimejifunza kutosheka hata hali zangu zikuwe namna gani.”—FLP. 4:11.
WAZO KUBWA
Namna kuwa na shukrani, kukazia akili mapenzi ya Yehova na kuwa wanyenyekevu, na kufikiri sana juu ya tumaini yetu ya wakati wenye kuya kunatusaidia kujifunza kutosheka.
1. Kutosheka inamaanisha nini, lakini haimaanishe nini?
UNAKUWAKA mutu wa kutosheka? Mutu wa kutosheka anafurahiaka mambo yenye iko nayo. Hajisikie mubaya ao hakasirike juu kuko byenye anakosa. Lakini kuwa mwenye kutosheka haimaanishe kama mutu atajiachilia tu. Kwa mufano ni muzuri Mukristo aendelee kutafuta nafasi za kumutumikia Yehova zaidi. (Ro. 12:1; 1 Ti. 3:1) Lakini kama pendeleo zenye anapenda kuwa nazo hazifike mbio, hapoteze furaha yake.
2. Juu ya nini ni hatari sana kama mutu hatoshekake?
2 Kama hatutosheke na byenye tuko nabyo, tunaweza kuingia mu mambo mingi ya mubaya. Mutu mwenye hatosheke anaweza kutumika sana na kwa wakati murefu juu apate bitu byenye hana hata nabyo lazima. Jambo ya kuhuzunisha ni kama, Bakristo fulani bamefikia hata kuiba makuta ao bitu bingine byenye balipenda kupata. Bamoya balijiambia hivi: ‘Ninastahili kabisa kupata hii kitu,’ ao ‘nilishachunga sana hii kitu,’ ao tena ‘nibebe kwanza, nitarudisha kisha.’ Lakini Yehova anachukia sana kila namna ya kuiba. (Mez. 30:9) Bengine balivunjika moyo juu habakupata pendeleo yenye balichunga kwa wakati murefu, na bameacha hata kumutumikia Yehova. (Gal. 6:9) Namna gani mutu mwenye alijitoa kwa Yehova anaweza kufanya bya vile? Shida inaweza kuwa kwamba ule Mukristo hajikaze tena kuwa mwenye kutosheka.
3. Wafilipi 4:11, 12 inatufundisha jambo gani ya maana?
3 Siye bote tunaweza kujifunza kutosheka. Mutume Paulo aliandika kama ‘amejifunza kutosheka hata hali [zake] zikuwe namna gani.’ (Soma Wafilipi 4:11, 12.) Aliandika ile maneno wakati alikuwa mu gereza. Hata kama alikuwa mu gereza, hakupoteza furaha yake juu alijifunza siri ya kutosheka. Kama ni nguvu kwetu kutosheka, maneno na mufano wa Paulo inaweza kutusaidia kujifunza kutosheka. Tusiwaze kama tutatosheka na hali yetu hivi tu bila kujikaza. Inaomba tujifunze kutosheka. Tutafanya vile namna gani? Acha tuzungumuzie sifa zenye zinaweza kutusaidia tujifunze siri ya kutosheka.
UKUWE NA SHUKRANI
4. Juu ya nini kuwa na shukrani kunatusaidia kutosheka? (1 Watesalonike 5:18)
4 Mutu mwenye iko na shukrani anakuwaka pia wa kutosheka. (Soma 1 Watesalonike 5:18.) Kwa mufano, wakati tuko na shukrani juu ya mambo ya lazima yenye tuko nayo, hatuhangaikie sana mambo yenye tunapenda kupata lakini yenye hatuna. Wakati uko mwenye shukrani juu ya pendeleo yenye uko nayo, unafanya yako yote ili kuitumikia muzuri zaidi, kuliko kuhangaika sana juu upate mapendeleo ingine. Njo maana hata Maandiko inatutia moyo tukuwe namushukuru Yehova mu sala zetu. Kuwa na shukrani kunatusaidia kuwa na “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.”—Flp. 4:6, 7.
5. Baisraeli balikuwa na sababu gani za kuwa na shukrani? (Ona pia picha.)
5 Tufikirie mambo yenye ilifikia Baisraeli. Mara mingi balikuwa nalalamika mbele ya Yehova na kusema kama balikosa chakula yenye balikuwa nayo mu Misri. (Hes. 11:4-6) Ni kweli kama maisha haikukuwa mwepesi mu jangwa. Lakini, nini njo ingebasaidia bakuwe benye kutosheka? Balipaswa kufikiria mambo yote yenye Yehova alikuwa alishabafanyia na kuonyesha shukrani juu ya ile mambo. Kwa mufano, mu Misri balibatesa sana juu balikuwa batumwa. Lakini Yehova alipiga Bamisri kwa pigo kumi na kukomboa Baisraeli. Kisha kukombolewa, ‘balinyanganya Bamisri’ feza, zahabu, na manguo. (Kut. 12:35, 36) Wakati Bamisri balibafuata mupaka ku Bahari Nyekundu, kwa muujiza Yehova alifungula bahari na bakaponyoka. Zaidi ya ile, Yehova alikuwa nabapatia mana kila siku. Sasa shida ya Baisraeli ilikuwa nini? Shida yabo haikukuwa kukosa chakula, lakini ilikuwa kukosa shukrani juu ya mambo yenye tayari balikuwa nayo. Na njo maana habakukuwa benye kutosheka.
Juu ya nini Baisraeli habakutosheka? (Ona fungu ya 5)
6. Namna gani tunaweza kujifunza kuwa na shukrani?
6 Namna gani unaweza kujifunza kuwa mwenye shukrani? Kwanza, kila siku ukamate wakati wa kufikiri juu ya mambo yenye uko nayo. Unaweza hata kuandika mambo mbili ao tatu yenye uko nayo yenye inakufurahisha. (Omb. 3:22, 23) Pili, ushukuru bengine. Uambie bengine aksanti juu ya mambo yenye banakufanyia. Zaidi ya yote umushukuru Yehova kila wakati. (Zb. 75:1) Tatu, fanya urafiki na batu benye banaonyeshaka shukrani. Juu ya nini? Juu kama barafiki yetu ni benye shukrani na siye tutakuwa na shukrani, lakini kama habana shukrani na siye hatutakuwa na shukrani. (Kum. 1:26-28; 2 Ti. 3:1, 2, 5) Wakati tunatafuta nafasi za kuonyesha shukrani, hatutakuwa tena na wakati wa kujisikia mubaya juu ya mambo yenye tungependa kuwa nayo yenye hatuna.
7. Namna gani dada Aci alifikia kuwa na shukrani na ile ilikuwa na matokeo gani?
7 Fikiria mambo yenye ilimupata dada Aci, wa Indonesia. Anasema hivi: “Mu kipindi ya Korona nilianza kulinganisha hali yangu na ya bengine. Ile ilifanya nisitosheke tena.” (Gal. 6:4) Nini njo ilisaidia dada yetu kubadilisha mawazo yake? Dada Aci anasema hivi: “Nilianza kuhesabia mambo yenye Yehova alikuwa nanipatia kila siku. Na nilikuwa nafikiria baraka mingi zenye niko nazo juu niko mu tengenezo ya Yehova. Kisha nilikuwa namushukuru Yehova. Ile ilinisaidia nikuwe mwenye kutosheka kabisa.” Kama na weye haufurahie hali yako, kufanya vile dada Aci alifanya kunaweza kukusaidia ukuwe na shukrani.
UKAZIE AKILI MAPENZI YA YEHOVA NA UENDELEE KUWA MUNYENYEKEVU
8. Ni nini ilimufikia Baruku?
8 Wakati fulani Baruku, mwandishi wa nabii Yeremia, hakutosheka tena na hali yake. Alikuwa na kazi ya nguvu. Alipaswa kumusaidia Yeremia wakati Yeremia alikuwa natolea Baisraeli benye habana shukrani ujumbe wa hukumu. Wakati fulani Baruku alianza kukazia akili mambo yenye yeye anapenda, kuliko kukazia akili mambo yenye Yehova anapenda afanye. Kupitia Yeremia Yehova alimuambia hivi Baruku: “Unajitafutia mambo makubwa. Acha kutafuta mambo hayo.” (Yer. 45:3-5) Ni sawa vile Yehova alikuwa namuambia hivi: “Tosheka na hali yako ya sasa.” Baruku alikubali ile shauri na Yehova aliendelea kumukubali.
9. 1 Wakorinto 4:6, 7 inatufundisha nini? (Ona pia picha.)
9 Wakati fulani, Mukristo anaweza kuwaza kama anastahili kupewa pendeleo fulani. Anaweza kuwaza vile juu pengine iko na uwezo fulani ao anatumikaka sana ao tena iko na uzoefu mingi. Na pengine iko na ile mambo yote tatu. Lakini inawezekana banapatia mutu mwingine pendeleo yenye ule Mukristo alikuwa napenda. Atafanya nini kama anajisikia mubaya juu ya ile jambo? Anaweza kufikiria maneno yenye mutume Paulo aliandika, yenye inapatikana mu 1 Wakorinto 4:6, 7. (Soma.) Kila pendeleo yenye tunapata na uwezo wowote wenye tuko nao unatoka kwa Yehova. Yehova hatupatiake ile mambo juu tuko ba maana kupita bengine. Lakini ile mambo ni zawadi yenye hatustahili, yenye Yehova anatupatia juu anatupenda.—Ro. 12:3, 6; Efe. 2:8, 9.
Yehova njo alitupatia kila uwezo wenye tuko nao (Ona fungu ya 9)b
10. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe banyenyekevu?
10 Kama tunafikiri sana juu ya mufano wa Yesu na tunamuiga, tunaweza kujifunza kuwa b anyenyekevu. Yesu alinawisha mitume wake migulu, hata kama alijua kama yeye ni mutoto wa Mungu na iko na mamlaka ya mingi. Mutume Yohana aliandika hivi: “Yesu, kwa sababu alijua kwamba Baba alikuwa ametia vitu vyote katika mikono yake na kwamba alikuja kutoka kwa Mungu na alikuwa anaenda kwa Mungu, . . . akaanza kunawisha wanafunzi miguu.” (Yoh. 13:3-5) Yesu angewaza kama ni yeye njo balipaswa kunawisha migulu. Lakini hakuwaza vile juu alikuwa munyenyekevu. Hakuna hata siku moya yenye aliwaza kama, juu yeye ni Mwana wa Mungu anapaswa kuwa na nyumba ya muzuri, makuta ya mingi, na maisha ya bila magumu. (Lu. 9:58) Alitosheka na hali yake. Yesu alituachia mufano muzuri wa kufuata.—Yoh. 13:15.
11. Ni nini imesaidia Dennis akuwe na unyenyekevu?
11 Ndugu Dennis, wa Pays-bas anajikaza kufuata mufano wa Yesu, hata kama wakati fulani haiko mwepesi kufanya vile. Anasema hivi: “Wakati fulani ninajisikiaka mubaya wakati mutu mwingine anapata pendeleo yenye niliwaza kama miye njo ninastahili kupata. Wakati ile inanifikia ninajifunza habari zenye zinahusu unyenyekevu. Mu JW Library® nilishafanya liste ya maandiko yenye inazungumuzia unyenyekevu juu niweze kuipata haraka na kuisoma tena. Pia, nilishatia mu telefone yangu mahotuba zenye zinazungumuzia unyenyekevu, na ninazisikilizaka mara kwa mara.a Nimejifunza kama kazi yote yenye tunafanya ni juu tumusifu Yehova, hapana juu tujisifu. Haiko kwa nguvu yetu njo tunafanyaka ile kazi.” Ukiona kama hauna tena furaha juu haupate pendeleo fulani yenye unapenda, ujifunze kuwa na unyenyekevu.—Yak. 4:6, 8.
FIKIRI SANA JUU YA TUMAINI YAKO
12. Ni tumaini gani yenye inatusaidia tukuwe wenye kutosheka? (Isaya 65:21-25)
12 Tunakuwa wenye kutosheka zaidi wakati tunafikiri sana juu ya tumaini ya muzuri yenye iko mbele yetu. Mu kitabu ya Isaya, Yehova anaonyesha kama anaelewa kama maisha ya leo iko nguvu. Lakini anaahidi pia kama atatosha magumu yote. (Soma Isaya 65:21-25.) Tutakuwa na manyumba ya muzuri, tutakuwa na kazi ya muzuri, na tutakula chakula ya butamu na ya kujenga mwili. Hatutakuwa tena na wasiwasi kwamba kitu ya mubaya itatufikia siye ao batoto yetu. (Isa. 32:17, 18; Eze. 34:25) Kwa kweli, maisha yetu itakuwa ya muzuri sana.
13. Ni mu hali gani njo tunapaswa fikiria sana tumaini yetu?
13 Leo njo tunapaswa kufikiria sana tumaini yetu kupita wakati ingine. Juu ya nini? Juu tunaishi mu “siku za mwisho” na siye bote tuko napata magumu yenye iko “ngumu kuvumilia.” (2 Ti. 3:1) Kila siku Yehova anatusaidia kuvumilia kwa kutuongoza, kwa kututia nguvu na kutupatia musaada wenye tuko nao lazima. (Zb. 145:14) Zaidi ya ile, tumaini yetu inaweza kutusaidia sana wakati tuko na magumu. Ni nguvu kwako kupata bitu byenye familia yako iko nabyo lazima juu ya kuishi? Je, ni kusema kama utaendelea tu kuwa maskini? Hapana! Yehova ameahidi kama mu Paradiso atakupatia mambo yote yenye uko nayo lazima, na hataishia pale, atakupatia pia mambo ingine ya mingi. (Zb. 9:18; 72:12-14) Uko na maumivu ya kila siku, magonjwa ya kushuka moyo ao magonjwa ingine ya nguvu? Je, ni kusema hautaponaka na maisha yako itaendelea tu kuwa ya maumivu? Hapana. Magonjwa na kifo habitakuwa mu dunia mupya ya Mungu. (Ufu. 21:3, 4) Ile tumaini inatusaidia tusivunjike moyo ao kukasirika juu ya mambo yenye iko natufikia leo. Tunaweza kuendelea kuwa na furaha na amani, hata kama tunatendewa bila haki, tunafisha mupendwa wetu, ao hata kama kitu ingine ya mubaya inatufikia. Juu ya nini? Juu hata tukuwe mu magumu ya namna gani leo, tunajua kama “taabu ni ya wakati kidogo,” na kama mu dunia mupya hatutatesekaka tena.—2 Ko. 4:17, 18.
14. Namna gani tunaweza kutia nguvu tumaini yetu?
14 Tunajua kama tumaini ni ya maana sana juu tutosheke na hali yetu. Sasa namna gani tunaweza kutia nguvu tumaini yetu? Kwa mufano, mutu anaweza kuwa na lazima ya kuvala malineti juu aweze kuona muzuri bitu byenye biko mbali. Na siye tunapaswa kuvala malineti ya mufano, ni kusema kukamata hatua ya kutia nguvu tumaini yetu. Ile itatusaidia tuone muzuri Paradiso yenye iko mbele yetu. Wakati tuko nahangaika juu hatuna makuta, tufikirie namna maisha itakuwa wakati makuta, madeni, na umaskini hautakuwa tena. (1 Ti. 6:19) Na ikiwa tuko nahangaika juu hatuyapata mapendeleo fulani, tunaweza kufikiria namna ile mambo haitakuwa tena ya maana wakati tutakuwa wakamilifu na tutakuwa tulishatumikia Yehova kwa miaka mingi sana. Juu leo tuko na mambo mingi sana yenye inatuhangaisha, inaweza kuwa nguvu kwetu kutafakari juu ya ahadi za wakati wenye kuya. Lakini kama tunaendelea kujifunza kufikiria zile ahadi kila wakati, itakuwa mwepesi kukazia akili tumaini yetu, kuliko kukazia akili magumu yenye tuko nayo.
15. Maneno ya Christa inakufundisha nini?
15 Tuone namna tumaini imesaidia dada Christa, bibi ya ndugu Dennis mwenye tulizungumuzia. Dada Christa anasema hivi “Niko na ugonjwa wenye unanimaliza nguvu mu mwili. Siwezi hata kutembea. Ninalazimika kutumikisha kinga ya vilema. Ninapitishaka wakati mingi ku kitanda na ninasikiaka maumivu kila siku. Munganga wangu aliniambia kama hali yangu haitatengemana. Palepale niliwaza hivi: ‘Yeye haone maisha yangu ya kesho sawa vile niko naiona.’ Nakazia akili tumaini yangu na ile inanipatia amani. Leo niko navumilia magumu ya mingi mu hii dunia. Lakini mu dunia mupya nitakuwa na maisha ya muzuri sana!”
“WALE WENYE KUMUOGOPA HAWAKOSE KITU”
16. Juu ya nini Mufalme Daudi aliandika kama benye banamuogopa Yehova ‘habakose kitu’?
16 Hata kama siye batumishi ya Yehova tuko benye kutosheka, tutapata tu magumu. Fikiria Mufalme Daudi. Biblia inasema kama batoto yake tatu balikufa. Zaidi ya ile, batu balimusemea mambo ya bongo, balimusaliti, na aliishi maisha ya kukimbia-kimbia kwa miaka mingi juu Mufalme Sauli alikuwa natafuta kumuua. Hata kama Daudi alikuwa na ile magumu yote, alikuwa mwenye kutosheka. Alisema hivi juu ya Yehova: “Wale wenye kumuogopa hawakose kitu.” (Zb. 34:9, 10) Juu ya nini Daudi alisema vile? Juu alijua kama, hata kama Yehova hatazuia magumu ipate batumishi yake, atabapatia mambo yote yenye biko nayo lazima kabisa. (Zb. 145:16) Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatutegemeza mu magumu yetu yote. Ile inatusaidia tukuwe wenye kutosheka.
17. Juu ya nini unapaswa kuazimia kujifunza siri ya kutosheka?
17 Yehova anapenda tukuwe batu benye kutosheka. (Zb. 131:1, 2) Kwa hiyo, fanya yote yenye unaweza juu ujifunze siri ya kuwa mwenye kutosheka. Kama unajikaza kuwa na shukrani, kukazia akili mapenzi ya Yehova, kukuwa munyenyekevu, na kama unatia nguvu tumaini yako, utaweza kusema: “Ndiyo, nimetosheka.”—Zb. 16:5, 6.
WIMBO 118 “Unipatie Imani Zaidi”
a Kwa mufano, ku jw.org uangalie hizi video za Ibada ya Asubui zenye kichwa Yehova Anahangaikiaka Wanyenyekevu na Kiburi Hutangulia Kuanguka kwa Kishindo.
b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu iko nafanya kazi ya kutunza majengo fulani ya tengenezo, dada mwenye alijifunza luga ya ishara iko naulizwa maulizo ku mukusanyiko wa muzunguko, na ndugu iko natoa hotuba ya watu wote.