Usiache Makosa ya Wengine Yakukwaze
‘Muendelee . . . kusameheana kwa hiari [kwa kupenda].’—WAKOLOSAI 3:13.
1, 2. Namna gani Biblia ilitabiri kuongezeka kwa watu wa Yehova?
KATIKA dunia yote, kuko tengenezo moja lenye kufanyizwa na watu wenye wanapenda Yehova na wanapenda kumutumikia. Watu hao ni Mashahidi wa Yehova. Hata kama wako na uzaifu na wanafanya makosa, Yehova anawaongoza kupitia roho yake takatifu. Tuzungumuzie basi njia fulani zenye kuonyesha kama amewabariki.
2 Katika mwaka wa 1914, hesabu ya watu wa Yehova ilikuwa kidogo sana. Lakini Yehova amebariki kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, mamilioni ya watu wamejifunza mafundisho ya Biblia na wamekuwa Mashahidi wake. Yehova alizungumuzia ongezeko hilo lenye kushangaza wakati alisema hivi: ‘Mudogo atakuwa elfu, na munyonge [asiyekuwa na nguvu] atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.’ (Isaya 60:22) Leo, tunaona wazi kama unabii huo umetimizwa. Watu wa Yehova wako kama taifa kubwa. Kwa kweli, katika dunia yote, kuko inchi nyingi zenye kuwa na wakaaji kidogo sana kuliko hesabu yote ya watu wa Yehova.
3. Namna gani watumishi wa Mungu wameonyesha upendo?
3 Katika siku hizi za mwisho, Yehova amesaidia watu wake wapendane sana. Wanamuiga Mungu kwa sababu “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Yesu aliwapatia wanafunzi wake amri ya ‘kupendana.’ Pia, aliwaambia hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukikuwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yohana 13:34, 35) Katika miaka ya hivi karibuni, watumishi wa Yehova wameonyesha kama wanapendana hata wakati mataifa yalikuwa yanapigana vita. Kwa mufano, wakati wa vita ya pili ya ulimwengu, watu karibu milioni 55 walikufa. Lakini watu wa Yehova hawakuua mutu yeyote katika vita hiyo. (Soma Mika 4:1, 3.) Hilo limewasaidia waendelee kuwa ‘safi kutokana na damu ya watu wote.’—Matendo 20:26.
4. Sababu gani kuongezeka kwa watu wa Mungu kunashangaza sana?
4 Hesabu ya watu wa Mungu inaendelea kuongezeka hata kama wako na adui mwenye nguvu sana, ni kusema, Shetani. Yeye ndiye ‘mungu wa mufumo huu wa mambo.’ (2 Wakorintho 4:4) Shetani anaongoza matengenezo ya politike ya ulimwengu huu na pia vyombo vya kutangaza habari, na anajikaza kutumia mambo hayo ili kusimamisha kazi ya kuhubiri habari njema. Lakini hawezi kusimamisha kazi hiyo. Hata hivyo, Shetani anajua kama ana wakati mufupi tu, kwa hiyo anaendelea kujikaza ili kutuzuia kumuabudu Yehova.—Ufunuo 12:12.
UTAENDELEA KUWA MUSHIKAMANIFU WAKATI WENGINE WANAFANYA MAKOSA?
5. Sababu gani wengine wanaweza kutukwaza wakati fulani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)
5 Watumishi wa Mungu wanajifunza kama ni jambo la maana sana kupenda Mungu na watu wengine. Yesu alisema hivi: “‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ Hii ndiyo amri iliyo kubwa na ya kwanza. Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘umupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Mathayo 22:35-39) Lakini, Biblia inaonyesha kama watu wote wanazaliwa wasiokamilika kwa sababu ya zambi ya Adamu. (Soma Waroma 5:12, 19.) Kwa hiyo, wakati fulani, wengine katika kutaniko wanaweza kusema ao kufanya jambo fulani lenye kutukwaza. Ikiwa hilo linatokea, tutafanya nini? Upendo wetu kwa Yehova utaendelea kuwa wenye nguvu? Tutaendelea kuwa washikamanifu kwake na kwa watu wake? Biblia inazungumuzia watumishi fulani wa Mungu wenye walisema ao kufanya mambo yenye yalikwaza wengine. Tuone basi mambo yenye yaliwapata yanaweza kutufundisha nini.
Ikiwa ulikuwa unaishi katika Israeli wakati wa Eli na watoto wake, ungetenda namna gani? (Picha hizi zinapatana na fungu la 6)
6. Ni katika njia gani Eli alishindwa kupatia watoto wake nizamu?
6 Kwa mufano, Eli alikuwa kuhani mukubwa katika Israeli, lakini watoto wake wawili walikosa kutii sheria za Yehova. Biblia inasema hivi: ‘Wana wa Eli walikuwa watu wasiofaa kitu; hawakumutambua Yehova.’ (1 Samweli 2:12) Eli alijua kama watoto wake walikuwa wanafanya mambo ya mubaya sana. Lakini, hakuwapatia kabisa nizamu (discipline). Kisha wakati fulani, Yehova alipatia Eli malipizi na watoto wake wawili. Na kisha, Yehova hakuruhusu tena watu wa kizazi cha Eli wakuwe makuhani wakubwa. (1 Samweli 3:10-14) Ikiwa ulikuwa unaishi wakati wa Eli na kujua kama aliacha watoto wake wafanye mambo ya mubaya sana, ungeacha hilo likukwaze? Hali hiyo ingeregeza imani yako kwa Yehova, na kukufanya uache kumutumikia?
7. Daudi alifanya zambi gani nzito, lakini Mungu alimutendea namna gani?
7 Daudi alikuwa na sifa za muzuri sana, na ndiyo sababu Yehova alimupenda sana. (1 Samweli 13:13, 14; Matendo 13:22) Lakini, Daudi alifanya jambo fulani la mubaya sana. Wakati Uria alikuwa ameenda kupigana vita, Daudi alilala na Bath-sheba, bibi ya Uria, na akapata mimba. Daudi hakupenda mutu yeyote ajue jambo lenye alikuwa amefanya. Alitoa amri ili Uria arudie kumuona na kisha alijaribu kumusadikisha aende nyumbani kwake. Daudi aliwaza kama Uria angelala na Bath-sheba ili watu wafikiri kama Uria ndiye baba ya mutoto mwenye angezaliwa. Lakini Uria alikataa kuenda nyumbani kwake. Kwa hiyo, Daudi alifanya mipango ili Uria auawe kwenye vita. Daudi na watu wa familia yake walipatwa na matokeo ya mubaya sana kwa sababu ya zambi zake nzito. (2 Samweli 12:9-12) Lakini Yehova alikuwa mwenye rehema na alimusamehe. Alijua kama Daudi alipenda kufanya mambo ya muzuri. (1 Wafalme 9:4) Ikiwa uliishi wakati huo, ungejisikia namna gani juu ya mambo yenye Daudi alifanya? Ungeacha kumutumikia Yehova?
8. (a) Namna gani mutume Petro alishindwa kutimiza maneno yake? (b) Kisha Petro kufanya makosa, sababu gani Yehova aliendelea kumutumikisha?
8 Mufano mwingine wenye kupatikana katika Biblia ni wa mutume Petro. Yesu alimuchagua ili akuwe mutume. Lakini, wakati fulani Petro alisema ao kufanya mambo ya mubaya. Kwa mufano, Petro alisema kama hatamuacha Yesu hata kidogo hata kama wengine wote wangemuacha. (Marko 14:27-31, 50) Lakini, kisha Yesu kukamatwa, mitume wote walimuacha na hata Petro naye alimuacha. Kisha, Petro alisema mara tatu kama hakumujua Yesu. (Marko 14:53, 54, 66-72) Lakini, Petro alihuzunika sana juu ya mambo yenye alikuwa amefanya. Kwa hiyo, Yehova alimusamehe na aliendelea kumutumikisha. Ikiwa ulikuwa mwanafunzi wakati huo na ulijua mambo yenye Petro alifanya, ungeendelea kumutumainia Yehova?
Tunaweza kuwa hakika kabisa kama Yehova atafanya sikuzote mambo yenye kuwa sawa na ya haki
9. Sababu gani unaamini kama Mungu ni mwenye haki sikuzote?
9 Mifano hiyo inatuonyesha kama watumishi fulani wa Yehova wamefanya mambo ya mubaya na wameumiza wengine sana. Ikiwa jambo hilo linatokea leo, utatenda namna gani? Utaacha kuenda kwenye mikutano ao hata kumuacha kabisa Yehova na watu wake? Ao utaelewa kama Yehova ni mwenye rehema na kama anaweza kungojea mutu atubu? Lakini, wakati fulani mutu mwenye alitenda zambi nzito anaweza kukosa kuhuzunika juu ya mambo yenye alifanya. Utatumainia kama Yehova anajua jambo hilo na kama atafanya jambo fulani kwa wakati wenye kufaa? Anaweza hata kuondoa mutu huyo katika kutaniko ikiwa ni lazima. Unaamini kama Yehova atafanya sikuzote mambo yenye kuwa sawa na ya haki?
ENDELEA KUWA MUSHIKAMANIFU
10. Yesu alitenda namna gani wakati Yuda Iskariote na Petro walimukosea?
10 Biblia inazungumuzia watu wengi wenye walibakia washikamanifu kwa Yehova na watu wake hata kama watu wenye walikuwa wanaishi pamoja nao walifanya zambi nzito. Yesu ni mufano muzuri zaidi. Kisha kumuomba Baba yake musaada katika sala usiku muzima, alichagua mitume 12. Lakini Yuda Iskariote, mumoja kati ya mitume hao, alimutoa. Pia, mutume Petro alisema kama hakumujua Yesu. (Luka 6:12-16; 22:2-6, 31, 32) Yesu hakusema kama ni kosa la Yehova, ao la wanafunzi wengine wakati wanafunzi fulani walimuvunja moyo. Lakini, Yesu aliendelea kumukaribia Baba yake na kumutumikia kwa ushikaminifu. Kwa hiyo, Yehova alimubariki kwa kumufufua na kisha alimufanya kuwa Mufalme wa Ufalme wa mbinguni.—Mathayo 28:7, 18-20.
11. Biblia ilitabiri nini juu ya watumishi wa Yehova katika siku zetu?
11 Mufano wa Yesu unatufundisha kubakia washikamanifu kwa Yehova na watu wake. Na tuko na sababu za muzuri za kufanya hivyo. Tunaona kama Yehova anaongoza watumishi wake katika siku hizi za mwisho. Anaendelea kuwasaidia wahubiri kweli katika dunia yote, na ni wao tu ndio wanafanya kazi hiyo. Mambo yote yenye Yehova anawafundisha yanawafanya pia wakuwe na umoja kabisa na furaha. Yehova alizungumuzia jambo hilo wakati alisema hivi: ‘Watumishi wangu watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali ya muzuri ya moyo.’—Isaya 65:14.
Itakuwa mubaya na kukosa hekima kabisa ikiwa tunaacha Yehova na watu wake kwa sababu tu mutu fulani katika kutaniko anafanya kosa
12. Namna gani tunapaswa kuona makosa ya wengine?
12 Tuko wenye furaha kabisa kwa sababu Yehova anatuongoza na anatusaidia kufanya mambo mengi ya muzuri. Lakini, watu katika ulimwengu wa Shetani hawana furaha na hawana tumaini la kweli juu ya wakati unaokuja. Itakuwa mubaya na kukosa hekima kabisa ikiwa tunaacha Yehova na watu wake kwa sababu tu mutu fulani katika kutaniko anasema ao kufanya jambo fulani la mubaya! Kuliko kufanya hivyo, tunapaswa kubakia washikamanifu kwa Yehova na kufuata muongozo wake. Tunapaswa pia kujua namna ya kutenda wakati wengine wanatukosea na namna ya kuona makosa yao.
UNAPASWA KUTENDA NAMNA GANI?
13, 14. (a) Sababu gani tunapaswa kuvumiliana? (b) Ni ahadi gani tunapaswa kukumbuka?
13 Unapaswa kutenda namna gani ikiwa ndugu ao dada yako anasema ao kufanya jambo fulani lenye kukukwaza? Biblia inatushauria hivi: ‘Usikuwe na haraka kuuzika [kukwazika] katika roho yako, kwa maana kuuzika kunakaa katika kifua cha wajinga.’ (Mhubiri 7:9) Sisi wote hatukamilike na tunafanya makosa. Kwa hiyo, hatuwezi kutazamia kama sikuzote ndugu ao dada zetu watasema ao kufanya tu mambo ya muzuri. Na haitakuwa muzuri kwetu kuendelea kuwaza juu ya makosa yao. Ikiwa tunafanya hivyo, tunaweza kupoteza furaha ya kuendelea kumutumikia Yehova. Jambo la mubaya zaidi, imani yetu kwa Yehova inaweza kuwa zaifu, na tunaweza hata kuacha tengenezo lake. Kisha, tunaweza kuacha kumutumikia Yehova ao kupoteza tumaini la kuishi katika dunia mupya.
14 Kwa hiyo, ni nini inaweza kukusaidia uendelee kumutumikia Yehova kwa furaha wakati wengine wanafanya jambo fulani lenye linakusumbua? Kumbuka sikuzote ahadi hii yenye kutia moyo: ‘Tazama, mimi ninaumba mbingu mupya na dunia mupya; na mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.’ (Isaya 65:17; 2 Petro 3:13) Yehova atakupatia baraka hizo ikiwa unaendelea kuwa mushikamanifu kwake.
15. Yesu alisema tunapaswa kufanya nini wakati wengine wanatukosea?
15 Kwa kweli, hatujakuwa katika dunia mupya. Kwa hiyo, ikiwa mutu fulani anatukwaza, tunapaswa kufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova anapenda tufanye. Kwa mufano, Yesu alisema hivi: ‘Ikiwa munawasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia; lakini ikiwa hamutawasamehe watu makosa yao, Baba yenu naye hatawasamehe makosa yenu.’ Na wakati Petro aliuliza Yesu ikiwa tunapaswa kusamehe ‘mupaka mara 7,’ Yesu alimujibu hivi: ‘Ninakuambia, si, mupaka mara 7, bali [lakini], mupaka mara 77.’ Yesu alitufundisha kama sikuzote tunapaswa kuwa tayari kusamehe wengine.—Mathayo 6:14, 15; 18:21, 22.
16. Ni mufano gani muzuri Yosefu alituachia?
16 Mufano wa Yosefu unatufundisha namna ya kutenda wakati wengine wanatuvunja moyo. Yosefu na mudogo yake walikuwa watoto wawili tu wenye Yakobo alizaa na Raheli. Yakobo alikuwa na watoto wengine kumi, lakini alimupenda Yosefu sana kuliko wengine wote. Jambo hilo lilifanya wamusikilie Yosefu wivu sana. Kwa kweli, walimuchukia sana, kwa hiyo walimuuzisha kuwa mutumwa, na akapelekwa Misri. Kisha miaka mingi, mufalme wa Misri alimufanya Yosefu kuwa mutu wa pili mwenye kuwa na mamlaka makubwa katika inchi hiyo kwa sababu alifurahia sana kazi ya muzuri ya Yosefu. Kisha, ndugu za Yosefu walienda Misri ili kuuza chakula kwa sababu njaa ilitokea katika inchi yao. Wakati walimuona Yosefu, hawakumujua tena, lakini yeye alijua kama walikuwa ndugu zake. Hata kama walikuwa wamemutendea mubaya, Yosefu hakulipiza kisasi. Lakini aliwajaribu ili kuona ikiwa walikuwa wamebadilika. Wakati Yosefu alitambua kama walikuwa wamebadilika, aliwaambia kama alikuwa ndugu yao. Kisha aliwatuliza. Na alisema hivi: ‘Musiogope. Mimi nitaendelea kuwapa chakula ninyi na watoto wenu wadogo.’—Mwanzo 50:21.
17. Utatenda namna gani wakati wengine wanakukosea?
17 Ukumbuke kama, kwa sababu kila mutu ana makosa, wewe pia unaweza kukosea wengine. Kwa hiyo, ikiwa unatambua kama umekwaza mutu fulani, fuata shauri la Biblia. Umuombe akusamehe, na ujikaze kufanya amani pamoja naye. (Soma Mathayo 5:23, 24.) Tunafurahi wakati wengine wanatusamehe. Kwa hiyo, sisi pia tunapaswa kuwasamehe. Andiko la Wakolosai 3:13 linasema hivi: ‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwengine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi kwa hiari, nanyi mufanye vivyo hivyo pia.’ Ikiwa tunapenda kabisa ndugu na dada zetu, hatutaendelea kukwazika juu jambo fulani lenye walitutendea zamani. (1 Wakorintho 13:5) Na ikiwa tunasamehe wengine, Yehova atatusamehe pia. Kwa hiyo, wakati wengine wanatukosea, ni muzuri tuwaonyeshe rehema kama vile Baba yetu, Yehova, anatuonyesha rehema.—Soma Zaburi 103:12-14.