Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/98 uku. 1
  • Roho Ya Yehova Ni Pamoja Nasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Roho Ya Yehova Ni Pamoja Nasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Walijiacha Waongozwe na Roho ya Mungu: Wakati wa Mitume na Katika Siku Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kwa Nini Tujiache Kuongozwa na Roho ya Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 6/98 uku. 1

Roho Ya Yehova Ni Pamoja Nasi

1 Kazi kubwa imekabidhiwa kwetu sisi, Mashahidi wa Yehova. Kwa kweli, Yesu alisema: “Katika mataifa yote lazima habari njema ihubiriwe kwanza.” (Mk. 13:10) Kwa maoni ya kibinadamu, hilo lingeonekana kuwa jambo lisilowezekana. Lakini katika ulimwengu, kunayo nguvu yenye uwezo inayotutegemeza​—Roho ya Mungu!​—Mt. 19:26.

2 Ushududa wa Karne ya Kwanza: Akitumia unabii wa Isaya juu yake mwenyewe, Yesu alisema: “Roho ya Yehova iko juu yangu, . . . [ili] kutangaza habari njema.” (Lk. 4:​17, 18) Kabla ya kupanda mbinguni, yeye aliambia mitume wake kwamba wao pia wangepokea nguvu ya roho takatifu ili wahubiri “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” Baadaye, roho takatifu ilimwamuru Filipo ahubiri towashi Mwethiopia, iliongoza Petro kwa akida Mroma, na pia ni roho takatifu iliyotuma Paulo na Barnaba kuhubiri kwa mataifa ya kipagani. Ni nani angaliamini kwamba watu kutoka mahali mbalimbali hivyo wangalikubali kweli? Lakini walifanya hivyo!​—Mdo. 1:8; 8:​29-​38; 10:19, 20, 44-​48; 13:​2-4, 46-​48.

3 Ushuhuda wa Siku za Leo: Kitabu cha Ufunuo kinatia mkazo juu ya utendaji wa roho takatifu siku zetu za kisasa katika kazi ya kuhubiri. Inaandikwa humo: “Na roho na bibi-arusi hufuliza kusema: ‘Njoo!’  . . . Acha yeyote atakaye achukue maji ya uhai bure.” (Ufu. 22:17) Roho ilisukuma jamii ya bibi-arusi wa Kristo na wenzi wao, “kondoo wengine,” kuhubiri habari njema kwa vikundi vyote vya watu. (Yn. 10:16) Kwa hiyo, tungepaswa kuhubiri kwa ujasiri. Tusisite kamwe kuongea na watu wa kila aina, lakini tuwe hakika sikuzote kwamba roho ya Mungu itatusaidia. Kitabu-Mwaka 1998 kinathibitisha kwa njia yenye kusadikisha kwamba roho ya Mungu sikuzote ni pamoja na watumishi wake. Je! umetazama idadi humo? Mnamo miaka miwili ya utumishi iliyopita, kwa wastani, zaidi ya watu 1 000 walibatizwa kila siku!

4 Uwe hakika kwamba roho ya Mungu itaendelea kuwa pamoja nasi kadiri Yehova atakavyotaka kwamba tuhubiri ujumbe wa Ufalme. Tukijua hilo, na tuendelee kujitoa kwa nguvu katika kazi ya maana ya Ufalme.​—1 Tim. 4:​10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine