Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 155
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Ni kutoa ya namna gani njo inafurahishaka Mungu?
  • Ni kutoa ya namna gani njo haifurahishake Mungu?
  • ‘Mungu Anamupenda Mutoaji Muchangamufu’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Furahia Baraka ya Kutoa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Watu Wenye Kutoa kwa Ukarimu Ni Wenye Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Watu Wanajikaza Kupata Zawadi ya Muzuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 155
Mwanaume iko na zawadi mu mikono

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?

Jibu ya Biblia

Biblia inatutia moyo tutoe kwa kujipendea na kwa nia ya muzuri. Inaonyesha kama kutoa kunaleteaka furaha mwenye anapokea na mwenye anatoa. (Mezali 11:25; Luka 6:38) Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

  • Ni kutoa ya namna gani njo inafurahishaka Mungu?

  • Ni kutoa ya namna gani njo haifurahishake Mungu?

  • Maandiko yenye kuzungumuzia kutoa

Ni kutoa ya namna gani njo inafurahishaka Mungu?

Mungu anafurahiaka wakati tunatoa kwa kujipendea. Biblia inasema hivi: “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokutaka wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”​—2 Wakorinto 9:7, maelezo ya chini.

Tunapaswa kutoa kwa moyo wote ikiwa tunapenda Mungu akubali “ibada” yetu. (Yakobo 1:27) Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya musaada anamufurahisha Mungu, na Mungu anaona kama kufanya vile ni kumukopesha. (Mezali 19:17) Biblia inafundisha kama Mungu yeye mwenyewe atamulipa.​—Luka 14:12-​14.

Ni kutoa ya namna gani njo haifurahishake Mungu?

Wakati nia ya mubaya njo inatuchochea kutoa. Kwa mufano, wakati tunatoa:

  • Juu wengine watuone.​—Matayo 6:2.

  • Juu na siye tupewe kitu fulani.​—Luka 14:12-14.

  • Juu ya kujaribu kuuza uzima wa milele.​—Zaburi 49:6, 7.

Wakati tunatoa juu ya kutegemeza mambo yenye Mungu anakataza. Kwa mufano, ni mubaya kupatia mutu makuta juu aende kucheza michezo ya makuta, juu auze dawa za kulewesha, ao juu akunywe pombe kupita kiasi. (1 Wakorinto 6:9, 10; 2 Wakorinto 7:1) Vilevile, haiko muzuri kupatia mutu mwenye iko na nguvu ya kutumika juu ajitimizie mahitaji yake, lakini hapendi tu kutumika.​—2 Watesalonike 3:10.

Wakati tunatoa kupita kiasi mupaka familia yetu inakosa mambo ya lazima. Biblia inafundisha kama vichwa vya familia wanapaswa kutimiza mahitaji ya watu wa familia yao. (1 Timoteo 5:8) Haiko muzuri kichwa cha familia akuwe mukarimu sana na kisha watu wa familia yake wakose mambo ya lazima. Vilevile, Yesu alilaumu wale wenye walikatala kuhangaikia wazazi wao wenye kuzeeka juu ya kusema kama mali yao yote ilikuwa “zawadi yenye imetolewa kwa Mungu.”​—Marko 7:9-​13.

Maandiko yenye kuzungumuzia kutoa

Mezali 11:25: “Mutu mukarimu atafanikiwa, na ule mwenye kuburudisha wengine yeye mwenyewe ataburudishwa.”

Ni kusema: Kutoa kunaletea faida mwenye anapokea na mwenye anatoa.

Mezali 19:17: “Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova, na Yeye atamulipa kwa sababu ya mambo yenye anatenda.”

Ni kusema: Mungu anaona kama iko na deni ya wale wenye wanasaidia watu wenye kuwa na lazima ya musaada, na anaahidi kama atawalipa kwa sababu ya ukarimu wao.

Matayo 6:2: “Wakati unatoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako, kama vile wanafiki wanafanya . . . ili watu wawasifu.”

Ni kusema: Hatupaswe kutoa juu tu wengine watuone.

Matendo 20:35: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”

Ni kusema: Kutoa kwa moyo wote kunaletaka furaha.

2 Wakorinto 9:7: “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”

Ni kusema: Mungu anafurahi wakati tunatoa kwa kupenda.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine