HABARI YA KUJIFUNZA YA 35
WIMBO 121 Tukomalishe Sifa ya Kujizuia
Namna ya Kupiganisha Tamaa za Mubaya
“Musiruhusu zambi iendelee kutawala kama mufalme katika miili yenu yenye inaweza kufa ili kutii tamaa zake.”—RO. 6:12.
WAZO KUBWA
Mambo yenye itatusaidia tusivunjike moyo wakati tuko na tamaa za mubaya na namna ya kupiganisha tamaa za mubaya.
1. Banadamu bote banapiganishaka nini?
ULISHAKATAMANI sana kufanya jambo yenye haimufurahishe Yehova? Kama ilishakakufikia, ujue kama ile inafikiaka batu yote. Biblia inasema hivi: “Hakuna jaribu lenye limewapata ninyi isipokuwa lile lenye kuwa la kawaida kwa watu.” (1 Ko. 10:13) Ni kusema hata ukuwe na tamaa gani, kuko batu bengine benye biko napiganisha tamaa ya vile. Hauko weye peke, na kwa musaada wa Yehova utaweza kuipiganisha.
2. Zungumuzia mifano ya tamaa fulani zenye Bakristo fulani na banafunzi fulani ya Biblia biko napiganisha. (Ona pia picha.)
2 Biblia inasema pia hivi: “Kila mutu anajaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.” (Yak. 1:14) Kitu yenye inajaribu mutu moya haiko njo yenye itajaribu mwingine. Kwa mufano, Bakristo fulani banaweza kujaribiwa kufanya uasherati na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yabo, Bakristo bengine banaweza kujaribiwa kufanya uasherati na mwanaume mwenzabo ao na mwanamuke mwenzabo. Benye zamani balikuwaka na tabia ya kuangalia pornografia banaweza kujaribiwa kurudilia ile tabia. Na benye balikuwa na tabia ya kutumia dawa za kulewesha ao kunywa sana banaweza kujaribiwa kurudilia tena zile tabia. Ile ni mifano fulani ya tamaa zenye Bakristo na banafunzi fulani ya Biblia biko napiganisha. Inawezekana siye bote tulishakajisikia vile mutume Paulo alijisikiaka wakati aliandika hivi: “Wakati ninataka kufanya mambo yenye kuwa sawa, mambo ya mubaya yako pamoja na mimi.”—Ro. 7:21.
Majaribu inaweza kutokea bila kutazamia, saa yoyote na fasi yoyote (See paragraph 2)c
3. Kama mutu alishashindwa kuachana na tamaa yenye iko napiganisha, anaweza kuwa na mawazo gani?
3 Kama uko na tamaa ya mubaya yenye ulishapiganisha kwa siku mingi lakini haiishe tu, unaweza kuwaza kama hautawezaka kuimaliza. Unaweza pia kuwaza kama hakuna tena tumaini, ni kusema Yehova hatakukubali tena juu tu uko na tamaa ya mubaya. Lakini ukuwe hakika kama ile mawazo yote mbili haiko ya kweli. Juu ya kujua juu ya nini tunasema vile, tutazungumuzia maulizo mbili mu hii habari: (1) Juu ya nini tunajisikiaka kama hatutaweza kupiganisha tamaa zetu na kama hakuna tena tumaini? (2) Unaweza kufanya nini juu uweze kupiganisha tamaa za mubaya?
“ULE MUOVU” ANAPENDA TUWAZE NINI?
4. (a) Juu ya nini Shetani anapenda tuwaze kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya? (b) Juu ya nini tuko hakika kama tutaweza kupiganisha tamaa za mubaya?
4 Shetani anapenda tuwaze kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya. Yesu alijua kama Shetani atafanya yake yote juu ya kutujaribu, njo maana alifundisha banafunzi yake kusali hivi: “Usituingize katika jaribu, lakini utukomboe na ule muovu.” (Mt. 6:13) Shetani anasema kama banadamu habataendelea kumutumikia Yehova kama banajaribiwa. (Yob. 2:4, 5) Namna gani Shetani anaweza kusema vile japo yeye njo alijaribiwa na tamaa yake na hakuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova? Kisha anawaza kama na siye tuko sawa yeye! Anawaza kama tutakuwa tayari kumuacha Yehova kama tunajaribiwa. Na hata aliwaza kama angeweza kushawishi Mwana wa Mungu afanye mambo ya mubaya! (Mt. 4:8, 9) Lakini, hatuna kabisa nguvu ya kupiganisha tamaa za mubaya? Tuko nayo! Sawa vile mutume Paulo alisema: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”—Flp. 4:13.
5. Tunajua namna gani kama Yehova iko hakika kama tunaweza kupiganisha tamaa za mubaya?
5 Yehova iko tofauti kabisa na Shetani. Yehova yeye iko hakika kabisa kama tutaweza kupiganisha tamaa za mubaya. Tunajua vile namna gani? Juu Yehova alitabiri kama kundi kubwa ya batu baaminifu bataokoka taabu kubwa. Waza kidogo: Yehova hawezi kusema bongo, na yeye peke anasema kama batu mingi, hapana batu kidogo tu, bataingia mu ulimwengu mupya bakiwa ‘bamefua kanzu zao na kuzifanya mweupe katika damu ya Mwana-Kondoo,’ ni kusema Yehova anabaona kuwa safi. (Ufu. 7:9, 13, 14) Ni wazi kama Yehova yeye iko hakika kama tunaweza kupiganisha tamaa za mubaya.
6-7. Juu ya nini Shetani anapenda tuwaze kama hakuna tena tumaini?
6 Pia, Shetani anapenda uwaze kama hakuna tena tumaini, Yehova hatakukubali juu tu uko na tamaa za mubaya. Lakini waza kidogo: Kati ya siye na Shetani, nani njo hana tumaini? Shetani njo hana tumaini. Yeye njo Yehova hatapatia uzima wa milele. (Mwa. 3:15; Ufu. 20:10) Lakini Shetani anapenda tuwaze kama na siye hatuna tumaini. Juu ya nini? Juu anatusikilia wivu, anajua kama tunaweza kupata baraka zenye yeye hawezi kupata. Biblia inatuhakikishia kama Yehova anapenda kutusaidia, hapana kutuhukumu. “Hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.”—2 Pe. 3:9.
7 Kwa hiyo, hatupaswe kuwaza kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya ao kama hakuna tena tumaini. Kama tunawaza vile, tutakuwa nawaza vile Shetani anapenda tuwaze. Tukielewa kama Shetani njo anapenda tuwaze vile, tutafanya yetu yote juu tumupinge.—1 Pe. 5:8, 9.
KUTOKAMILIKA INAWEZA KUFANYA TUWAZE NINI?
8. Zambi iko na maana gani ingine? (Zaburi 51:5) (Ona pia “Mafasirio ya Maneno Fulani.”)
8 Kuko jambo ingine yeye inaweza kufanya tuwaze kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya na kama hakuna tena tumaini, Yehova hatatukubali. Ni zambi yenye tuliriti kutoka kwa bazazi yetu ba kwanza.a—Yob. 14:4; soma Zaburi 51:5.
9-10. (a) Adamu na Eva balijisikia namna gani kisha kufanya zambi? (Ona pia picha.) (b) Zambi inafanya tujisikie namna gani?
9 Fikiria namna Adamu na Eva balijisikia kisha kufanya zambi. Balijificha na bakajaribu kujifunika. Kitabu Étude perspicace des Écritures inasema hivi juu ya ile: “Zambi ilifanya bajihukumu, bakuwe na mahangaiko, bajisikie kuwa habiko salama, na basikie haya.” Adamu na Eva habangekuwa tena na uhusiano wa muzuri pamoya na Yehova. Habangeweza kutoka mu hali ya kutokamilika. Ni sawa vile balibafungia mu nyumba yenye habangeweza kutoka ndani.
10 Lakini hali yetu iko tofauti kidogo na ya Adamu na Eva. Kupitia bei ya ukombozi, siye tunasamehewa na tunakuwa na zamiri safi. Lakini Adamu na Eva habafaidike na bei ya ukombozi. (1 Ko. 6:11) Hata vile, tuliriti zambi. Njo maana na siye tunakuwaka najihukumu, tunakuwaka na mahangaiko, tunajisikiaka hatuko salama, na tunasikiaka haya. Biblia inasema kama zambi inatawala banadamu yote. Inatawala “hata juu ya wale wenye hawakukuwa wamefanya zambi kwa njia ileile yenye Adamu alifanya kosa.” (Ro. 5:14) Kujua ile isituvunje moyo. Isitufanye tuwaze kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya na hakuna tena tumaini. Sasa tutafanya nini juu tusiwaze vile?
Zambi ilifanya Adamu na Eva bajihukumu, bakuwe na mahangaiko, bajisikie kama habiko salama, na basikie haya (Ona fungu ya 9)
11. Tunaweza kufanya nini kama tunajisikia kuwa hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya, na juu ya nini? (Waroma 6:12)
11 Vilevile juu hatukamilike, tunaweza kuwaza kama hatutaweza kupiganisha tamaa za mubaya. Ni sawa vile tuko nasikia sauti ndani yetu yenye iko “natuambia” hatutaweza. Juu ya nini hatupaswe kusikiliza ile sauti? Juu Biblia inatuambia kama hatulazimike kuacha zambi ‘itutawale kama mufalme.’ (Soma Waroma 6:12.) Ni kusema tunaweza kuamua kama hatutafanya mambo yenye tamaa fulani ya mubaya iko natusukuma kufanya. (Gal. 5:16) Yehova iko hakika kama tunaweza kushinda tamaa za mubaya. Kama hangekuwa hakika na ile jambo hangetuomba tupiganishe tamaa za mubaya. (Kum. 30:11-14; Ro. 6:6; 1 Te. 4:3) Kwa kweli tuko na uwezo wa kupiganisha tamaa za mubaya.
12. Tunaweza kufanya nini kama tunawaza kama Yehova hatatukubali, na juu ya nini?
12 Vilevile, juu hatukamilike tunaweza kuwaza kama hakuna tena tumaini, Yehova hatatukubali juu tu tuko na tamaa za mubaya. Ni sawa vile ndani yetu muko sauti yenye iko “natuambia” hakuna tena tumaini. Lakini hatupaswe kusikiliza ile sauti. Juu ya nini? Juu Biblia inafundisha kama Yehova anaelewa kama tuko batenda-zambi. (Zb. 103:13, 14) “Anajua mambo yote” juu yetu, anajua matokeo yenye zambi iko nayo juu ya kila mumoya wetu. (1 Yo. 3:19, 20) Kama tunajikaza kupiganisha tamaa za mubaya kwa kuepuka kufanya mambo yenye ile tamaa inatusukuma kufanya, Yehova atatuona kuwa safi. Juu ya nini tuko hakika na ile jambo?
13-14. Yehova hatatukubali juu tu tuko na tamaa ya mubaya? Fasiria.
13 Biblia inaonyesha kama kuko tofauti kati ya kutenda mambo ya mubaya na kuwa na tamaa ya mubaya. Mutu yeye peke njo anaamuaka kutenda jambo ya mubaya, lakini tamaa ya mubaya inaweza kuya tu bila mutu kupenda. Kwa mufano, mbele Bakorinto fulani bakuwe Bakristo, balikuwa nafanya uasherati pamoya na banaume benzabo. Paulo aliandika hivi: “Wengine wenu mulikuwa vile.” Je, ni kusema kisha kuwa Bakristo hakuna siku yenye balikuwaka tena na tamaa ya kufanya ile tendo ya buchafu? Inawezekana ile tamaa ilikuwa nabarudilia wakati fulani juu tamaa ya vile inakuwaka ilishatia mizizi. Lakini Yehova alikubali Bakristo benye balijizuia na kuepuka kutenda kulingana na ile tamaa. Alibaona kuwa ‘bamesafishwa bakakuwa safi.’ (1 Ko. 6:9-11) Ni vile leo pia.
14 Hata kama uko napiganisha tamaa ya namna gani unaweza kuishinda. Pengine hautaimaliza kabisa-kabisa, lakini unaweza kujizuia na kuepuka ‘kutimiza mapenzi ya mwili na ya mawazo yako.’ (Efe. 2:3) Unaweza kufanya vile namna gani na kufikia kushinda tamaa za mubaya?
NAMNA YA KUPIGANISHA TAMAA ZA MUBAYA
15. Juu tuweze kupiganisha tamaa za mubaya, juu ya nini tunapaswa kwanza kuitika kama tuko na uzaifu fulani?
15 Juu uweze kupiganisha tamaa za mubaya unapaswa kwanza kuitika kama uko na uzaifu fulani. Ukuwe muangalifu juu usijidanganye kwa “mawazo ya uongo.” (Yak. 1:22) Kupunguza buzito ya tatizo yenye uko nayo inaweza kufanya ikuwe mwepesi kuangukia mu jaribu. Kwa mufano, kama tatizo ya mutu ni kunywa sana, anaweza kujitetea hivi, ‘mbona fulani anakunywaka sana kunipita.’ Jambo ingine yenye inaweza kufanya ikuwe mwepesi kuangukia mu jaribu ni kulaumu bengine juu ya makosa yetu. Kwa mufano, kama mutu iko na tatizo ya kuangalia pornografia, anaweza kujitetea hivi, ‘kama bibi yangu angekuwa nanionyesha upendo, singekuwa naangalia pornografia.’ Kwa hiyo, usijaribu kufunika-funika makosa yako. Kama ulikosea, itika tu.—Gal. 6:7.
16. Unaweza kufanya nini juu usiangukie mu jaribu?
16 Zaidi ya kuitika kama uko na uzaifu fulani, unapaswa kuazimia kabisa kama hautajiachilia. Utajikaza sana juu usifanye jambo ya mubaya. (1 Ko. 9:26, 27; 1 Te. 4:4; 1 Pe. 1:15, 16) Ujiulize ni kitu gani njo inakuwaka nakujaribu sana na ni wakati gani njo inakuwaka nguvu kwako kupiganisha ile jaribu. Kwa mufano, inakuwaka nguvu kwako kupiganisha jaribu fulani wakati ulishachoka ao busiku sana? Ujitayarishe mu akili na uamue utafanya nini wakati ile jaribu itafika. Ni muzuri kufanya vile mbele ile jaribu ifike.—Mez. 22:3.
17. Mufano wa Yosefu unatufundisha nini? (Mwanzo 39:7-9) (Ona pia picha.)
17 Fikiria namna Yosefu alitenda wakati bibi ya Potifa alimutongoza. Alikatala palepale. (Soma Mwanzo 39:7-9.) Ile inaonyesha nini? Hata mbele bibi ya Potifa amutongoze, Yosefu alikuwa alishaamua kama hawezi kukamata bibi ya batu. Vilevile, mbele jaribu fulani ifike, ukuwe ulishaamua kama hautafanya jambo yoyote ya mubaya. Kama unafanya vile itakuwa mwepesi kwako kufanya jambo ya muzuri juu utakuwa ulishaamua bya kufanya.
Sawa Yosefu, upinge majaribu palepale! (Ona fungu ya 17)
‘ENDELEA KUJIJARIBU’
18. Unaweza kufanya nini ingine juu uweze kupiganisha tamaa za mubaya? (2 Wakorinto 13:5)
18 Juu ya kupiganisha tamaa za mubaya, unapaswa ‘kuendelea kujijaribu,’ maana yake unapaswa kuendelea kujichunguza juu ya kuona kwenye ulishafikia. (Soma 2 Wakorinto 13:5.) Mara kwa mara, chunguza mawazo yako na matendo yako na ufanye mabadiliko ikiwa ni lazima. Kwa mufano, hata kama uliweza kupinga jaribu fulani ujiulize hivi: ‘Ilinikamata wakati gani juu nikatale?’ Kama unaona kuwa ilikukamata wakati murefu, usijihukumu lakini ufanye mambo yenye itakusaidia utende muzuri zaidi siku ingine. Ujiulize maulizo sawa vile: ‘Wakati mawazo ya mubaya inanikuya mu kichwa, ninaweza kutenda bila kukawia na kuacha kuifikiria? Mambo yenye niko najifurahisha nayo inafanya ikuwe nguvu kwangu kupiganisha jaribu fulani? Ninageuzaka macho yangu palepale wakati picha za mubaya zinatokea? Ninaelewa juu ya nini kanuni za Yehova zinakuwaka tu na faida hata kama inaniomba nijizuie ili niweze kuzifuata?’—Zb. 101:3.
19. Namna gani makosa yenye inaweza kuonekana kuwa ya kidogo-kidogo inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kupiganisha tamaa za mubaya?
19 Wakati tuko najichunguza, tusijaribu kutetea tamaa ya mubaya. Biblia inasema hivi: “Moyo ni mudanganyifu kuliko kitu kingine chochote na uko hatari.” (Yer. 17:9) Yesu alisema kama moyo unatokeza “mawazo mabaya.” (Mt. 15:19) Kwa mufano, kisha wakati mutu mwenye alishaacha kuangalia pornografia anaweza kuwaza kama haiko mubaya kuangalia picha fulani za mubaya juu zile picha hazionyeshe waziwazi batu benye habavale, ao anaweza kuwaza hivi: ‘Haiko mubaya kujiwazia niko nafanya mambo ya mubaya juu ni kuwazia tu, sitabifanya.’ Ni sawa vile moyo mudanganyifu wa ule mutu uko ‘unapanga mbele ya wakati kwa ajili ya tamaa za mwili.’ (Ro. 13:14) Utafanya nini juu uepuke kufanya vile? Ukumbuke kama makosa ya kidogo-kidogo inapelekaka mutu ku makosa ya kabambi-kabambi. Mutu anaweza hata kufikia kufanya zambi nzito.b Kwa hiyo, tuepuke ile makosa ya kidogo-kidogo, na tuepuke “mawazo mabaya” yenye inaweza kufanya tutetee tabia ya mubaya.
20. Tuko na tumaini gani, na tunapata musaada gani leo?
20 Tumeona kama kwa musaada wa Yehova tunaweza kupiganisha tamaa za mubaya. Na kwa rehema yake tuko na tumaini ya kuishi milele mu ulimwengu mupya. Ile wakati tutakuwa na furaha ya kumutumikia Yehova kwa moyo safi na akili safi! Mbele ile wakati ifike, tukuwe hakika kama Yehova atabariki mambo yenye tuko najikaza kufanya juu ya kupiganisha tamaa za mubaya na kuendelea kuwa na tumaini. Kwa kweli, Yehova atatusaidia kupata ushindi!
WIMBO 122 Tukuwe na Nguvu na Tusitikisike!
a MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu Biblia mara mingi neno “zambi” inazungumuzia matendo ya mubaya, sawa vile kuiba, kufanya uzinifu, ao kuua. (Kut. 20:13-15; 1 Ko. 6:18) Lakini mu maandiko fulani, “zambi” inamaanisha hali ya kutokamilika yenye tunazaliwa nayo hata kama hatuyafanya matendo yoyote ya mubaya.
b Kijana mwanaume mwenye anazungumuziwa mu Mezali 7:7-23 alikamata maamuzi ya mubaya mu mambo ya kidogo-kidogo na ile ilimufikisha mu zambi nzito, alifikia kufanya uasherati.
c MAFASIRIO YA PICHA: Kushoto: Ndugu iko mu restora, anaona banaume bawili biko naonyeshana mapenzi. Kuume: Dada anaona batu mbili biko navuta tumbako.