Kalenda ya 2011 Inakazia Ibada ya Familia
Kichwa cha Kalenda ya 2011 ya Mashahidi wa Yehova ni Ibada ya Familia. Kalenda hiyo inaonyesha familia za leo na familia za watu wa zamani wanaozungumziwa katika Biblia. Inaonyesha pia wenzi wa ndoa na watumishi wa Yehova walio waseja wakijifunza Neno lake.
Watu wanaozungumziwa katika Biblia wanaoonyeshwa kwenye kalenda walipendezwa na sheria ya Yehova, na hilo liliwasaidia washinde matatizo ya pekee waliyopambana nayo. (Zab. 1:2, 3) Tunapochunguza kila picha, hilo litatukumbusha kwamba Ibada ya Familia ni jambo la maana, iwe tunapatikana katika familia kubwa ao ndogo, familia ambayo washiriki wote ni mashahidi ao iliyo na washiriki fulani wasio mashahidi. Katika kalenda hiyo kuna nafasi iliyo wazi ambayo munaweza kutumia ili kuonyesha siku munayofanya Ibada ya Familia. Je, umekwisha kujaza nafasi hiyo?