Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mrt habari 36
  • Kuko Siku Hatutakosa Mambo ya Lazima?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuko Siku Hatutakosa Mambo ya Lazima?
  • Habari Zingine
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Magumu yenye Mungu atamaliza
  • Umasikini
    Amuka!—2015
  • Bei ya Vitu Imepanda mu Dunia Yote—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Ufalme wa Mungu—Sababu Gani Yesu Anauona Kuwa wa Maana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Habari Zingine
mrt habari 36
Mwanaume mwenye kusimama kati ya nyumba za ovyo-ovyo iko naangalia nyumba zenye kujengwa muzuri sana.

Kuko Siku Hatutakosa Mambo ya Lazima?

Mu inchi za mingi, watu wanafanya maandamano mu barabara juu wanakosa mambo ya lazima. Mambo ilikuwa mubaya tena zaidi wakati ya ugonjwa wa Coronavirus wenye ulifanya watu wakose furaha juu ya kubakia tu ku nyumba, kukosa chakula, na kukosa matunzo. Na ile ilifanya tofauti kati ya matajiri na maskini ikuwe wazi zaidi.

Kuko siku hatutakosa mambo ya lazima? Ndiyo. Biblia inaonyesha mambo yenye Mungu atafanya juu ya kumaliza magumu yetu.

Magumu yenye Mungu atamaliza

Magumu: Serikali zimeshindwa kutimizia kila mutu mambo ya lazima.

Mambo yenye Mungu atafanya: Mungu atatosha serikali zote za wanadamu na kutia serikali yake yenye inaitwa Ufalme wa Mungu. Itakuwa mbinguni na itatawala dunia yote.—Danieli 2:44; Matayo 6:10.

Matokeo: Juu Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote, utasimamia muzuri mambo yote ku dunia. Hakutakuwa tena watu maskini, na watu hawatakosa mambo ya lazima. (Zaburi 9:7-9, 18) Watafurahia matokeo ya kazi yao, na kuishi maisha yenye kutosheka pamoya na familia zao. Biblia inasema hivi: “Watajenga nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani, wala hawatapanda ili wengine wakule.”—Isaya 65:21, 22.

Magumu: Watu hawawezi kuepuka hali zenye zinafanya wateseke na wakose mambo ya lazima.

Mambo yenye Mungu atafanya: Kupitia Ufalme wake, Mungu atamaliza mambo yote yenye inafanya watu waogope na wakose usalama.

Matokeo: Wakati Ufalme wa Mungu utatawala, watu na familia zao hazitakosa tena mambo ya lazima. Kwa mufano, vita, kukosa chakula, na magonjwa haitakuwa tena. (Zaburi 46:9; 72:16; Isaya 33:24) Mungu anasema hivi: “Watu wangu watakaa katika makao yenye amani, katika makao salama na katika mahali pa kupumuzikia penye utulivu.”—Isaya 32:18.

Magumu: Mara nyingi watu wenye kutafuta tu faida zao na wenye pupa wanatesaka wanadamu wenzao.

Mambo yenye Mungu atafanya: Watu wenye watatawaliwa na Ufalme wa Mungu watajifunza kupenda wengine zaidi ya vile wanajipenda wenyewe.—Matayo 22:37-39.

Matokeo: Wakati Ufalme wa Mungu utatawala, kila mutu ataiga upendo wa Mungu wenye “hautafute faida zake wenyewe.” (1 Wakorinto 13:4, 5) Biblia inasema hivi: “Hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza wala uharibifu wowote katika mulima wangu wote mutakatifu, kwa maana dunia hakika itajaa ujuzi juu ya Yehovaa kama vile maji yanafunika bahari.”—Isaya 11:9.

Biblia inaonyesha kama tunaishi siku za mwisho za hii dunia na kama karibuni Mungu atatimiza ahadi yake ya kumaliza magumu yote yenye inafanya watu wakose mambo ya lazima.b (Zaburi 12:5) Mbele ile wakati ifike, kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia wakati tunakosa mambo ya lazima. Kwa mufano, ona habari “Jinsi ya Kuishi Ukiwa na Pesa Kidogo” na “Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza.”

Mawazo ya uongo juu ya Biblia, umaskini, na utajiri

Wazo ya uongo: Umaskini hautaishaka, juu Yesu alisemaka hivi: “Maskini muko nao sikuzote, lakini hamutakuwa na mimi sikuzote.”—Matayo 26:11.

Kweli njo hii: Yesu alikuwa tu nazungumuzia jambo fulani yenye ni ya kweli. Ni kusema, vile tutaendelea kuishi mu hii dunia yenye kukosa haki, watu fulani wataendelea kuwa maskini. Lakini Yesu alitangazia “maskini habari njema.” Kwa mufano, alisema kama Ufalme wa Mungu utamaliza umaskini milele.—Luka 4:18, 43.

Wazo ya uongo: Watu wenye wanapenda kumufurahisha Mungu wanapaswa kuwa maskini, juu Yesu alisamaka hivi: “Uende uuzishe mali yako na upatie maskini.”—Matayo 19:21.

Kweli njo hii: Wakati Yesu alisemaka vile, hakumaanisha kama kila mwanafunzi wake anapaswa kuwa maskini. Yesu alikuwa nazungumuza na mwanaume fulani kijana mwenye alikengeushwa na mali yake, na alikuwa tu namuonyesha jambo yenye alipaswa kufanya. Yesu alimuambia afanye maisha yake ikuwe mwepesi juu afikie kuwa mwanafunzi wa Yesu.

Wazo ya uongo: Mungu anabariki watu kwa kuwapatia utajiri, juu Biblia inasema hivi: “Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri.”—Mezali 10:22.

Kweli njo hii: Mu Biblia, “baraka ya Yehova” inakuwaka kila mara ya kiroho. Kwa mufano, maisha yenye kusudi, uhusiano muzuri na Yehova, na tumaini ya uzima wa milele. (Zaburi 25:14; Yohana 17:3) Ni kweli Mungu alibariki watumishi wake fulani kwa kuwapatia utajiri. Lakini, Wakristo wengi walikuwa maskini. (Mwanzo 24:34, 35; Yakobo 2:5) Hata Yesu hakukuwa na vitu mingi vya kimwili.—Matayo 8:20.

Wazo ya uongo: Biblia inafundisha aina fulani ya ukomunisti, ni kusema, kuchangia mambo yote pamoya, kwa sababu inasema hivi kuhusu Wakristo wa kwanza-kwanza: “Walichangia mambo yote pamoja, na walikuwa wanauzisha vitu vyao na mali zao.”—Matendo 2:44, 45.

Kweli njo hii: Ile maandiko inazungumuzia jambo fulani yenye Wakristo wa kwanza-kwanza walifanya kwa wakati kidogo juu ya kuhangaikia wapya fulani wenye walitokea tu kubatizwa. Wale wapya walikuya Yerusalemu juu ya kuhuzuria sikukuu ya Wayahudi yenye kuitwa Pentekoste. (Matendo 2:5) Lakini, wakati waligeuka na kuwa Wakristo, walibakia Yerusalemu kwa siku mingi zaidi ya vile walipanga kufanya ili kujifunza mambo mingi zaidi. Njo maana, Wakristo wenzao walitoa kwa kujipendea mambo yenye walikuwa nayo juu ya kuwasaidia wapate chakula na fasi ya kulala.—Matendo 2:41, 42, 46, 47.

a Biblia inaonyesha kama Yehova njo jina ya Mungu.—Zaburi 83:18.

b Juu ya kujifunza sababu gani unaweza kutegemea Biblia, ona habari “Biblia Ni Kitabu Chenye Kinatusaidia Kupata Kweli.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine