Ninapenda Kufa—Biblia Inaweza Kunisaidia Wakati Niko na Mawazo ya Kujiua?
Jibu ya Biblia
Ndiyo! Biblia ni kitabu ya “Mungu, mwenye kufariji wale wenye wameshuka moyo.” (2 Wakorinto 7:6) Hata kama Biblia haiko kitabu ya kuonyesha namna ya kutunza magonjwa ya akili, imesaidia watu wengi kupiganisha mawazo ya kujiua. Mashauri yake inaweza kukusaidia na weye.
Biblia inatupatia mashauri gani ya muzuri?
● Ambia wengine namna uko najisikia.
Biblia inasema hivi: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”—Mezali 17:17.
Ni kusema: Tuko na lazima ya musaada wa wengine wakati tuko na mawazo yenye kutuhangaisha.
Kama hauambie wengine namna uko najisikia, ni sawa vile uko nabeba muzigo wenye unakupita nguvu. Lakini kama unaambia wengine namna uko najisikia, utatulia na utaanza kuwa na mawazo ya muzuri zaidi juu ya hali yako.
Jaribu kufanya hivi: Zungumuza na mutu fulani leo, anaweza kuwa mutu wa familia ao rafiki mwenye unatumainia. Tena, unaweza kuandika ku karatasi namna uko najisikia.
● Uende kuonana na munganga.
Biblia inasema hivi: “Watu wenye afya ya muzuri hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake.”—Matayo 9:12.
Ni kusema: Tunapaswa kuonana na munganga wakati tunagonjwa.
Mawazo ya kujiua ni alama yenye kuonyesha kama pengine tuko na ugonjwa fulani wa kiakili ao wa kihisia. Ni sawa tu magonjwa ingine. Hatupaswe kuisikilia haya. Magonjwa ya kiakili na kihisia inaweza kutunzwa.
Jaribu kufanya hivi: Uende kuonana na munganga mwenye uzoefu haraka kadiri inawezekana.
● Kumbuka kama Mungu anakuhangaikia.
Biblia inasema hivi: “Ndege shomoro tano (5) wanauzishwa kwa feza mbili za vichele zenye samani kidogo, haiko vile? Hata hivyo Mungu hamusahau hata mumoja wao. . . . Musiogope; ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.”—Luka 12:6, 7.
Ni kusema: Mungu anakuona kuwa wa maana.
Pengine unawaza kama hakuna mwenye anakuhangaikia, lakini Mungu iko naona mambo yote yenye uko napita ndani. Anakuhangaikia, hata kama hauna tena hamu ya kuishi. Zaburi 51:17 inasema hivi: “Moyo wenye kuvunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautaukataa.” Mungu anataka uendelee kuishi juu anakupenda.
Jaribu kufanya hivi: Tafuta maandiko yenye inahakikisha kama Mungu anakupenda. Kwa mufano, ona sura ya 24 ya kitabu Mkaribie Yehova.
● Sali kwa Mungu.
Biblia inasema hivi: “Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.”—1 Petro 5:7.
Ni kusema: Mungu anakuomba umuelezee waziwazi mambo yote yenye iko nakuhangaisha.
Mungu anaweza kukupatia amani ya akili na nguvu ya kuendelea kuvumilia hali yako. (Wafilipi 4:6, 7, 13) Ni vile anafanyaka juu ya kusaidia wale wenye wanamuomba musaada.—Zaburi 55:22.
Jaribu kufanya hivi: Sali kwa Mungu leo. Tumia jina yake, Yehova, na umuambie namna uko najisikia. (Zaburi 83:18) Umuambie akusaidie uendelee kuvumilia.
● Fikiri sana juu ya mambo yenye Mungu atatufanyia mu siku zenye ziko nakuya.
Biblia inasema hivi: “Tuko na tumaini hilo kama nanga ya uzima wetu, likiwa hakika na pia imara.”—Waebrania 6:19, maelezo ya chini.
Ni kusema: Hisia zako zinaweza kupanda na kushuka sawa vile mashua yenye iko napelekwa na upepo mukali, lakini tumaini yenye Mungu anatupatia mu Biblia inaweza kukusaidia utulie.
Ile tumaini haiko ndoto. Ni ahadi yenye Mungu anatupatia. Anatuambia kama atamaliza mambo yote yenye kutuletea maumivu.—Ufunuo 21:4.
Jaribu kufanya hivi: Soma Shabari yenye kichwa “Tumaini Bora la Wakati Ujao.“ ya broshua Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu! juu uone mambo yenye Mungu atatufanyia mu siku zenye ziko nakuya.
● Fanya jambo fulani yenye unafurahiaka.
Biblia inasema hivi: “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri.”—Mezali 17:22.
Ni kusema: Kufanya mambo yenye tunafurahiaka kunaweza kusaidia afya yetu ya kiakili na kihisia ikuwe muzuri zaidi.
Jaribu kufanya hivi: Fanya jambo fulani yenye unafurahiaka. Kwa mufano, sikiliza muziki muzuri, soma habari yenye kutia moyo, ao fanya jambo ingine yenye unafurahiaka. Tena, utakuwa na furaha zaidi kama unafanya mambo fulani juu ya kusaidia wengine, hata mu mambo ya kidogo-kidogo.—Matendo 20:35.
● Hangaikia afya yako.
Biblia inasema hivi: “Mazoezi ya mwili ni yenye faida kidogo.”—1 Timoteo 4:8.
Ni kusema: Tunapata faida wakati tunafanya mazoezi, wakati tunalala saa za kutosha, na wakati tunakula chakula ya kujenga mwili.
Jaribu kufanya hivi: Uende utembee inje mbio-mbio, hata kwa dakika 15 tu.
● Ukumbuke kama hisia na mambo ingine inabadilikaka mu maisha.
Biblia inasema hivi: “Hamujue maisha yenu yatakuwa namna gani kesho.”—Yakobo 4:14.
Ni kusema: Tatizo yenye iko nakusumbua sana, yenye pengine unaona kama haitaishaka, inaweza kuwa ya wakati kidogo tu.
Hata kama leo hali yako inaonekana kuwa ya nguvu sana, inaweza kubadilika kesho. Kwa hiyo, uvumilie. (2 Wakorinto 4:8) Hali yenye iko nakuhangaisha sana inaweza kubadilika kisha wakati fulani. Lakini kama unajiua, mambo inaishia pale.
Jaribu kufanya hivi: Soma mu Biblia habari za watu wenye walivunjika moyo sana na hata wakapenda kufa. Ona namna maisha yao ilifikia kubadilika na kuwa ya muzuri zaidi, na mara mingi maisha yao ilibadilika mu namna yenye hawakuwazia. Ona mifano fulani.
Biblia inazungumuzia watu wenye walipendaka kufa?
Ndiyo. Biblia inazungumuzia watu fulani wenye walisemaka kwa njia fulani hivi: “Ninapenda kufa.” Mungu hakuwakaripia, lakini aliwasaidia. Na weye, anaweza kukusaidia.
Eliya
● Alikuwa nani? Eliya alikuwa nabii mwenye uhodari. Lakini yeye pia alivunjikaka moyo. Yakobo 5: 17 inasema kama “Eliya alikuwa mutu mwenye hisia kama zetu.”
● Juu ya nini alipenda kufa? Wakati fulani, Eliya alijisikia kuwa peke yake, alikuwa na woga, na alijiona kuwa mutu wa bure. Kwa hiyo, aliomba hivi: “Yehova, ondoa uzima wangu.”—1 Wafalme 19:4.
● Nini njo ilimusaidia? Eliya alimuambia Mungu namna alikuwa najisikia kabisa. Mungu alifanya nini juu ya kumutia moyo? Mungu alimuonyesha kama anamuhangaikia na akamuonyesha namna iko na nguvu mingi sana. Tena, alimuhakikishia Eliya kama angali mutu wa maana na akamupatia mutu wa kumusaidia na kumutegemeza.
▸ Soma habari kuhusu Eliya: 1 Wafalme 19:2-18.
Yobu
● Alikuwa nani? Yobu alikuwa tajiri, alikuwa na bibi na watoto, na alikuwa namuabudu Mungu wa kweli kwa uaminifu.
● Juu ya nini alipenda kufa? Mambo mingi ya mubaya ilimufikia Yobu bila kutazamia. Alipoteza mali yake yote. Watoto wake wote walikufa katika musiba. Alipatwa na ugonjwa mubaya sana. Na ku mwisho, marafiki wake walimushitaki mambo ya uongo kwa kusema kama yeye njo alijiletea ile magumu. Yobu alisema hivi: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.”—Yobu 7:16.
● Nini njo ilimusaidia? Yobu alisali kwa Mungu na alizungumuza na wengine. (Yobu 10:1-3) Elihu, rafiki yake mwenye huruma, alimutia moyo na kumusaidia akuwe na mawazo yenye kufaa juu ya hali yake. Na zaidi ya yote, Yobu alikubali mashauri na musaada wa Mungu.
▸ Soma habari kuhusu Yobu: Yobu 1:1-3, 13-22; 2:7; 3:1-13; 36:1-7; 38:1-3; 42:1, 2, 10-13.
Musa
● Alikuwa nani? Musa alikuwa kiongozi wa Israeli ya zamani na alikuwa nabii muaminifu
Juu ya nini alipenda kufa? Musa alikuwa na kazi mingi sana, watu walimuchambua mara kwa mara, na alichoka sana. Njo maana alimulilia Mungu hivi: “Tafazali uniue sasa hivi.”—Hesabu 11:11, 15.
● Nini njo ilimusaidia? Musa aliambia Mungu namna alikuwa najisikia. Mungu alichagua watu fulani juu wamusaidie kutumika kazi yake na ile ilifanya asikuwe na mahangaiko ya mingi.
▸ Soma habari kuhusu Musa: Hesabu 11:4-6, 10-17.