Maelezo ya Chini
b Sara alikuwa dada-nusu ya Abrahamu. Tera alikuwa baba yao wote wawili, lakini walikuwa na mama tofauti. (Mwanzo 20:12) Hata kama leo ni mubaya kufunga ndoa kama hiyo, ni jambo la maana kujua kwamba mambo yalikuwa tofauti wakati huo. Wanadamu walikuwa karibu na ukamilifu wenye Adamu na Eva walipoteza. Kwa watu hao wenye afya nzuri, ndoa kati ya watu wa jamaa ya karibu haikuwa na hatari yoyote juu ya watoto wenye walizaliwa. Lakini, miaka 400 kisha, urefu wa maisha ulikuwa kama wetu. Wakati huo sasa, Sheria ya Musa ilikataza ngono kati ya watu wa jamaa ya karibu sana.—Mambo ya Walawi 18:6.