Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 34
  • Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 34

Je, Mungu Atajibu Sala Zangu?

Jibu la Biblia

Ndiyo, atajibu sala zako. Biblia na mambo tunayojionea katika maisha yanaonyesha kwamba Mungu anajibu sala. Biblia inasema hivi: ‘[Mungu] Atawatimizia wale wanaomuogopa tamaa yao, naye atasikia kilio chao cha kuomba musaada, naye atawaokoa.’ (Zaburi 145:19) Lakini, unapaswa kufanya mambo fulani ili Mungu ajibu sala zako.

Mambo ambayo Mungu anataka ufanye

  • Sali kwake, hapana kwa Yesu, Maria, watakatifu, malaika ao mifano (sanamu). Yehova Mungu pekee ndiye ‘musikiaji wa sala.’​—Zaburi 65:2.

  • Sali kulingana na mambo ambayo Mungu anakubali, kama inavyoonyeshwa katika Biblia.​—1 Yohana 5:14.

  • Sali katika jina la Yesu, kwa kufanya hivyo, unakubali mamlaka ya Yesu. Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia.”​—Yohana 14:6.

  • Sali bila kuwa na mashaka, uombe Mungu akupe imani zaidi.​—Mathayo 21:22; Luka 17:5.

  • Uwe munyenyekevu na mwenye nia nzuri. Biblia inasema hivi: ‘Kwa maana Yehova yuko juu, hata hivyo anamuona munyenyekevu.’​—Zaburi 138:6.

  • Sali bila kuacha. Yesu alisema hivi: ‘Endeleeni kuomba, nanyi mutapewa.’​—Luka 11:9.

Mambo ambayo Mungu haangalie

  • Rangi ya ngozi yako ao taifa lako. ‘Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’​—Matendo 10:34, 35.

  • Ikiwa unakuwa katika hali gani unaposali. Unaweza kukaa, kuinama, kupiga magoti, ao kusimama unaposali.​—1 Mambo ya Nyakati 17:16; Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25.

  • Ikiwa unasali kwa sauti ndefu ao kimya-kimya. Mungu anasikia sala kama hizo hata ikiwa wengine walio pembeni yetu hawasikie mambo tunayosema.​—Nehemia 2:1-6.

  • Ikiwa sala yako inahusu mambo mazito ao hapana. Mungu anakutia moyo ‘umutupie mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’​—1 Petro 5:7.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine