Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 24
  • Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Juu ya Nini Wanadamu Wanashindwa Kuleta Amani?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Amani—Namna Gani Unaweza Kuipata?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 24
Ndege ya vita

Majibu ya Maulizo juu ya Biblia / Ufalme wa Mungu / Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?

Jibu ya Biblia

Wanadamu wamefanya yao yote juu ya kuleta amani, lakini wapi! Na kusema kweli, hawataweza kuleta amani juu ya sababu zenye kufuata:

  • “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Wanadamu hawakuumbwa na uwezo ao haki ya kujiongoza wao wenyewe, kwa hiyo hawana uwezo wa kuleta amani ya milele.

  • “Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu. Roho yake inatoka, anarudia kwenye udongo; siku ileile mawazo yake yanapotea.” (Zaburi 146:3, 4) Viongozi wa serikali, hata wale wenye kuwa na nia ya muzuri, hawana uwezo wa kutosha mambo yenye kuleta vita.

  • “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa . . . wakali, wenye hawapendi wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.” (2 Timoteo 3:1–4) Tuko naishi mu “siku za mwisho” za hii dunia, mu wakati yenye tabia za watu zinafanya ikuwe nguvu kupata amani.

  • “Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ibilisi, adui ya Mungu, alishatupwa mu ujirani wa dunia na anachochea watu wakuwe na roho ya mubaya sana sawa yeye. Kama yeye angali tu “mutawala wa ulimwengu huu,” hatuwezi kuishi kwa amani.​—Yohana 12:31.

  • “[Ufame wa Mungu] utaponda na kumaliza falme hizi zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu njo utatimiza tamaa yetu ya kuwa na dunia yenye amani milele, hapana serikali za wanadamu.​—Zaburi 145:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine