Maelezo ya Chini
c Kuna mambo mawili katika habari yao yanayoonyesha namna walivyokosa heshima. Jambo la kwanza: Sheria ilionyesha waziwazi sehemu ya nyama iliyotolewa zabihu ambayo makuhani waliruhusiwa kula. (Kum. 18:3) Lakini katika hema ya ibada, makuhani hao waovu walianzisha jambo tofauti kabisa. Waliwalazimisha watu wao kuingiza kanya kubwa katika chungu cha kupikia ambacho kilikuwa na nyama zilizokuwa zikitokota, na kuchukua kipande chochote kizuri walichopata! Jambo la pili: Watu walipoleta zabihu zao ili zichomwe kwenye mazabahu, makuhani hao waovu waliwatuma watu wao kuwaogopesha watu walioleta zabihu, waliwalazimisha wawapatie nyama ya mubichi mbele ya kumutolea Yehova zabihu ya sehemu ya mafuta.—Law. 3:3-5; 1 Sam. 2:13-17.