Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 53
  • Mutu Anakuwa Katika Hali Gani Anapokufa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutu Anakuwa Katika Hali Gani Anapokufa?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Roho Hawako Watu Wenye Waliishi ku Dunia Kisha Wakakufa
    Roho za Wafu—Zinaweza Kukusaidia ao Kukutendea Mubaya? Zinakuwaka Kabisa?
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Ulizo la 2: Nitakapokufa, Nitaenda Wapi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Watu Waliokufa Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 53

Mutu Anakuwa Katika Hali Gani Anapokufa?

Jibu la Biblia

Biblia inasema hivi: “Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5; Zaburi 146:4) Kwa hiyo, tunapokufa hatuendelee kuishi. Wafu hawawezi kuwaza, kutenda ao kufanya jambo lolote.

“Utarudi mavumbini”

Alipozungumuza na mwanaume wa kwanza, Adamu, Mungu alionyesha hali ya mutu ambaye amekufa. Adamu hakumutii Mungu, kwa hiyo Mungu alimuambia hivi: “Wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.” (Mwanzo 3:19) Mbele Mungu amuumbe Adamu ‘kutoka katika mavumbi ya inchi,’ Adamu hakuwa anaishi. (Mwanzo 2:7) Vivyo hivyo, Adamu alipokufa, alirudi katika mavumbi na maisha yake yaliishia hapo.

Hiyo ndio hali ya wale wanaokufa leo. Kuhusu watu na wanyama, Biblia inasema hivi: “Wote wametoka katika mavumbi, nao wote wanarudi mavumbini.”​—Mhubiri 3:19, 20.

Kifo si mwisho wa mambo yote

Biblia inalinganisha kifo na usingizi. (Zaburi 13:3; Yohana 11:11-14; Matendo 7:60) Mutu anayelala usingizi muzito hawezi kujua jambo lolote linalofanywa pembeni yake. Vivyo hivyo, wafu hawajue jambo lolote. Lakini, Biblia inafundisha kwamba Mungu anaweza kuwaamusha wale waliokufa kama kumuamusha mutu katika usingizi na kuwarudishia uzima. (Ayubu 14:13-15) Kwa wale ambao Mungu atafufua, kifo si mwisho wa mambo yote.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine