Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 140
  • Yesu Anatuokoa Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anatuokoa Namna Gani?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanamuamini Yesu?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 140
Yesu anazungukwa na watu wa rangi mbalimbali ya ngozi

Yesu Anatuokoa Namna Gani?

Jibu ya Biblia

Yesu aliokoa wanadamu waaminifu wakati alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi. (Matayo 20:28) Njo maana Biblia inamuita “mwokozi wa ulimwengu.” (1 Yohana 4:14) Biblia inasema tena hivi: “Hakuna wokovu katika mutu mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu lenye wanadamu walipewa, lenye kupitia hilo tunapaswa kuokolewa.”​—Matendo 4:12.

Yesu ‘alionja kifo kwa ajili ya kila mutu’ mwenye anamuamini. (Waebrania 2:9; Yohana 3:16) Kisha, “Mungu alimufufua kutoka kwa wafu,” na Yesu akarudia mbinguni akiwa kiumbe wa roho. (Matendo 3:15) Kule mbinguni, Yesu anaweza “kuokoa kwa ukamili wale wenye wanamukaribia Mungu kupitia yeye, kwa sababu sikuzote iko muzima ili kuwaombea.”​—Waebrania 7:25.

Juu ya nini tuko na lazima Yesu atukomboe?

Siye wote tuko watenda-zambi. (Waroma 3:23) Zambi Inatutenganisha na Mungu, na inatupeleka ku kifo. (Waroma 6:23) Lakini Yesu ni “muteteaji” wa wale ambao wanaamini bei yake ya ukombozi. (1 Yohana 2:1, maelezo ya chini) Anawatetea mbele ya Mungu, kwa kumuomba asikilize sala zao na awasamehe zambi zao kwa musingi wa zabihu yake ya ukombozi. (Matayo 1:21; Waroma 8:34) Mungu anasikilizaka ile maombi ya Yesu juu inapatana na mapenzi yake. Mungu alimutuma Yesu ku dunia “ili ulimwengu uokolewe kupitia yeye.”​—Yohana 3:17.

Kama tu unaamini Yesu ni kusema utaokolewa?

Hapana. Ni kweli kama tunapaswa kuamini Yesu juu tuokolewe, lakini kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufanya. (Matendo 16:30, 31) Biblia inasema hivi: “Kama vile mwili bila roho umekufa, vilevile pia imani bila matendo imekufa.” (Yakobo 2:26) Juu tuokolewe, tunapaswa:

  • Kujifunza juu ya Yesu na Baba yake, Yehova.​—Yohana 17:3.

  • Kuwaamini.​—Yohana 12:44; 14:1.

  • Kuonyesha imani yetu kwa kutii amri zao (Luka 6:46; 1 Yohana 2:17) Yesu alifundisha kama haiko kila mutu mwenye anamuita “Bwana” njo ataokolewa, lakini ni ule tu mwenye “kufanya mapenzi ya Baba [yake] mwenye kuwa mbinguni.”​—Matayo 7:21.

  • Kuendelea kuonyesha imani hata wakati wa magumu. Yesu alionyesha waziwazi ile jambo wakati alisema hivi: “Lakini ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.”​—Matayo 24:13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine