Maelezo ya Chini
a Ikiwa hakuna mapainia wapya wa kutosha, mapainia fulani ambao hawakupata kusoma masomo hayo miaka tano iliyopita wanaweza kualikwa tena.
Masomo ya Wazee wa Kutaniko
Kusudi: Kusaidia wazee washugulikie vizuri madaraka yao katika kutaniko na kuwasaidia watengeneze vizuri zaidi hali yao ya kiroho.
Muda: Siku tano.
Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu ao Jumba la Mikusanyiko linatumiwa.
Wanaostahili Kuhuzuria: Wazee.
Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee wanaalikwa na biro ya tawi.
Wazee fulani waliohuzuria darasa la 92 la Masomo hayo katika États-Unis walitoa maelezo yafuatayo:
“Masomo haya yameniletea faida nyingi, yamenisaidia kujichunguza na kuona namna ninavyoweza kutunza kondoo za Yehova.”
“Sasa niko tayari ili niweze kuwatia wengine moyo zaidi kwa kukazia mambo makubwa ya Maandiko.”
“Nitatumia mambo niliyojifunza maisha yangu yote.”
Masomo ya Waangalizi Wasafiri na Bibi Zao
Kusudi: Kusaidia waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya wawe na matokeo mazuri zaidi katika kutumikia makutaniko na ‘wanapofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.’—1 Tim. 5:17; 1 Pet. 5:2, 3.
Muda: Miezi miwili.
Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi.
Wanaostahili Kuhuzuria: Waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya.
Jinsi ya Kujiandikisha: Waangalizi wasafiri na bibi zao wanaalikwa na biro ya tawi.
Ndugu Joel, aliyehuzuria somo la 1, katika mwaka wa 1999, alisema hivi: Furaha yetu kuhusu namna Yesu anavyosimamia tengenezo iliongezeka zaidi. Tuliona kama ni lazima kuwatia ndugu moyo na kusaidia kila kutaniko liwe na umoja. Masomo yalitufundisha kama hata ikiwa wakati fulani mwangalizi anapaswa kutoa shauri na kukaripia, kusudi lake kubwa ni kuwasaidia ndugu wajue kama Yehova anawapenda.”
Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi
Kusudi: Kutayarisha wazee na watumishi wa huduma wasio na bibi ili wachukue madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova. Wengi kati ya wale wanaomaliza masomo hayo wanapewa mugawo wa kutumikia mahali ambapo kuna lazima kubwa katika inchi yao. Wengine kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wako tayari kukubali hilo. Na wengine wanaweza kuwa mapainia wa pekee wa muda ili kufungua maeneo mapya na kupanua kazi ya kuhubiri katika maeneo ya mbali na maeneo yasiyogawiwa makutaniko.
Muda: Miezi miwili.
Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme linatumiwa.
Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu wasio na bibi walio na umri wa miaka kati ya 23 na 62 ambao wana afya nzuri na wanaotaka kutumikia mahali popote palipo na lazima kubwa. (Mk. 10:29, 30) Wanapaswa kuwa wamefanya kazi ya upainia wa kawaida kwa miaka miwili ao zaidi na kuwa wazee ao watumishi wa huduma kwa miaka miwili hivi ao zaidi bila kukatiza.
Jinsi ya Kujiandikisha: Mukutano unafanywa kwenye mukusanyiko wa muzunguko kwa ajili ya wale wanaotaka kuhuzuria masomo hayo.
Ndugu Rick, mwanafunzi wa somo la 23 katika États-Unis anasema hivi: “Kuzama katika mafundisho ya masomo hayo kumefanya roho ya Yehova inibadilishe kabisa. Yehova anapokupatia kazi fulani, anakusaidia ili uitimize. Nimejifunza kama ikiwa ninajitoa kabisa katika kufanya mapenzi ya Mungu wala si yangu, Yehova atanipa nguvu.”
Andreas, ambaye sasa anatumikia Alemanye, anaeleza hivi: “Nimejifunza kuona kama namna tengenezo la Mungu linavyofanya kazi leo ni muujiza. Masomo hayo yalinisaidia kwa sababu yalinitayarisha kwa ajili ya kazi ya wakati ujao. Tena, mifano mbalimbali ya Biblia ilinifundisha kweli hii ya musingi: Kumutumikia Yehova na ndugu zangu kunaleta furaha ya kweli.”
Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Bibi Zao
Kusudi: Kutolea ndugu na bibi zao mazoezi ya pekee ili Yehova na tengenezo lake wawatumie zaidi. Kati ya wale wanaomaliza masomo hayo, wengi wanapewa mugawo wa kutumikia mahali palipo na lazima katika inchi yao. Wengine kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wanakubali. Wanaohuzuria masomo hayo wanaweza kuwa mapainia wa pekee wa muda ili kufungua maeneo mapya na kupanua kazi ya kuhubiri katika maeneo ya mbali na maeneo yasiyogawiwa makutaniko.
Muda: Miezi miwili.
Mahali: Kwa sasa masomo hayo yanaongozwa katika États-Unis, na kuanzia Mwezi wa 9 2012, biro za tawi fulani katika dunia zitachaguliwa ili kupanga masomo hayo, kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme litatumiwa.
Wanoastahili Kuhuzuria: Ndugu na bibi zao walio na miaka kati ya 25 na 50 na wenye afya nzuri ambao hali zao zinawaruhusu kutumikia mahali popote palipo na lazima na walio na mwelekeo wa kusema: “Mimi hapa! Nitume mimi.” (Isa. 6:8) Pia, wanapaswa kuwa wameoana kwa miaka miwili hivi ao zaidi na kuwa katika utumishi wa wakati wote kwa miaka miwili ao zaidi bila kukatiza. Ndugu anapaswa kuwa muzee ao mutumishi wa huduma kwa miaka miwili hivi ao zaidi bila kukatiza.
Jinsi ya Kujiandikisha: Mukutano unafanywa kwenye mukusanyiko wa wilaya kwa ajili ya wale wanaotaka kuhuzuria masomo hayo. Ikiwa mukutano huo haufanyike katika inchi unamoishi na ikiwa unataka kuhuzuria masomo hayo, unaweza kuandikia biro ya tawi ya inchi yenu ili kupata habari zaidi.
Ndugu Eric na bibi yake Corina (hapa chini), waliohuzuria somo la 1, mwaka wa 2011 wanasema hivi: “Majuma munane hayo yalibadili maisha yetu kabisa na ni pendeleo kabisa kwa wenzi wa ndoa wanaotaka kufanya mengi katika kazi ya Yehova kuhuzuria masomo haya! Tumeazimia kuwa na maoni yanayofaa juu ya maisha, hilo litatusaidia kutumia wakati wetu kwa hekima.”
Masomo ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower
Kusudi: Kuzoeza wanafunzi ili kuwa wamisionere katika maeneo yaliyo na watu wengi, kuwa waangalizi wanaosafiri ao Wanabeteli. Kusudi ni kutia nguvu na kuimarisha kazi ya kuhubiri na biro za tawi.
Muda: Miezi tano.
Mahali: Mahali Pakubwa pa Mafundisho ya Watchtower, huko Patterson, New York, États-Unis.
Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu na bibi zao ambao wamekuwa katika aina fulani ya utumishi wa pekee, ni kusema, wamisionere ambao hawajahuzuria masomo hayo, mapainia wa pekee, waangalizi wanaosafiri, ao Wanabeteli. Wote wawili, ni kusema bwana na bibi, wanapaswa kuwa katika utumishi wa pekee pamoja kwa miaka mitatu hivi ao zaidi bila kukatiza. Wanapaswa kujua kusema, kusoma na kuandika Kiingereza vizuri.
Jinsi ya Kujiandikisha: Biro ya Tawi inaweza kuwaomba wenzi wa ndoa wajaze ombi.
Ndugu Lade na bibi yake Monique walitoka États-Unis na sasa wanatumikia Afrika. Ndugu Lade anasema hivi: “Masomo ya Gileadi yalitutayarisha kuenda mahali popote duniani, sasa tuko tayari kutumika pamoja na ndugu zetu wapendwa.”
Monique anaongezea hivi: “Ninapata furaha kubwa ninapotumia mambo ambayo nimejifunza katika Neno la Mungu. Furaha hiyo inaonyesha kama Yehova anatupenda.”
Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na Bibi Zao
Kusudi: Kusaidia ndugu wanaotumikia katika Halmashauri ya Tawi wasimamie vizuri makao ya Beteli, washugulikie makutaniko, na kazi inayofanywa na waangalizi wa muzunguko na wa wilaya. Wanajifunza pia kuhusu kazi ya kutafsiri, kuchapisha, na kusafirisha vitabu.
Muda: Miezi miwili.
Mahali: Mahali pa kubwa pa Mafundisho ya Watchtower, huko Patterson, New York, États-Unis.
Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu wanaotumika katika Halmashauri ya Tawi ao Halmashauri ya Inchi ao wengine wanaoweza kupewa migawo hiyo kisha kuhuzuria masomo hayo.
Jinsi ya Kujiandikisha: Baraza Linaloongoza linaalika ndugu hao na bibi zao.
Ndugu Lowell na bibi yake Cara, walihuzuria somo la 25, na sasa wanatumika katika Nigeria. Ndugu Lowell anasema hivi: “Nilikumbushwa kama hata kazi yangu iwe nyingi namna gani ao hata kazi yangu iwe ya namna gani, jambo la maana ni kufanya mambo jinsi Yehova anavyotaka ili kumupendeza. Masomo yalionyesha kama ni jambo la maana tuige upendo ambao Yehova anawaonyesha watumishi wake.”
Dada Cara aliongezea hivi: “Nimefikiria shauri hili: Ikiwa siweze kufasiria jambo fulani kwa urahisi, ni lazima nijifunze kwanza habari hiyo mbele ya kuifundisha wengine.”