-
Unabii wa Biblia Haukose KutimiaMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Unabii wa Biblia Haukose Kutimia
“Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi.”—YOSHUA 23:14.
SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Inajulikana sana kama mambo ambayo waaguzi walikuwa wakitabiri hayakuwa hakika na hayangeweza kutumainiwa, ni vilevile juu ya wale wanaotabiri leo matukio ya wakati ujao kwa kuangalia nyota (kama vile mambo ya horoscope). Elimu ya uchunguzi wa mambo yanayowezekana kufanyika wakati ujao kwa kutegemea muelekeo wa wakati wa sasa haiwezi kutabiri bila kukosea matukio fulani ya wakati ujao miaka mingi mbele yatukie. Lakini unabii mbalimbali wa Biblia unaonyesha mambo yote waziwazi na mambo hayo yanatimia kabisa, hata ikiwa unabii unasemea “kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.”—Isaya 46:10.
KWA MUFANO: Katika miaka ya 500 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, nabii Danieli alitabiri namna ufalme wa Wamedi na Waperse utakavyoangushwa na ufalme wa Ugiriki (Grèce). Tena, alitabiri kama mufalme wa Ugiriki ‘atakapokuwa mwenye nguvu,’ ufalme wake ‘ungevunjwa.’ Ni nani angechukua nafasi yake? Danieli aliandika hivi: ‘Kuna falme ine zitakazosimama kutoka katika taifa lake, lakini si kwa nguvu zake.’—Danieli 8:5-8, 20-22.
YALE WANAHISTORIA WANASEMA JUU YA JAMBO HILO: Miaka zaidi ya 200 kisha Danieli kutabiri hivyo, Alexandre le Grand akawa mufalme wa Ugiriki. Katika miaka kumi, Alexandre alishinda ufalme wa Wamedi na Waperse na akapanua ufalme wa Ugiriki mupaka Muto Indus (leo muto huo unapatikana katika Pakistan). Lakini alikufa kwa kushitukia akiwa na miaka 32. Mwishowe, ufalme wake ulivunjwa kabisa kutokana na vita iliyofanyika karibu na Ipsus huko Asia Ndogo. Wale majenerali ine walioshinda katika vita hiyo wakagawanya ufalme wa Ugiriki kati yao. Lakini kati yao hakuna aliyekuwa mwenye nguvu kama Alexandre.
UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine ambacho kilitabiri mambo na yakatokea hivyo bila kukosea? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 4]
Katika kitabu chake (A LAWYER EXAMINES THE BIBLE), IRWIN LINTON alisema hivi: “Unabii wa Biblia uliotimia ni mwingi sana, . . . hatuwezi kuwaza kama ingewezekana utimie kwa bahati tu.”
[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 4]
© Robert Harding Picture Library/SuperStock
-
-
Katika Biblia, Hamuna Hadisi za KutungaMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Katika Biblia, Hamuna Hadisi za Kutunga
“Nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi.”—LUKA 1:3.
SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Hadisi za kutunga tu ni habari zenye kupendeza ambazo hazionyeshe mahali kabisa na tarehe ambapo mambo yalitendeka, na hata majina ya watu wanaozungumuziwa ni ya kuwazia tu. Lakini, Biblia inaeleza waziwazi namna mambo yote yalivyotokea, na hilo linawahakikishia wasomaji kama Biblia inasema maneno ya kweli kabisa.—Zaburi 119:160.
KWA MUFANO: Biblia inasema kama ‘Nebukadneza mufalme wa Babiloni . . . alimupeleka Yehoyakini [Mufalme wa Yuda] uhamishoni Babiloni.’ Baadaye, ‘Evil-merodaki mufalme wa Babiloni, katika mwaka wa kuwa kwake mufalme, akakiinua kichwa cha Yehoyakini mufalme wa Yuda kutoka katika nyumba ya kifungo.’ Tena Biblia inasema kama Yehoyakini ‘alipewa posho daima kutoka kwa mufalme, kila siku kama inavyostahili, siku zote za maisha yake.’—2 Wafalme 24:11, 15; 25:27-30.
YALE WACHUNGUZI WA VITU VYA ZAMANI WAMEVUMBUA: Wachunguzi wa vitu vya zamani wamevumbua maandishi fulani ya serikali ao guvernema mahali palipokuwa muji wa Babiloni zamani. Maandishi hayo yaliandikwa tangu Mufalme Nebukadneza alipokuwa akitawala. Maandishi hayo yanazungumuzia kiasi cha chakula ambacho wafanyakazi na wafungwa wa vita walipewa. Yanazungumuzia pia “Yaukini [Yehoyakini],” aliyekuwa “mufalme wa inchi ya Yahud (Yuda),” na watu wa nyumba yake. Je, kuna kitu fulani kilichovumbuliwa ambacho kinaonyesha kama Evil-merodaki aliyetawala kisha Nebukadneza aliishi kweli? Ndiyo, chombo fulani cha udongo kilivumbuliwa karibu na muji wa Susa. Kwenye chombo hicho kuliandikiwa maneno haya: “Nyumba ya kifalme ya Amil-Marduk [Evil-merodaki], Mufalme wa Babiloni, mwana wa Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni.”
UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine kitakatifu kinachoeleza waziwazi na bila kudanganyika hata kidogo habari za historia? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 5]
Katika kitabu chake (A SCIENTIFIC INVESTIGATION OF THE OLD TESTAMENT), ROBERT WILSON aliandika hivi: “Mambo ambayo Biblia inasema juu ya wakati na mahali ambapo matukio fulani yalitendeka ni ya kweli kabisa na ni yenye kutumainika zaidi kuliko yale yaliyo katika vitabu vingine vyote vya zamani.”
[Picha katika ukurasa wa 5]
Maandishi ya Babiloni yaliyomutaja mufalme Yehoyakini wa Yuda
[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 5]
© bpk, Berlin/Vorderasiatisches Museum, SMB/Olaf M. Tessmer/Art Resource, NY
-
-
Biblia Inapatana Kabisa na Mambo ya Kweli ya SayansiMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Biblia Inapatana Kabisa na Mambo ya Kweli ya Sayansi
“Je, kufikia sasa sikukuandikia mashauri na ujuzi, nikuonyeshe ukweli wa maneno ya kweli, ili urudishe maneno yaliyo kweli?”—METHALI 22:20, 21.
SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Mara nyingi, vitabu vya zamani vina mawazo ya uongo na yenye kuhatarisha maisha ambayo yamekataliwa kabisa na sayansi leo. Hata leo, kwa sababu mambo mapya yanaendelea kuvumbuliwa, waandikaji wanalazimishwa kuandika vitabu vipya ili kurekebisha mawazo yaliyo katika vitabu vyao vya zamani. Lakini Biblia haina lazima ya kurekebishwa kwa sababu ilitoka kwa Muumbaji na Neno lake “linadumu milele.”—1 Petro 1:25.
KWA MUFANO: Sheria ya Musa iliwaamuru Waisraeli wazike mavi ‘inje ya kambi.’ (Kumbukumbu la Torati 23:12, 13) Ikiwa wangegusa mwili wa munyama aliyekufa ao maiti ya mutu, walipaswa kujisafisha na maji. (Mambo ya Walawi 11:27, 28; Hesabu 19:14-16) Tangu wakati huo, watu wenye ukoma walikuwa wakitengwa na watu wengine mupaka kuhani alipowaangalia na kuhakikisha kama hawawezi tena kuwaambukiza wengine.—Mambo ya Walawi 13:1-8.
YALE WAGANGA WANASEMA LEO: Leo waganga wanasema kama kuwa na choo ao W.C zinazofaa, kunawa mikono kila mara, na kutenga watu walio na magonjwa ya kuambukiza zingali njia nzuri za kugombanisha magonjwa. Vituo vya Kugombanisha Magonjwa huko Etats-Unis vinatoa mashauri haya: Ikiwa mutu hana W.C ni vizuri afanye choo kubwa kwenye umbali wa metre 30 kutoka mahali palipo na maji na kisha azike mavi yake. Na Shirika la Afya Duniani Pote (OMS) linaonyesha kama ikiwa watu wana choo ao W.C zinazofaa, wanapunguza magonjwa ya kuhara kwa kiasi cha 36%. Kumepita karibu miaka 200, waganga walivumbua kama walikuwa wakiambukiza watu wengi magonjwa kwa sababu hawakuwa wakinawa mikono yao kisha kugusa maiti. Vituo vya États-Unis vya Kugombanisha Magonjwa vinaonyesha kama kunawa mikono kila mara ingali “njia nzuri zaidi inayosaidia watu wasiambukizwe na magonjwa.” Waganga wanasema nini juu ya kutenga watu walio na ukoma ao magonjwa mengine ya kuambukiza? Hivi karibuni, gazeti moja (Saudi Medical Journal) lilisema hivi: “Ugonjwa wa kuambukiza unapoanza, njia moja tu iliyo nzuri zaidi ya kuugombanisha ni kutenga watu walio na ugonjwa huo.”
UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine kitakatifu cha zamani ambacho kina mawazo yenye kupatana na sayansi ya kisasa? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 6]
Kitabu kimoja (MANUAL OF TROPICAL MEDICINE) kilichoandikwa na Muganga ALDO CASTELLANI NA ALBERT CHALMERS kinasema hivi: “Kila mutu anavutiwa kabisa na maagizo juu ya usafi ili kujilinda; maagizo yanayoelezwa katika Sheria ya Musa.”
-
-
Vitabu Vyote vya Biblia VinapatanaMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Vitabu Vyote vya Biblia Vinapatana
“Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”—2 PETRO 1:21.
SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Mara nyingi vitabu vya zamani vinapingana, hata ikiwa viliandikwa wakati mumoja. Ni vigumu kabisa vitabu vipatane ikiwa viliandikwa na watu tofauti, mahali tofauti, wakati tofauti. Lakini, ijapokuwa Biblia iliandikwa na watu tofauti, vitabu vyote 66 vilivyo ndani vina ujumbe wenye kupatana kwa sababu Mutu aliyeiandikisha ni mumoja.—2 Timotheo 3:16.
KWA MUFANO: Katika kitabu cha kwanza cha Biblia, Musa, aliyekuwa muchungaji wa kondoo katika miaka ya 1 500 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, aliandika juu ya “uzao” ambao ungekuja kuokoa wanadamu. Baadaye, kitabu hicho kilitabiri kama uzao huo ungetokea katika kizazi cha Abrahamu, Isaka, na Yakobo. (Mwanzo 3:15; 22:17, 18; 26:24; 28:14) Miaka 500 hivi kisha hapo, nabii Nathani alionyesha kama uzao huo ungetokea katika kizazi cha mufalme Daudi. (2 Samweli 7:12) Miaka 1 000 baadaye, mutume Paulo alieleza kama uzao huo ungefanyizwa na Yesu na kikundi cha wafuasi wake waliochaguliwa. (Waroma 1:1-4; Wagalatia 3:16, 29) Mwishowe, katika mwaka wa 96 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mutume Yohana alitabiri katika kitabu cha mwisho cha Biblia kama wale wanaofanyiza uzao huo wangetoa ushahidi juu ya Yesu duniani, wangefufuliwa na kwenda mbinguni, na kutawala pamoja naye kwa miaka 1 000. Uzao huo unaoundwa na Yesu na wafuasi wake utamuharibu Shetani na kuokoa wanadamu.—Ufunuo 12:17; 20:6-10.
YALE WACHUNGUZI WA MAMBO YA BIBLIA WANASEMA: Kisha kujifunza kwa uangalifu vitabu 66 vya Biblia, Louis Gaussen aliandika katika kitabu chake (Théopneustie ou Inspiration Plénière des Saintes Écritures) kama alishangazwa sana na “upatano wenye kuvutia wa kitabu hicho, kilichoandikwa na watu wengi, . . . ambao yaonekana walikuwa na kusudi moja, hata ikiwa hawakuelewa kusudi hilo, waliendelea kulifuatilia, mupaka wakatimiza kusudi hilo kubwa, ni kusema, ukombozi wa ulimwengu kupitia Mwana wa Mungu.”
UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine kilichoandikwa na watu tofauti tofauti karibu 40 katika kipindi cha miaka zaidi ya 1 500 ambacho kina ujumbe wenye kupatana kabisa? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 7]
Katika kitabu chake (THE PROBLEM OF THE OLD TESTAMENT), JAMES ORR aliandika hivi: “Maandishi hayo yanapokusanywa pamoja, yanakuwa kitabu kimoja chenye kuundwa vizuri . . . Hakuna kitabu kingine duniani kinachoweza kujilinganisha kabisa na kitabu hicho, ao kinachokikaribia.”
-
-
Kanuni za Biblia Zingali Zenye Kufaa leoMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Kanuni za Biblia Zingali Zenye Kufaa leo
‘Neno lako ni taa ya muguu wangu, na nuru kwa barabara yangu.’—ZABURI 119:105.
SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Vitabu fulani vinaweza kuonwa kuwa vitabu vilivyoandikwa na watu waliosoma sana, lakini haviwasaidie watu katika maisha. Na vitabu vya leo vya mafundisho wanavisahihisha mara kwa mara. Lakini, Biblia inasema kama “mambo yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha.”—Waroma 15:4.
KWA MUFANO: Hata ikiwa Biblia si kitabu kinachofundisha mambo ya matunzo, ina mashauri yanayoweza kumusaidia mutu awe na afya nzuri na moyo mutulivu. Tuchukue mufano, Biblia inasema kama ‘moyo mutulivu ni uzima wa mwili.’ (Methali 14:30) Tena Biblia inasema kama ‘mutu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe; atashindana na hekima yote inayotumika.’ (Methali 18:1) Pia, inasema kama “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.
YALE WACHUNGUZI WANASEMA: Kuwa mutulivu, kuwa na marafiki wa kweli, na kuwa mukarimu kunaweza kufanya mutu awe na afya nzuri. Gazeti moja (The Journal of the American Medical Association) linasema hivi: “Watu wanaokasirika sana wana hatari mara mbili ya kupatwa na magonjwa ya ubongo yanayofanya sehemu fulani ya mwili ipooze, kuliko wale wanaozuia kasirani yao.” Uchunguzi fulani uliofanywa kwa muda wa miaka kumi huko Australie ulionyesha kama watu waliozeeka ambao walikuwa wakizungumuza na watu wengi kwenye Internete na ambao walikuwa pia na marafiki ambao walikuwa wakizungumuza nao mambo ya siri, wanaweza kuishi kwa muda murefu. Uchunguzi mwingine ulifanywa katika mwaka wa 2008 huko Canada na États-unis. Uchunguzi huo ulionyesha pia kama “mutu anayetumia feza zake ili kusaidia watu wengine ana furaha zaidi kuliko yule anayezitumia kwa ajili yake mwenyewe.”
UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kama unaweza kutumainia mashauri ya afya yaliyo katika kitabu kingine kilichoandikwa kumepita miaka karibu 2 000? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 8]
HOWARD KELLY, MUGANGA KWENYE MASOMO YA JUU YA KIGANGA (THE JOHNS HOPKINS UNIVERSITY) alisema hivi: “Biblia inanipendeza sana . . . kwa sababu ina mashauri mazuri ya kiganga.”
-