Maelezo ya Chini
a Wachunguzi fulani wanasema kwamba ndugu za Yosefu waliona zawadi ambayo baba yao alimupatia Yosefu kuwa uhakika wa kwamba alitaka kumupatia kijana huyo haki ya muzaliwa wa kwanza. Walijua kwamba Yosefu alikuwa mutoto wa kwanza ambaye Yakobo alizaa na bibi aliyekuwa anapenda sana—bibi ambaye alipanga kuoa mbele. Zaidi ya hayo, Reubeni, mutoto wa kwanza wa Yakobo alilala na kijakazi aliyekuwa bibi wa baba yake, kwa kufanya hivyo alikosa heshima kwa baba yake na alipoteza haki yake ya muzaliwa wa kwanza.—Mwanzo 35:22; 49:3, 4.