Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 5 uku. 10-11
  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anapenda Dunia Ikuwe Namna Gani?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Tutaonana Katika Paradiso!”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Mungu Anapenda Wanadamu Wakuwe na Maisha ya Namna Gani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 5 uku. 10-11

Somo 5

Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?

Sababu gani Yehova aliumba dunia? (1, 2)

Sababu gani sasa dunia si paradiso? (3)

Jambo gani litawafikia watu waovu? (4)

Katika wakati ujao, Yesu atafanya nini kwa ajili ya wagonjwa? wazee? wafu? (5, 6)

Ili ushiriki katika baraka za wakati ujao, unahitaji kufanya nini? (7)

1. Yehova aliumba dunia hii ili kwamba binadamu waweze kufurahia kuishi juu yake milele. Alipenda kwamba dunia ikaliwe siku zote na watu wenye haki, wenye furaha. (Zaburi 115:16; Isaya 45:18) Dunia haitaharibiwa kamwe; itadumu milele.​—⁠Zaburi 104:5; Muhubiri 1:⁠4.

2. Kabla ya Mungu kumufanya mutu, Yeye alichagua sehemu ndogo ya dunia na kuifanya kuwa paradiso nzuri sana. Hiyo aliiita bustani ya Edeni. Hapa ndipo aliwatia mwanamume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Hawa. Mungu alikusudia kwamba wao wawe na watoto na kuijaza dunia yote. Polepole wangeweza kufanya dunia yote iwe paradiso.​—⁠Mwanzo 1:28; 2:​8, 15.

3. Adamu na Hawa walifanya zambi kwa kuvunja kimakusudi sheria ya Mungu. Hivyo Yehova aliwatia inje ya bustani ya Edeni. Paradiso ikapotea. (Mwanzo 3:​1-6, 23) Lakini Yehova hakusahau kusudi lake kuhusu dunia hii. Yeye ahidi kuifanya paradiso, mahali ambapo binadamu wataishi milele. Atafanya hivyo namna gani?​—⁠Zaburi 37:⁠29.

4. Kabla dunia hii haijaweza kuwa paradiso, watu waovu wanapaswa kuondolewa. (Zaburi 37:38) Jambo hilo litatukia kwenye Harmagedoni, ambayo ni vita ya Mungu itakayomaliza uovu. Baadaye, Shetani atatiwa gerezani kwa miaka 1 000. Hilo linamaanisha kwamba watu waovu wote hawataachwa hata mumoja aiharibu dunia. Ni watu wa Mungu peke yao ndiyo watakaookoka.​—⁠Ufunuo 16:​14, 16; 20:​1-3.

5. Ndipo Kristo Yesu atatawala dunia hii akiwa Mufalme kwa miaka 1 000. (Ufunuo 20:⁠6) Polepole Yeye ataondolea zambi mbali kutoka akili zetu na miili yetu. Tutakuwa binadamu wakamilifu kama vile walivyokuwa Adamu na Hawa kabla ya wao kufanya zambi. Ndipo hakutakuwa ugonjwa tena, uzee, na kifo. Watu wagonjwa wataponyeshwa, na watu wazee watakuwa vijana tena.​—⁠Yobu 33:25; Isaya 33:24; Ufunuo 21:​3, 4.

6. Katika Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu, binadamu waaminifu watafanya kazi kuigeuza dunia yote kuwa paradiso. (Luka 23:43) Pia, mamilioni ya waliokufa watafufuliwa kwenye uhai wa kibinadamu duniani. (Matendo 24:15) Wakifanya yale Mungu anataka kwao, wataendelea kuishi milele duniani. Ikiwa sivyo, wataangamizwa milele.​—⁠Yoane 5:​28, 29; Ufunuo 20:​11-15.

7. Kusudi la kwanza la Mungu juu ya dunia litakuwa hivyo limeshinda. Je, ungependa kushiriki katika baraka hizi za wakati ujao? Ikiwa ndiyo, unahitaji kuendelea kujifunza juu ya Yehova na kutii matakwa yake. Kuhuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi kutakusaidia kufanya hivyo.​—⁠Isaya 11:9; Waebrania 10:​24, 25.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Paradiso iliyopotea

[Picha katika ukurasa wa 11]

Kisha Harmagedoni, dunia itafanywa kuwa paradiso

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine