Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 143
  • Kuvuta Tumbako Ni Zambi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuvuta Tumbako Ni Zambi?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Biblia inasema jambo fulani juu ya kutumia bangi ao dawa zingine za kulewesha?
  • Ninapovuta tumbaku, je, Mungu anachukia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mawazo ya Mungu Ni Gani Juu ya Kuvuta Tumbaku?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 143
Mutu mwenye kuvuta tumbako

Kuvuta Tumbako Ni Zambi?

Jibu ya Biblia

Biblia haizungumuzie kuvuta tumbakoa ao njia zingine za kutumia tumbako. Lakini iko na kanuni zenye kuonyesha kama Mungu anachukia mazoea machafu yenye kuharibisha afya, njo maana kwake, kuvuta tumbako ni zambi.

  • Kuheshimia uzima. “Mungu . . . anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:24, 25) Kwa kuwa uzima ni zawadi kutoka kwa Mungu, hatupaswe kufanya jambo yoyote yenye inaweza kufupisha maisha yetu, kama vile kuvuta tumbako. Kuvuta tumbako iko kati ya mambo ya nguvu yenye inatokeza vifo vyenye vingeweza kuzuiliwa mu dunia.

  • Kupenda jirani. “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Matayo 22:39) Kuvuta tumbako pembeni ya watu wengine, kunaonyesha kama hauwapendi. Watu wenye kwa ukawaida wanapumua moshi kutoka kwa mutu mwenye kuvuta tumbako, wako mu hatari sana ya kupata ileile ugonjwa yenye mara mingi inapataka wavuta-tumbako.

  • Ulazima wa kuwa mutakatifu. “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.” (Waroma 12:1) “Tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho, tukikamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.” (2 Wakorinto 7:1) Kuvuta tumbako haiko jambo ya asili na haipatane na kuwa mutakatifu, ni kusema, kitu safi na yenye kutakata. Juu watu wenye kutumia tumbako wanaingiza kwa makusudi mu mwili yao sumu yenye inaweza kuharibu mwili yao.

Biblia inasema jambo fulani juu ya kutumia bangi ao dawa zingine za kulewesha?

Biblia haizungumuzie bangi ao dawa zingine za kulewesha. Lakini iko na kanuni zenye kuonyesha kama haifae kutumia vitu kama vile vyenye vinafanya mutu akuwe mutumwa. Zaidi ya zile kanuni zenye tulizungumuzia, hizi ni kanuni zingine zenye zinatumika mu hii hali:

  • Ulazima wa kulinda uwezo wetu wa kufikiri. “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako . . . kwa akili yako yote.” (Matayo 22:37, 38) “Mulinde akili zenu kwa ukamili.” (1 Petro 1:13) Mutu hawezi kulinda muzuri akili yake wakati iko anatumia dawa kwa njia ya mubaya. Watu wengi hata wanakuwa watumwa wa zile dawa. Akili yao inakuwa tu inawaza namna ya kupata na kutumia dawa za kulewesha kuliko kukaza akili juu ya mawazo yenye kujenga.​—Wafilipi 4:8.

  • Kutii sheria za serikali. “[Watii] serikali na mamlaka.” (Tito 3:1) Mu mainchi ya mingi, sheria zinakataza kabisa kutumia dawa fulani. Kama tunataka kumupendeza Mungu, tunapaswa kutii sheria za serikali.​—Waroma 13:1.

Tumbako na Afya Yako

Shirika ya Afya Ulimwenguni (OMS) inaonyesha kama kila mwaka, karibu watu milioni sita wanakufa na magonjwa yenye kuhusiana na tumbako, kutia ndani zaidi ya watu 600 000 wenye wamevuta moshi ya wavuta-tumbako. Ona matokeo ya mubaya ya tumbako kwa wale wenye kuivuta na kwa wale wenye kuwa pembeni yao.

Kansere. Moshi ya tumbako iko na kemikali (composés chimiques) zaidi ya 50 zenye zinaweza kuleta kansere. Encyclopædia Britannica inasema kama “moshi ya tumbako njo yenye inaleta 90% ya kansere ya mapafu.” Moshi ya tumbako inaweza kuleta kansere mu sehemu zingine za mwili, sawa vile kinywa, koromeo (trachée), umio (œsophage), koo, zoloto (larynx), maini, kongosho (pancréas), na kibofu (vessie).

Magonjwa ya mufumo (système) wa kupumua. Moshi ya tumbako inaongeza uwezekano wa kupata ugonjwa wa mufumo wa kupumua, sawa vile nimonia (pneumonie) na homa. Watoto wenye wanapumua moshi ya wavuta-tumbako wako mu hatari sana ya kupata ugonjwa wa pumu (asthme), kikohozi yenye haiishake, na inafanya mapafu (poumons) isitumike muzuri.

Ugonjwa wa moyo. Wavuta-tumbako wako mu hatari kubwa sana ya kupata AVC na ugonjwa wa moyo. Kaboni monoksidi (monoxyde de carbone) yenye kuwa mu moshi ya tumbako inapita kwa urahisi kutoka mu mapafu kuingia kwenye mufumo wa damu, na kuchukua mahali pa oksijeni. Juu mu damu munakuwa oksijeni kidogo, moyo unalazimika kufanya kazi kwa nguvu zaidi ili kusambaza oksijeni mu mwili.

Hatari kwa wanamuke wenye kuwa na mimba. Wanamuke wenye kuwa na mimba wenye wanazoea kuvuta tumbako, wanaongezea watoto wao hatari ya kuzaliwa mbele ya wakati (prématurés), kuzaliwa na kilo ya kidogo, ao na shida fulani kama vile mudomo wenye kupasuka. Wale watoto wanaweza kupatwa na matatizo ya kupumua ao wanaweza kufa kwa kushtukia.

a Hapa, kuvuta maana yake kukokota kwa makusudi moshi ya tumbako ao ya paipo. Lakini kanuni zenye tutazungumuzia zinahusu pia kutafuna majani ya tumbako ao kutumia kwa njia ya kielektroniki tumbako yenye kuwa na nicotine na vitu vingine sawa ile.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine