Kusonga Mbele Kwako Kuwe Wazi!
1 Kumbuka mara ya kwanza uliposikia ujumbe wa Ufalme. Kweli rahisi ziliamsha hamu yako ya kujua na kuelewa. Ukitambua kwamba njia za Yehova ni za juu zaidi kuliko njia zako, haukukawia kutambua kwamba ilikuomba kubadili namna yako ya kuishi. (Is. 55:8, 9) Ulisonga mbele, uliweka uhai wako wakfu kwa Mungu na ulibatizwa.
2 Hata baada ya kutimiza maendeleo fulani kwa upande wa kiroho, kulikubakilia udhaifu fulani wa kushindana nao. (Rom. 12:2) Labda ulikuwa ukienda kuhuburi pasipo kutaka, kwa sababu ya woga wa wanadamu. Au ulikuwa na magumu ya kukomaza matunda ya roho ya Mungu. Lakini haukujiachilia, kwani ulikuwa mwenye kuazimia kusonga mbele kwa kujiwekea miradi ya kitheokrasi.
3 Tangu ulipojiweka wakfu kwa Mungu, labda miaka mingi imekwisha kupita. Miaka nenda, ni maendeleo gani unaweza kutaja? Je! ulifikia mojawapo ya miradi yako? Sikuzote je! una juhudi ile ‘uliokuwa nayo hapo mwanzoni?’ (Ebr. 3:14) Paulo alipomwambia: “Fikiri kwa uzito juu ya mambo haya; vama katika hayo, ili kusonga mbele kwako kupate kuwa dhahiri kwa watu wote,” tayari Timotheo alikuwa amekwisha kuwa Mkristo mkomavu kupitia miaka ya ujuzi.—1 Tim. 4:15, TUM.
4 Tujichunguze: Ikiwa tunafikiria namna maisha yetu yalivyo kufikia sasa, tunaona nini? Je! tuna sikuzote udhaifu fulani fulani tuliokuwa nao tangu mwanzoni? Je! tuliepa miradi yetu? Ikiwa ndiyo, kwa nini? Labda tulikuwa na makusudi mazuri, lakini tulikuwa tukiyasukumia mbele. Iwe labda tulijiacha kuregezwa na mahangaiko ya maisha.—Lu. 17:28-30.
5 Hakika, haiwezekani kurudilia wakati uliopita, lakini wakati ujao ni wetu. Tujichunguze wenyewe kwa unyofu, tutambue udhaifu wetu, kisha tukusanye nguvu zetu ili kujiboresha. Labda imetupasa kuonyesha vizuri zaidi matunda ya roho ya Mungu, kujidhibiti (kujiweza), upole au ustahimilivu kwa mfano. (Gal. 5:22, 23, TUM) Ikiwa tuna magumu ya kusikilizana na wengine au kushirikiana na wazee, ni jambo la lazima kwamba tukomaze unyenyekevu wa roho.—Flp. 2:2, 3.
6 Je! kusonga mbele kwetu kungeonekana wazi zaidi ikiwa tungetumika kwa kufikia mapendeleo ya utumishi? Akina ndugu bila shaka wanaweza kuwa watumishi wa huduma au wazee, kwa kufanya bidii fulani ya ziada. Wamoja kati yetu wako labda katika hali ya kuwa mapainia wa kawaida. Kwa wengine wengi, utumishi wa upainia msaidizi ni mradi unaoweza kufikiwa. Wengine tena wangeweza kushikilia kuboresha mazoea yao ya funzo, kushiriki maelezo zaidi wakati wa mikutano ya kutaniko, au kuwa wahubiri wenye kuzaa matunda zaidi.
7 Ni kwa kila mmoja, bila shaka, kusema ni katika mambo gani imempasa kusonga mbele. Tuweni hakika kwamba tutakuwa wenye shangwe zaidi na wenye kuzaa matunda zaidi katika kutaniko ikiwa tunafanya bidii nyofu ili ‘tuzidi kusonga mbele kwenye ukomavu.’—Ebr. 6:1, TUM.