-
Tushangilie Katika Tumaini LetuMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 3 15
-
-
10, 11. (a) Kondoo wengine wana tumaini gani? (b) Namna gani kutimizwa kwa tumaini la kidunia kunahusiana na Kristo na kufunuliwa kwa “wana wa Mungu”?
10 Mutume Paulo aliandika kuhusu tumaini nzuri la “wana wa Mungu” waliozaliwa kwa roho ambao ni ‘wariti’ pamoja na Kristo. Kisha akazungumuzia tumaini lingine nzuri ajabu ambalo Yehova anatolea kondoo wengine: ‘Kwa maana uumbaji [wanadamu] unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu [watiwa-mafuta]. Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yeye aliyeutiisha hivyo, juu ya musingi wa tumaini kwamba uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.’—Rom. 8:14-21.
-
-
Tushangilie Katika Tumaini LetuMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 3 15
-
-
12. Kufunuliwa kwa watiwa-mafuta kutawafaidi wanadamu namna gani?
12 Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu moja utawafariji wanadamu kabisa! Wakati huo, “wana wa Mungu” waliotukuzwa ‘watafunuliwa’ katika njia nyingine. Wakiwa makuhani pamoja na Kristo, watatumika ili kusaidia wanadamu wafaidike na zabihu ya ukombozi wa Yesu. “Uumbaji,” yaani, wanadamu watakuwa raia wa Ufalme wa Mungu, wataanza kukombolewa kutoka katika matokeo ya zambi na kifo. Hatua kwa hatua wanadamu watiifu ‘watawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu.’ Ikiwa wanabaki waaminifu kwa Yehova wakati wa utawala wa Miaka Elfu moja na wakati wa jaribu la mwisho litakalotokea mwisho wa utawala huo, majina yao yatabaki yenye kuandikwa milele katika “kitabu cha uzima.” Wataingia katika “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ufu. 20:7, 8, 11, 12) Hilo ni tumaini nzuri kabisa!
-