Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwyp habari 90
  • Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya?
  • Vijana Wanauliza
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unajionaka namna gani?
  • Juu ya nini ni jambo la maana?
  • Mambo yenye unaweza kufanya
  • Soma habari yenye itakusaidia ukuwe na mutazamo muzuri
  • Mawazo Yako Ni ya Maana Sana!
    Amuka!—2016
  • Nifanye Nini Kama Inaonekana Kuwa Wengine Hawanipendi?
    Vijana Wanauliza
Vijana Wanauliza
ijwyp habari 90
Mwanamuke mumoja iko anawaza mubaya juu ya maisha na mvua iko inamunyeshea

VIJANA WANAULIZA

Namna Gani Ninaweza Kuepuka Mawazo ya Mubaya?

  • Uko na mawazo gani juu yako?

  • Juu ya nini ni jambo la maana?

  • Mambo yenye unaweza kufanya

  • Soma habari yenye itakusaidia ukuwe na mawazo ya muzuri

  • Mambo vijana wenzako wanasema

Unajionaka namna gani?

  • Niko na mutazamo muzuri

    “Ninajikaza kuwa mwenye furaha na mwenye kuepuka kukasirika. Ninapenda kuwa na sura yenye furaha kila siku.”—Valerie.

  • Niko na mutazamo mubaya

    “Wakati jambo la muzuri linatokea, mara moja ninawaza kama haiwezi kuwa kweli, ao haiwezekane.”—Rebecca.

  • Niko na mawazo yenye kufaa

    “Kama niko na mutazamo muzuri nitavunjika moyo wakati mambo haiende muzuri, na kama niko na mutazamo mubaya nitaishi bila furaha. Kuwa na mawazo yenye kufaa kunanisaidia nione mambo vile iko kwa kweli.”—Anna.

Juu ya nini ni jambo la maana?

Biblia inasema kama “mutu mwenye moyo wa furaha iko na karamu sikuzote.” (Mezali 15:15) Ni wazi kuwa, mara mingi watu wenye kuepuka mawazo ya mubaya na wenye kuwa na mawazo ya muzuri juu ya maisha, wanakuwaka na furaha. Wanaweza pia kuwa na marafiki wengi. Kusema kweli, ni nani anapendaka kupitisha wakati na watu wenye kuwa na huzuni kila mara?

Lakini, hata kama uko mutu mwenye kuwa na mutazamo muzuri unaweza tu kupata magumu. Kwa mufano:

  • Kila mara vyombo vya habari vinatangaza mambo ya vita, ugaidi (terrorisme), ao matendo ya kuvunja sheria.

  • Unaweza kupambana na matatizo katika familia yako.

  • Bila shaka uko unapambana na uzaifu wako mwenyewe.

  • Rafiki yako anaweza kukuhuzunisha.

Kuliko kufanya kama vile ile matatizo haiko, ao kuikazia akili sana, ujikaze kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya ile matatizo. Kuwa na mawazo yenye kufaa kutakusaidia usikuwe na mawazo ya mubaya kupita kiasi, na pia kutakusaidia ukubali matatizo ya maisha bila kuvunjika moyo sana.

Mwanamuke mumoja iko anawaza muzuri juu ya maisha na mvua inaacha kunyesha

Unaweza kupambana na pepo kali za maisha, na ukuwe hakika kama hali itakuwa muzuri tu

Mambo yenye unaweza kufanya

  • Ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya makosa yako.

    Biblia inasema kama: “Hakuna mwenye haki katika dunia mwenye anafanya mema sikuzote na hafanyake zambi.” (Muhubiri 7:20) Wakati unafanya makosa ile inaonyesha tu kama uko mwanadamu, haionyeshe kama uko wa bure.

    Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Ujikaze kubadilika, lakini usitazamie kama utakuwa mukamilifu. Kijana mwenye kuitwa Caleb anasema hivi: “Ninajikaza kuepuka kufikiri sana juu ya makosa yangu. Kuliko kufanya vile, ninajikaza kujifunza kutokana na makosa yangu ili nifanye mabadiliko.”

  • Epuka kujilinganisha na wengine.

    Biblia inasema hivi: “Tusikuwe tunajisifu, tusichochee mashindano kati yetu, tusisikiliane wivu.” (Wagalatia 5:26) Wakati unaangalia picha za matukio yote yenye haukualikwa, zenye watu wanatia ku site za Enternete za kupashana habari, unaweza kukasirika na kuvunjika moyo. Ile inaweza kufanya uone marafiki wako wa sana kuwa maadui wako wa sana.

    Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Jua kama hawatakualika ku kila karamu. Zaidi ya ile, picha zenye watu wanatia ku site za Enternete za kupashana habari hazionyeshe mambo yote. Kijana mumoja mwenye kuitwa Alexis anasema hivi: “Mara mingi, ku site za Enternete za kupashana habari, watu wanatia picha za matukio ya maana sana ya maisha yao. Mara mingi hawatie picha zenye kuonyesha mambo ya kawaida.”

  • Ukuwe mutu mwenye kufanya amani, zaidi sana katika familia yako.

    Biblia inasema hivi: “Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani.” (Waroma 12:18) Hauwezi kuzuia kabisa matendo ya wengine, lakini unaweza kuzuia matendo yako. Unaweza kuchagua kuwa mutu mwenye kufanya amani.

    Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Ujikaze sana usiongezee familia yako matatizo, lakini ukuwe mutu mwenye kufanya amani, kama vile ungefanya na marafiki wako. Kijana mumoja mwenye kuitwa Melinda anasema hivi: “Hakuna mutu mwenye iko mukamilifu, na sisi wote tunaweza kukosea wengine kila mara. Ni daraka letu kuamua ikiwa tutafanya amani na wengine ao hapana.”

  • Ukuwe mwenye shukrani.

    Biblia inasema: “Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.” (Wakolosai 3:15) Kuwa mwenye shukrani kutakusaidia ukazie akili mambo ya muzuri katika maisha yako, kuliko kukazia akili mambo yenye haikufurahishe.

    Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Kubali kama uko na matatizo, lakini usisahau kama kuko pia mambo ya muzuri katika maisha yako. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Rebecca anasema hivi: “Kila siku, ninaandika jambo moja la muzuri katika buku langu. Ninapenda kujikumbusha kama, hata kama niko na magumu, niko pia na mambo mingi ya muzuri ya kufikiria.”

  • Chunguza marafiki wako.

    Biblia inasema hivi: “Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.” (1 Wakorinto 15:33) Kama unazoea kupitisha wakati pamoja na watu wenye kuwa na tabia ya kuchekelea wengine, ao watu wenye kuweka kinyongo, wewe pia utakuwa na tabia hizo.

    Namna ya kuwa na mawazo yenye kufaa: Wakati marafiki wako wanapata magumu, wanaweza kuhuzunika na kushuka moyo kwa wakati fulani. Uwategemeze, lakini usiache magumu yao ikuhangaishe sana. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Michelle anasema hivi: “Hatupaswe tu kupitisha wakati na watu wenye kuwa na mawazo ya mubaya.”

Soma habari yenye itakusaidia ukuwe na mutazamo muzuri

Tunaishi wakati wenye Biblia inaita “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Timoteo 3:1) Unaona ni nguvu kuwa na mutazamo muzuri katika dunia yenye kujaa magumu? Soma habari yenye kichwa “Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?”

Mambo vijana wenzako wanasema

Emma

“Wakati ninakuwa na mawazo ya mubaya, ninafanya liste ya mambo ya muzuri na ya mambo ya mubaya kuhusu jambo lenye linanisumbua. Ile inanisaidia nione mambo vile iko kabisa, hapana tu kulingana na namna ninajisikia. Mara mingi, kunakuwaka mambo fulani ya muzuri hata wakati hali inaonekana kuwa ya mubaya.”—Emma.

Jesse

“Wakati ninakuwa na mawazo ya mubaya, ninatafuta namna ya kusaidia mutu fulani ao ninatafuta jambo fulani lenye ninaweza kufanyia watu wengine. Yesu alisema kama kuko furaha mingi katika kutoa, na mara mingi, wakati ninapatia wengine, ile inanisaidia nisifikirie mambo ya mubaya yenye ninapambana nayo.”—Jesse.

Kwa kifupi: Namna Gani Ninaweza Kuepuka Kuwa na Mawazo ya Mubaya?

Ukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya makosa yako. Ujikaze kubadilika, lakini usitazamie kuwa mukamilifu.

Epuka kujilinganisha na wengine. Usijisikie mubaya kama haualikwe kwenye sherehe fulani.

Ukuwe mutu mwenye kufanya amani, zaidi sana katika familia yako. Usiongezee familia yako matatizo, fanya yote yenye unaweza ili kukuwe amani.

Ukuwe mwenye shukrani. Kubali matatizo yako, lakini usisahau kama kuko pia mambo ya muzuri katika maisha yako.

Chunguza marafiki wako. Tafuta marafiki wenye hawaache matatizo ya maisha iwahangaishe sana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine