Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 87
  • Mupinga-Kristo Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mupinga-Kristo Ni Nani?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Namna ya kutambua wapinga-Kristo
  • Mupinga-Kristo Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 87
Mwalimu wa dini anahubiri kwenye televizyo

Mupinga-Kristo Ni Nani?

Jibu la Biblia

Mupinga-Kristo haiko mutu mumoja, shirika ao kikundi fulani cha pekee, kwa sababu Biblia inasema kwamba kuna “wapinga-Kristo wengi.” (1 Yohana 2:​18) Neno ‘mupinga-kristo,’ lenye kutoka katika neno la Kigiriki ambalo linamaanisha “zidi (ao badala) ya Kristo,” linahusu watu wote wenye:

  • Kukataa kwamba Yesu ndiye Kristo (Masiya) ao kukataa kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.​—1 Yohana 2:​22.

  • Kupinga Kristo, Mutiwa-Mafuta wa Mungu.​—Zaburi 2:​1, 2; Luka 11:23.

  • Kujifanya kuwa Kristo.​—Mathayo 24:24.

  • Kutesa wanafunzi wa Kristo, kwa sababu Yesu anaona mambo yenye wanatendea wanafunzi wake kuwa ni yeye anatendewa hivyo.​—Matendo 9:5.

  • Kujiita Wakristo lakini wanafanya matendo ya uasi-sheria ao ya udanganyifu.​—Mathayo 7:​22, 23; 2 Wakorintho 11:13.

Biblia inaita wapinga-Kristo watu wote wenye kufanya matendo hayo, lakini pia inawaita wote kwa ujumla ‘mupinga-Kristo.’ (2 Yohana 7) Mupinga-Kristo alitokea mara ya kwanza wakati wa mitume na tangu wakati huo anaendelea kufanya kazi. Unabii wa Biblia ulitabiri jambo hilo.​—1 Yohana 4:3.

Namna ya kutambua wapinga-Kristo

  • Wanaeneza mawazo ya uongo kuhusu Yesu. (Mathayo 24:​9, 11) Kwa mufano, watu wenye wanafundisha Utatu ao wenye kufundisha kwamba Yesu ndiye Mungu Mweza-Yote wanapinga kabisa mafundisho ya Yesu. Yesu alisema hivi: ‘Baba ni mukuu kuliko mimi.’​—Yohana 14:28.

  • Wapinga-Kristo wanakataa mambo Yesu alisema kuhusu kazi ya Ufalme wa Mungu. Kwa mufano, viongozi fulani wa dini wanasema kwamba Kristo anatenda kupitia serikali ao guvernema za wanadamu. Lakini, hilo linapingana na maneno haya ya Yesu: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”​—Yohana 18:36.

  • Wanasema kwamba Yesu ni Bwana wao, lakini hawatii amri zake, kutia ndani amri ya kuhubiri habari njema ya Ufalme.​—Mathayo 28:19, 20; Luka 6:​46; Matendo 10:42.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine