Majibu kwa Maswali Yenu
◼ Je! ni jambo lenye kufaa kwa Mkristo kuvaa kitambaa cheupe wakati wa mapiganob?
Wakati wa mapigano ya hivi karibuni yaliyofanyika katika nchi yetu, raia wengi walivaa kitambaa cheupe kuzunguka mkono au kichwa. Sababu gani? Katika nafasi moja, wavaaji wa kitambaa cheupe walitangaza hivyo uungaji-mkono wao upande ulioonekana kwao wenye ushindi. Wakati mwingine, uvaaji wa kitambaa cheupe ulikuwa alama ya kukiri kushindwa vita. Mahali kwengine, hata hivyo, jambo la kuvaa kitambaa cheupe lilionwa kuwa kama mpango wa usalama. Watu walikuwa wakivaa vitambaa ili kuhakikisha ulinzi wao.
Ni nini ungepaswa kuwa msimamo wa Mkristo? Ikiwa kuvaa kitambaa cheupe kunamaanisha kuunga-mkono upande mmoja au mwingine, mvaaji hangekuwa asiyekuwamo. Ikiwa kitambaa cheupe ni alama ya kukiri kushindwa vita, hilo linamaanisha kwamba mvaaji anadai kwamba alikuwa mpiganaji. Katika hali kama hizo, Mkristo angepaswa kukumbuka maneno ya Yesu katika Yohana 17:16 ambayo kulingana na hiyo wanafunzi wake “si sehemu ya ulimwengu.” Angepaswa pia kukumbuka habari ya kiunabii ya waabudu wa kweli wa Yehova kulingana na Isaya 2:2-4. Maandiko hayo yanatusaidia kuwa na wazo la Mungu juu ya maswali yanayojitokeza wakati wa vita.
Namna gani kuhusu mahali ambapo kuvaa vitambaa vyeupe kulikuwa tu mpango wa usalama, ambao mtu fulani angaweza kuchukua ili kuepuka kufyatuliwa risasi? Katika hali hiyo, ni kwa kila Mkristo kujiamulia mwenyewe ikiwa atavaa au hatavaa kitambaa cheupe. Ikiwa alifanya hivyo mahali ambapo kuvaa kitambaa kulionwa kuwa mpango wa usalama, hakuna mtu angepaswa kumlaumu.a Wazee hawangepaswa kutafuta kujua ikiwa yeye ni asiyekuwamo au hapana. Badala yake, inafaa kukumbuka kanuni inayotokana na Warumi 14:4: “Wewe ni nani umhukumu mtumishi wa nyumbani mwa mwingine? Kwa bwana-mkubwa wake mwenyewe yeye husimama au huanguka.” Ni nini liwezalo kufikiriwa wakati watu wote hawakubaliani juu ya maana ya kitambaa cheupe? Katika hali hiyo, kila mtu atachukua uamzi wake mwenyewe mbele ya Yehova Mungu, ikiwa atavaa au hatavaa kitambaa cheupe.—Gal. 6:5.
Namna gani kupanga mikutano wakati wa mapigano ikiwa hilo linaweka maisha ya ndugu zetu katika hatari? Miongozo bora juu ya jambo hilo inapatikana katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa 168, mafungu 1-3. Miongozo hiyo ni ya kusoma kwa uangalifu.
Kama tunavyojua, vita ni chanzo cha mikazo mingi na inatia Wakristo mbele ya mito mikubwa ya kushindana. Uhitaji mara nyingi ni mkubwa wa “kukaa macho na kutunza hisi zetu.” (1 Thes. 5:6) Wazee wangepaswa hasa kuwa waangalifu ili kulinda faida za kiroho za ndugu zao na kuwatolea mwongozo mzuri kwa kutumia kanuni za kibiblia kwa usawaziko.—Isaya 32:2.
[Footnote]
a Ona mambo yaliyoonwa yanayozungumziwa katika Amkeni! ya Januari 8, 1980, ukurasa 15, ambapo wamashonari walipeperusha bendera nyeupe wakati walipotafuta kujipatia njia nje ya eneo la mapigano.