Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 8 uku. 2-7
  • Namna Yehova Anatusaidia Kuvumilia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Yehova Anatusaidia Kuvumilia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SALA
  • BIBLIA
  • NDUGU NA DADA
  • TUMAINI YETU
  • Kumbuka Kama Yehova Ni “Mungu Mwenye Kuishi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Barua Yenye Inaweza Kutusaidia Kuvumilia kwa Uaminifu Mupaka Mwisho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 8 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

Namna Yehova Anatusaidia Kuvumilia

“Mungu wa fazili zote zenye hazistahiliwe . . . atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.”—1 PE. 5:10.

WAZO KUBWA

Mambo yenye Yehova anatupatia juu tuweze kuvumilia, na namna tunaweza kutumikisha ile mambo.

1. Juu ya nini tuko na lazima ya uvumilivu, na ni nani njo atatusaidia? (1 Petro 5:10)

MU HIZI siku za mwisho muko magumu ya mingi. Njo maana siye batu ya Yehova tuko na lazima ya uvumilivu. Bamoya biko na magonjwa kwa wakati murefu, bengine bamefisha, na bengine banapambana na upinzani mu familia ao kutoka kwa serikali. (Mt. 10:18, 36, 37) Ukuwe hakika kama hata ukuwe na magumu gani, Yehova atakusaidia kuvumilia.—Soma 1 Petro 5:10.

2. Nguvu ya kuvumilia ya Bakristo inatoka wapi?

2 Kuvumilia ni kuendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu na kwa furaha hata kama tunakutana na magumu, majaribu, na upinzani. Kuvumilia ni kuwa pia hakika kama mambo itakuwa muzuri. Siye Bakristo tunaweza kuvumilia, lakini haiko kwa nguvu yetu. Nguvu ya kuvumilia inatoka kwa Yehova mwenye anatupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Ko. 4:7) Mu hii habari tutazungumuzia mambo ine yenye Yehova anatupatia juu tuweze kuvumilia. Tutaona pia namna tunaweza kutumikisha ile mambo.

SALA

3. Juu ya nini tunaweza kusema kama sala ni muujiza?

3 Sala ni jambo ya ajabu sana yenye Yehova ametupatia juu tuweze kuvumilia. Kupitia sala tunaweza kuzungumuza na Yehova hata kama tuko banadamu benye zambi. (Ebr. 4:16) Waza kidogo: Tunaweza kusali kwa Yehova saa yoyote, na tunaweza kumuambia mambo yote. Yehova anaweza kutusikiliza hata tuseme luga gani na hata tuko wapi, hata tuko mbali na batu bengine ao tuko mu gereza. (Yon. 2:1, 2; Mdo. 16:25, 26) Na kama tuko na mahangaiko ya mingi mupaka tunashindwa namna ya kujieleza, Yehova anaelewa mambo yenye tulipenda kusema. (Ro. 8:26, 27) Kwa kweli, sala ni muujiza!

4. Juu ya nini kuomba Yehova atusaidie kuvumilia kunapatana na mapenzi yake?

4 Yehova anatuhakikishia mu Neno yake kama “hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” (1 Yo. 5:14) Tunaweza kumuomba Yehova atusaidie kuvumilia? Ndiyo! Kufanya vile kunapatana na mapenzi yake. Juu ya nini? Juu wakati tunavumilia magumu, tunamupatia nafasi ya kujibia Shetani mwenye anamuchokoza. (Mez. 27:11) Zaidi ya ile, Biblia inatuambia kama Yehova anapenda “kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.” (2 Ny. 16:9) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo na iko pia na nia ya kutusaidia kuvumilia.—Isa. 30:18; 41:10; Lu. 11:13.

5. Namna gani sala inatusaidia kutulia? (Isaya 26:3)

5 Biblia inasema kama wakati tunasali juu ya mambo yenye iko natuhangaisha, ‘amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili.’ (Flp. 4:7) Tunamushukuru sana Yehova kwa ile. Batu benye habamutumikie Yehova, nabo banapataka magumu na banajaribu njia mbalimbali za kubasaidia kupata amani ya akili. Lakini amani yenye Yehova anatupatia wakati tunasali ni ya hali ya juu sana. Wakati tunasali kwa Yehova tunaonyesha kama tunamutegemea kabisa, na anatupatia “amani ya kudumu.” (Soma Isaya 26:3.) Njia moya yenye Yehova anatumia juu ya kutupatia amani yake ni kutusaidia tukumbuke maandiko yenye inatufariji. Ile maandiko inatukumbusha kama Yehova anatupenda na anapenda kutusaidia. Kukumbuka vile kunatutuliza.—Zb. 62:1, 2.

6. Unaweza kufanya nini juu sala ikusaidie? (Ona pia picha.)

6 Mambo yenye unaweza kufanya. Wakati uko na magumu, “umutupie Yehova muzigo wako” na umuombe akupatie amani yake. (Zb. 55:22) Umuombe pia akupatie hekima yenye itakusaidia ujue mambo ya kufanya. (Mez. 2:10, 11) Lakini usisaabu pia kumushukuru. (Flp. 4:6) Tafuta mambo yenye inaonyesha kama Yehova iko nakusaidia kuvumilia magumu yako na umushukuru juu ya ile mambo. Usiache magumu ikufunge macho mupaka ushindwe kuona baraka zenye uko nazo.—Zb. 16:5, 6.

Mu kipindi ya baridi, ndugu mwenye kukomala anaikala mu nyumba yake na iko nasali. Ku migulu yake kuko Biblia yenye iko wazi na ku meza yenye kuwa pembeni yake kuko chupa ya dawa.

Wakati unasali unaambia Yehova mambo yako. Wakati unasoma Biblia unasikiliza maneno ya Yehova (Ona fungu ya 6)b


BIBLIA

7. Namna gani kujifunza Biblia kunaweza kutusaidia tuvumilie?

7 Yehova ametupatia Neno yake juu itusaidie kuvumilia. Mu Biblia muko maandiko ya mingi yenye inatuhakikishia kama Yehova atatusaidia kuvumilia. Kwa mufano, Matayo 6:8 inasema hivi: “Baba yenu anajua kile chenye muko nacho lazima hata mbele mumuombe.” Juu ya nini tuko hakika kama Yehova atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima wakati tuko na magumu? Juu Yesu njo alisema ile maneno na anajua Yehova muzuri sana. Mu Biblia muko maandiko ingine ya mingi yenye inaweza kutupatia nguvu ya kuendelea kuvumilia.—Zb. 94:19.

8. (a) Toa mufano wa kanuni fulani ya Biblia yenye inaweza kutusaidia kuvumilia. (b) Ni nini inaweza kutusaidia kukumbuka kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia?

8 Mu Biblia muko kanuni zenye zinaweza kutusaidia kuvumilia. Zile kanuni zinaweza kutusaidia tukuwe na hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri. (Mez. 2:6, 7) Kwa mufano, Biblia inatutia moyo tusihangaikie sana byenye binaweza fika kesho ao kesho yake. Kila siku na magumu yake. (Mt. 6:34) Kama tunazoea kusoma Biblia na kutafakari juu ya mambo yenye tuko nasoma, wakati tunajikuta mu magumu itakuwa mwepesi kwetu kukumbuka kanuni za Biblia zenye zinaweza kutusaidia.

9. Habari zenye ziko mu Biblia za batumishi ya Yehova zinatusaidia namna gani?

9 Mu Biblia muko pia hadisi za batu benye balikuwa tu sawa siye benye balimutegemea Yehova, na Yehova alibasaidia. (Ebr. 11:32-34; Yak. 5:17) Wakati tunafikiria vile Yehova alibasaidia, tunakuwa hakika kama na siye atatusaidia. Yehova ni “kimbilio letu na nguvu zetu, musaada wenye kupatikana kwa urahisi nyakati za taabu.” (Zb. 46:1) Na wakati tunafikiria namna batumishi ba zamani ba Yehova baliendelea kuwa baaminifu mu magumu, na siye tunatiwa moyo kuiga imani yao na uvumilivu wao.—Yak. 5:10, 11.

10. Unaweza kufanya nini juu Neno ya Mungu ikusaidie?

10 Mambo yenye unaweza kufanya. Soma Biblia kila siku na ufanye liste ya maandiko yenye unaona inaweza kukusaidia sana. Ndugu na dada ba mingi banasomaka andiko ya siku asubui. Ile inafanya bafikirie mawazo ya ile andiko muchana yote. Dada Mariea alijionea kama kufanya vile kulimusaidia sana wakati bazazi yake bote bawili baligonjwa kansere. Ni nini njo ilimusaidia avumilie wakati alikuwa nashugulikia bazazi yake mbele bakufe? Anasema hivi: “Kila asubui nilikuwa nasoma andiko ya siku mu broshua Tuchunguze Maandiko Kila Siku na nilikuwa natafakari juu ya mambo yenye ninasoma. Ile ilinisaidia nikazie akili Yehova na mambo ya muzuri yenye anatufundisha mu Neno yake, kuliko kukazia akili magumu yangu.”—Zb. 61:2.

NDUGU NA DADA

11. Juu ya nini inatia moyo kujua kama hatuko siye peke wakati tunapata magumu?

11 Yehova ametupatia ndugu na dada ba mu dunia yote juu batusaidie kuvumilia. Kujua tu kama ‘mateso yaleyale yanapata ushirika muzima wa ndugu zetu’ kunatusaidia tukuwe hakika kama hatuko siye peke. (1 Pe. 5:9) Hata tupate magumu gani, tuko hakika kama bengine balipata magumu ya vile na bakaweza kuivumilia. Ile inaonyesha kama na siye tunaweza kuivumilia!—Mdo. 14:22.

12. Namna gani ndugu na dada banatusaidia, na siye tunaweza kubasaidia namna gani? (2 Wakorinto 1:3, 4)

12 Ndugu na dada banaweza kutusaidia kuvumilia kupitia maneno na matendo yabo. Mutume Paulo naye alijionea ile. Ndugu na dada balimufariji, balimutia moyo, na balimupatia mambo yenye alikuwa nayo lazima. Njo maana mu barua zake Paulo alitaya na kushukuru ndugu na dada benye balimusaidia wakati alifungwa mu nyumba. (Flp. 2:25, 29, 30; Kol. 4:10, 11) Na leo mambo inakuwaka vile. Wakati tuko na lazima ya musaada juu ya kuvumilia, ndugu na dada biko pale juu yetu. Na wakati biko na lazima ya musaada na siye tuko pale juu yabo.—Soma 2 Wakorinto 1:3, 4.

13. Ni nini njo ilisaidia dada Maya kuvumilia?

13 Mu 2020 mu inchi ya Urusi, siku moya polisi iliingia mu nyumba ya dada mwenye kuitwa Maya na kuanza kutafuta-tafuta bitu. Kisha Maya alipaswa kuenda kusamba mbele ya tribinali juu tu alikuwa naongea na batu juu ya imani yake. Dada Maya anasema kama ndugu na dada balimutia moya sana mu ile kipindi ya nguvu. Anasema hivi: “Mu ile wakati sikukuwa najisikia muzuri, nilikuwa na mahangaiko na nilikuwa nachoka sana. Lakini ndugu na dada baliniita na kuniandikia juu ya kunihakikishia kama bananipenda. Tangu zamani nilikuwa najua kama tuko familia kubwa ya ndugu na dada benye upendo, lakini tangu 2020 njo nimeelewa muzuri zaidi ile jambo.”

14. Tunaweza kufanya nini juu tufaidike na musaada wa ndugu na dada wakati tuko na magumu? (Ona pia picha.)

14 Mambo yenye unaweza kufanya. Wakati uko navumilia magumu, bakia karibu ya ndugu na dada. Usisite kulomba bazee musaada. Biblia inasema kama bazee biko kama “mahali pa kujificha kwa sababu ya upepo, kimbilio kwa sababu ya zoruba ya mvua.” (Isa. 32:2, maelezo ya chini) Usisaabu kama Bakristo benzako nabo biko na magumu na biko naivumilia. Njo maana wakati unasaidia ndugu ao dada mwenye iko na magumu, ile inakuletea furaha na inakusaidia uendelee kuvumilia magumu yako.—Mdo. 20:35.

Mu kipindi ya kivukutu, ule ndugu mwenye kukomala anaikala mu nyumba yake na iko naongea kwa furaha pamoya na bibi na bwana na batoto yabo bawili banamuke. Pembeni yake kuko fimbo ya kumusaidia kutembea na chupa fulani za dawa. Mutoto moya iko namuonyesha picha ya Paradiso yenye alichora.

Bakia karibu na ndugu na dada zako (Ona fungu ya 14)c


TUMAINI YETU

15. Namna gani tumaini ilimusaidia Yesu, na namna gani tumaini yetu inatusaidia? (Waebrania 12:2)

15 Yehova ametupatia tumaini yenye iko hakika yenye inatusaidia kuvumilia. (Ro. 15:13) Ni tumaini njo ilisaidia Yesu avumilie majaribu ya nguvu sana yenye alipata siku ya kifo yake. (Soma Waebrania 12:2.) Yesu alijua kama ikiwa anabakia muaminifu, ile itasaidia kutakasa jina ya Yehova. Alijua tena kama atarudia mbinguni na kuwa tena pamoya na Baba yake, na kisha wakati atatawala pamoya na ndugu zake watiwa-mafuta. Na siye tumaini yetu ya kuishi milele mu dunia mupya ya Mungu inatusaidia kuvumilia magumu yote yenye tunapata mu hii ulimwengu ya Shetani.

16. Namna gani tumaini ilisaidia dada yetu avumilie, na maneno yake inakufundisha nini?

16 Ona namna tumaini yetu ya kuishi mu dunia mupya ilisaidia dada Alla wa Urusi. Balikamata bwana yake na kumufunga wakati alikuwa anachunga asambe. Dada Alla anasema hivi: “Kusali na kufikiri sana kuhusu tumaini yetu ya wakati yenye kuya njo ilinisaidia nisivunjike moyo wakati balifunga bwana yangu. Nimeelewa kama magumu haitaendelea milele. Yehova atapata ushindi juu ya maadui wake, na siye pia tutapata ushindi.”

17. Tunaweza kuonyesha namna gani kama tuko na shukrani juu ya tumaini yenye Yehova anatupatia? (Ona pia picha.)

17 Mambo yenye unaweza kufanya. Kamata wakati ya kufikiria tumaini ya muzuri sana yenye Yehova anatuahidi. Ujiwazie uko mu dunia mupya na uone baraka zote zenye tutakuwa nazo. Ukifanya vile utaona kama majaribu na magumu yote yenye tuko nayo leo ni ya “wakati kidogo na ni nyepesi.” (2 Ko. 4:17) Ujikaze pia kuambia bengine kuhusu tumaini ya muzuri yenye Yehova anatupatia. Fikiria hali ya batu benye habamutumikie Yehova, nabo banapataka magumu lakini habajue mambo ya muzuri yenye Yehova anatuahidi. Ukibaambia hata tu mambo kidogo, ile inaweza kubapatia hamu ya kujua mambo mingi zaidi juu ya Ufalme wa Mungu na ahadi zake.

Ku mwanzo wa kipindi ya baridi, ule ndugu anaikala mu nyumba yake na iko nafikiri juu ya picha ya Paradiso yenye anaona ku tablete yake. Pembeni yake kuko kitu ya kumusaidia kutembea na machupa mingi ya dawa.

Kamata wakati wa kufikiria tumaini ya muzuri yenye Yehova anatuahidi (Ona fungu ya 17)d


18. Juu ya nini tuko hakika kama ahadi za Yehova zitatimia?

18 Kisha Yobu kuvumilia kwa uaminifu majaribu ya mingi, alimuambia hivi Yehova: “Sasa ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote na hauwezi kushindwa kutimiza kila jambo lenye unafikiria kufanya.” (Yob. 42:2) Yobu alijifunza kweli ya maana, alijifunza kama hakuna kitu yenye inaweza zuia Yehova kutimiza kusudi yake. Kujua ile kweli ya maana inaweza kututia nguvu wakati tuko navumilia magumu. Wazia hii hali: mwanamuke moya anagonjwa kwa wakati murefu. Anaenda kuona banganga ba mingi, lakini banashindwa kutunza magonjwa yake. Na ile inamuvunja moyo. Kisha anakutana na munganga mwenye iko na uzoefu mwenye anaelewa muzuri magonjwa yake na anamufasiria namna atamutunza. Mara moya ule mwanamuke anajisikia muzuri hata kama itaomba wakati mbele apone. Anaweza sasa kuvumilia juu sasa iko na tumaini kama atapona. Ni vile na siye, tuko hakika kama ahadi ya Mungu juu ya Paradiso itatimia, na ile inatusaidia tuendelee kuvumilia.

19. Tunapaswa kufanya nini juu tuweze kuvumilia?

19 Sawa vile tumeona Yehova anatupatia sala, Biblia, ndugu na dada, na tumaini juu ya kutusaidia kuvumilia. Kama tunatumikisha muzuri ile mambo, Yehova atatusaidia tuvumilie magumu yote yenye tunaweza kutana nayo mupaka wakati ulimwengu wa Shetani hautakuwa tena.—Flp. 4:13.

NAMNA GANI YEHOVA ANATUSAIDIA TUVUMILIE KUPITIA . . .

  • sala na Biblia?

  • ndugu na dada zetu?

  • tumaini yetu?

WIMBO 33 Umutupie Yehova Muzigo Wako

a Mu hii habari majina fulani imebadilishwa.

b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye kukomala anaendelea kuvumilia kwa uaminifu vile miaka iko napita.

c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye kukomala anaendelea kuvumilia kwa uaminifu vile miaka iko napita.

d MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye kukomala anaendelea kuvumilia kwa uaminifu vile miaka iko napita.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine