HABARI YA KUJIFUNZA YA 40
WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha
Yehova Anaweza Kutusaidia Tukuwe na Furaha ya Kweli
“Nitakuja . . . kwa Mungu, shangwe yangu nyingi sana.”—ZB. 43:4.
WAZO KUBWA
Kujua mambo yenye inaweza kutuiba furaha, na namna tunaweza tena kuipata.
1-2. (a) Leo batu mingi banapambana na hali gani? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?
LEO batu mingi banafanya yabo yote juu bakuwe na furaha. Lakini habapate furaha ya kweli. Batu mingi biko na huzuni na banaona kama mambo haitakuwaka muzuri. Na siye batumishi ya Yehova tunaweza kujisikia vile wakati fulani. Juu tunaishi mu “siku za mwisho,” tunaweza kupata magumu yenye itatuletea huzuni na mahangaiko.—2 Ti. 3:1.
2 Mu hii habari, tutaona mambo yenye inaweza kutuiba furaha, na namna tunaweza kuipata tena. Lakini tuone kwanza wapi njo furaha ya kweli inatokaka.
KWENYE FURAHA YA KWELI INATOKAKA
3. Uumbaji unatufundisha nini juu ya Yehova? (Ona pia picha.)
3 Yehova anakuwaka tu na furaha. Na anapenda na siye tukuwe na furaha. Njo maana hatushangale kuona namna bitu byenye aliumba binaonyesha kama ni Mungu mwenye furaha. Kwa mufano tunafurahia kuona dunia yetu yenye kupendeza, rangi mbalimbali, namna wanyama wako nacheza, na chakula mingi ya butamu. Mungu anatupenda kabisa na anapenda tufurahie maisha!
Kitoto kya tembo: Image © Romi Gamit/Shutterstock; Bitoto bya pingouins: Vladimir Seliverstov/500px via Getty Images; Bitoto bya mbuzi: Rita Kochmarjova/stock.adobe.com; Dauphins mbili: georgeclerk/E+ via Getty Images
Wakati tunaona wanyama wako nacheza, tunakumbuka kama Yehova ni Mungu mwenye furaha (Ona fungu ya 3)
4. (a) Juu ya nini Yehova anaendelea kuwa na furaha hata kama iko naona mateso mingi yenye iko ku dunia? (b) Yehova ametupatia zawadi gani? (Zaburi 16:11)
4 Hata kama Yehova ni “Mungu mwenye furaha,” anajua muzuri maumivu na mateso yenye iko ku dunia. (1 Ti. 1:11) Lakini haruhusu ile ipunguze furaha yake. Anajua kama hii magumu yote ni ya wakati kidogo tu. Alishaamua siku yenye atatosha mateso na magumu yote milele, na iko nangoya ile siku kwa hamu. Lakini kwa sasa anajua mambo yenye tuko napitia na anapenda kutusaidia. Anatusaidia namna gani? Anatupatia furaha; ile ni zawadi kabisa. (Soma Zaburi 16:11.) Acha tuone vile Yehova alipatia Yesu naye ile zawadi.
5-6. Juu ya nini Yesu iko na furaha?
5 Kati ya viumbe vyote vya Yehova, Yesu njo iko na furaha ya mingi. Juu ya nini? Juu ya hizi sababu mbili: (1) “Yeye ni mufano wa Mungu mwenye haonekane” na anaonyesha sifa za Baba yake kwa ukamili. (Kol. 1:15; 1 Ti. 6:15) (2) Yesu njo amepitisha wakati mingi sana pamoya na Baba yake Yehova, mwenye furaha ya kweli inatoka kwake.
6 Sikuzote Yesu anafanyaka mambo yenye Baba yake anamuomba afanye. Na ile inamuleteaka furaha. (Mez. 8:30, 31; Yoh. 8:29) Njo maana Yehova anamupenda na kumukubali.—Mt. 3:17.
7. Tunaweza kufanya nini juu tupate furaha ya kweli?
7 Furaha ya kweli inatoka kwa Yehova. Kwa hiyo tunaweza kupata furaha ya kweli kama tunamukaribia. Njo maana kama tunapitisha wakati mingi na tuko najifunza juu ya Yehova, tutamuiga zaidi, na ile itafanya furaha yetu iongezeke. Zaidi ya ile, kufanya mapenzi ya Mungu na kujua kama anatukubali kutatuletea furaha.a (Zb. 33:12) Lakini inaweza fika tunapoteza furaha yetu kwa wakati mufupi ao hata kwa wakati murefu. Kama ile inatufikia, ni kusema Yehova hatukubali tena? Hapana! Juu hatukamilike, wakati fulani tunaweza kuhuzunika na kuvunjika moyo. Na Yehova anaelewa ile. (Zb. 103:14) Tuzungumuzie sasa mambo yenye inaweza kutuiba furaha na mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe tena na furaha.
USIACHE KITU YOYOTE IKUIBE FURAHA YAKO
8. Magumu inaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?
8 Mwizi wa 1: Magumu. Biko nakutendea mubaya juu uko namutumikia Yehova? Uko nateseka juu ya musiba wa asili, umaskini, magonjwa, ao uzee? Ile magumu inaweza kutuiba furaha, zaidi sana kama hakuna byenye tunaweza fanya juu ya kubadilisha mambo. Biblia inasema kama “maumivu ya moyo yanaponda roho.” (Mez. 15:13) Muzee moya wa kutaniko mwenye jina yake Babis, alipata magumu ya mingi. Mu miaka ine tu kaka yake na bazazi yake balikufa. Anasema hivi: “Nilijisikia kuwa peke yangu na niliona sawa vile hakuna mwenye anaweza kunisaidia. Wakati fulani roho iliniluma sana juu mbele bakufe haikuwezekana nipitishe nabo wakati mingi, hata kama nilipenda kufanya vile.” Sawa ule ndugu, magumu yetu inaweza kuwa ya nguvu sana mupaka inatuchokesha na kufanya tuvunjike moyo.
9. Tunaweza kufanya nini juu tukuwe tena na furaha? (Yeremia 29:4-7, 10)
9 Tunaweza kufanya nini juu tukuwe tena na furaha? Tuache kuhangaikia mambo yenye hatuwezi kubadilisha na tukuwe wenye shukrani juu ya mambo yenye tuko nayo. Mu dunia batu banawazaka kama mutu mwenye iko na furaha ni mutu mwenye hana magumu. Lakini ile haiko kweli. Kwa mufano, Yehova aliambia Bayahudi benye balienda mu uhamisho Babiloni kama, balipaswa kuitika kama ile njo ilikuwa sasa maisha yabo. Hata kama kulikuwa magumu balipaswa kujikaza kujipatanisha na hali na kufurahia maisha. (Soma Yeremia 29:4-7, 10.) Ile inaweza kukufundisha nini? Ujikaze kuitika hali yako, na ukuwe mwenye shukrani juu ya mambo ya muzuri yenye uko nayo. Ukumbuke kama Yehova hatakuacha, atakusaidia. (Zb. 63:7; 146:5) Dada moya mwenye jina yake Effie alifanya aksida yenye ilifanya apooze. Anasema hivi: “Yehova, familia yangu, na kutaniko, balinisaidia sana na kunitegemeza. Kwa hiyo, niliona kama nikivunjika moyo itakuwa kukosa shukrani. Juu Yehova na barafiki yangu bananisaidia sana, napenda kubaonyesha shukrani.”
10. Juu ya nini tunaweza kuwa na furaha hata kama tuko na magumu?
10 Tunaweza kuendelea kuwa na furaha hata wakati tuko na magumu ao wakati mambo ya mubaya inatufikia, ao inafikia batu ya familia yetu.b (Zb. 126:5) Juu ya nini? Juu furaha yetu haitegemee hali yetu. Dada moya painia mwenye jina yake Maria, anasema hivi: “Kuendelea kuwa na furaha wakati wa magumu haimaanishe kama hautalia, ao kusema vile uko najisikia. Lakini, inamaanisha kama hauyasahau ahadi za Yehova. Baba yetu atatusaidia tuendelee kuwa na furaha.” Ukumbuke kama, hata kama uko napata magumu ya nguvu sana leo, ni ya wakati kidogo tu, haitaendelea milele. Iko sawa vile mutu mwenye iko natembea ku muchanga pembeni ya bahari. Saa mayi itapita itapoteza alama ya kwenye alikanyanga. Na siye ni vile, karibuni magumu yetu yote itapotea kabisa.
11. Namna gani mufano wa mutume Paulo unaweza kukutia moyo?
11 Wakati tunapata magumu tunaweza anza kujiuliza kama Yehova angali tu anatukubali. Kama uko najiuliza vile, ufikirie mufano wa batumishi bengine baaminifu ba Yehova benye balipataka magumu. Kufanya vile kunaweza kusaidia. Fikiria mufano wa mutume Paulo. Yesu yeye peke njo alimuchagula juu ahubiri habari njema “kwa mataifa na vilevile kwa wafalme na kwa wana wa Israeli.” (Mdo. 9:15) Ile ilikuwa pendeleo kubwa sana! Hata vile, Paulo naye alipataka magumu ya mingi. (2 Ko. 11:23-27) Juu alipataka ile magumu, ni kusema kama Yehova hakukuwa tena namukubali? Hapana! Kuona tu vile alikuwa navumilia ile magumu ilionyesha kama Yehova alikuwa namubariki. (Ro. 5:3-5) Na weye waza juu ya hali yako. Uko navumilia magumu kwa uaminifu. Kwa hiyo, ukuwe hakika kama Yehova anakukubali.
12. Wakati hatufikie miradi yetu mu kazi ya Yehova, namna gani ile inaweza kuiba furaha yetu?
12 Mwizi wa 2: Wakati hatufikie miradi yetu. (Mez. 13:12) Juu tunamupenda Yehova na tunapenda kumuonyesha shukrani, tunapendaka kufanya mambo mingi zaidi mu kazi yake. Lakini, kama tunajiwekea miradi yenye hatuwezi kufikia kulingana na hali yetu, tunaweza kuvunjika moyo. (Mez. 17:22) Dada moya painia mwenye jina yake Holly anasema hivi: “Nilipenda kusoma Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, kutumikia mu inchi ingine, ao kusaidia mu ujenzi wa Ramapo. Lakini hali yangu ilibadilika, na singeweza tena kufikia ile miradi. Nilivunjika moyo. Mutu anajisikiaka mubaya wakati anapenda kufanya mambo fulani lakini hawezi.” Ile inafikiaka batumishi mingi ba Yehova.
13. Tunaweza kujitilia miradi gani kama hali yetu haituruhusu kufanya mambo yenye tungependa kufanya?
13 Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe tena na furaha? Kumbuka kama Yehova hatulombe kufanya mambo yenye hatutaweza. Anatuona kuwa ba maana hata kama hatuwezi kufanya mambo mingi sawa bengine. Anapenda tukuwe baaminifu na benye kiasi. (Mik. 6:8; 1 Ko. 4:2) Anahangaikia zaidi sana kile tuko mu moyo, kuliko migao yenye tunatumikia. Sasa kama Yehova hatulombe tufanye byenye binapita uwezo wetu, juu ya nini siye tujilazimishe kufanya byenye binatupita uwezo?c Kwa hiyo, kama hali yako haikuruhusu kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya. Kwa mufano unaweza kusaidia vijana mu kutaniko yenu ao kusaidia benye kuzeeka. Ao tena unaweza kujitilia muradi wa kutembelea mutu juu ya kumutia moyo, kumuita ku telefone, ao kumuandikia ujumbe. Kama unajitilia miradi yenye unaweza kufikia, Yehova atakubariki na atakusaidia ukuwe na furaha! Na ukumbuke kama hivi karibuni mu dunia mupya tutakuwa na nafasi za mingi za kumutumikia Yehova mu njia zenye hatuwezi hata kuwazia! Holly, mwenye tulizungumuzia, naye alielewa ile. Alimalizia hivi: “Kama ninaanza kuvunjika moyo, ninatuliaka kwanza na kukumbuka kama kwa musaada wa Yehova, nitaweza kutimiza miradi yangu fulani mu dunia mupya.”
14. Nini ingine njo inaweza kutuiba furaha yetu?
14 Mwizi wa 3: Kutia mambo ya kujifurahisha fasi ya kwanza. Ku Enternete tunaweza kuona batu benye banaonekana sawa vile biko na furaha, juu biko nafanya mambo mbalimbali ya kujifurahisha. Tunaweza kuwaza kama kufanya mambo yenye tunapenda, kuuza byenye tunapenda, na kusafiri fasi tofauti-tofauti, kunaweza kutuletea furaha. Haiko mubaya kufanya vile juu ya kujifurahisha. Yehova alituumba na hamu ya kufurahia mambo ya muzuri. Lakini, batu mingi benye balipenda kujifurahisha sana balifikia kuona kama mambo yenye baliwaza itabaletea furaha njo ilibaiba furaha. Dada moya painia mwenye jina yake Eva, anasema hivi: “Kama mu maisha yako jambo yenye unahangaikia sana ni kujifurahisha, hautatoshekaka.” Kama tunapenda sana kujifurahisha, tutahuzunika na kuvunjika moyo.
15. Mufano wa Mufalme Sulemani unatufundisha nini?
15 Mufano wa Mufalme Sulemani unatufundisha kama kujifurahisha kupita mipaka haikuwake na matokeo ya muzuri. Alijaribu kupata furaha kwa kujipatia kila kitu kyenye alipenda, sawa vile kula chakula ya muzuri, kusikiliza miziki ya muzuri, na kuuza kila kitu ya muzuri yenye ilikuwa ile wakati. Lakini hakutosheka. Alisema hivi: “Jicho halishibake kuona; na sikio halijae kwa sababu ya kusikia.” (Muh. 1:8; 2:1-11) Batu fulani banawazaka kama bakikuwa na makuta ya mingi ao kama banafanya byote byenye banapenda, batakuwa na furaha. Lakini ile haiko kweli, ile mambo haiwezi kuleta furaha ya kweli.
16. Juu ya nini kusaidia bengine kunaweza kufanya tukuwe tena na furaha? (Ona pia picha.)
16 Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe tena na furaha? Yesu alifundisha kama “kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Muzee moya wa kutaniko mwenye jina yake Alekos anasema hivi: “Ninajikazaka kufanyia bengine mambo ya kidogo-kidogo juu ya kubasaidia. Wakati minasaidia bengine, ile inanisaidia nisijifikirie sana na inaniletea furaha.” Na weye unaweza kufanya nini juu ya kusaidia bengine? Kama unaona mutu iko na magumu, ujikaze kumutia moyo. Pengine hautamaliza magumu yake, lakini unaweza kumufariji kwa kumusikiliza kwa uangalifu, kwa kumuonyesha huruma, na kwa kumuambia atupie Yehova muzigo wake. (Zb. 55:22; 68:19) Umuhakikishie pia kama Yehova hayamuacha. (Zb. 37:28; Isa. 59:1) Unaweza hata kufanya jambo fulani juu ya kumusaidia. Kwa mufano unaweza kumupigia chakula ao kuenda kujitembeza pamoya naye. Unaweza pia kuhubiri pamoya naye, juu ile inaweza kumuletea furaha. Tuache Yehova atutumikishe juu ya kutia bengine moyo. Kama tunajikaza kusaidia bengine kuliko kujifikiria siye benyewe, tutakuwa na furaha ya kweli!—Mez. 11:25.
Kuliko kufanya tu byenye unapenda, usaidie bengine (Ona fungu ya 16)d
17. Kama tunapenda kuwa na furaha ya kweli, tunapaswa kufanya nini? (Zaburi 43:4)
17 Tunaweza kuwa na furaha ya kweli kama tunaendelea kumukaribia Baba yetu wa mbinguni. Biblia inatuhakikishia kama Yehova ni ‘shangwe yetu.’ (Soma Zaburi 43:4.) Kwa hiyo hata tukuwe na magumu gani mu maisha, tusihangaike wala kuogopa. Kama Yehova ni rafiki yetu, atatusaidia tukuwe na furaha milele!—Zb. 144:15.
WIMBO 155 Furaha Yetu ya Milele Inatoka kwa Yehova
a Ona kisanduku “Namna Yehova Anatupatia Furaha.”
b Kwa mufano, ona ku jw.org video ya Ripoti ya 5 ya Baraza Yenye Kuongoza ya 2023, kwenye ndugu Dennis Christensen na bibi yake Irina biko naulizwa maulizo.
c Juu ya kujua mambo mingi zaidi, ona habari “Uwe na Matarajio Yenye Usawaziko, na Uwe Mwenye Shangwe,” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2008.
d MAFASIRIO YA PICHA: Dada anajiuzia bitu bya mingi. Lakini anakuwa na furaha zaidi wakati anauzia maua dada mwenye kuzeeka mwenye iko na lazima ya kutiwa moyo.