Maelezo ya Chini
a Waandishi wa zamani walibadilisha maneno “nafsi yako” katika andiko hilo na kusema “nafsi yangu,” ili kuonyesha kama yanamuhusu Yeremia. Labda waliwaza kama kusema nafsi ya Mungu ni kumukosea heshima, kwa sababu Biblia inatumia neno nafsi kwa ajili ya viumbe vilivyo duniani. Lakini, Biblia inapozungumuza juu ya Mungu, mara nyingi inatumia maneno ambayo watu wanaweza kuelewa. Kwa sababu neno “nafsi” linaweza kumaanisha “uzima tulio nao,” maneno “nafsi yako” yanamaanisha “wewe.”