Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Maumivu ya Kufiwa
    Amuka!—2018 | No. 3
    • Mutu mwenye huzuni ya kufiwa anakaa peke yake ku meza mu restora

      MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

      Maumivu ya Kufiwa

      “Mimi na Sophiaa tulikuwa tumefanya miaka zaidi ya 39 mu ndoa wakati Sophia alikufa na ugonjwa wenye kukawia. Marafiki wangu walinisaidia sana, na niliendelea kuwa na mambo mengi ya kufanya. Lakini kwa mwaka wote muzima, nilisikia maumivu sana. Hisia zangu zilibadilika-badilika. Hata kama kumepita miaka tatu hivi tangu akufe, ningali nasikia maumivu makali, na mara nyingi inatokea kwa kushitukia.”​—Kostas.

      Je, umefiwa na mupendwa wako? Ikiwa ni vile, pengine unajisikia kama vile Kosta alijisikia. Hakuna jambo lenye kuhangaisha sana na kuumiza moyo kuliko kifo cha bibi ao bwana, mutu wa jamaa, ao rafiki mupendwa. Watu wenye kufanya uchunguzi kuhusu maumivu yenye kuletwa na kifo wanakubaliana na hilo. Habari moja yenye ilichapishwa mu gazeti The American Journal of Psychiatry inasema kama “wakati mupendwa anakufa, watu wengi wanajisikia kuwa wamemupoteza milele na wanapatwa na maumivu makali sana.” Wakati mutu iko mu maumivu makali kwa sababu ya kufiwa, anaweza kujiuliza: ‘Hali hii itaisha wakati gani? Nitakuwaka tena na furaha? Namna gani ninaweza kupata kitulizo?’

      Majibu ya maulizo hayo yatazungumuziwa mu gazeti hili la Amuka! Habari yenye kufuata itazungumuzia mambo yenye unaweza kutazamia ikiwa umefiwa hivi karibuni. Habari zingine zitazungumuzia njia mbalimbali zenye zinaweza kukusaidia kupunguza huzuni yako.

      Tunatumaini kabisa kuwa habari zenye kufuata zitatuliza na zitasaidia kabisa mutu yeyote mwenye kuwa na huzuni kwa sababu ya kufiwa.

      a Majina fulani katika habari hizi zenye kufuatana imebadilishwa.

  • Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia
    Amuka!—2018 | No. 3
    • Bibi na bwana wenye huzuni ya kufiwa

      MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

      Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia

      Hata kama wachunguzi wanasema kuwa mutu mwenye amefiwa anapaswa kupita mu hatua fulani za kuonyesha huzuni, kila mutu iko na namna yake ya pekee ya kuonyesha huzuni. Je, tofauti hizo zinamaanisha kama watu fulani wanahuzunika kidogo ao “wanazuia” hisia zao? Haiko vile kabisa. Hata kama kukubali huzuni na kuionyesha kunaweza kufanya mutu ajisikie muzuri, hakuna “njia moja tu ya muzuri” ya kuonyesha huzuni. Jambo hilo linategemea sana desturi ya mutu mwenye amefiwa, utu wake, na mambo yenye yalimupata mu maisha, na pia namna alipenda mutu mwenye amekufa.

      HALI ITAKUWA MUBAYA KWA KIASI GANI?

      Pengine watu wenye wamefiwa hawawezi kujua mambo yenye wanapaswa kutazamia kisha kifo cha mupendwa wao. Lakini kwa kawaida, kuko hisia na magumu mbalimbali yenye inatokea, na mara nyingi mutu anaweza kutazamia itokee. Tufikirie mambo yenye kufuata:

      Kuwa na hisia nyingi sana. Kulia, kutamani kuona mutu mwenye alikufa, na hisia kubadilika haraka, ni mambo yenye inaweza kufikia mutu mwenye amefiwa. Zaidi ya kuwa na hisia, mutu mwenye amefiwa anaweza kukumbuka sana mupendwa wake na anaweza kuota ndoto. Hata hivyo, jambo la kwanza lenye linaweza kutokea ni kushtuka na kushindwa kuamini. Tiina anakumbuka vile alitenda wakati bwana yake Timo, alipatwa na kifo cha kushtukia. Anasema hivi: “Ku mwanzo nilisikia kama vile mwili hautumike tena. Ku mwanzo nilishindwa hata kulia. Nilichoka sana hivi kwamba wakati fulani ilikuwa nguvu kupumua. Sikuamini jambo lenye lilikuwa limefanyika.”

      Pia, ni kawaida kuwa na mahangaiko, kisirani na kujilaumu. Ivan anasema hivi: “Kwa muda fulani kisha kifo cha Eric mutoto wetu mwanaume wa miaka 24, mimi na bibi yangu Yolanda, tulikasirika sana! Jambo hilo lilitushangaza, juu tulikuwa hatujawazaka kama tunaweza kukasirika. Tulijilaumu pia, juu tuliwaza kama pengine hatukufanya mengi zaidi ili kusaidia mutoto wetu.” Alejandro, mwenye bibi yake alikufa na ugonjwa wenye kukawia, alijisikia pia kuwa mwenye kosa. Anasema hivi: “Ku mwanzo, niliwaza kuwa, ikiwa Mungu anaruhusu niteseke hivi, ninapaswa kuwa mutu mubaya. Kisha, nilijisikia kuwa mwenye kosa, juu ilionekana kama vile nilikuwa ninamulaumu Mungu juu ya jambo lenye lilikuwa limefanyika.” Kostas mwenye tulizungumuzia mu habari yenye ilitangulia, yeye pia anasema hivi: “Wakati fulani hata nilimukasirikia Sophia juu alikufa. Kisha, kujisikia vile kulifanya nijilaumu. Kwa kweli, haikuwa kosa lake.”

      Kushindwa kufikiri muzuri. Kuko wakati wenye mutu mwenye amefiwa anaweza kuwa na mawazo yenye haifuatane muzuri. Kwa mufano, mutu mwenye amefiwa anaweza kufikiri kuwa inawezekana kusikia mutu mwenye amekufa, ao kumuona. Pia, mutu mwenye amefiwa anaweza kushindwa kukaza akili juu ya jambo fulani ao kukumbuka. Tiina anasema hivi: “Wakati fulani tungekuwa na mazungumuzo, lakini ningetambua kuwa mawazo yangu ilikuwa fasi ingine! Wakati huo, mambo yenye yalifanyika mbele na kisha kifo cha Timo, yalikuja haraka sana mu akili yangu. Kushindwa kukaza akili juu ya mambo, kulileta pia mahangaiko.”

      Mutu kupenda kuwa peke yake. Mutu mwenye huzuni kwa sababu ya kufiwa anaweza kukosa kutulia wakati iko na watu wengine. Kostas anasema hivi: “Wakati nilikuwa pamoja na watu wenye kuoana, nilijiona kama vile mugeni. Lakini pia wakati nilikuwa pamoja na watu wenye hawajaoa ao kuolewa, nilijiona kama mugeni.” Yolanda bibi ya Ivan, anakumbuka: “Ilikuwa nguvu sana kuwa kati ya watu wenye walilalamika juu ya magumu yenye yalionekana kuwa ya kidogo sana kama yangelinganishwa na magumu yetu! Kisha, kulikuwa watu wenye walituambia namna watoto wao walikuwa wanafanya maendeleo ya muzuri. Nilifurahi wakati waliniambia vile, lakini haikuwa mwepesi kuendelea kuwasikiliza. Mimi na bwana yangu tulielewa kuwa maisha inaendelea, lakini ni sisi njo tulikosa nia na uvumilivu.”

      Matatizo ya Afya. Ni kawaida kupata mabadiliko katika hamu ya kula, kilo ya mwili kuongezeka ao kupunguka, ao kuwa na matatizo ya usingizi. Aaron anakumbuka jambo lenye lilitokea mwaka moja kisha kifo cha baba yake. Anasema hivi: “Nilifikia kabisa kuwa na matatizo ya usingizi. Kila usiku niliamuka wakati uleule nikifiri juu ya kifo cha baba yangu.”

      Alejandro anakumbuka kama alikuwa na matatizo ya afya yenye ilikuwa nguvu kuelewa. Anasema hivi: “Mara mingi nilichunguzwa na munganga na alinihakikishia kama nilikuwa na afya ya muzuri. Niliwaza kuwa ni huzuni njo yenye ilifanya nikuwe na alama za mutu mwenye kugonjwa.” Alama hizo zilifikia kuisha. Hata hivyo, uamuzi wa Alejandro wa kuona munganga ulikuwa wenye hekima. Huzuni inaweza kupunguza uwezo wa mwili wa kujikinga na magonjwa, kufanya tatizo fulani la afya liongezeke, ao kutokeza tatizo lingine la afya.

      Kuwa na magumu ya kufanya kazi za maana. Ivan anakumbuka: “Kisha kifo cha Eric, tulipaswa kujulisha jambo hilo kwa watu wa jamaa na marafiki, lakini pia kwa watu wengine kama vile mukubwa wake wa kazi na mutu mwenye alikuwa anamupangisha. Kulikuwa pia vikaratasi vingi vyenye kuombwa na sheria vyenye tulipaswa kujaza. Kisha tulipaswa kuangalia vitu vyenye Eric alikuwa navyo. Mambo hayo yote yalituomba kutumikisha sana akili hata kama wakati huo tulikuwa wenye kuchoka kiakili, kimwili, na hata kama tulikuwa na huzuni nyingi.”

      Lakini kwa watu fulani, hali inakuwa nguvu kabisa kisha muda fulani, wakati wanakuwa na lazima ya kufanya mambo yenye yalikuwa yanafanywa na mupendwa wao mwenye alikufa. Jambo hilo lilimufikia Tiina. Anasema hivi: “Sikuzote Timo alikuwa anaangalia mambo yetu ya benki na mambo mengine yenye kuhusu biashara. Sasa mimi njo nilipaswa kuangalia mambo hayo, na hilo liliniongezea mahangaiko. Je, ningeweza kabisa kutimiza mambo yote hayo bila kufanya makosa?”

      Magumu yenye tumezungumuzia hapo juu, ni kusema, ya kiakili, ya kimwili, na yenye kuhusu hisia, yanaonyesha kama inaweza kuwa nguvu sana kupambana na huzuni ya kufiwa. Ukweli ni kwamba, maumivu ya kufiwa na mupendwa yanaweza kuwa makali sana, lakini kujua hilo mbele ya wakati kunaweza kusaidia mutu mwenye amefiwa hivi karibuni avumilie. Kumbuka pia kama haiko kila mutu anapatwa na matokeo hayo yote yenye yanaweza kuletwa na huzuni. Zaidi ya hilo, watu wenye wamefiwa wanaweza kupata kitulizo kwa kujua kama hisia kali zenye kuletwa na huzuni ya kufiwa ni za kawaida.

      NITAKUWAKA TENA NA FURAHA?

      Kile unapaswa kutazamia: Maumivu ya kufiwa haiendeleake milele; inafikia kupunguka. Hilo halimaanishe kuwa mutu mwenye amefiwa “anapona” kabisa ao anasahau mupendwa wake. Lakini, maumivu makali yenye kuletwa na huzuni yanapunguka polepole. Yanaweza kutokea tena wakati mutu anakumbuka mambo fulani bila kutazamia, ao wakati wa siku fulani katika mwaka, kama vile siku ya ndoa ao siku yenye mupendwa alikufa, na mambo mengine. Lakini, watu wengi wanafikia kuwa na usawaziko katika namna yao ya kuonyesha hisia na wanafikia tena kukaza akili juu ya kazi zao za kila siku. Mambo inakuwa kabisa vile, wakati watu wa familia ao marafiki wanategemeza mutu mwenye amefiwa na wakati anakamata hatua zenye kufaa ili kuvumilia.

      Hali hiyo itaendelea mupaka wakati gani? Kwa watu fulani, hali hiyo yenye kuwa mubaya zaidi inaweza kufanya miezi. Kwa watu wengi, hali hiyo inaweza kuchukua mwaka moja ao mbili mbele wajisikie muzuri zaidi. Na kwa watu fulani inaomba wakati murefu zaidi.a Alejandro anakumbuka: “Kwangu mimi, huzuni kubwa ya kufiwa ilifanya karibu miaka tatu.”

      Ujivumilie. Kaza akili juu ya mambo ya leo, ufanye mambo kama zamani, na ujue kuwa maumivu ya kufiwa haiwezi kuendelea milele. Hata hivyo, ni mambo gani yenye unaweza kufanya ili kupunguza huzuni yako sasa na hata kuizuia iendelee bila sababu yoyote?

      Hisia kali zenye kuletwa na huzuni ya kufiwa ni za kawaida

      a Watu kidogo wanaweza kupatwa na huzuni kali sana na yenye kuendelea hivi kwamba huzuni hiyo imefikia kuitwa huzuni yenye kuwa “nguvu kuelewa” ao huzuni yenye “kukawia.” Watu kama hao wanaweza kuwa na lazima ya kusaidiwa na wanganga wa akili.

  • Namna ya Kupambana na Huzuni—Mambo Yenye Unaweza Kufanya Leo
    Amuka!—2018 | No. 3
    • Watu kwenye plage wanapeperusha tiara na kukamata picha

      MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

      Namna ya Kupambana na huzuni Mambo Yenye Unaweza Kufanya Leo

      Kama unatafuta mashauri juu ya namna ya kupambana na huzuni, bila shaka utapata mawazo mengi sana​—mawazo fulani yanasaidia zaidi kuliko mengine. Pengine ni kwa sababu, kama vile tumeona, kila mutu iko na namna yake ya kuonyesha huzuni. Pengine mashauri yenye yanasaidia mutu mumoja hayawezi kusaidia mwengine.

      Lakini, kuko mashauri ya musingi yenye watu wengi wameona kuwa ni yenye kufaa. Mashauri hayo yanatajwa mara nyingi na watu wenye kushauria wale wenye wamefiwa, na yanapatana na kanuni zenye kutumainika na zenye kupatikana mu Biblia, kitabu cha zamani chenye hekima.

      1: KUBALI MUSAADA WENYE WATU WA FAMILIA NA MARAFIKI WANAKUTOLEA

      • Watu kwenye plage wanapeperusha tiara na kukamata picha

        Watu fulani wenye elimu wameona hilo kuwa jambo la maana lenye linasaidia kupambana na huzuni ya kufiwa. Hata hivyo, wakati fulani unaweza kupenda kuwa peke yako. Unaweza hata kukasirikia wale wenye wanajaribu kukusaidia. Hilo ni jambo la kawaida.

      • Usiwaze kama sikuzote unapaswa kuwa pembeni ya watu wengine, lakini pia usijitenge kabisa nao. Kwa kweli, unaweza kuwa na lazima ya musaada wao wakati wenye kuja. Kwa upole, uwaambie kile unapenda wakati huo na kile haupendi.

      • Kulingana na hali yako, uonyeshe usawaziko kati ya wakati wa kuwa pamoja na watu wengine na wakati wa kuwa peke yako.

      KANUNI: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja . . . Kwa maana kama mumoja wao anaanguka, ule mwingine anaweza kusimamisha mwenzake.”​—Muhubiri 4:9, 10.

      2: UKUWE MUANGALIFU KUHUSU CHAKULA CHENYE UNATUMIA, NA UPANGE KUFANYA MAZOEZI

      • Chakula ya muzuri inaweza kusaidia kupambana na mahangaiko yenye kuletwa na huzuni. Ujaribu kula matunda mbalimbali, mboga za majani, na chakula chenye kuwa na proteine, lakini chenye hakina mafuta mengi.

      • Kunywa maji mengi na vinywaji vingine vyenye kuwa muzuri kwa afya.

      • Kama uko na hamu kidogo ya kula, kula sehemu kidogo-kidogo kila mara. Unaweza pia kuuliza munganga wako juu ya chakula kingine chenye kujenga mwili chenye unaweza kutumia.a

      • Kufanya mazoezi ya kutembea haraka na aina zingine za mazoezi ya mwili kunaweza kupunguza hisia zenye hazifae. Kufanya mazoezi kunaweza kupatia mutu nafasi ya kufikiri juu ya kifo cha mupendwa wake ao nafasi ya kusahau kwanza jambo hilo.

      KANUNI: “Hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.”​—Waefeso 5:29.

      3: ULALE SAA ZA KUENEA

      • Kitanda

        Usingizi ni wa maana sikuzote, lakini zaidi sana kwa wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa, juu huzuni inaweza kufanya mutu achoke zaidi.

      • Ukuwe mwangalifu kuhusu kiasi cha kafeini na pombe yenye unatumia, juu vinaweza kuvuruga usingizi wako.

      KANUNI: “Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.”​—Muhubiri 4:6.

      4: UKUWE TAYARI KUBADILIKA

      • Mwanamuke mwenye huzuni anazungumuza na rafiki yake

        Ujue kama kila mutu iko na namna yake ya kuonyesha huzuni. Mwishowe, itakuomba kuamua ni njia gani ya muzuri zaidi yenye unaweza kutumia ili kupambana na huzuni.

      • Watu wengi wanaona kama kuambia wengine huzuni yao kunawasaidia kupambana nayo, lakini wengine wanaamua kuficha huzuni yao. Kuonyesha hisia kunaweza kusaidia mutu aweze kupambana na huzuni yake, lakini watu wenye elimu wako na mawazo tofauti juu ya jambo hilo. Ikiwa unapenda kuambia mutu mwengine namna unajisikia, lakini uko unasita kufanya vile, pengine inaweza kuwa mwepesi zaidi kwako ikiwa unaelezea rafiki yako wa karibu hisia zako fulani.

      • Watu fulani wanaona kama kulia kunawasaidia kupambana na huzuni yao, lakini inaonekana kuwa wengine wanapambana na huzuni yao hata kama wanalia kidogo tu.

      KANUNI: “Moyo unajua uchungu wake mwenyewe.”​—Mezali 14:10.

      5: EPUKA MAZOEA YENYE KUHARIBU AFYA

      • Mwanaume mumoja anakunywa pombe

        Watu fulani wenye wamefiwa wanajaribu kupunguza maumivu yao ya moyoni kwa kutumia mubaya pombe na dawa za kulewesha. Kujaribu kupunguza huzuni kwa njia hiyo kunaharibu afya. Kujituliza kwa njia hiyo ni kwa muda mufupi, na kunaweza kuleta tu matokeo makubwa ya mubaya. Jaribu kutumia njia zenye hazina hatari ili kupunguza mahangaiko yako.

      KANUNI: “Tujisafishe kila uchafu.”​—2 Wakorinto 7:1.

      6: TUMIA WAKATI WAKO KWA USAWAZIKO

      • Watu wengi wanaona kuwa ni jambo lenye kufaa kubadilisha vipindi vya kuonyesha huzuni (wakati wa kuonyesha na kupambana na hisia zao) na vipindi vya kubakia bila huzuni (wakati wa kufanya mambo yenye kuwasaidia wasahau kwanza maumivu yao).

      • Unaweza kupata kitulizo kwa muda fulani kwa kuanzisha urafiki ao kwa kukomalisha uhusiano na marafiki wako, kwa kujifunza ufundi mupya, ao kwa kutafuta wakati wa kujifurahisha.

      • Kadiri wakati unapita, bila shaka namna unatumia wakati itabadilika. Unaweza kutambua kuwa mara mingi zaidi unaanza kuwa na wakati murefu wa kubakia bila huzuni​—jambo lenye kwa kawaida ni hatua ya kupona kutokana na huzuni yako.

      KANUNI: “Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa, . . . wakati wa kulia na wakati wa kucheka; wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza.”​—Muhubiri 3:1, 4.

      7: RUDILIA PROGRAMU YAKO YA KAWAIDA NA UIHESHIMIE

      • Mwanamuke mumoja anatumia kalendari ili kupanga programu yake

        Kadiri inawezekana, rudilia bila kukawia maisha yako ya kawaida.

      • Kama unaheshimia programu yako ya kulala, ya kazi, na programu ya kufanya mambo mengine, bila shaka utafikia kufanya mambo kama zamani.

      • Kuendelea kuwa na mambo mengi ya muzuri ya kufanya kunaweza kukusaidia kupunguza maumivu ya moyoni.

      KANUNI: “Itakuwa vigumu kwake kutambua kwamba siku za maisha yake zinapita haraka, kwa sababu Mungu wa kweli anamufanya aendelee kufurahi sana katika moyo wake.”​—Muhubiri 5:20.

      8: EPUKA KUFANYA MAAMUZI MAKUBWA HARAKA-HARAKA

      • Watu wengi wenye wanafanya maamuzi makubwa kisha tu kufiwa na mupendwa wao wanafikia kuhuzunika juu ya maamuzi yao.

      • Kama inawezekana, chunga kipindi fulani cha wakati kipite mbele uhame, ubadilishe kazi, ao upatie watu wengine vitu vya mupendwa wako mwenye amekufa.

      KANUNI: “Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.”​—Mezali 21:5.

      9: KUMBUKA MUPENDWA WAKO MWENYE ALIKUFA

      • Mwanaume mumoja anaonyesha marafiki wake picha ya bibi yake mwenye alikufa

        Watu wengi wenye wamefiwa wanaona kama ni muzuri kufanya mambo yenye yanaweza kuwasaidia wakumbuke mutu mwenye amekufa.

      • Pengine unaweza kupata kitulizo kwa kukusanya picha ao vitu vingine vyenye kusaidia kukumbuka, ao kuandika matukio ao mambo fulani yenye ungependa kukumbuka.

      • Uchunge vitu vyenye vinaweza kukukumbusha mambo ya muzuri, na kisha muda fulani wenye unapenda, uviangalie.

      KANUNI: “Kumbuka siku za zamani.”​—Kumbukumbu la Torati 32:7.

      10: UTOKE KIDOGO

      • Unaweza kupanga kuenda mapumuziko.

      • Ikiwa unaona kama haitawezekana kuenda mapumuziko kwa muda murefu, pengine unaweza kufanya jambo fulani lenye kufurahisha kwa siku moja ao mbili, kama vile kutembea kwa muda murefu, kutembelea nyumba ya makumbusho (ao, musée), ao kutembea na motokari.

      • Hata kufanya jambo fulani tofauti na mambo yenye unazoea kufanya, kunaweza kukusaidia upambane na huzuni yako.

      KANUNI: “Mukuje ninyi wenyewe mahali kwenye hakuna watu ili mupumuzike kidogo.”​—Marko 6:31.

      11: USAIDIE WENGINE

      • Mwanamuke mumoja kijana anasaidia mwanamuke mwenye kuzeeka kuuza vitu

        Kumbuka kama wakati wowote wenye unaweza kutumia ili kusaidia wengine, unaweza kukusaidia ujisikie muzuri zaidi.

      • Unaweza kuanza kwa kusaidia watu wenye wako pia na huzuni juu ya kifo cha mupendwa wako, kama vile marafiki ao watu wa jamaa yako wenye wanaweza kuwa na lazima ya mutu mwenye kuwa pia na huzuni ao mwenye kuelewa namna wanajisikia.

      • Kutegemeza na kutuliza watu wengine kunaweza kukufanya ukuwe tena na furaha na kufanya uone kama unaweza kutimiza tena jambo fulani la maana na kuwa ungali na kusudi katika maisha.

      KANUNI: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

      12: CHUNGUZA UPYA MAMBO YENYE UNATANGULIZA

      • Huzuni ya kufiwa inaweza kufanya mutu aelewe muzuri zaidi ni mambo gani yenye kuwa ya maana kabisa.

      • Tumia nafasi hiyo ili kuchunguza namna unatumia maisha yako.

      • Kama ni lazima, fanya mabadiliko kuhusu mambo yenye unatanguliza mu maisha yako.

      KANUNI: “Ni muzuri zaidi kuenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kuenda katika nyumba ya karamu, kwa sababu huo ndio mwisho wa kila mwanadamu, na wenye kuwa wazima wanapaswa kuweka jambo hilo katika moyo.”​—Muhubiri 7:2.

      NAMNA YA KUPAMBANA NA HUZUNI YAKO | KIFUPI

      • 1: KUBALI MUSAADA WENYE WATU WA FAMILIA NA MARAFIKI WANAKUTOLEA

        Kulingana na hali yako, uonyeshe usawaziko kati ya wakati wa kuwa pamoja na watu wengine na wakati wa kuwa peke yako.

      • 2: UKUWE MUANGALIFU KUHUSU CHAKULA CHENYE UNATUMIA, NA UPANGE KUFANYA MAZOEZI

        Ukule chakula chenye kuwa muzuri kwa afya, ukunywe maji mengi, na ufanye mazoezi kwa usawaziko.

      • 3: ULALE SAA ZA KUENEA

        Ujue kama usingizi ni wa maana ili kupambana na muchoko wenye kuletwa na huzuni ya kufiwa.

      • 4: UKUWE TAYARI KUBADILIKA

        Kwa kuwa kila mutu iko na namna yake ya kuonyesha huzuni, chagua njia ya muzuri yenye unaweza kutumia ili kupambana na huzuni.

      • 5: EPUKA MAZOEA YENYE KUHARIBU AFYA

        Epuka kutumia mubaya pombe na dawa za kulewesha​—juu vitu hivyo vinaweza kuongeza matatizo kuliko kuimaliza.

      • 6 TUMIA WAKATI WAKO KWA USAWAZIKO

        Badilisha vipindi vya kuonyesha huzuni na vipindi vya kuwa pamoja na watu wengine na kujifurahisha.

      • 7: RUDILIA PROGRAMU YAKO YA KAWAIDA NA UIHESHIMIE

        Kuendelea kuwa na mambo mengi ya kufanya na kuheshimia programu yako ya kawaida kutakusaidia ufanye mambo kama zamani.

      • 8: EPUKA KUFANYA MAAMUZI MAKUBWA HARAKA-HARAKA

        Kama inawezekana, chunga mwaka moja ao zaidi mbele ufanye maamuzi makubwa ili usifikie kuhuzunika juu ya maamuzi yako.

      • 9: KUMBUKA MUPENDWA WAKO MWENYE ALIKUFA

        Ukusanye picha na vitu vyenye kusaidia kukumbuka ao andika mambo yenye yanaweza kukusaidia ukumbuke mutu mwenye amekufa.

      • 10: UTOKE KIDOGO

        Ufanye jambo fulani lenye kuwa tofauti na mambo yenye unazoea kufanya​—hata kwa saa fulani ao siku muzima.

      • 11: USAIDIE WENGINE

        Kusaidia watu wengine wenye kuwa na lazima ya musaada, kutia ndani watu wenye wako pia na huzuni juu ya kifo cha mupendwa, kunaweza kukusaidia ukuwe tena na kusudi katika maisha.

      • 12: CHUNGUZA UPYA MAMBO YENYE UNATANGULIZA

        Utumie nafasi hiyo ili kuelewa mambo ya maana kabisa mu maisha na, kama ni lazima, ufanye mabadiliko kuhusu mambo yenye unatanguliza mu maisha yako.

      Ni kweli kwamba, hakuna kitu chenye kinaweza kumaliza kabisa maumivu yenye unasikia. Lakini, watu wengi wenye wamefiwa na mupendwa wao, wanaweza kushuhudia kuwa, kufuata hatua zenye kufaa, kama zile zenye tumezungumuzia katika habari hii, kuliwasaidia kupata kitulizo. Kwa kweli, liste hii haizungumuzie mambo yote yenye mutu anaweza kufanya ili kupunguza huzuni. Lakini, kama unajaribu kutumia mapendekezo fulani kati ya mapendekezo hayo, utaona kuwa yatakusaidia utulie kwa kiasi kikubwa.

      a Amuka! haipendekeze aina yoyote ya matunzo.

  • Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa
    Amuka!—2018 | No. 3
    • Katika Paradiso, watu wako tayari kukaribisha wapendwa wao wenye wamefufuliwa

      MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

      Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa

      HIVI KARIBUNI, WATU WENGI WAMETAFUTA HABARI ZAIDI JUU YA MAUMIVU YENYE MUTU ANAPATA WAKATI ANAFIWA NA MUTU MWENYE ANAPENDA. Lakini, kama vile tumekwisha kuzungumuzia, mashauri ya muzuri zaidi yenye yametolewa na watu wenye elimu, mara nyingi yanapatana na hekima ya zamani yenye kupatikana mu Biblia. Hilo linaonyesha wazi kuwa muongozo wa Biblia ni wenye faida sikuzote. Hata hivyo, Biblia iko na mambo mengi zaidi ya mashauri yenye kutumainika. Inatoa habari zenye haziwezi kupatikana fasi zingine, habari zenye zinaweza kuletea kitulizo wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa.

      • Inatuhakikishia kwamba wapendwa wetu wenye wamekufa hawateseke

        Katika Muhubiri 9:5, Biblia inasema hivi: “Wafu hawajue kitu chochote.” ‘Mawazo yao yanapotea.’ (Zaburi 146:4) Kufuatana na jambo hilo, Biblia inalinganisha kifo na usingizi muzito.​—Yohana 11:11.

      • Kuwa na imani yenye nguvu katika Mungu mwenye upendo kunaleta kitulizo

        Katika Zaburi 34:15, Biblia inasema hivi: “Macho ya Yehovaa yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.” Wakati tunamuambia Mungu katika sala namna tunajisikia, tunapata kitulizo zaidi kuliko kitulizo chenye tunaweza kupata kwa kuambia mutu fulani ao kwa kutumia njia fulani ya kuzuia mawazo yetu. Kufanya vile kunatusaidia kuanzisha uhusiano wa pekee pamoja na Muumbaji wetu, mwenye anaweza kutumia nguvu zake ili kutupatia kitulizo.

      • Inatupatia tumaini kwa ajili ya wakati wenye kuja wa muzuri zaidi

        Wazia namna mambo itakuwa wakati watu wenye kuwa katika makaburi wataishi tena katika dunia! Biblia inazungumuzia wakati huo mara nyingi. Ili kuonyesha namna hali itakuwa katika dunia wakati huo, Biblia inasema kama Mungu “atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

      Watu wengi wenye kumuamini Yehova, Mungu mwenye kutajwa mu Biblia, wanapata kabisa nguvu ya kupambana na huzuni yao juu wako na imani kuwa wataona tena wapendwa wao wenye wamekufa. Kwa mufano, Ann, mwenye alifiwa na bwana yake wa miaka 65, anasema hivi: “Biblia inanihakikishia kuwa wapendwa wetu wenye wamekufa hawateseke na kuwa Mungu atafufua wale wote wenye kuwa mu kumbukumbu lake. Nakumbuka mambo hayo wakati wowote nafikiria kifo cha mupendwa wangu, na matokeo ni kwamba, sasa niko na uwezo wa kupambana na jambo la mubaya zaidi lenye limekwisha kunifikia!”

      Tiina, mwenye tumekwisha kuzungumuzia katika gazeti hili, anasema hivi: “Tangu siku Timo akufe, Mungu amekuwa akinitegemeza. Nimeona kabisa mukono wa Yehova ukinisaidia wakati wa magumu. Na ahadi ya Mungu kuhusu ufufuo ni ya kweli kabisa kwangu. Inanitia nguvu kusonga mbele mupaka wakati wenye nitamuona tena Timo.”

      Maneno hayo yanapatana na maneno ya mamilioni ya watu wenye kuwa hakika kama Biblia inasemaka kweli. Hata kama unawaza kuwa mambo yenye Biblia inasema haiko ya kweli ao ni ndoto tu, unapaswa kutafuta ushuhuda wenye kuonyesha kuwa mashauri na ahadi zake ni za kweli. Bila shaka utaona kuwa Biblia inatoa musaada wa muzuri zaidi kwa wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa.

      UJIFUNZE MENGI ZAIDI KUHUSU TUMAINI KWA AJILI YA WATU WENYE WAMEKUFA

      Angalia Video juu ya habari hii kwenye site yetu ya Enternete, jw.org

      Katika Paradiso, watu wako tayari kukaribisha wapendwa wao wenye wamefufuliwa

      Biblia inaahidi kuwa wakati wenye kuja tutakaribisha wapendwa wetu wenye wamekufa

      WATU WENYE WAMEKUFA WAKO KATIKA HALI GANI?

      Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?

      Ni nini inatokea wakati mutu anakufa? Jibu la Biblia lenye kuwa wazi linatuliza na kutia moyo

      Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO (Ona chini ya kichwa Video: Biblia)

      UTAPENDA KUSIKIA HABARI NJEMA?

      Utapenda Kusikia Habari Njema?

      Kwa kuwa habari za mubaya ziko nyingi sana, ni wapi unaweza kupata habari njema? Video hii inatanguliza broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!

      Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO (Ona chini ya kichwa Video: Mikutano na kazi yetu ya Mahubiri)

      a Yehova ni jina la pekee la Mungu kama vile inaonyeshwa mu Biblia.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine