Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwfq habari 23
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawapiganake vita?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawapiganake vita?
  • Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tunasaidiaka Wengine
  • Vita
    Amuka!—2017
Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
ijwfq habari 23
Maaskari wenye kifichama wako napiga masasi ku vita.

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawapiganake vita?

Siye Mashahidi wa Yehova hatupiganake vita juu ya sababu zenye kufuata:

  1. Tunamutii Mungu. Biblia inasema kama watumishi wa Mungu “Watafua panga zao kuwa majembe” na “hawatajifunza vita tena.”​—Isaya 2:4.

  2. Tunamutii Yesu. Yesu alimuambia mutume Petro hivi: “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote wenye wanatumikisha upanga watakufa kwa upanga.” (Matayo 26:52) Kwa hiyo,Yesu alionyesha kama mitume wake hawapaswe kutumia silaha.

    Wanafunzi wa Yesu wanatii amri ya kutokuwa “sehemu ya ulimwengu” kwa kuepuka kabisa kuunga mukono upande wowote mu mambo ya politike. (Yohana 17:16) Hawafanye maandamano kama kunafanyika mambo yenye hawafurahie, na hawakataze watu kujiunga na jeshi.

  3. Tunapenda Wengine. Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “mupendane.” (Yohana 13:34, 35) Kwa kufanya vile, wangekuwa familia moya ya ndugu na dada mu dunia yote na hakuna mutu mwenye alipaswa kupigana vita na ndugu ao dada yake.​—1 Yohana 3:10-12.

  4. Tunafuata Mufano wa Wakristo wa Kwanza. Kitabu Encyclopedia of Religion and War kinasema hivi: “Wanafunzi wa kwanza wa Yesu walikatala kupigana na kijiingiza mu kazi ya jeshi” juu walitambua kama ile mazoea “haipatane na kanuni ya upendo yenye Yesu alifundisha na agizo yake ya kama mutu anapaswa kupenda maadui wake.” Mwanatheolojia Mjerumani Peter Meinhold alisema hivi kuhusu wale wanafunzi wa kwanza wa Yesu: “Haingewezekana kuwa Mukristo na wakati uleule kuwa mwanajeshi.”

Tunasaidiaka Wengine

Siye Mashahidi wa Yehova tuko watu wazuri na tunaishi muzuri na watu wengine. Tunaheshimiaka wakubwa wa Serekali juu tunatii amri hizi za Biblia:

  • “Kila mutu ajitiishe kwa mamlaka zenye kuwa kubwa.”​—Waroma 13:1.

  • “Basi, mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”​—Matayo 22:21.

Njo maana, tunalipa kodi na tunaheshimia Serekali mu mambo ingine yenye wanatuomba kufanya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine