Maelezo ya Chini
a Mukristo anaweza kuamua kuwa na silaha ya kutumia risasi (kama vile bunduki) ili kuwinda wanyama kwa ajili ya chakula ao kujilinda kutokana na wanyama wa pori. Lakini, wakati haitumiwe, bunduki hiyo inawekwa bila kuwa na risasi ndani, pengine hata sehemu zake mbalimbali zinaachanishwa, na kuwekwa muzuri nafasi yenye kuwa salama. Mahali kwenye sheria inakataza kuwa na bunduki, ao inatoa muongozo fulani juu ya kutumia bunduki, Wakristo wanapaswa kutii sheria hiyo.—Rom. 13:1.