-
Kuwa na Tumaini Kunasaidiaka Kabisa?Amuka!—2004 | Mwezi wa 4 22
-
-
Kuwa na Tumaini Kunasaidiaka Kabisa?
DANIEL alikuwa na miaka 11 tu. Lakini, alikuwa amefanya mwaka moja na ugonjwa wa kansere. Wanganga wake, watu wa familia yake, na marafiki wake hawakukuwa tena na tumaini. Lakini, Daniel yeye aliendelea kuwa na tumaini. Aliamini kama wakati atakomala, atasaidia kutafuta dawa ya kansere. Munganga fulani mwenye alikuwa anajua kutunza kansere yenye Daniel alikuwa anagonjwa, alipaswa kuya kumuona. Na ile ilifanya Daniel aendelee kuwa na tumaini. Lakini, siku yenye ule munganga alipaswa kuya, hali ya hewa haikukuwa muzuri. Kwa hiyo, haikuwezekana tena akuje. Daniel alivunjika moyo sana. Kwa mara ya kwanza, alipoteza tumaini. Na kisha siku kidogo, akakufa.
Habari ya Daniel ilizungumuziwa na munganga fulani mwenye alijifunza namna kuwa na tumaini na kukosa tumaini kunaweza kuwa na matokeo juu ya afya. Pengine na weye ulishakasikia habari ya vile. Kwa mufano, mutu fulani mwenye kuzeeka anakaribia kufa. Lakini anangoya kwa hamu jambo fulani ya maana. Pengine anangoya kutembelewa na mutu fulani mwenye anapenda sana ao sikukuu fulani. Kisha ile jambo yenye alikuwa anachunga sana kufika, hakawiake kufa. Juu ya nini inakuwaka vile? Kweli kuwa na tumaini kunasaidiaka sawa vile watu fulani wanaamini?
Watu wengi wenye kujifunza mambo ya kinganga wanasema kama kutazamia kama mambo itakuwa muzuri na kuwa na tumaini kunaweza kusaidia maisha yetu na afya yetu ikuwe muzuri zaidi. Lakini wengine wanakatala ile mawazo. Wamoja wanasema kama hakuna ushuhuda wenye unaonyesha kabisa kama kuwa na tumaini kunasaidiaka. Wao wanaamini kama kuwa na tumaini hakuwezi kusaidia mugonjwa ajisikie muzuri zaidi.
Haiko leo njo ile mawazo ilianza. Hata zamani watu fulani hawakuamini kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia. Zamani sana, wakati watu waliulizaka Aristote, filozofe Mugiriki, afasirie tumaini, alijibiaka hivi: “Ni kuota ndoto na uko unatembea.” Na hakuyapita miaka mingi, Benjamin Franklin, mwenye alikuwa anafanya mambo ya politike mu inchi ya Amerika, alisema hivi: “Mwenye anaishi juu ya tumaini atakufa na njala.”
Sasa, tuseme nini juu ya tumaini? Ni ndoto tu ya kutusaidia tujisikie muzuri? Ao tuko na sababu kabisa za kuamini kama kuwa na tumaini kunaweza kutusaidia tukuwe na furaha na tukuwe na afya ya muzuri?
-
-
Juu ya Nini Ni Muzuri Kuwa na TumainiAmuka!—2004 | Mwezi wa 4 22
-
-
Juu ya Nini Ni Muzuri Kuwa na Tumaini
MAMBO ingekuwa namna gani kama Daniel, ule kijana mwenye alikuwa na kansere mwenye tulizungumuzia ku mwanzo ya habari yenye ilitangulia, angeendelea kuwa na tumaini yenye nguvu? Angepona? Angekuwa muzima leo? Inawezekana hata watu wenye wanaamini kabisa kama tumaini inaweza kusaidia hawawezi kusema vile. Na ile inaonyesha hii jambo ya maana yenye tunapaswa kukumbuka: Hatupaswe kuwaza kama tumaini ni dawa ya kila kitu.
Wakati munganga Nathan Cherney alikuwa anaulizwa maulizo na watangazaji wa habari wa CBS, alionyesha kama ni mubaya kuambia watu wenye wanagonjwa sana kama watasikia muzuri ikiwa wako na tumaini. Alisema hivi: “Tumejionea bwana wenye wanalaumu bibi zao kwa kuwaambia kama hawako najikaza kuamini kama watapona na kutumaini kama mambo itakuwa muzuri.” Munganga Cherney aliongeza hivi: “Ile namna ya kufikiri imefanya watu wakuwe na mawazo yenye haiko ya kweli. Wanawaza kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia kansere isiendelee. Na kama inaendelea, ni kusema mutu hakujikaza kuwa na tumaini. Lakini, ile haiko kweli.”
Kusema kweli, mambo haikuwake mwepesi kwa wale wenye wako na ugonjwa wenye unakaribia kuwaua. Watu wa familia yao na marafiki wao hawawezi kupenda hata kidogo kuwaongezea magumu kwa kufanya wawaze kama ikiwa hawapone ni juu hawako najikaza kuwa na tumaini. Ni kusema hakuna faida ya kuwa na tumaini?
Haiko vile, kuko faida. Kwa mufano, kuliko kutunza ugonjwa ao kujaribu kurefusha maisha ya wagonjwa, uleule munganga anasaidiaka watu wenye wako na magonjwa yenye haiwezi kupona juu waishi siku za mwisho-mwisho za maisha yao bila maumivu kadiri inawezekana. Wanganga wenye wanatunzaka watu vile wanaamini kama kusaidia mutu atazamie kama mambo itakuwa muzuri kuko na faida sana hata kwa watu wenye wanagonjwa sana. Kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia sana wagonjwa.
Faida ya Kuwa na Tumaini
Munganga Gifford-Jones anasema hivi: “Tumaini ni dawa ya nguvu sana.” Alijifunza uchunguzi mbalimbali wenye watu walifanya kuhusu faida ya kutia moyo wagonjwa wenye wanakaribia kufa. Watu wengi wanawaza kama kufanya vile kunasaidia wagonjwa wakuwe na tumaini zaidi na watazamie kama mambo itakuwa muzuri. Uchunguzi fulani wenye ulifanywa mu 1989 ulionyesha kama watu wenye walikuwa wanatiwa moyo waliishi wakati murefu zaidi. Lakini uchunguzi mbalimbali wenye ulifanywa kisha pale haukuonyesha vile. Hata vile, uchunguzi mbalimbali umeonyesha kama wagonjwa wenye wanatiwa moyo hawakuwake na huzuni ya kupita kiasi na hawasikiake maumivu sana sawa wagonjwa wenye hawatiwe moyo.
Fikiria uchunguzi mwingine wenye ulifanywa juu ya kutafuta kujua ikiwa kuwa na tumaini ao kukosa tumaini kunaweza kufanya mutu apate ugonjwa wa mishipa ya moyo ao hapana. Wanaume 1 300 walichunguzwa kwa uangalifu juu ya kuona ikiwa walikuwa na tumaini ao hapana. Kisha miaka 10, wanaume 160 kati ya wale wanaume walikuwa wamepata aina fulani ya ugonjwa wa mishipa ya moyo. Wengi kati ya wale wanaume 160 walikuwa wale wenye hawakukuwa na tumaini. Laura Kubzansky, mwenye anafundishaka ku masomo fulani ya kinganga, anasema hivi kuhusu ule uchunguzi: “Mupaka sasa hakukuwa ushuhuda wenye kuonyesha wazi kabisa kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia afya. Huu ni ushuhuda wa kwanza wa kinganga wenye unaonyesha kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia moyo.”
Uchunguzi fulani umeonyesha kama wale wenye wanaonaka kama afya yao haiko muzuri, hawaponake mbio kisha kufanyiwa upasuaji (opération) kwa kulinganisha na wale wenye wanaonaka kama wako na afya ya muzuri. Hata ushuhuda umeonyesha kama wale wenye wako na tumaini wanakuwaka wanaishi siku mingi. Watu fulani wenye kufanya uchunguzi walitafuta kujua kama mambo inakuwaka namna gani wakati muzee iko na mawazo ya muzuri ao ya mubaya juu ya uzee. Wakati wazee walionyeshwa habari zenye zilisema kama watu wenye kuzeeka wako na hekima na uzoefu, wale wazee walitembea na nguvu zaidi. Faida yenye walipata ilikuwa sawa vile faida yenye wangepata kisha kufanya mazoezi mu majuma 12!
Juu ya nini inaonekana kama kuwa na tumaini na kutazamia kama mambo itakuwa muzuri kunaweza kusaidia afya? Inaonekana kama watu wenye kujifunza sayansi na wanganga hawawezi kujibia muzuri ile ulizo juu hawayaelewa muzuri kabisa namna akili na mwili wa mwanadamu vinafanya kazi. Lakini, wale wenye kujifunza ile mambo wanaweza kutoa mawazo fulani. Kwa mufano, mutu mumoja mwenye kujifunza ubongo anasema hivi: “Mutu anajisikiaka muzuri kama iko na furaha na tumaini. Wakati mutu iko na furaha, hakuwake na mahangaiko mingi, na ile inamusaidia akuwe na afya ya muzuri. Ile ni kati ya mambo yenye watu wanaweza kujitafutia juu waendelee kuwa na afya ya muzuri.”
Wanganga, watu wenye kujifunza saikolojia, na watu wenye kujifunza sayansi wanaweza kuona kama ile ni mawazo ya mupya. Lakini, haiko ya mupya kwa watu wenye kujifunza Biblia. Miaka 3 000 yenye imepita, roho ya Mungu iliongoza Mufalme Sulemani aandike hivi: “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri, lakini roho yenye kupondwa inamaliza mutu nguvu.” (Mezali 17:22) Maneno ya ile andiko iko na usawaziko. Haiseme kama moyo wenye furaha unaponyeshaka magonjwa yote, lakini inasema tu kama moyo wenye furaha “ni dawa ya muzuri.”
Na kusema kweli, kama tumaini ingekuwa dawa ya magonjwa yote, wanganga wote wangeiandikia wagonjwa wao. Kuwa na tumaini hakusaidiake tu afya, lakini kuko na faida zingine za mingi.
Kuwa na Tumani na Kukosa Tumaini Kunaweza Kuwa na Matokeo Gani Juu ya Maisha Yako?
Watu wenye kufanya uchunguzi wametambua kama watu wenye kuwa na tumaini wanapataka faida mingi. Wanawezaka ku masomo, wanatumikaka muzuri, na wanafanyaka muzuri mu mambo ya michezo. Kwa mufano, uchunguzi ulifanywa mu kikundi ya wanamuke wenye kufanya michezo ya kukimbia. Wenye kuwazoeza walichunguza kwa uangalifu mambo yenye kila mwanamuke iko na uwezo wa kufanya wakati wa mashindano. Wale wanamuke pia waliulizwa maulizo juu ya kuona ni kwa kadiri gani walikuwa na tumaini. Ku mwisho, ilionekana kama mambo yenye wale wanamuke walitumaini kama wanaweza kutimiza njo ilionyesha kabisa uwezo wenye walikuwa nao kuliko vile wale wenye kuwazoeza waliwaza. Juu ya nini tumaini iko na nguvu vile?
Watu wenye kujifunza mambo ya sayansi wamejifunza mambo ingine ya mingi kwa kuchunguza watu wenye kukosa tumaini. Zaidi ya miaka 50 yenye imepita, watu wenye kujifunza mambo ya sayansi walivumbula kama wanyama na hata wanadamu wanaweza kujifunza kuishi bila tumaini. Kwa mufano, walitia watu mu chumba yenye iko na fujo na kuwaambia kama wanaweza kunyamazisha ile fujo kwa kuponda boutons mbalimbali. Na waliweza kunyamazisha ile fujo.
Kisha waliambia kikundi ya pili wafanye pia vile, lakini fujo haikuisha kisha kuponda zile boutons. Vile unaweza kuwazia, wengi kati ya wale wa kikundi ya pili walipoteza tumaini. Wakati waliambiwa wafanye tena vile, hawakupenda kupima tena. Walikuwa wamejiambia kama hata wafanye nini mambo haitabadilika. Lakini, hata mu ile kikundi ya pili, wale wenye walitazamia kama mambo itakuwa muzuri, hawakupoteza tumaini.
Martin Seligman, mwalimu wa saikolojia, alisaidiaka kufanya uchunguzi fulani kati ya zile uchunguzi. Kwa hiyo aliamua kuendelea kujifunza juu ya matokeo ya kuwa na tumaini na kukosa tumaini. Alijifunza mawazo ya watu wenye wanazoeaka kujiona kuwa wa bure. Alivumbula kama ile mawazo inazuiaka watu kutimiza mambo mingi mu maisha, na hata inawafanya wasipime kutimiza jambo yoyote. Seligman alifasiriaka hivi matokeo ya kukosa tumaini: “Nimejifunza matokeo ya kukosa tumaini kwa miaka 25. Nimejifunza juu ya watu wenye hawana tumaini wenye wanaamini kuwa ni kosa yao kama mambo ya mubaya iko nawafikia, na kama ile mambo itaendelea kuwapata hata wafanye nini. Niko hakika kama juu wako na ile mawazo, mambo ya mingi ya mubaya itawapata kuliko wale wenye wako na tumaini.”
Kama vile tuliona, leo wengine wanaweza kuona ile mawazo kuwa ya mupya, lakini haiko ya mupya kwa wale wenye kujifunza Biblia. Mezali moja inasema hivi: “Kama unavunjika moyo siku ya taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.” (Mezali 24:10) Kwa kweli, Biblia inafasiria waziwazi kama kuvunjika moyo na kukosa tumaini kunaweza kufanya mutu akose nguvu ya kutenda. Sasa, unaweza kufanya nini juu usikuwe mutu wa kukosa tumaini lakini ukuwe mutu mwenye anatazamia kama mambo itakuwa muzuri na mwenye iko na tumaini mu maisha?
[Picha]
Kuwa na tumaini kunaweza kusaidia sana
-
-
Unaweza Kuachana na Mawazo ya Kukosa TumainiAmuka!—2004 | Mwezi wa 4 22
-
-
Unaweza Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini
UNAFANYAKA nini wakati unapata magumu? Watu wengi wenye elimu wanaamini kama namna unatendaka wakati unapata magumu njo inaonyesha kama uko na tumaini ao hapana. Siye wote tunapataka magumu mu maisha, wamoja wanapataka magumu mingi kuliko wengine. Sasa, juu ya nini watu fulani wenye wanapata magumu ya kidogo wanavunjikaka moyo na kuacha kujikaza, lakini wengine wanapataka tena nguvu na kujikaza kuendelea na maisha hata kama walipata magumu ya nguvu sana?
Kwa mufano, tuseme uko unatafuta kazi. Unaenda kuzungumuza na mukubwa wa kazi lakini hakupatie kazi. Kisha pale, utajisikia namna gani? Unaweza kuwaza kama ni kosa yako, na kama hakuna mutu mwenye atakupatiaka kazi. Ao, jambo ya mubaya zaidi, unaweza kuwaza kama, vile tu haukupata ile kazi, maana yake hauko mutu wa maana na hakuna mutu mwenye anaweza kuwa na lazima yako. Kuwaza vile ni alama ya kukosa tumaini.
Namna ya Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini
Unaweza kufanya nini juu upiganishe mawazo ya kukosa tumaini? Kwanza, ni muzuri ujikaze kutambua mawazo ya kukosa tumaini yenye uko nayo. Kisha uipiganishe. Ujikaze kuelewa ni juu ya nini haukupata kazi. Kwa mufano, ni kweli kama haukupata kazi juu hakuna mutu mwenye anakufurahia? Ao ni juu tu mukubwa wa kazi alikuwa anatafuta mutu mwenye iko na uwezo tofauti na wako?
Kama unachunguza mambo muzuri, utaona kama mawazo ya kukosa tumaini yenye uko nayo, haina musingi. Juu jambo moja tu inashindikana, ni kusema hauwezi kuweza kitu? Hakuna mambo ingine yenye iko inaendeka muzuri kwa kadiri fulani mu maisha yako, sawa vile urafiki wako na Mungu, hali ya familia yako, na urafiki wako na watu wengine? Ujikaze juu usikuwe unawaza kama kila kitu yenye unafanya itashindikana. Tuseme tu kweli, unaweza kabisa kujua kama hautapataka kazi? Kuko mambo ingine yenye unaweza kufanya juu upiganishe mawazo ya kukosa tumaini.
Uamini Kama Unaweza Kutimiza Mipango Yako
Mu miaka yenye imepita, watu wenye kufanya uchunguzi wamefasiria muzuri maana ya kuwa na tumaini. Lakini, ile mafasirio haineze kabisa maana yote ya kuwa na tumaini. Wanasema kama kuwa na tumaini ni kuamini kama utaweza kutimiza mipango yako. Kama vile tutaona mu habari yenye kufuata, maana ya kuwa na tumaini haiishie pale. Lakini, ile mafasirio inaweza kusaidia mu njia mingi. Inaweza kutusaidia tuamini kama tunaweza kutimiza mipango yetu.
Kusudi tuamini kama tunaweza kutimiza mipango yetu, ni muzuri tuanze na mipango ya kidogo-kidogo. Wakati tunaitimiza, tutaamini kabisa kama tunaweza kutimiza mipango ingine ya mukubwa. Kama unaona kuwa hauyatimiza mupango hata moja, pengine ni muzuri ufikirie mipango yenye unajiwekea. Uko kwanza na mipango? Juu tuko na mambo mingi ya kufanya, ni mwepesi kusahau kupanga mambo yenye tunapenda kabisa kufanya mu maisha. Kuhusu kupanga mambo, Biblia inatushauria hivi: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”—Wafilipi 1:10.
Wakati tunajua mambo ya maana mu maisha yetu, inakuwa mwepesi kupanga mambo yenye tunapenda kufanya mu sehemu mbalimbali za maisha, sawa vile mu urafiki wetu pamoja na Mungu, mu familia yetu, na mu mambo ingine. Lakini, ni muzuri tusijipangie mambo mingi ya kufanya, na ni muzuri tujipangie mambo yenye haitakuwa nguvu kutimiza. Juu kama tunajipangia mambo yenye iko nguvu kutimiza, tunaweza kuvunjika moyo na kuacha kujikaza. Njo maana, kama kuko jambo fulani kubwa yenye tunapenda kutimiza, inakuwaka muzuri kuigawanya mu mambo ya kidogo-kidogo yenye tunaweza kutimiza mu wakati kidogo-kidogo.
Kama mutu anapenda kabisa kufanya jambo fulani, anaweza kuitimiza. Ni kusema, kama tulishapanga kufanya mambo fulani, tunapaswa kuwa na nia ya kujikaza kuitimiza. Juu tukuwe na nia kabisa ya kutimiza ile mambo ni muzuri tufikirie faida zenye tutapata kama tunaitimiza. Kusema kweli, kutakuwa matatizo fulani yenye itafanya ikuwe nguvu kutimiza mipango yetu, lakini tusiache ile matatizo ituvunje moyo na kufanya tuache kujikaza.
Zaidi ya ile, tunapaswa kufikiria mambo yenye tunapaswa kufanya juu tutimize mipango yetu. Rick Snyder, muandikaji mwenye amejifunza sana juu ya faida ya kuwa na tumaini, anasema kama ni muzuri kufikiria njia mbalimbali za kutimiza mupango fulani. Juu kama njia moja haiendeke muzuri, tunaweza kutumia njia ya pili, ya tatu, na kuendelea.
Snyder anasema pia kama wakati fulani inakuwaka muzuri kubadilisha mipango yetu. Kama tumeshindwa kutimiza mupango fulani, kuendelea kujihangaisha juu ya ule mupango kutatuvunja tu moyo. Lakini, kama tunaachana na ule mupango na tunajiwekea mupango mwingine wenye tunaweza kutimiza, tunaweza kuwa tena na tumaini.
Kuhusu kubadilisha mipango yetu, Biblia iko na mufano wenye unaweza kutusaidia. Mufalme Daudi alipanga kujenga hekalu kwa ajili ya Yehova, Mungu wake. Lakini, Mungu aliambia Daudi kama mwana wake Sulemani njo atafanya ile kazi. Kuliko kuvunjika moyo na kutafuta tu kuijenga, Daudi alibadilisha mipango yake. Alitumikisha nguvu yake juu ya kukusanya feza na vitu vyenye Sulemani angetumikisha mu ile kazi.—1 Wafalme 8:17-19; 1 Mambo ya Nyakati 29:3-7.
Hata kama tulishajikaza kupiganisha mawazo ya kukosa tumaini na tumekuwa watu wenye kutazamia kama mambo itakuwa muzuri, wakati fulani tunaweza kukosa tumaini. Juu ya nini? Juu hatuna uwezo wa kumaliza mambo mingi yenye inafanyaka watu wakose tumaini mu hii dunia. Inawezekana kabisa kuwa na tumaini wakati tunafikiria mambo mingi yenye iko inatesa wanadamu leo, sawa vile umaskini, vita, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo?
[Picha]
Wakati hawakupatie kazi yenye ulikuwa unatafuta, unawaza mara moja kama hautapataka kazi?
[Picha
Mufalme Daudi alikuwa tayari kubadilisha mipango yake
-
-
Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya KweliAmuka!—2004 | Mwezi wa 4 22
-
-
Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya Kweli
Saa yako imesimama na inaonekana imeharibika. Unapenda fundi airekebishe lakini haujue, ni fundi gani njo atairekebisha. Watu wengi wanasema kama wanaweza kurekebisha saa lakini mawazo yao inapingana. Kisha unavumbula kama jirani yako njo alitengenezaka ile saa na anakuambia kama atakusaidia kuirekebisha bila kukuomba feza. Ni wazi kama yeye njo utachagua.
Sasa linganisha ile saa na uwezo wako wa kuwa na tumaini. Kama unatambua kama unaanza kupoteza tumaini, sawa watu wengi leo mu hii wakati wa magumu, wapi njo utatafutia musaada? Watu wengi wanasema kama wanaweza kukusaidia lakini mawazo yao inavuruga akili na inapingana. Hauone kama ni muzuri utafute ule mwenye alipatiaka wanadamu uwezo wa kuwa na tumaini? Biblia inasema kama Mungu “haiko mbali sana na kila mumoja wetu” na iko tayari kutusaidia.—Matendo 17:27; 1 Petro 5:7.
Kuwa na Tumaini Kunamaanisha Nini Kabisa?
Biblia inafasiria muzuri zaidi maana ya kuwa na tumaini kuliko vile wanganga, watu wenye kujifunza sayansi, na watu wenye kujifunza saikolojia wanaifasiria. Mu Biblia, maneno ya luga ya kwanza-kwanza yenye inatafsiriwa “tumaini” iko na maana ya kungoya kwa hamu na kutazamia mambo ya muzuri. Ni kusema tumaini inafanyizwa na mambo mbili. Kwanza, ni kutamani mambo ya muzuri ifanyike. Na pili, ni kuwa na sababu ya kuamini kama ile mambo itafanyika. Tumaini yenye Biblia inatupatia, haiko ndoto. Inategemea mambo yenye iko hakika.
Kwa hiyo, tumaini iko sawa vile imani, juu imani nayo inategemea mambo yenye iko hakika, hapana mambo ya kuwazia-wazia tu. (Waebrania 11:1) Hata vile, Biblia inaonyesha kama kuko fofauti fulani kati ya imani na tumaini.—1 Wakorinto 13:13.
Juu uelewe, fikiria hii mufano: Wakati unaomba rafiki yako akufanyie jambo fulani unaweza kutumainia kama atakusaidia. Uko na sababu ya kumutumainia juu unamuaminia. Na kama unamuaminia, ni juu unamujua muzuri na alishakakusaidia zamani. Kuko upatano kati ya imani na tumaini, na zile sifa zinaendaka pamoja hata kama ziko tofauti. Inawezekana umutumainie Mungu naye vile?
Sababu za Kuwa na Tumaini
Mungu njo anapatiaka watu tumaini ya kweli. Zamani, Biblia ilimuita Yehova kuwa “tumaini la Israeli.” (Yeremia 14:8) Tumaini yoyote ya kweli yenye watu wake walikuwa nayo ilitoka kwake, ni mu ile maana njo alikuwa tumaini la Israeli. Ile tumaini haikukuwa ndoto tu. Mungu aliwapatia sababu za kuwa na tumaini. Kwa miaka mingi, alikuwa anawaahidi mambo mbalimbali na alikuwa anaitimiza. Yoshua, kiongozi wao, aliwaambia hivi: “Munajua muzuri . . . kwamba hakuna hata neno moja lenye halikutimia kati ya ahadi zote za muzuri zenye Yehova Mungu wenu aliwaahidi.”—Yoshua 23:14.
Hata leo, Yehova angali anatimiza ahadi zake. Biblia iko na ahadi za muzuri zenye Mungu alitoaka na inaonyesha waziwazi namna zilitimiaka. Ahadi za Mungu ni za kweli kabisa kiasi ya kwamba, wakati fulani, wenye waliziandika walitumia maneno yenye ilifanya zionekane kama zilishatimia.
Njo maana, tunaweza kusema kama Biblia ni kitabu yenye inatoa tumaini. Wakati utaendelea kujifunza namna Mungu alikuwa anatendea watu, utapata sababu za mingi za kumutumainia. Mutume Paulo aliandika hivi: “Mambo yote yenye yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.”—Waroma 15:4.
Mungu Anatupatia Tumaini Gani?
Ni wakati gani njo tunakuwaka na lazima kabisa ya tumaini? Zaidi sana wakati mutu mwenye tunapenda anakufa. Lakini, ni ile wakati tena njo watu wengi wanapotezaka tumaini. Kusema kweli, kifo inafanyaka mutu aishiwe kabisa. Kifo inaweza kutufikia saa ni saa. Hakuna mutu mwenye anaweza kuepuka kifo, na hatuwezi kurudishia uzima mupendwa wetu. Njo maana, Biblia iko na sababu kabisa ya kuita kifo “adui wa mwisho.”—1 Wakorinto 15:26.
Sasa, kuko tumaini kwa ajili ya wale wenye wamekufa? Ile andiko ya Biblia yenye inaita kifo kuwa adui, inasema tena kama ule adui “ataharibiwa.” Yehova Mungu iko na nguvu kuliko kifo. Na ameonyesha vile mara mingi. Namna gani? Kwa kufufua wafu. Biblia inazungumuzia watu kenda wenye Mungu alifufua kwa kutumia nguvu yake.
Kwa mufano, Yehova alipatia Yesu, Mwana wake, nguvu ya kufufua rafiki yake mupendwa, Lazaro, mwenye alikuwa alishafanya siku ine mu kaburi. Yesu hakufanya vile kwa uficho, lakini mbele ya watu wengi.—Yohana 11:38-48, 53; 12:9, 10.
Unaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini sasa Mungu alifufuaka wale watu? Si walizeekaka tena na wakakufa!’ Ni kweli walizeekaka tena na wakakufa. Lakini, zile habari za ufufuo zinatufanya tutamani kuona tena wapendwa wetu na zinatupatia sababu ya kuamini kama kuko siku wataishi tena. Ni kusema, tuko na tumaini ya kweli kabisa.
Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” (Yohana 11:25) Yeye njo Yehova atapatia nguvu ya kufufua watu mu dunia yote. Yesu alisema tena hivi: “Saa inakuja yenye wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti [ya Kristo] na watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Kwa kweli, wale wote wenye kuwa mu kaburi wako na tumaini ya kufufuliwa na kuishi mu dunia paradiso.
Nabii Isaya alizungumuzia ufufuo kwa kutumia hii maneno yenye kufurahisha: “Wafu wako wataishi. Maiti wangu wataamuka. Muamuke na mupige vigelegele vya shangwe, ninyi wenye kukaa katika mavumbi! Kwa maana umande wako ni kama umande wa asubui, na dunia itaacha wale wenye hawana uwezo katika kifo ili waishi tena.”—Isaya 26:19.
Ile maneno inatia moyo kabisa. Wafu wako mu hali yenye kuwa salama kabisa, sawa vile mutoto anakuwaka salama mu tumbo ya mama yake. Tunasema vile juu Yehova anakumbuka muzuri watu wote wenye wamekufa. (Luka 20:37, 38) Na hivi karibuni watafufuliwa na kukaribishwa kwa furaha mu dunia, sawa vile familia yenye upendo inakaribishaka mutoto mwenye anazaliwa! Kwa hiyo, kuko tumaini hata kwa ajili ya wapendwa wetu wenye wamekufa.
Utapata Faida Gani Kama Unakuwa na Tumaini?
Paulo anatufundisha mambo mingi juu ya faida ya kuwa na tumaini. Alisema kama tumaini ni sehemu ya maana ya silaha za kiroho, aliifananisha na kofia ya chuma. (1 Watesalonike 5:8) Juu ya nini? Zamani, wakati askari alikuwa anaenda ku vita, alikuwa anavala kofia ya chuma juu ya kofia ingine ya nguo ao ya ngozi. Ile kofia ilikuwa inalinda kichwa yake ili asiumie ao hata kufikia kufa ikiwa wanamutupia kitu fulani ku kichwa. Paulo alipenda kusema nini wakati alizungumuzia kofia ya chuma? Sawa vile tu kofia ya chuma inalinda kichwa, vilevile tumaini inalinda akili, ni kusema uwezo wetu wa kufikiri. Kama unatumainia kabisa ahadi za Mungu, utakuwa na amani ya akili ao utatulia hata wakati wa magumu. Nani njo atasema kama hana lazima ya ile kofia ya chuma?
Paulo alitumia mufano ingine juu ya kuonyesha faida ya kutumainia kabisa mapenzi ya Mungu. Aliandika hivi: “Tumaini hilo [liko] kama nanga ya nafsi, likiwa hakika na pia imara.” (Waebrania 6:19) Paulo alivunjikiwaka na mashua mara mingi, kwa hiyo, alijua faida ya kuwa na nanga mu mashua. Wakati mashua ilipigwa na upepo mukali, watu wenye kutumika mu mashua walikuwa wanashusha nanga. Nanga ilikuwa inasaidia mashua isitikisike-tikisike sana wakati wa upepo mukali na ilikuwa inaisaidia isiende kujigonga ku miamba.
Vilevile, kama tunaona ahadi za Mungu kuwa tumaini yenye kuwa “hakika na pia imara,” tutaweza kupiganisha magumu yenye inafanana na upepo mukali. Yehova anaahidi kama karibuni wanadamu hawatateseka tena kwa sababu ya vita, jeuri, huzuni, ao hata kifo. (Ona kisanduku “Sababu za Kuwa na Tumaini.”) Kama tunashikamana na ile tumaini, itatulinda, na itatusaidia tutii kanuni za Mungu mu maisha yetu na tutaepuka matendo ya mubaya yenye watu wengi wako nayo leo.
Tumaini yenye Yehova anatoa inaweza kukusaidia na weye. Anapenda ukuwe na maisha ya muzuri. Na anapenda “watu wa namna zote waokolewe.” Sasa, wanaweza kufanya nini juu waokolewe? Kwanza, kila mutu anapaswa ‘kupata ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.’ (1 Timoteo 2:4) Wachapishaji wa hii gazeti wanakutia moyo upate ujuzi juu ya kweli ya Neno ya Mungu. Ni ule ujuzi njo utakusaidia upate uzima wa milele. Tumaini yenye Mungu atakupatia inapita kabisa tumaini yoyote yenye unaweza kupata mu hii dunia.
Kama uko na ile tumaini, hautavunjika moyo, juu Mungu anaweza kukupatia nguvu ya kutimiza mipango yoyote yenye uko nayo kama tu inapatana na mapenzi yake. (2 Wakorinto 4:7; Wafilipi 4:13) Siye wote tuko na lazima ya ile tumaini. Kwa hiyo, kama na weye uko na lazima ya ile tumaini, na kama uko unaitafuta, ujue kama unaweza kuipata!
[Kisanduku]
Sababu za Kuwa na Tumaini
Hii mawazo yenye iko mu Maandiko inaweza kukusaidia ukuwe na tumaini kabisa:
◼ Mungu anasema kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya.
Biblia inasema kama dunia yote itakuwa paradiso na mutakuwa watu wenye furaha na umoja.—Zaburi 37:11, 29; Isaya 25:8; Ufunuo 21:3, 4
◼ Mungu hawezi kusema uongo.
Yehova anachukia kila namna ya uongo. Iko mutakatifu kabisa, ni kusema iko safi. Kwa hiyo, haiwezekane aseme uongo.—Mezali 6:16-19; Isaya 6:2, 3; Tito 1:2; Waebrania 6:18.
◼ Nguvu ya Mungu haina mipaka.
Yehova tu njo Mweza-Yote. Hakuna kitu mu ulimwengu yenye inaweza kumuzuia kutimiza mambo yenye amesema kama atafanya.—Kutoka 15:11; Isaya 40:25, 26.
◼ Mungu anapenda uishi milele.
—Yohana 3:16; 1 Timoteo 2:3, 4.
◼ Mungu anatutumainia.
Anaamua kukaza akili juu ya sifa zetu za muzuri na juu ya mambo yenye tuko najikaza kufanya, hapana juu ya makosa yetu na uzaifu wetu. (Zaburi 103:12-14; 130:3; Waebrania 6:10) Anatumainia kama tutafanya mambo ya muzuri na anafurahi wakati tunafanya vile.—Mezali 27:11.
◼ Mungu anatuambia kama atatusaidia tutimize mipango yetu kama inapatana na mapenzi yake.
Watumishi wake hawapaswe kuvunjika moyo. Iko tayari kuwapatia roho yake takatifu, ni kusema nguvu yake, juu ya kuwasaidia.—Wafilipi 4:13.
◼ Kumutumainia Mungu haiko kuchokea bure.
Unaweza kumutumainia kabisa, hawezi kukuvunja moyo.—Zaburi 25:3.
[Picha]
Sawa vile kofia ya chuma inalinda kichwa, vilevile tumaini inalinda akili
[Picha]
Sawa vile nanga, tumaini yenye kuwa hakika inaweza kutusaidia tutulie
[Picha imetolewa na]
Courtesy René Seindal/Su concessione del Museo Archeologico Regionale A. Salinas di Palermo
-